Tundu Lissu: Ninampinga Magufuli hadharani. Sio mnafiki na sijahongwa

Tundu Lissu: Ninampinga Magufuli hadharani. Sio mnafiki na sijahongwa

Kwenye siasa na hasa siasa za kipumbavu za ccm ni kutengeneza matatizo na kuja kujifanya wanayatatua baadae.....yaani hiki ni chama cha sanaa na wizi mtupu. Matukio mengine yapo hawayatatui mpaka watz wateseke ndipo wao wanakuja na kujifanya wanatatua.....
Magufuli was is and will never be a hero coz he is a member of corrupt system of ccm which consistently destroys watz.....
I will the very last person to agree on any move initiated by ccm

Mkuu Big up
 
Rais piga kazi achana na wanao bwabwaja kwenye mitandao.
 
Mbona povu jingi linamtoka, asubiri wanasheria wenzake waje na hii tathmini. Kuwatukana wenzako kwenye hili ni kutafuta kiki tu. Ni sawa tumejikwaa hata kama wakati huo mheshimiwa Rais alikuwa upande huo asingeweza kukurupuka tu lazima Lisu ajue hilo, sasa hivi yeye ndio dereva hivyo keshaanza tumsupport.
 
Ukiangalia hata yeye Tundu Lisu anataka sifa na hulka kujiona yeye anajua kila kitu itamgharmu muda si mrefu.
 
Sisi wana singida kwa ujumla tunampongeza kijana wetu huyu ambaye anaipigania nchi yetu kila uchao,ewe mtanzania mwenzetu mzalendo popote ulipo jitahidi kumuombea huyu kijana TUNDU LISSU kwa mwenyezi mungu amuongezee ulinzi ili aendelee kutupigania na kutufumbua macho.
 
Ngoja nisogeze kigoda na popukoni nione hili li series linaendaje.
 
Najiuliza sana swali dogo tu kila nikiona post ya Lisu kiufupi nasubiri apost kuwa amepima yeye au kashuhudia upimaji wa huo mchanga na kajiridhisha kuwa hatuibiwi,nitamuelewa sana,tofauti na hapo aendelee kusoma takwimu na historia kwenye makaratasi hadi pale atakapo ikomboa nchi kwa takwimu na sheria
Kwani umeisoma vizuri andiko lililotolewa humu au unakurupuka tu,,maana kina sizonje mpo wengi. Labda nikueleweshe tu kauli na maana ya anachokiongea Tundu Lissu,, yy hajasema wala kukataa kuibiwa mchanga wenye madini,maana kwa miaka mingi wamekuwa wakiongea kuhusu uwizi huo na mkuu wa kaya na maficm wenzake wamekuwa wakitetea kwa kuipitisha tena kwa vifijo na nderemo na huyuhuyu mkuu akiwa mmoja wao hatujawahi kumsikia hata mara moja akihoji zaidi ya kusuport kila miswada ya madini ambayo ni mibovu ikiletwa bungeni wakati huo,na ni hawahawa wakina Tundu walikuwa wakiwaasa kuwa kuna uwizi mkubwa unafanyika,,. Sasa alichokiongea Tundu Lissu ni kuwa hapo tunachoibiwa sisi ni mikataba mibovu tuliyoingia na ndio maana akasema siku ya mwisho tutawarudishia aidha mchanga wao huo tunaojibatiza kuwa ni wetu na tunaibiwa au tukitumia mabavu kuuchukua na kuvunja nao mikataba tuliyoingia chaka wenyewe na kuipitisha kwa kuibariki kwa zimwi la kiitikadi na kuacha uzalendo eti sababu upo chini ya himaya yetu basi itabidi tuwalipe hela nyingi ambayo tutajuta kwa kutafuta sifa ya kisiasa ya mda mfupi,. Yaani maana yake badala ya kuangalia tulipojikwaa tunaangalia tulipoangukia,,au hamkumbuki ngano mbovu ya bakressa,,?? Kilichotokea kwa kumpa utajiri wa bure kama fidia iliyopelekea hadi leo ni mmoja kati ya matajiri wakubwa Afrika na yote ni nn,,!!? Sifa za kijinga
 
Sisi wana singida kwa ujumla tunampongeza kijana wetu huyu ambaye anaipigania nchi yetu kila uchao,ewe mtanzania mwenzetu mzalendo popote ulipo jitahidi kumuombea huyu kijana TUNDU LISSU kwa mwenyezi mungu amuongezee ulinzi ili aendelee kutupigania na kutufumbua macho.


Labda Mungu wa chadema, Mange Kimambi!
 
