Pre GE2025 Tundu Lissu na John Heche watangaza kuipeleka ajenda yao ya "No Reform No Election" nje ya nchi

Pre GE2025 Tundu Lissu na John Heche watangaza kuipeleka ajenda yao ya "No Reform No Election" nje ya nchi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Wakuu,

Kumbe Heche na Lissu walikuwa na mpango wa kando kuendeleza kampeni yao ya No Reforms No Election ukiachana na kuwaambia watu walale barabarani

Erythrocyte nimeanza kukuelewa sasa

===================================================

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Bara, John Heche amesema yeye na Mwenyekiti wa chama hicho, Tundu Lissu wanatarajia kupeleka ajenda ya no reform, no election hadi nje ya nchi.

Akizungumza na wanachama wa chama hicho wa Kanda ya Kaskazini, mkoani Arusha leo Heche amesema tayari chama hicho kimewashirikisha wadau mbalimbali kuhusu ajenda hiyo na kwamba wataipeleka mbali zaidi.

“Ajenda yetu no reform, no election inazungumzika hata kama wanaizungumzia negatively (kwa mtazamo hasi) lakini wanazungumza ajenda ya CHADEMA, tumetoka na ajenda hiyo ndiyo kila siku Wasira anaimba na leo ndio Makala alikuwa anaizungumza” amesema Heche.

“Sisi ni watu tunatumia brain (akili) tume engage (kushirikisha) tumeandika mapungufu 16 ya uchaguzi ambayo hayamuwezeshi mpinzani yoyote kushinda uchaguzi, nani miongoni mwenu anaweza kusema kwamba anaweza kushinda uchaguzi kwa utaratibu huu tulionao?” amehoji Heche

Source: Nipashe
Tutakomaa lini ikiwa Viongozi wanahamasisha zaidi kutatua matatizo ya ndani kupitia wa watu wa nje.
Hao wa nje ni WEMA sana kwetu au ndio mianya ya baadae kuwa watumwa wa sera zao kama ilivyo Sasa.
Wananchi wanafurahishwa kwa maneno matamu wanayotaka kuyasikia kisa ya changamoto wanazipitia badala ya kuangalia vyema njia ya utatuzi wa tatizo, we can't solve the problem through same mind created.
We obsessed to rule but not ending the problems.
Tuepuke maneno ya Viongozi wasio leta hoja zenye tija. Hatupendwi hata na nchi zinazotuzunguka sembuse za nje.
 
No reform no election . Niliwahi kusema hapa kuwa hii ni Ngoma ya chadema ambayo ccm wanaicheza pasipokujua beat na wimbo unamaanisha Nini.
Ni "ngoma" inayo wapagaisha CCM, ngoma inayo watia kiwewe kwelikweli.

Tatizokuu kwa sasalinalo wakabili CHADEMA ni moja. Mbali ya Mwenyekiti, na makamu wake, pengine na baadhi ya viongozi wachache ndani ya chama hicho wanajuwa kweli maana ya maneno hayo na uzito wake ulipo.
Ndiyo maana sasa CCM wanatumia baadhi ya hao wajinga waliopo huko CHADEMA kuvuruga kazi hiyo huko huko ndani ya chama, hata kabla ya kufikisha ajenda hiyo inakohitajika zaidi, kwa wananchi.

CHADEMA wasipokuwa waangalifu watavurugwa sana na kupotezewa muda wasiweze kuifikisha ajenda hiyo kwa ufanisi inakotakiwa kufikishwa, kwa wananchi.

Na wakati huo huo, CCM sasa hivi wanafanya juhudi zote kuwalaghai na kuwatia hofu wananchi huko huko mitaani na vijijini!
 
Uko nje ya nchi ndiko kuna wapiga kura?.Hawa jamaa nikama wanawaza vyeo vyakisiasa tu ili nawao wanufaike.Sioni kama wana agenda ya maana yakuwasaidia wananchi kwa lolote Zaidi ya fikra za nasisi ni zamu yetu ya kula.
 
Nimesoma maelezo yaliyowekwa kwenye mada "kirasharasha".
Pamoja na kukubali lengo la hatua hiyo (kueneza kampeni hadi huku nje); nawasihi sana viongozi wetu hawa wasisahau kuwa mwamuzi pekee wa hatma ya nchi yetu ni mwananchi, mTanzania mwenyewe; ambaye hakuna nguvu yoyote inayoweza kutumiwa na hawa walaghai wa CCM kuzuia lengo la haya mabadiliko.

