Pre GE2025 Tundu Lissu: Nimewasilisha kusudio la kugombea nafasi ya Mwenyekiti CHADEMA

Pre GE2025 Tundu Lissu: Nimewasilisha kusudio la kugombea nafasi ya Mwenyekiti CHADEMA

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Unaumwa wewe usidhani kila mtu ana akili za kimasikini kama zako. Eti utawala unaamua watu waamke saa ngapi kwa akili hizi Tanzania ina safari ndefu sana.

Nakuuliza swali, huo utawala ndio unapiga kura? Chadema haiko compromised hivo huo utawala unaoupamba unavyokudanganya.

Pata muda wa kupitia malalamiko ya watu ambao wameshiriki uchaguzi

Pia pata muda wa kupitia hotuba ya mkuu wa wilaya ambae alitumbuliwa Kwa kusema mambo ambayo watawala walifanya kwenye uchaguzi

So yes Kura yako itakuwa na maana kama utawala watataka kura yako iwe na maana otherwise hata kama utashiriki kupiga kura itakuwa no tofaut na mtu ambae aliamua kulala nyumbani
 
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) bara Tundu Lissu ametangaza nia ya kugombea uenyekiti wa CHADEMA Taifa, nafasi ambayo kwa sasa inashikiliwa na Freeman Mbowe.

Lissu ametoa rasmi tamko hilo, wakati akizungumza na wanahabari siku ya Alhamisi Desemba 12, 2024 Mlimani City mkoani Dar es Salaam.

"Ninaamini na ninapenda kuamini ninyi wanachama wenzangu nina sifa za kutosha za kugombea nafasi ya juu kabisa ya chama chetu (Chadema) yaani nafasi ya mwenyekiti wa chama Taifa."

“Kwa sasa Mimi ni Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara lakini pia nimewahi kuwa Rais wa TLS, Wakili, Mwanaharakati na Mtetezi wa Wananchi pamoja na nafasi nyingine, kwasababu zote hizi naamini Wanachama wenzangu mnaamini kuwa nina sifa ya kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Chama Taifa”

“Napenda kuwajulisha rasmi kwamba nimeshawasilisha taarifa rasmi kwa Katibu wa Chama chetu la kuondoa kusudio langu la kugombea nafasi ya Makamumi Mwenyekiti na badala yake mimewasilisha rasmi kusudia langu la kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Chama chetu”
Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti wa Chadema-Bara​
View attachment 3175126
Misukule ya mzee mbowe kwisha habari
 
Lissu ni mropokaji tu anatakiwa kuongozwa na si kuongoza.sioni nafasi yake ya ushindi pale CHADEMA.
Lakini anayo haki ya kidemokrasia kugombea nafasi yoyote anayodhani anastahili.Lakini akumbuke kuna wapiga kura watakao amua asije na matokeo yake kichwani hapo atakuwa amefeli saana.
Bila DJ Kamanda Mbowe saa hizi Lissu angekuwa shimo la Tewa !
Bila Lissu chadema isingekuwepo
 
Pata muda wa kupitia malalamiko ya watu ambao wameshiriki uchaguzi

Pia pata muda wa kupitia hotuba ya mkuu wa wilaya ambae alitumbuliwa Kwa kusema mambo ambayo watawala walifanya kwenye uchaguzi

So yes Kura yako itakuwa na maana kama utawala watataka kura yako iwe na maana otherwise hata kama utashiriki kupiga kura itakuwa no tofaut na mtu ambae aliamua kulala nyumbani
Mkuu mimi naongelea uchaguzi wa ndani ya CHADEMA siongelei uchaguzi wa viongozi wa serikali na mitaa. Unachanganya mambo.

Upo sawa kama unaongelea uchaguzi mkuu na serikali za mitaa.
 
Cha ajabu ni kuwa Mbowe hajatangaza kuwa ana nia ya kugombea nafasi ya Uenyekiti. Lakini kitendo cha Lissu kufanyia mkutano Mlimani kinanikumbusha Slaa na Serena. Mtihani uliopo mbele yake ni kuhakikisha kuwa anatimiza ndoto yake bila kukivuruga chama anachosema bado anakipenda. Wasiwasi wangu ni kuwa inaelekea kuwa ameanza kuamini kuwa yeye ndie Mkombozi wa CDM na hivyo itatumika kumtumia kukivuruga chama chake hata kama hilo sio kusudio lake. Inabidi atumie busara sana. Huu mwanzo wake haunipi matumaini makubwa.

Amandla...
 
Cha ajabu ni kuwa Mbowe hajatangaza kuwa ana nia ya kugombea nafasi ya Uenyekiti. Lakini kitendo cha Lissu kufanyia mkutano Mlimani kinanikumbusha Slaa na Serena. Mtihani uliopo mbele yake ni kuhakikisha kuwa anatimiza ndoto yake bila kukivuruga chama anachosema bado anakipenda. Wasiwasi wangu ni kuwa inaelekea kuwa ameanza kuamini kuwa yeye ndie Mkombozi wa CDM na hivyo itatumika kumtumia kukivuruga chama chake hata kama hilo sio kusudio lake. Inabidi atumie busara sana. Huu mwanzo wake haunipi matumaini makubwa.

Amandla...
Ok, kikubwa ana baraka za VIONGOZI
 
Mkuu mimi naongelea uchaguzi wa ndani ya CHADEMA siongelei uchaguzi wa viongozi wa serikali na mitaa. Unachanganya mambo.

Upo sawa kama unaongelea uchaguzi mkuu na serikali za mitaa.


Hata za ndani ya chama just wait utaona figisu zake,

Utaona watu wapya wanavyoongea na vyombo vya habari kila siku

Mbowe Hana msimamo, na ni mtu ambae anashaurika

Ila lissu ni mgumu kushaurika siku akisema maandamano basi yeye atakuwa wa kwanza kuwa front
 
Navyojua mimi ukitaka position nyeti ndani ya taasisi ni LAZIMA kwanza ukubalike na viongozi waliopo, muweke maridhiano namna utakavyoongoza taasisi hiyo, mabadiliko unayotaka kuyaingiza ni LAZIMA yajadiliwe ha hao hao viongozi waliopo na LAZIMA mkubaliane kwa maandishi ya kisheria namna utakavyoingizwa bila kuijeruhi taasisi husika.

Hakuna taasisi nyeti itakupa madaraka hata kama una uwezo- yaani unatoka unakwenda kuita waandishi - then unagombea hiyo oosition hilo sahau milele. Mbowe alivyopewa uwenyekiti wa CDM wale wazee walimpitisha kwenye tanuru na kuna mambo aliambiwa ambayo hajawahi hata kuyasema kwetu na kama angebisha ama kuonyeshankutokuwa tayari wasingempa mamlaka ya kuongoza taasisi.

Mandela kabla ya kupewa nchi na Makaburu alipitia hayo niliyoyasema, kama angebisha nankuemdela na misimamonyake ya kulipiza visasi asinheweza kupata huo Urais.
 
Back
Top Bottom