Pre GE2025 Tundu Lissu: Tubadilishe tarehe ya Uchaguzi Mkuu kwa Miaka miwili ili tuwe na tume Huru

Pre GE2025 Tundu Lissu: Tubadilishe tarehe ya Uchaguzi Mkuu kwa Miaka miwili ili tuwe na tume Huru

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kwa mawazo yangu wazo la kusogeza mbele uchaguzi ni baya kwa sababu:
1. Linatoa loop hole ya kubadilisha term ya urais.
2. Hamna guarantee ya mabadiliko yeyote maana inategemea mno nia njema ya waliopo sasa madarakani.
3. Rais aliyepo hatakubali kuwa Rais wa kwanza wa CCM aliyedumu kwa muhula mmoja. Hilo CDM wasahau.

Badala yake CDM iweke nguvu katika kuhakikisha vyama vya upinzani makini vinapata wabunge na madiwani wengi. Muda uliobaki utumike katika kupata wagombea wanaokubalika na kujenga ushirikiano na vyama vingine. Wakiweza kupata wabunge makini watakuwa katika nafasi ya kusukuma jambo hili nje na nfani ya Bunge.

CDM itumie vilevile kupata resources za kujiendesha na kuwahamasisha wananchi.

Aidha, mwaka 2030 patakuwa na mabadiliko ya uongozi CCM na hivyo kukifanya kuwa vulnerable kuliko sasa kwa sababu patakuwa na mnyukano wa wanaoyaka kugombea urais.

Aidha, Rais wa sasa atataka kuacha legacy ya kuacha nchi yenye Katiba bora inayowapa watanzania uhuru wa dhati wa kuchagua viongozi wanaowataka ambao watawajibika kwao. Tukumbuke kuwa Samia alihusika sana katika juhudi zilizopita za kupata Katiba Mpya. Naamini angependa kumalizia kazi aliyoanza.

Mwisho, miaka mitano utaipa CDM muda wa kutosha wa kutibu majeraha ya uchaguzi wa Mwenyekiti wake na hivyo kuunganisha wanachama na wafuasi wake. Watakuwa wanajidanganya kama wataamini hayapo.

Amandla...

Hakuna mbunge wa CCM au diwani anayependa kushindwa kwenye uchaguzi .
Kwa hiyo huo ujinga wa kusema uweke nguvu kwenye udiwani na ubunge ni upuuzi mtupu.

Samia siotanganyika na katika Hali ya kawaida hana uwezo wa kuiongoza Tangayika na anawaogopa mafisadi kwa sababu anadhani kuwa Magufuli walimtishia kumbe ni mapenzi ya Mungu tu na sio nani wala nani ?

Hakuna mtu asiyeka ashinde hata zezeta ndani ya CCM lakini ashinde kwa haki.

Kama hawapo tayari kushinda kwa haki basi waendelee na madaraka mpaka watakapokuwa tayari kushindana na sio kuleta uchaguzi wa hadaa kuua ili kuua watu.

Hivi kama wanaua watu uchaguzi wa serikali za mitaa usio na mshahara watamuacha mtu kwenye uchaguzi wa kumpata Rais anayelipwa mamilioni ya pesa na Fungu la matumizi kubwa kuliko Wizara zote na halihijiwi wala kuulizwa matumizi yake . Wataacha mtu kwenye Ubunge mshahara mil. 18 kwa mwezi na posho ya jimbo juu na hakuna anayejoji matumizi yake maana wote ni wale wale .

Jiulize huyu ndiye Samia yule wa wakati anaingia Ikulu . Ni kitu gani kimembadili na kuwa na roho mbaya kuliko marais wote waliowahi kutawala Tanzania na hata Zanzibar .
Rais asiyejali raslimali za umma ,hajali uhai wa watu ,hasjali demokrasia ndani ya Chama chake ,hajali demokrasia nje ya chama chake . HAJALI MATUMIZI YA FEDHA ZA UMMA . Anachowaza ni kushinda uchaguzi tu.