Sisi wana singida kwa ujumla tunampongeza kijana wetu huyu ambaye anaipigania nchi yetu kila uchao,ewe mtanzania mwenzetu mzalendo popote ulipo jitahidi kumuombea huyu kijana TUNDU LISSU kwa mwenyezi mungu amuongezee ulinzi ili aendelee kutupigania na kutufumbua macho.
AMINA na kila mtanzania atamuombea ili huyo kiongozi wetu azidi kutupigania
 
Kama ni kweli Lisu mkweli, angepingana na chama chake ujio wa Lowasa CHADEMA kwa sababu ni yeye aliyekuja na list of shame. Sasa swali kwake ni kitu gani kilichomfanya amkubali Lowasa wakati kwa miaka nane anamwimba kuwa fisadi. Hii inadhihirisha kuwa watanzania ni vigeugeu, Lisu anajua kwa nini alimkubali Lowasa kwa sababu pesa yake tu na si vinginevyo na nina imani hata leo Rais akimteua kwa mwanasheria Mkuu wa serikali hatakataa kabisa na atawageuka wenzake.
 
Watanzania tunamuombea tena bila ya kulazimishwa kwani yeye ndiyo mzalendo wa kweli kuliko maccm wanao lazimisha kuaminiwa


Watanzania wepi hao? Mbona anapita kwa tabu Jimboni kwake huyo kilaza wako?
 
KUNA HAJA MHESHIMIWA RAIS, KUWEKA SIASA PEMBENI NA KUMTUMIA MH. TUNDU ANTIPAS LINDU LISU KWENYE MAMBO HAYA, MANAKE SIJAONA WAZIRI KABUDI AKISEMA JAMBO KATIKA SWALA HILI. INAONEKANA MH. LISU ANAJUA ANACHOKISEMA NA HATA UKISOMA POST YAKE UNASHAWISHIKA KUAMINI KUWA KUNA JAMBO LITATOKEA AMBALO NI BAYA KUZIDI HILI, NI WAZI KAZI MH. RAIS WETU NZURI SANA SANA LAKINI NAMSHAURI AJARIBU KUANGALIA PIA MAWAZO YA WADAU KAMA MH. LISU N.K


~Ramadan kareem!!

GREAT POINT!

Tuliofuatilia harakati za Lissu akipambana na manyanyaso na mikataba mibovu ya uwekezaji katika sekta ya madini tangu enzi za Mkapa, tunaheshimu sana mchango wake. Kikwete aliposema "heri Slaa kuwa rais kuliko Lissu kuwa mbunge", alikuwa akikumbuka jinsi Lissu alivyowapa taabu katika harakati zao hasa za kusuka dili kwenye mikataba ya madini.

Kama kweli Magufuli ana nia ya dhati ya kuinyosha sekta hiyo, basi amwalike Lissu kwa mashauriano makini ya ana kwa ana ya kuachana na malumbano ya kishabiki yasiyo na tija kabisa kwa taifa. Wapeane mikakati thabiti ya kung'oa na kufagilia mbali mizizi ya ufisadi iliyosimikwa ndani ya sekta ya madini na chama chake kwa miaka mingi. He needs to swallow his false pride and woo resourceful persons like Lissu to his side.

Magufuli ajue kuwa si kila anayemchekea huko CCM ni rafiki yake. Na si kila aliye upinzani anayeikosoa serikali yake ni adui yake. Tanzania ina watu wa ajabu sana. Wamejaa CCM wanampigia mahesabu tu kila hatua anayochukua. Asijekuta akiishia kushangaa sana huko siku za mbeleni. Mwalimu Nyerere mwenyewe siku zake za mwisho aliishia kuwa mpweke na aliyekata tamaa kuhusu mwelekeo wa CCM na nchi kwa ujumla (sikilliza hotuba zake za mwisho).
 
18622446_1126398777465538_2060351389369899505_n.jpg



Na mimi ni Mtanzania pia.

Tofauti kati yangu mimi na wewe na Magufuli ni hii: Mimi nimepigania nchi yangu katika masuala haya tangu mwaka '99.

Wakati huo tulikuwa na mgodi mmoja tu wa dhahabu, Resolute Golden Pride Nzega. Bulyanhulu ilikuwa haijajengwa. Geita ndio kwanza walikuwa wanafukuza wanakijiji wa Mtakuja.

Nadhani nilikuwa wa kwanza katika nchi hii kupiga yowe kwamba tutaibiwa sana kwenye sekta ya madini.

Wewe sijui ulikuwa wapi wakati huo. Najua Magufuli alikuwa wapi: upande wa MaCCM na wawekezaji hawa.

