Pre GE2025 Tundu Lissu: Tume ya Uchaguzi sio Huru, ni Tume ya Rais

Pre GE2025 Tundu Lissu: Tume ya Uchaguzi sio Huru, ni Tume ya Rais

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
12 April 2024

TUNDU LISSU - TUME HURU YA UCHAGUZI SIYO HURU, RAIS ANATEUA NA KUTENGUA WAJUMBE WAKATI PIA NI MGOMBEA KTK UCHAGUZI

View: https://m.youtube.com/watch?v=gbl_dbYBof0

Toka maktaba :

6 August 2022

Tundu Lissu: Idadi ya wabunge wa kuchaguliwa iwiane na idadi ya raia wanaowakilisha​


Makamu mwenyekiti wa CHADEMA Mh. Tundu Antipas Lissu akiangalia mgawanyo wa majimbo yenye watu wengi zaidi anagundua kuwa haiwakilishi na idadi inayostahili ya wabunge. Wilaya ya Temeke mkoa wa Dar es Salaam Mwanzo

Mfano mkoa wa Dar es Salaam ulitakiwa kuwa na wabunge wasiopungua 25. Lakini una wabunge wachache sana wakati ina idadi kubwa ya wapiga kura .

Mkoa wa Lindi yenye wabunge 9 huku idadi ya wapiga kura ni ndogo sana. Mkoa wa Tabora ina idadi ndogo ya wapiga kura lakini ina wabunge wa kuchaguliwa 12 huku mkoa wa Tanga wenye idadi ndogo pia ya watu ina wabunge 12. Mikoa hii iliyotajwa kama mfano wa uwiano usiolingana baina ya idadi ya wapiga kura na wingi wa wabunge pia ni maeneo yaliyo ngome ya CCM.

Na kwa hiyo mgawanyo wa majimbo umeiba uchaguzi kwa kutumia mifumo ya kikatiba na kitaasisi kwa maana Tume ya Uchaguzi ni ya rais na mwenye mamlaka ya kutengeneza mikoa ni rais na mteuzi wa viongozi wa Tume ya Uchaguzi ni rais pia. Orodha ya Jumla ya majimbo ya uchaguzi kwa kufuata na tovuti ya bunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni majimbo 273 : source : Parliament of Tanzania

Huko nchini Kenya Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka ya Majimbo ya Uchaguzi yaani IEBC ndiyo yenye mamlaka ya kutengeneza mipaka ya majimbo ktk Kenya yote inayotumia formula ya idadi ya watu ktk sehemu ndiyo itatoa mwangaza kutakuwepo wabunge wangapi. Sababu ni kuwa nchini Kenya demokrasia inaangazia kuwa wabunge wanawakilisha watu kwa kura na siyo eneo.

Tofauti na Tanzania ambapo ambapo Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC haina nguvu kikatiba kutengeneza majimbo kwa kufuatana na idadi ya wapiga kura.

Mfumo huo wa kuangalia eneo hata kama lina wapiga kura wachache na kuwapatia idadi kubwa ya wabunge huku mikoa kama Dar es Salaam, Mwanza yenye idadi kubwa ya wapiga kura inapewa wabunge wachache sana.

Sababu ni kuwa imeonekana maeneo yenye watu wengi ambao ni wapiga kura huwa wana tabia au mazoea ya kuchagua wapinzani hivyo kwa Tanzania wengi hao wanapewa wabunge wachache ili kudhibiti idadi ya wabunge wa upinzani wanaoweza kuchaguliwa . Parliament of Tanzania

Wawakilishi wa waangalizi wa chaguzi toka ndani na nje wameona mapungufu haya ya kuwa kuna maeneo yana wapiga kura wachache sana lakini ina wabunge wengi, huku kuna maeneo yenye wapiga kura wengi inawakilishwa na wabunge wachache sana na hii Indonesia kukosekana uwiano kati ya idadi ya wabunge na wapiga kura wao.

