Tundu Lissu, vita na Wasafi hutoiweza, utagalagazwa wewe na chama chako

sio "mume" sema "mmedandia gari kwa mbele"...BURNA BOY KWA AFYA YA JAMII
Hayo mambo tulishayaacha huko zamani sasa hivi music,michezo ni biashara hivyo diamond, music unamalengo makuu matatu kuelimisha,kuburudisha na ajila sasa mtu ukichagua music kama ajila kuna ubaya gani? , wakina roma na ney wamechagua music wa uhanaharakati na kuelimisha kwani kuna ubaya gani tubadilike.
 
Kwanza nyimbo zake za kitandani tu hazina lolote la kujifunza. Kmawe kura yangu siwezi kuwapigia wahuni. Angekuwa Christina Shusho ningempa kura.
Ujitambui wewe, malengo makuu ya music (1)Ajila (2)burudani (1)kuelimisha yeye amechagua muziki kuwa ni ajila.
 
Mkuu niwapi Tundu lissu kasema tusimpigie kura Dangote? Tundu anamjibu Goodluck kwamba asilazimishe upendo..ana sissitiza kua uzalendo sio kuunga mkono kila kitu hata kama ni kiovu...anasema Chibu hajawahi simama kwenye haki...maanake chibu anafata maslahi binafsi...pia kasema hata yeye yaani yeye Tundu sio muumini wa Dangote..

Hebu nambie ni wapi kasema tusimpigie kura Dai..au wapi kasema wafuasi wachadema tusipige kura....

Hebu rudi kipindi cha JK kwani Dai hakusupport Chama pendwa!!!!!! uliwahi sikia kiongozi wa upinzani aliinua neno la kusema wazi kua haungi mkoni kundi flani la wasanii? na umejiuliza kwa nn kasema sasa..

Je uliwajiuliza kwa nn Roma alivyotekwa hao wasanii wako walikaa kimya..!!!!!

Kwahiyo acheni kuchanganya siasa na mambo binafsi...

Pumba kubwa kuna mtu hapo juu kafikia kusema eti Biyonce alisapoti Clinton na Trumpa akashinda...hapo unajiuliza huyu anawaza kwa kutumia nn?
 
Ningekubaliana na Lissu kama sababu za kutomuunga mkono Diamond zingekuwa ni performance ya kimuziki.Lakini kusema mtu yeyote ambaye yuko tofauti na CHADEMA sio mpenda haki huko ni kupotoka.
Ni wapi Lissu amesema shida yake ni kwamba Diamond "Yuko tofauti na CHADEMA"?



Lissu ameongelea "kusimama kwenye haki", unaweza kuwa tofauti na CHADEMA na bado ukasimamia haki
 


Yaani uelewa wako bado mdogo sana kusema ukweli tangu lini kumekuwa vita! sasa ukibisha ukweli utaonekana mjinga. Halafu hizi media ziko overrated hiyo Wasafi hata Tanzania kuna vyombo vya habari bora zaidi vingi tu!!!. Hii ni kampuni tu lakini bado sana hapo itakapo kuwa media company ya EA nzima ndiyo tutaweza kusema lolote sasa ni sehemu ya kuongea uzushi na umbeya tu kwa vijana
 
Lissu anataka Diamond awe kama Nay wa mitego au Bob Marley ndio angemsapoti, yani ni kwamba chadema waislamu wasiswalishwe nyuma ya imamu ambaye ni ccm wanataka imamu awe kama Shehe Ponda.

Sasa hapo ndio kwenye tatizo kwa maana uhuru wa Diamond kushabikia ccm kwa chadema huo ni uadui.
 
Atahitaji kura za wananchi, acha ujuha wewe
Mwendazake kawaachia akili chafu.
Kura za wananchi wapi?

Maana yeye wanachi ni wale wlio chadema tu!

Alafu nilishakwambia hiyo mimba aliyokuachia mwenda zake inayokufanya kila kitu umtaje ilete huku mimi niileee ili umsahau.
 