Lakini pia ushindi wake hauna umuhimu wowote kwa nchi maana hana malengo yake binafsi na nchi hizi hasa Tanaganyika . Anajua wazi kuwa akifanya chochote na vyovyote siku akistaafu akirudi kwenye nchi ya Zanzibar hakuna mtu atakayeweza kumshitaki hata kama katiba itabadilishwa maana ile ni nchi nyingine na atakua kama yupo uhamishoni .
Labda tu kama patakuwa na mali zake zitaifushwe lakini kumfuata na kumkamata akiwa nchini nchi za nje sio Rahisi .

Kwa nini watanzania tuzuiwe kumchagua Rais na viongozi tunawataka .

Huo utamaduni wa CCM utauliza watu mpaka lini na kwa manufaa ya nani ?
Yaani Samia akikosa urais kwa haki atapata hasara gani wakati Nchi itabaki kuwa na amani .?
Au yeye ni nani katika hii nchi kwamba bila yeye kuendelea na urais ambao kimsingi hakuwahi kugombea wala kuomba nafasi ya urais lakini leo eti ni lazima aendelee .Aendelee kutoka wapi wakati awamu yake ni kuanzia 2025 ndipo atajipima kwa kuomba kura .? Nani anayemngangania mtu ambaye hata ndani ya chama chake hawezi kushinda ?

Kwa nini CCM ilete mtu asiyekubaliaka hata ndani ya chama chake halafu utegemee kuua watu ili awekwe madarakani ?
Hayo ni mapinduzi ?
Kwa nini yafanyike mapinduzi kwa mgongo wa uchaguzi halafu apachikwe raia kuongoza utawala wa kijeshi .

Hivi Kuna tofauti gani kati ya chaguzi za Rwanda ,Uganda na Somalia ,Sudani na Chaguzi za Tanzania?
Kwa nini tunamuona Kagame na Museveni ni Dikteta wakati anashinda kwa kura kama Tanzania inavyoshinda kwa chaguzi za Hadaa. ?

Yaani Samia anaingia madarakani kilaini kabisa halafu yeye anataka wenzake wa aingie kwa jasho na damu ? Kwa nini asiheshimu katiba iliyomweka madarakani ?

Kwa nini asijisikie vibaya kwa chaguzi za dhumlma zilizoleta mauaji kuanzia Zanzibar na Sasa Bara ?
Hivi haoni kuwa ni bahati tu huku bara hakuna watu wenye imani kali kama kule Zanzibar ambapo chuki za kisiasa zilizaa chuki za kidini mpaka makanisa yakawa yanachomwa Moto na mapadri kumwagiwa tindikali . Chuki za kidini kule Zanzibar wakati wa Mashehe wa uamsho yalisababisha nchi kuwa kwenye taharuki kubwa sana chanzo kikiwa ni kukosekana kwa haki wakati wa uchaguzi hali iliyowafanya wazanzibar wengi kukenga chuki dhidi ya watu wa bara na hata kuwaona kuwa wote ni makafiru wasiojua dini kutokana na matendo mabaya wakati wa uchaguzi.
 
Kuna viongozi wenu huko CCM wana watoto wenye uraia wa US, mbona hatuoni ni nongwa, sembuse watoto kuwa ughaibuni kwa masomo!

Mtanzania wa kweli? Familia yake ni raia wa USA, yeye anaishi Ubeleji, utamwitaje Mtanzania wa kweli? Wewe na mimi wenye familia na ndugu zetu hapa tutaitwaje sasa?
 
Hakuna mbunge wa CCM au diwani anayependa kushindwa kwenye uchaguzi .
Kwa hiyo huo ujinga wa kusema uweke nguvu kwenye udiwani na ubunge ni upuuzi mtupu.

Samia siotanganyika na katika Hali ya kawaida hana uwezo wa kuiongoza Tangayika na anawaogopa mafisadi kwa sababu anadhani kuwa Magufuli walimtishia kumbe ni mapenzi ya Mungu tu na sio nani wala nani ?