Nwasihi sana viongozi hawa nguvu zote wazielekeze katika kuwa elimisha wananchi hawa kuzitambua haki zao na kukataa kuvurugwa kwa njia zozote za haki zao za kuwachagua viongozi wanao wataka kwa haki na uhuru kamili.

Mkuu, Erythro, ninayo mengi na wewe tokea hapa kwenda mbele. Ninakuelewa vizuri.
Kuanzia February 27 kila mwananchi atafikiwa, ondoa shaka, tumeanza na Taasisi za Dini, ambako tumewaambia hakuna kuombea wanaoiba uchaguzi, kimsingi wamekubali ila wanaangalia namna ya kufanya, Bado wawili tu ambao nao tumeshatuma timu kuwaelimisha, wawili wenyewe ni BAKWATA na Mwamposa
 
Uko nje ya nchi ndiko kuna wapiga kura?.Hawa jamaa nikama wanawaza vyeo vyakisiasa tu ili nawao wanufaike.Sioni kama wana agenda ya maana yakuwasaidia wananchi kwa lolote Zaidi ya fikra za nasisi ni zamu yetu ya kula.
Ni muhimu sana wale wanaowapa hela kujua uchafu wenu
 
USAID wanajiondoa ,agencies za EU zinatafakari tena kuhusu misaada....

Misaada ya masharti inakwenda kubadilika.....

Tundu Lissu na CHADEMA wako nyuma ya W.A.K.A.T.I.....
Jibu hoja zao kwa hoja!
Acha mazoea ..unataka waishie ndani ya nchi ili iwaje?
Nchi yetu inategemea misaada Toka nje na ndiko wanakoenda kuongelea hizo hoja.
Mzee Wasira kashasema uchaguzi hauzuiliki,sasa hofu yako msingi wake uko wapi?
Watu kama wewe ndio mnatutia mashaka .
 
CCM haijawahi kuwa na mgombea DHAIFU....haijawahi....ni mindset yako tu....

Mgombea dhaifu kwa kuwa ni MWANAMKE ,si ndio ee wewe MISOGYNYIST ?!!
NI DHAIFU! unakataa nini? Utamlinganisha huyo mama na Dr Asharose migiro? Prof Tibaijuka na wamama wengine wenye upeo na ilimu ya kutosha?
 
Ha ha ha ha wahuni ni wale wanaotaka ukibaraka kutoka kwa WATU wa nje......hakuna awezaye kuzuia UCHAGUZI wa kisheria....nakuapia HAYUPO HAYUPO HAYUPO.....

Hamna lolote la kufanya.....ha ha ha ha

Ukiwa punguani unaweza kupiga kelele sana kuwa kitu fulani hakitakuwepo bila ya kuwa na sababu ya kuwepo au kutokuwepo.

Kwa kila mwenye akili, mpaka sasa anajua akilini na moyoni mwake kuwa uchaguzi unaweza kuwepo au usiwepo, kwa kutegemea upokeaji wa hoja za wanaosema usiwepo na wale wanaosema uwepo, kwa wananchi. LAKINI kuna nguvu nyingine kubwa sana yenye kuchangia maamuzi yoyote yale, JAMII YA KIMATAIFA.

Rejea historia ya huko nyuma:
Katika Afrika Kusini ya ubaguzi wa rangi, waafrika kusini walipambana kwa miaka lakini hawakufanikiwa. AU ilipambana kwa miaka bila mafanikio. Jamii ya kimataifa, na hasa Marekani na UK walipokubali kuiwekea vikwazo vya kiuchumi Setikali ya makaburu, mwaka huo huo ubaguzi wa rangi ukatokomezwa. Hakuna mwenye akili timamu anayeweza kupuuza nguvu ya jamii ya kimataifa.
 