Source : Forbs Media

Tundu lissu Wakimsikiliza tutaokoa pesa nyingi za Watanzania na kuwa na uongoi wenye Tija
 
KWenye hili naomba Nipingane na wewe..
Tanzania hatuna Tume Huru Endapo Mgombea Wa urais (Mmoja ya wagombea) Ndio Anayechagua Tume na Tume iko chini yake..

Tume Huru wakati Tamisemi "Serikali" Ndo inasimamia Uchaguzi wa Serkali za Mitaa..?

Kuhusu Kuwa Huru kwa Jina Kweli jina lake limeitwa Tume huru...Je iko Huru??

Mimi ninaweza kuita au kuandika Tanzania Ni Nchi tajiri na TunaIzidi Dollar kwa Thamani ila je Kiuhalisia Tunaizidi Dollar??
Huyo si kwamba hajui ila ni Chawa
 
Chadema ni waramba asali mara munamsifu mama na kumtukuza, hamuishi vikao na Samia Ikulu, mulisema Chadema hatapiga magoti kwa serikali ya ccm, hatimae Tundu Lissu alimualika mama belgium bila kuweka wazi hadi leo waliongea nini belgium, lakini mbowe alipotoka jela breki ya kwanza Ikulu, alibadilisha koti na tai akiwa Ikulu ndio akaenda nyumbani kwake sasa mnalalamika nini.

Mmeramba asali sasa wanaoumia ni wananchi, Tundu Lissu haya anaongea sio kutoka moyoni ni kama anamfurahisha mfalme, chadema sasa ni CCM B hawaeleweki, Zamani chadema ikitetea Zanzibar huru sasa wanawatukana wazanzibari waziwazi baada mama kuwa Rais, Chadema haieleweki

Nafkiri Tanzania vyama vya upinzani hasa Chadema kimekosa muelekeo, Watanzania wanahitaji upinzani mpya usio na unafiki ndani yake, Chadema muda wake umekwisha, Mbowe sasa anakazia suruali tu muda wote Ikulu hana tena habari ya Katiba wala Tume huyu ya Uchaguzi. Mbowe siye tena yule wa zamani kwisha habari yake.
Asante kwa andiko hili. Huu ndio ukweli.
Upinzani ni biashara kama biashara zingine. Wapo likizo 11months.

Kama wananchi ‘maamuzi magumu ndio uponyaji’
Wahalifu wanateuliwa wapo kimya

Wengine tukiandika haya washika filimbi wanafuta.
 
Kwenye nchi ambayo Ina utawala wa Sheria ambapo Rais ndiye anayeapishwa kuilinda katiba ya nchi haiwezekani iwepo ogani au mamlaka yoyote ambayo haiwajibiki kwa mkuu wa nchi (Rais) hiyo haiwezekani.

Ogani au mamlaka yoyote kuwa huru kiutendaji inawezekana lakini inapotenda shughuli zake tayari inakuwa inawajibika kutimiza mipango ya nchi ambapo msimamizi mkuu wa nchi ni Rais kwahyo huwezi kutenganisha majukumu yoyote yaliyopo ndani ya nchi na ofisi ya Rais.

Mifumo ya nchi yetu kiutawala na kiutendaji hata kama itatenganishwa ili kila mfumo au ogani ifanyekazi kwa uhuru wake Bado ni ngumu kuitenganisha na Rais. Mfano Tuna mihimili mitatu bunge, mahakama na Serikali; Sasa mahakama haiwezi kuwajibika bila kumzingatia msimamizi mkuu wa Sheria wa nchi lakini pia je mahakama inaundwajwe na watumishi wake wanapatikanaje?
Ukiacha kuhusu mahakama Bado tunaona chama chenye wabunge wengi ndo kinachokuwa na Rais kwahyo watunga Sheria wetu wakiwa bungeni tusitegemee kuwaona wakawa tofauti na Rais wao lakini pia katiba inampa mamlaka Rais ya kuteua baadhi ya wabunge kuingia kwenye muhimili wa serikali kama mawaziri.

Lakini pia Rais anawajibu wa kutengeneza timu yake ya kufanya nae kazi kitaifa, kimikoa, na kiwilaya na hizo timu lazima ziwajibike kufuata maagizo ya Rais ndani ya eneo husika katika kuwahudumia wananchi.