Hakuna mtu asiyeka ashinde hata zezeta ndani ya CCM lakini ashinde kwa haki.

Kama hawapo tayari kushinda kwa haki basi waendelee na madaraka mpaka watakapokuwa tayari kushindana na sio kuleta uchaguzi wa hadaa kuua ili kuua watu.

Hivi kama wanaua watu uchaguzi wa serikali za mitaa usio na mshahara watamuacha mtu kwenye uchaguzi wa kumpata Rais anayelipwa mamilioni ya pesa na Fungu la matumizi kubwa kuliko Wizara zote na halihijiwi wala kuulizwa matumizi yake . Wataacha mtu kwenye Ubunge mshahara mil. 18 kwa mwezi na posho ya jimbo juu na hakuna anayejoji matumizi yake maana wote ni wale wale .

Jiulize huyu ndiye Samia yule wa wakati anaingia Ikulu . Ni kitu gani kimembadili na kuwa na roho mbaya kuliko marais wote waliowahi kutawala Tanzania na hata Zanzibar .
Rais asiyejali raslimali za umma ,hajali uhai wa watu ,hasjali demokrasia ndani ya Chama chake ,hajali demokrasia nje ya chama chake . HAJALI MATUMIZI YA FEDHA ZA UMMA . Anachowaza ni kushinda uchaguzi tu.

Lakini pia ushindi wake hauna umuhimu wowote kwa nchi maana hana malengo yake binafsi na nchi hizi hasa Tanaganyika . Anajua wazi kuwa akifanya chochote na vyovyote siku akistaafu akirudi kwenye nchi ya Zanzibar hakuna mtu atakayeweza kumshitaki hata kama katiba itabadilishwa maana ile ni nchi nyingine na atakua kama yupo uhamishoni .
Labda tu kama patakuwa na mali zake zitaifushwe lakini kumfuata na kumkamata akiwa nchini nchi za nje sio Rahisi .

Kwa nini watanzania tuzuiwe kumchagua Rais na viongozi tunawataka .

Huo utamaduni wa CCM utauliza watu mpaka lini na kwa manufaa ya nani ?
Yaani Samia akikosa urais kwa haki atapata hasara gani wakati Nchi itabaki kuwa na amani .?
Au yeye ni nani katika hii nchi kwamba bila yeye kuendelea na urais ambao kimsingi hakuwahi kugombea wala kuomba nafasi ya urais lakini leo eti ni lazima aendelee .Aendelee kutoka wapi wakati awamu yake ni kuanzia 2025 ndipo atajipima kwa kuomba kura .? Nani anayemngangania mtu ambaye hata ndani ya chama chake hawezi kushinda ?

Kwa nini CCM ilete mtu asiyekubaliaka hata ndani ya chama chake halafu utegemee kuua watu ili awekwe madarakani ?
Hayo ni mapinduzi ?
Kwa nini yafanyike mapinduzi kwa mgongo wa uchaguzi halafu apachikwe raia kuongoza utawala wa kijeshi .

Hivi Kuna tofauti gani kati ya chaguzi za Rwanda ,Uganda na Somalia ,Sudani na Chaguzi za Tanzania?
Kwa nini tunamuona Kagame na Museveni ni Dikteta wakati anashinda kwa kura kama Tanzania inavyoshinda kwa chaguzi za Hadaa. ?

Yaani Samia anaingia madarakani kilaini kabisa halafu yeye anataka wenzake wa aingie kwa jasho na damu ? Kwa nini asiheshimu katiba iliyomweka madarakani ?