No reform no election . Niliwahi kusema hapa kuwa hii ni Ngoma ya chadema ambayo ccm wanaicheza pasipokujua beat na wimbo unamaanisha Nini.
Hakuna kitu kama hicho huku EU wako busy na Ukraine na ufaransa ndo kabisa yupo amechanganyikiwa na kufurushwa kwenye makoloni yake Trump yupo busy na madini ya Ukraine
 
NI DHAIFU! unakataa nini? Utamlinganisha huyo mama na Dr Asharose migiro? Prof Tibaijuka na wamama wengine wenye upeo na ilimu ya kutosha?
Ni kweli Asha Rose Migiro mama yangu huyo ni msomi wa PhD ya darasani.....lakini hana CHARISMA ya siasa aliyonayo mh.Rais Samia Suluhu Hassan....na ndio maana pamoja na kuingia zile 5 bora kule Dodoma ,CCM haikumfanya mgombea mwenza wa hayati JPM....ninasema kutoka moyoni....

Prof.Tibaijuka ni gogo la elimu lakini hana hata punje ya katiba ya kisiasa aliyonayo mh.Rais Samia Suluhu Hassan....hana ,hana ,hana mkuu wangu.....

USOMI pekee si tija katika uongozi wa kisiasa kwani tungeamua tu tuwe na marais na mawaziri MAPROFESA WA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM na UDOM.....na rais mh.Trump asingechaguliwa wangemchagua yule mama......

#Think broadly !
 
Kila atamkapo neno nje ya nchi huwa ninazidi kumdharau ndugu Tundu Lissu......

Kwanini ninamdharau ?!!

Nje nje nje nje nje....

Boss wa huko nje ni mh.Rais Trump ambaye watu wa "nje" huko ULAYA hana mpango nao.....

"Nje" ya EU mh.Trump si lengo lake zaidi ya masuala mtambuka ya nchi yake....

Anashirikiana na Urusi ambayo ni adui wa EU na Brussels marafiki zake mh.Tundu Lissu....

Mh.Tundu Lissu aache ukale ,haumsaidii.....
Yeye na wenzake akina Robert Amsterdam walilobby wabunge wa CDU pale bungeni Bundestag ili waisukume serikali yao ya Ujerumani iishinikize Tanzania isitishe mradi mkubwa wa ujenzi wa bwawa la kufua umeme pale Rufiji.....

Yakawa matokeo hasi....

Leo hii tunakaribia kuwa na megawati 2215 kuingizwa gridi ya taifa.....

Ndugu Tundu Lissu aache "ushamba" ,chambilecho hayati JPM(resty easy) nje HATUNA WAJOMBA......

#Mwenyezi Mungu amhifadhi na kumlinda rais wetu mh.Samia Suluhu Hassan ,aaamin aaamin aaaaamin!

#Tanzania is a sovereign nation!
Hivi unajua COVID 19 waliingizwa kimagendo Bungeni ili kuzipata Fedha Fulani kutoka nje ya nchi? Wasingekuwepo Covid 19 Bungeni fedha hizo Tanzania tusingepewa.
Nje ya nchi kunamsukumo mkubwa sana wa kutuweka sawa kisiasa.
Kumbuka juzi kati Beberu lilimuuliza Mzee Wasira "Mko tayari kuzungumza na upinzani?" Mzee Wasira alijibu haraka sana "Ndiyo" Swali Hilo lilikuwa ni mtego kutoka kwa Beberu.
 
Hivi unajua COVID 19 waliingizwa kimagendo Bungeni ili kuzipata Fedha Fulani kutoka nje ya nchi? Wasingekuwepo Covid 19 Bungeni fedha hizo Tanzania tusingepewa.
Nje ya nchi kunamsukumo mkubwa sana wa kutuweka sawa kisiasa.
Kumbuka juzi kati Beberu lilimuuliza Mzee Wasira "Mko tayari kuzungumza na upinzani?" Mzee Wasira alijibu haraka sana "Ndiyo" Swali Hilo lilikuwa ni mtego kutoka kwa Beberu.
Siasa haiendi bila mazungumzo....

Tunachokikataa ni watu wajinga kuja na maamuzi na misimamo yao isiyo "partisan" na iliyo kinyume na UANZWISHWAJI WA TAIFA HILI....hapa si Kenya wala huko EU....tuna historia yetu ,mienendo yetu na malengo yetu kama taifa "as a secondary of independent goals".....

Uchaguzi wa nchi si MALI ya wanasiasa wa CCM na upinzani tu....ni matakwa ya KIDOLA na wale wasio na vyama na wasioshiriki siasa ya vyama ya aina yoyote.........

#Tanzania is a sovereign nation !!
#Nje HATUNA wajomba !!
 
Kila atamkapo neno nje ya nchi huwa ninazidi kumdharau ndugu Tundu Lissu......