TUJIULIZE:
1. Ili tume ya taifa ya uchaguzi iwe huru itakaa ndani ya nchi au nje ya nchi?
2. Je ili tume iwe huru iundweje?
3. Ikiwa vyama vya siasa kupitia wawakilishi wake vitahusika kufanya uchaguzi wa kuunda NEC (mwenyekiti na wajumbe wake) je tunaweza kuwa na uhakika gani kwamba hao watu wa NEC hawatakuwa na mapenzi na itikadi za chama chochote?
3. Ikiwa wakati wa uchaguzi tutakuwa na wagombea wawili nafasi ya urais mfano Makonda (CCM) na Lisu (Chadema) harafu matokeo ya uchaguzi NEC wakatangaza Lisu ameshinda urais lakin Makonda akawa na ushahidi na vielelezo vya kwamba uchaguzi haukuwa wa haki na yeye ndiye aliyeshinda uchaguzi je ni mahali gani sahihi ambapo Makonda anaweza kupeleka mashitaka yake ili aweze kupatiwa haki yake??
4. Ikiwa NEC itashindwa kusimamia na kumtangaza mshindi halali wa uchaguzi kutokana na mapenzi na itikadi je ni mahakama zipi sahihi kwa kupeleka mashitaka kati ya mahakama za ndani au za umoja wa Afrika au za umoja wa mataifa?
5. Je katiba ya nchi yetu inasemaje na inatao miongozo gani katika kuiwajibisha tume ya taifa ya uchaguzi endapo haitatenda haki?
6. Je nchi yetu Ina mahakama maalumu kwaajili ya mashitaka ya vyama vya siasa? Kama jibu ndio je zinaundwaje? Kama jibu hapani je ni kwanini?
7. Je tunawezaje kuwa na tume huru bila kuwa na miongozo ya kikatiba?
8. Je nchi haiwezi kuwa na utaratibu mwingine wa kuwapata mawaziri nje ya bunge kama inavyowezekana kwa kuwapata wakuu wa mikoa na wilaya? Kwani haiwezekani mawaziri kupatikana nje ya bunge na kuja bungeni wanapohitajika tu kwaajili ya kutoa majibu na kutekeleza shughuli za serikali bungeni?

MWISHO: Ishu sio tume huru Bali ishu ni kwamba ipo kanuni ipi inayoweza kutumika kuiwajibisha NEC na kutengua matokeo batili yaliyo tangazwa na NEC baada ya uchaguzi?? Je ni mahakama zipi sahihi zitakazotumika kuitafsiri hiyo Sheria au kanuni kwaajili ya kutoa hukumu ya utenguzi wa matokeo feki?
Je tume inatoa muda gani wa kusubiri mashitaka (kama yatakuwepo) kutoka kwa walioshindwa uchaguzi kabla ya aliyetangazwa kushinda uchaguzi kuapishwa?

BADO TUNAJITAFUTA.
 
kwahivyo kua na mihemko ndio unaona sifa?

uhuru ni pamoja na kuzira, kususa au kugomea uchaguzi kwan kuna shida gan,

au umelazimishwa kuamini uhuru wa hiyo tume 🐒

yaani wewe ukishinda uchaguzi ndio tume inakua huru, ukishindwa uchaguzi ndio inakua sio Huru 🤣

useless and none sense
Unaandika kama vile umekatwa kichwa vile! Bila shaka una phd ya unafiki.
 
Unaandika kama vile umekatwa kichwa vile! Bila shaka una phd ya unafiki.
sina mihemko hata ukiniita aje dhidi ya kusema ukweli 🐒

si ni ukweli ndivyo ulivyo mchungu, unaamsha mihemko 🤣

Tume huru ya uchaguzi ni huru tangu kimuundo hadi kiutendaji, that is the fact...

kwani ukikataa, ukizira au kugomea ukweli huu kuna ubaya wowote?
muhimu kua mstahimilivu japo huzuiwi kua na mihemko 🐒
 
Back
Top Bottom