Uchaguzi 2020 Tundu Lissu ndiye asimame na Magufuli 2020? Ameonyesha uwezo zaidi ya Magufuli!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi,

Hili ni bandiko la swali tuu, Ili uchaguzi wa 2020 usiwe ni igizo tuu la uchaguzi, Je tumchagize na kushinikiza Tundu Lissu ndiye asimamishwe na upinzani kumkabili John P. Magufuli? kwa sababu mpaka sasa, Tundu Lissu ndie mwanasiasa pekee wa upinzani ambaye so far, ameonyesha ana uwezo wa kumkabili Magufuli kwa vile uwezo wake ni zaidi ya Magufuli?

Kama kawaida yangu, kwenye kila mijadala yenye kuhusisha maoni ya kisiasa, mimi hupenda kuanza kwa declaration of interest kuwa mimi, japo ni mwana CCM, lakini kwenye kutanguliza mbele Maslahi ya taifa ni kama sina chama, sina kambi na sina upande, kwangu ni maslahi ya taifa mbele.

Baada ya rais Magufuli kuingia madarakani na kuanza na zile amsha amsha za uwajibikaji kwa ziara za kushtukiza , zilizofuatiwa na tumbua tumbua, nikauliza humu kama kweli Tanzania tunataka maendeleo ya kweli, je tuna haja ya kufanya Uchaguzi wa Rais 2020?,
Kwa Kasi hii ya Magufuli, kuna haja Kufanya Uchaguzi wa Rais 2020

Hivyo nikashauri, kufuatia Rais Dr. John Pombe Joseph Magufuli, kuonyesha uwezo wa kuibadili Tanzania, overnight, toka nchi masikini ya kutupa uliyodharaurika, hadi nchi tajiri inayoheshimika, Magufuli aachwe tuu hadi 2025 na hata ikibidi, hiyo 2025 tunaweza tubadili katiba yetu ili rais Magufuli aendelee tuu kama Nkuruzinza, Kagame, Museveni hadi awe kama Mugabe?.

Pia kufuatia trend ya chama kikuu cha upinzani kwa huku bara, Chadema kutoonyesha any seriousness yoyote kuelekea 2020,
Je, CHADEMA inaweza kushinda 2020? Is it serious, credible
nikaconclude kuwa Uchaguzi wa 2020 kwa upande wa urais, litakuwa ni igizo tuu la uchaguzi kwa ushindi wa kishindo cha walkover kwa CCM.
In 2015 Election, Tanzania had A Choice To Choose From. Je Kwa

Lakini kwa mwenendo na matamshi ya Tundu Lissu ya hivi karibuni kumhusu Magufuli, kwa maoni yangu, kwa hapa tulipo, ukimuondoa Zitto ambaye he looks a bit compromised, Tundu Lissu ndie mwanasiasa pekee wa upinzani aliyeonyesha angalau uwezo wa kuweza kumkabili mgombea wa CCM kwa Uchanguzi Mkuu wa 2020, Dr. John Pombe Joseph Magufuli kwenye Uchaguzi huo wa 2020 na Magufuli ukapata pata angalau kaji joto joto cha uchaguzi, vinginevyo wapinzani wakimsimamisha mgombea mwingine yoyote, mgombea wa CCM, Dr John Pombe Joseph Magufuli, hahitaji kufanya kampeni yoyote, ni ushindi wa kishindo straight forward kwa kwenda mbele kama ameokota embe dodo bivu chini ya mti wa mwambe!.

Kwa jinsi nilivyomsikia Tundu Lissu na namna anavyoongea, then huyu Tundu Lissu ni typical yuko kama Magufuli type tena yeye ni zaidi ya Magufuli!.

Hivyo kwa vile Watanzania huwa hawachagui sera wala hawachagui vyama bali huchagua watu, kama, Magufuli ameweza kuchaguliwa kihalali na kumshinda Edward Lowassa, kwenye uchaguzi Mkuu huru na wa haki, then you cannot tell about Watanzania huwa wanachagua nini, hivyo Tundu Lissu ambaye ni zaidi ya Magufuli, akisimama na Magufuli, you can never tell what will happen!, Magufuli naweza akaachwa mbali sana! , ila litabaki swali moja tu dogo, with reference ya kilichotokea Zanzibar, hata huku bara, je ikitokea kweli Chadema ikamsimamisha Tundu Lissu na ikatokea Tundu Lissu akishinda, jee atapewa?.