Kwanini ninamdharau ?!!

Nje nje nje nje nje....

Boss wa huko nje ni mh.Rais Trump ambaye watu wa "nje" huko ULAYA hana mpango nao.....

"Nje" ya EU mh.Trump si lengo lake zaidi ya masuala mtambuka ya nchi yake....

Anashirikiana na Urusi ambayo ni adui wa EU na Brussels marafiki zake mh.Tundu Lissu....

Mh.Tundu Lissu aache ukale ,haumsaidii.....
Yeye na wenzake akina Robert Amsterdam walilobby wabunge wa CDU pale bungeni Bundestag ili waisukume serikali yao ya Ujerumani iishinikize Tanzania isitishe mradi mkubwa wa ujenzi wa bwawa la kufua umeme pale Rufiji.....

Yakawa matokeo hasi....

Leo hii tunakaribia kuwa na megawati 2215 kuingizwa gridi ya taifa.....

Ndugu Tundu Lissu aache "ushamba" ,chambilecho hayati JPM(resty easy) nje HATUNA WAJOMBA......

#Mwenyezi Mungu amhifadhi na kumlinda rais wetu mh.Samia Suluhu Hassan ,aaamin aaamin aaaaamin!

#Tanzania is a sovereign nation!

Unazidi "kuwadharau" kwa sababu hujui historia ya nchi hii.

Leo tunawaongelea CHADEMA, ACT Wazalendo na vyama vingine vya siasa kwa sababu ya Marekani na washirika wengine wa nje kama IMF na World Bank.

Hao ndio walituletea mfumo wa Multiparty, sasa kuna shida gani kurudi huko kwenda kuomba msaada kama wao ndo walituletea huo mfumo?

Au unadhani CCM wao ndo walikubali wenyewe kwa utashi kuwa na mfumo wa vyama vingi?

Ukianza kulalamika kuwa CHADEMA inategemea sana "nje" lazima ujue pia huo mfumo umeletwa na nani?
 
USAID wanajiondoa ,agencies za EU zinatafakari tena kuhusu misaada....

Misaada ya masharti inakwenda kubadilika.....

Tundu Lissu na CHADEMA wako nyuma ya W.A.K.A.T.I.....

Kaa usali sana EU na Marekani wasibadilishe maamuzi yao kuhusu misaada.

Nahisi unahisi watakaokuwa affected mostly ni CCM sio CHADEMA maana serikali ya CCM inategemea sana misaada ya wahisani kuendesha nchi.

Siku wahisani wakitoa mikopo na misaada ndo itakuwa mwisho wa CCM
 
Ha ha ha ha wahuni ni wale wanaotaka ukibaraka kutoka kwa WATU wa nje......hakuna awezaye kuzuia UCHAGUZI wa kisheria....nakuapia HAYUPO HAYUPO HAYUPO.....

Hamna lolote la kufanya.....ha ha ha ha

Hapa ndani hamna anaeweza kuzuia Uchaguzi, sio wanachadema wala nani na ndio maana Lissu anaenda NJE kuomba msaada.

Wahisani wakikataa kutoa hela za kuendeshea Uchaguzi, huo Uchaguzi utafanyikaje?
 
Siasa haiendi bila mazungumzo....

Tunachokikataa ni watu wajinga kuja na maamuzi na misimamo yao isiyo "partisan" na iliyo kinyume na UANZWISHWAJI WA TAIFA HILI....hapa si Kenya wala huko EU....tuna historia yetu ,mienendo yetu na malengo yetu kama taifa "as a secondary of independent goals".....

Uchaguzi wa nchi si MALI ya wanasiasa wa CCM na upinzani tu....ni matakwa ya KIDOLA na wale wasio na vyama na wasioshiriki siasa ya vyama ya aina yoyote.........

#Tanzania is a sovereign nation !!
#Nje HATUNA wajomba !!

Kama mna mienendo yenu, mnachukuaga hela za watu za watu za nini?
 
Marehemu Maalim Seif (rip) aliwahi kuzunguka Duniani kuomba Tanzania na Zanzibar zifutiwe misaada.

Hata hili naona litafanikiwa.

..Zanzibar ilifutiwa misaada lakini Tanganyika ikawa inawabeba.

..CCM wanapaswa kufanya mabadiliko ya kweli ili Watanganyika tusiathirike na kukatiwa misaada na wahisani.
 
Back
Top Bottom