Nimepigana na wawekezaji hawa mahakamani, kwenye medani ya kisiasa ndani na nje ya nchi hii kwa zaidi ya miaka 15. Nimetetea wananchi completely free of charge Bulyanhulu, Tarime, Nzega, Geita, n.k.

Sijui wewe ulikuwa wapi lakini najua Magufuli alikuwa upande wa nani: wa MaCCM na wanyonyaji hawa.

Soma Rai ya tarehe 17 Julai, 2001, uone tulimwambia nini Mkapa siku anaenda kuzindua Mgodi wa Bulyanhulu.

Sijui ulikuwa wapi lakini najua Magufuli alikuwa wapi: alikuwa anatetea tumbo lake na matumbo ya wanyonyaji hawa.

Nilikamatwa na kushtakiwa kwa uchochezi kwa sababu ya Bulyanhulu. Hiyo ilikuwa December 2002. Nilikaa na kesi hiyo mahakamani Kisutu kwa miaka sita.

Sijui ulikuwa wapi ila najua Magufuli alikuwa wapi: upande wa watesi wa wananchi na wanyonyaji wa rasilmali zetu.

Leo Magufuli anajifanya mzalendo na anahoji uzalendo we yeyote anayepingana nae.

Ni muongo. Anatafuta umaarufu wa kisiasa kwa wasiojua na wasiokumbuka. Ataupata. Kwa siku chache tu. Mark my words: ataumbuka na mtaumbuka.

Mimi ninampinga hadharani. Sio mnafiki, na sijahongwa. Ninampinga kwa sababu atatusababishia matatizo makubwa zaidi kuliko tuliyonayo sasa.

Huo mchanga atauachia upelekwe ambako umepelekwa kwa miaka 16 iliyopita. Kama sheria ndiyo hiyo na mikataba ndiyo hiyo hana pakwenda.

Tatizo ninaloliona ni kwamba by the time anawarudishia mchanga wao, Tanzania itakuwa imekuwa a basket case kama Zimbabwe.

Na tutakuwa tumelipishwa mapesa mengi kama fidia na arbitral tribunals za kimataifa kwa kuvunja mikataba na wawekezaji hawa.

Kama kuna anayefikiri uzalendo ni kufumbia macho masuala haya basi huyo na amuunge mkono Magufuli kwenye upofu wake wa kujitakia.

Ripoti ya Prof. Mruma haitamaliza hata nusu saa under serious scrutiny. Zaidi ya majina ya maprofesa walioiandaa, ripoti hii haina credibility yoyote. Ni kazi ya kisiasa iliyopakwa rangi ya usomi.

Kama umefuatilia taarifa za kitaalamu za Bulyanhulu hata kabla ya Barrick Gold kuingia mwaka '99 utajua ninasema nini.

Sutton Resources, Outukumpu Oy na hata STAMICO walishafanya utafiti mkubwa juu ya utajiri wa Bulyanhulu. Taarifa zipo na zimekuwepo kwa hata mbumbumbu wa jiolojia ya madini kama mimi.

Hiki alichoambiwa Magufuli ni rubbish, hata kama ni ya kiprofesa. Rubbish. Hatuibiwi kwenye mchanga, that's the rubbish fed on the unlettered.

Tunaibiwa kwenye sheria. Kama hamuoni hilo then God have mercy on us.
Mi sisomagi makala za huyu taahira. Kwanza ndeeefu.
 
Sasa kwa taarifa yako wewe mpuuzi kuna kipengele kwenye mkataba kinachosema kuwa kinachochimbwa chote ni mali ya mwekezaji na sisi tutaambulia mrabaha ambao kila mwisho wa mwaka mnapeleka wakaguzi. Pia kumbuka kuwa kule ndani ya migodi mna maagent kibao mlioweka huko.

Ule mkataba aliosaini mkuu wako wa miaka 100 ndiyo chanzo cha tatizo.
Kila kinachochimbwa ni mali ya mwekezaji sawa, ila na sisi inabidi tukijue. Ila hawa wanatudanganya, hapo ndo wao wanapovunja mkataba kwasababu huo mkataba hauruhusu uongo.
 
Ni hicho chama kimekufanya mjinga, na ni rahisi kumficha mjinga kwa maandishi. Hata viongozi wako, wako hivyo wanashindwa kusoma kilichoandikwa wanaishia kutia sahihi kwenye mikataba ya kishetani leo eti tunaibiwa.
Swadakta kama ile mikataba 17 ya wachina iliyosainiwa kwa nusu saa
 
Back
Top Bottom