Kwa nini asijisikie vibaya kwa chaguzi za dhumlma zilizoleta mauaji kuanzia Zanzibar na Sasa Bara ?
Hivi haoni kuwa ni bahati tu huku bara hakuna watu wenye imani kali kama kule Zanzibar ambapo chuki za kisiasa zilizaa chuki za kidini mpaka makanisa yakawa yanachomwa Moto na mapadri kumwagiwa tindikali . Chuki za kidini kule Zanzibar wakati wa Mashehe wa uamsho yalisababisha nchi kuwa kwenye taharuki kubwa sana chanzo kikiwa ni kukosekana kwa haki wakati wa uchaguzi hali iliyowafanya wazanzibar wengi kukenga chuki dhidi ya watu wa bara na hata kuwaona kuwa wote ni makafiru wasiojua dini kutokana na matendo mabaya wakati wa uchaguzi.
Haya maandishi yamejaa ujumbe mzito.
Mungu akubariki sana.
Moderators ikiwapendeza wekeni huu mchango "sticky" pale juu.
 
Wewe unawaza urais tu kwa sababu ndiye mungu wako .

Biblia iko sahihi sana unaposema rushwa hupofusha macho .
Yaani ukiangalia kwenye mitandao utaona mpaka baadhi ya viongozi wa dini wamekua vipofu kwa sababu ya rushwa na hofu hata ya kutamka neno haki.

Leo viongozi wa baadhi ya dini wanaogopa kusema wazi kuwa bila haki amani ya nchi itayumba.

Watu hawaoni ubaya wa sheria kwa sababu wapo madarakani na familia zao zinanufaika.

Jifunzeni kitu kwa yule polisi anayefukuzwa kwenye nyumba za serikali wakati ametumikia kwa miaka zaidi ya 30 kwa kutii na uvumilivu hata pale alipodhulumiwa haki yake.
Yule polisi anatamani pangekuwa na watu wa kupigania haki yake mapema lakini hana watu.
Aliodhani ni wenzake hawana habari naye kwa sababu hao hao ndio waliokula pesa zilizopaswa kulipwa kwake .
Hana pa kukimbilia maana sheria za dhulma zinambana .Waliokula na kudhulumu malipo yake wapo salama zaidi kwa sababu wapo kwenye mfumo usiojali malalamiko ya watu . Pale amejitoa tu muhanga lakini maisha yake yako hatarini kwa sababu serikali iliyopo haitaki kuambiwa ukweli wala kulaumiwa zaidi ya kusifiwa kama Mungu.

Yule polisi atufungue macho tudai sheria za haki na katiba inayowajali watu wote ndani ya nchi hii.
Katiba iliyopo inapigania maslahi ya walioshiba na kuvimbiwa. Ndio maana wanaCCM wote wanaufyata wanapoona kakikundi kadogo kanakazimisha mtu asiye na maono yoyote kugombea urais bila kupingwa kwa sera na maono juu ya Taifa hili . Mtu asiye na maono hawazi namna ya kuwasimamia na kuwaelimisha watanzania namna ya kutumia rasilimali zao wenyewe. Anawaza tu kuuza kila kitu halafu watanzania wabaki kama manamba kwenye nchi yao.


Fuatilia uone kama ni sahihi Zoezi la kuhakiki wapiga kura liko sawa !!
Yaani nchi kwa sasa ina vijana zaidi ya mil. 30 halafu zoezi hilo linafanyika kwa siku zisizozidi kumi . Yote ni kwa sababu ya kutumia watumishi wa halmashauri .Yaani kusambaza tu vifaa vya kujiandikishia na kuhakiki ni zaidi ya wiki mbili lakini zoezi la kuandikishwa ni siku kama tisa au nane tu. Sasa hapo kitakachofanyika ni kutengeneza majina feki ili kuwafurahisha waliowatuma.
Ujinga huo waliufanya kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa .
Wanaandika majina feki na kutoa takwimu za uongo .

Hivi tangu 2015 mpaka leo wamekufa watu wangapi na wameongezeka wangapi ?
Watajuaje kuwa wengine ni marehemu wasiporudia na kuhakiki kwa watu wote na iwe ni zoezi la lazima na lifanyike bila kujali mtu atampigia wapi kura ili kwanza watolewe marehemu na kuandikisha wapya .