NB. Sijasema Lissu ni zaidi ya Magufuli kwenye nini, na nawaomba sana msiniulize!.

Mungu Ibariki Tanzania.
Paskali

=======
Hoja za wadau



 
Tundu Lissu naona amekaa kisheria sheria zaidu, nina wasi wasi na uwezo wake wa kusimamia maendeleo ya wananchi, ila all in all sidhani kama ana ushawishi mkubwa kwa wananchi kuliko lowassa , mbowe na zito. Kiufupi hafai na wala hafit hapo
 
Umeongea ukweli Mchungu ambao chama Chetu Pendwa sana CCM hakitaki kuusikia.Ukiniuliza nitasema hivi,kama siyo Lissu basi 2020 tunatakiwa tumeweke RAIS ambaye ni purely mwanasheria,siyo mwalimu wa chekechea wala wa secondary tunahitaji mwansheria.

Ukiangalia nchi nyingi duniani zimeendelea kwa kuwa na Rais mwanasheria,tukiangalia Zimbabwe first Lady wa enzi zile alikuwa Mwanasheria na alimsaidia sana Mugabe kuiweka Zimbabwe kwenye mstari,alipokufa Mama yule na Mzee kuchukua chicken & Chips,uchumi wa Zimbabwe ulidondoka kama mvua ya mawe.

Angalia Clinton na Obama wote ni wanasheria ona walivyojenga Uchumi wa Marekani,na leo muone Trump anachofanya kutwa kucha kugombana na wanaomkosoa,hana tofauti na Baba J.

Kama tungekuwa na Tume huru hakika TL fits for presidency.
 
Duh! Ama kweli akutukanaye hakuchagulii tusi!

Eti Tundu Lissu ni zaidi ya Rais Magufuli! Kwa wanaojua maana tumeelewa una maanisha ni zaidi kwenye 'kuropoka ropoka'.

Kama CHADEMA wanazo pesa za kumrudishia Lowassa alizowapa ili awe mgombea wa kudumu then Mtu yoyote anaweza kuwa mgombea kwa tiketi ya CHADEMA achilia mbali Tundu Lissu.

Kwa trends zinavyokwenda kuna uwezekano mkubwa hata wabunge wa kambi ya upinzani watapungua baada ya uchaguzi 2020 bila kujali nani atakuwa mgombea Urais kwa tiketi ya upinzani.
 

Hakika ni zaidi ya Magufuli, kwanza hana mascandle yule mwenyekiti wenu wa Chama Cha Makinikia si ndiye aliyetuletea kivuko kibovu kwa bilioni nane? Au si ndiye aliyekwapua nyumba za serikali akagawa kwa wadada na nduguze?
 
Nyongeza ya mwaka ya mshahara kwa watumishi wa umma iko kisheria lakini huyu mtukufu wetu ambaye pia ni Dikteta ametoa agizo watumishi wasipewe hiyo nyongeza mpaka itakapofikia 2020 ili waweze kumchagua yeye. Halafu ndo CCM wanasema anazingatia utawala wa sheria.
 
Hakika ni zaidi ya JPM,kwanza hana mascandle yule mwenyekiti wenu wa Chama Cha Makinikia si ndiye aliyetuletea kivuko kibovu kwa bilioni nane?Au si ndiye aliyekwapua nyumba za serikali akagawa kwa wadada na nduguze?
Yes, Tundu Lissu ni zaidi ya Rais Magufuli! Lazima awe mgombea Urais kwa tiketi ya CHADEMA! Happy?
 
Hakika ni zaidi ya JPM,kwanza hana mascandle yule mwenyekiti wenu wa Chama Cha Makinikia si ndiye aliyetuletea kivuko kibovu kwa bilioni nane?Au si ndiye aliyekwapua nyumba za serikali akagawa kwa wadada na nduguze?
Hivi kwanini mnajitoa akili? Hizo nyumba za selikali aliuza chini ya boss wake Sumaye, na mnae huko chadema, mfukuzeni huko ili tujue kweli hicho chama chenu hakilei mafisadi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…