Uzima Tele
JF-Expert Member
- Jan 20, 2023
- 1,270
- 2,822
- Thread starter
- #61
Bila shaka ulipokuwa darasa la 3 au 4 hukusoma na kuilewa methali hii rahisi isemayohizo ni ndoto za mchana huwezi kushindana na mtu anayeshika dola hata awe anapendwa kaisi gani mama anamchana mchana kweupeee watu wanarudi ikulu anabaki analalama tu huko kama mtu aliyefumaniwa akioga nje lisu hana lolote ni maneno matupu
"...siku ya kufa nyani, miti yote huteleza..."
Nyani ni bingwa wa kutembea na kuruka juu ya miti. Unaweza kusema kwenye pori la miti, nyani ndiyo maeneo yake ya kujidai.
Yaani humwambii kitu. Mtu aweza kusema "ni ngumu sana kumuua nyani kwenye pori la miti"
Yes, ni ngumu lakini kumbe anaweza kuuwawa..
Na ikifika siku yake ya kufa, miti yote humkataa (huteleza)!
Unaweza kuwa na fedha, dola, and mention anything else. Lakini ikifika siku ya kufa kwako (kutoka kwako madarakani), hayo yote yatakukataa mchana kweupe.
Roman Empire iko wapi? Utawala wa Makaburu SA uko wapi? Kina Idd Amin Dada wako wapi? Kina Adolf Hitler wako wapi? Kina Mobutu Seseseko wako wapi? Kina John Pombe Magufuli wako wapi?
Hujaelewa tu maana yake mpaka hapo?
Ndugu mihambope, ishi na furahia leo lakini huwezi kuyajua ya kesho..!!
Waache hawa waonevu waishi na kufurahia leo.
Labda wanaweza kusema kama usemavyo wrwe kuwa, "hiyo ni ndoto ya mchana".
Utashangaa mno kuja kujua kumbe hata ndito za mchana, hutoa ujumbe wa ukweli..!
Mwisho wao upo na unakuja kama tufani..