Kila kitu kinachofanywa na wanasiasa na wateule wa Rais kipo kimaslahi binafsi na sio taifa.

Hivi kama inawatumia wafanyakazi wa umma wanaolipwa na serikali kama walimu na polisi na watumishi wengine kwa nini wasifanye kazi hiyo kama Sehemu ya majukumu yao kwa mwajiri .
Walipwe wale tu wanaotoka nje ya ajira kama Migambo basi.

Tunpoteza pesa nyingi kulipa watumishi ambao ni kazi yao kwa mwajiri .
Basi ni bora tume itangaze nafasi za kuomamia uchaguzi kwa Wasio na ajira ili walipwe na wafanye kazi chini ya tume na sio mkurugenzi.


Zoezi la uhakiki wa Daftari la'mpiga kura liendelee mpaka mwezi wa nne miezi miwili ili watu wote wajiandikishe na marehemu waondolewe kwenye daftari la wapiga kura .

Nchi gani inapata viongozi waliochaguliwa na wafu .

CCM wanapenda madaraka sasa watanzania wengi wanataka rais na bunge lake waongezewe muda mpaka tume na katiba ifanyiwe marekebisho lakini pia daftari la mpiga kura lifanyiwe maboresho na majina yabandikwe mapema kila mtu aone orodha ya watu hai sio marehemu .

Nchi hii sio mali ya Samia wala CCM wala polisi bali ni ya watu wote mil.64. Sasa kama karibu nusu ya watanzania hawakubaliani na mfumo wa kupata wawakilishi basi ni bora ufanyiwe kazi kuepusha Shari . Watu karibu mil 40 hawataki mfumo wa uchaguzi hasa vijana .CCM mnataka mtumie majeshi kuwaua wote kwa sababu ya Kumfurahisha Mzanzibari mmoja na mkwe wake . ? Hapana hayo marekebisho hayana ubaya wowote kwa polisi wala jeshi zaidi ya hofu ya mafisadi wachache wanaoogopa kunyimwa kura.
Ndugu 1000 digits , haya madini leo ni baraka sana kwangu na naamini kwa yeyote mwenye akili timamu na mzalendo wa kweli wa Tanzania, yatakuwa baraka kwake pia.
Mungu aendelee kukubariki.
 
And what if nothing has been changed ?
Najua hiki chama watasusia tu uchaguzi.
 
  • Kicheko
Reactions: Tui
Lisu mjanja fulani huvi anachowinda gapi ni ruzuku iendelee kwa miaka miwili cha
CHADEMA ipate pesa za ruzuku

Kifupi Chadema haijajiandaa kwa uchaguzi na yeyebhajajiandaa.Chama hakina pesa kaligundua hilo baada ya mwenyekiti

Kila akipiga hesabu za pesa za uchaguzi mkuu anaona hazienei na muda wa kupokea ruzuku imebaki miezi minne tu bunge livunjwe na ruzuku isimame
Jamaa kapanda mashua ya vibwengo.Kwani 2025 walikuwa hawajui kuna Uchaguzi?
Anajua hawajitayarisha na hawana pesa za kampeni na uchaguzi wenyewe. Wanajaribu ku buy time.
If you fail to plan you plan to fail.
 
Hivi kiongozi umewahi kusimamia uchaguzi?, kwa sheria hizi za uchaguzi zilizopo ziweze kuwapa wapinzani wabunge wengi?, Kwa taarifa yako Samia hana tofauti na Magufuli kwenye uchaguzi.Nimesimamia serikali za mitaa nimeona wakurugenzi ambao ndoo wasimamizi wa uchaguzi jimboni wanavyokuja na mikakati iliyopangwa kutoka huko juu.Anakwsmbia kwenye kituo chako unatakiwa kufanya lolote ili mgombea wao apate asilimia zaidi ya 90.Kila dk katibu kata ,tarafa,viongozi wa chama wanakutembelea kukukumbusha suala hilo.Mgambo na polisi wote wameishaelekezwa cha kufanya mnashirikiana vyema kuhakikisha mambo yanaenda vyema.Sasa ndoo nakuuliza hao wabunge wengi unaowasema wanapatikanaje kwa staili hiyo?
Sijawahi kwa kweli. Sasa kama unatishiwa na Katibu Kata, Katibu Tarafa, mgambo, msimamizi wa uchaguzi kufanya maovu na unakubali, utaweza kweli kusimama kidete ili uchaguzi usifanyike? Kama unaweza mnashindwa kuwabana hao mgambo, katibu kata na wengine ili haki ifanyike? Najua sio vituo vyote vinaweza kufanya hivyo lakini kuna maeneo ambayo watu wake ni majasiri na wanaweza mtu wao anatangazwa. Msimamo huo uonyeshwe toka kwenye watu kuandikishwa, na urudishaji wa fomu. Kutegemea kuwa Lissu na wenzake ndio watakaoleta mabadiliko peke yao ni kuota ndoto mchana.

Amandla...
 
Tundu Lissu: Tubadilishe tarehe ya Uchaguzi Mkuu kwa Miaka miwili ili tuwe na tume Huru.
View attachment 3237446
Waati akihutubia Maelfu ya Watu huko Mkoani Singida hii leo, amesema Uchaguzi uahirishwe.

Amesema kuliko kufanya Uchaguzi katika mazingira haya ya sasa, Bora tarehe ya Uchaguzi isogezwe mbele kwani tarehe zimepangwa na binadamu.

Amedai kwamba CCM wanadai muda hautoshi wa kupitia katiba na sheria, kanuni za tume huru ya Uchaguzi. Kakubaliana na hali hiyo, ila akapendekeza kwasababu hiyo, bora tarehe isigogezwe mbele lakini sheria ifanyiwe marekebisho.

Tundu Lissu kadai bila mabadiliko ya Sheria ya Uchaguzi hakutakuwa na Uchaguzi
Pia Kohoji kwanini Mawakala wanaosimamia Uchaguzi wanaapa kwa Mkurugenzi kuficha siri, ni siri gani hiyo wanaoyoficha? Ya wizi wa kura?

Kasema hataki tena mambo ya kuapa kwa Mkurugenzi, Mambo ya Polisi kuingia vituo vya kupigia kura kwanini ndo wanaingiza kura feki
View attachment 3237163View attachment 3237164View attachment 3237165
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣😁😁😁😁😁😁😁
 
  • Kicheko
Reactions: Tui
Jamaa kapanda mashua ya vibwengo.Kwani 2025 walikuwa hawajui kuna Uchaguzi?
Anajua hawajitayarisha na hawana pesa za kampeni na uchaguzi wenyewe. Wanajaribu ku buy time.
If you fail to plan you plan to fail.
Uko sahihi mia kwa mia
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Tundu Lissu ana mahesabu Makali!
... yaani anajua ndani ya miaka hiyo miwili Makali ya zuia misaada ya Trump yatakuwa yameishawalegeza CCM, kwahiyo yeye atamshinda Mama Samia kirahisi sana!

👊 🤣✌️
 
Tundu Lissu ana mahesabu Makali!
... yaani anajua ndani ya miaka hiyo miwili Makali ya zuia misaada ya Trump yatakuwa yameishawalegeza CCM, kwahiyo yeye atamshinda Mama Samia kirahisi sana!

👊 🤣✌️
Inaelekea wewe hujui kuwa mirija ya marafiki zake na lisu ya kueneza ushoga duniani pia imekatwa!
 
Inaelekea wewe hujui kuwa mirija ya marafiki zake na lisu ya kueneza ushoga duniani pia imekatwa!
Hii propaganda yako ishapitwa na wakati. Nakushauri utafute nyingine ili uendelee kupata chumvi kutoka kwa wanaokutuma kuchafua viongozi
 
Back
Top Bottom