Wangejifunza toka kwa wanamuziki wa congo walishindwa kufanya show yeyeto ulaya kwa vikwazo vya macombatanti, sababu ya kumsapoti dikteta Kabila.Watawala wanapita wananchi wanaishi.
 
Dhalimu magufuli hakushinda kwenye Rais bora wa Afrika pamoja na maccm kukesha usiku kucha karibu kila siku kumpigia kura mtandaoni. Rais wa Ghana aliyekuwa chaguo la Twitter Republic ndiye aliibuka mshindi.
Ccm wote wakiungana kumpigia atashinda tuzo.
 
Kwanza nyimbo zake za kitandani tu hazina lolote la kujifunza. Kmawe kura yangu siwezi kuwapigia wahuni. Angekuwa Christina Shusho ningempa kura.
Sasa muulize Lissu anajifunza nini kwenye nyimbo za Nay wa mitego ambazo anaimba maisha mafupi anakula ujana? muziki ni burudani ndio maana unaweza kusikiliza wimbo hata kwa lugha usiyoielewa na bado ukaburudika, sasa hayo ya kuelemika sijui yanatoka wapi.
 
Wangejifunza toka kwa wanamuziki wa congo walishindwa kufanya show yeyeto ulaya kwa vikwazo vya macombatanti, sababu ya kumsapoti dikteta Kabila.Watawala wanapita wananchi wanaishi.
Wakati hao akina Diamond wanafanya show kwenye kampeni za ccm watu si walijaa hadi mkawa mnasema wanategemea wasanii kwamba watu wanafuata wasanii tu?
 
Uzuri watu wanajua kutenganisha burudani na haki, wanaccm ndio huwa hawajui kutenganisha haya mambo. Pigeni propaganda mtakavyo ila Diamond hapewi kura na wapenda haki kwani ameamua kujiunga na kundi la watu waovu wa ccm fullstop. Anejiona shabiki wa Diamond asiipe kura cdm.
 
Hata ukiwa malaika ukajiunga na shetani wewe ni shetani, kama alijiunga na watesi wa kupinga haki za watu naye ni mtesi tuu hastahili kupewa na wanachadema, ccm wampe
 
Ndiyo apambane na UNAFIKI wake wa kukaa kimya kuhusu maovu ya Watanzania wakati huo huo kukemea maovu dhidi wa Wanigeria.
Kwa utawala ule wa jiwe Nan angezubutu kwenda kinyume ....angepoteza kila kitu kina Roma na ney hawakuwa na Mali yoyote yakutisha kuogopa jpm ..hvyo diamond alisoma upepo wa kisiasa

 
Sio kila atachosema Lissu ndio kifuatwe na kila mtu, na sio kila anayekuwa kinyume chake anakuwa mhaini, akili kama hizi, ndio udicteta,

Lissu aamini anachoamini, na sio kulazimisha wengine kuamini anachoamini kwamba ni sahihi

Tutakuwa Taifa la kijinga Sana kama wote tutakuwa kama Lissu ama kama mawazo ya Wana chadema

Daimond atapigiwa Kura na Watanzania wapenda mziki na sio wanachama wa Chama cha awaye yote, mwanasiasa kuingia malumbano na mwanamziki, ni ujinga mtupu, Kwanza ieleweke, Lissu na Daimond ni watu wawili tofauti, na kila mmoja ako na mtazamo wake na focus zao ni tofauti

Halafu ukweli mwingine ni kwamba, Lissu Kwa namna yoyote Ile na Kwa Hali yoyote Ile, hawezi kumfikia Daimond kiuchumi na pengine kiushawishi hawezi, Ila atamzidi kielimu n.k

Kwa hiyo, niungane na mwandishi kuwa, Lissu ameamua kucheza Ngoma asiyoiweza
 
Simtetei Tundu Lissu wala Simtetei Daimond ila nadhani hili swali lisichukukiwe kisiasa na wanasiasa hawapaswi kuingilia kwa itikadi zao bali mashabiki waamue wenyewe, au watanzania waamue wenyewe ingawa daimond hakusimama kutete haki pale alipohitajika lakini sioni sababu ya wanasiasa kuhamasisha wananchi, nadhani mashabiki wenyewe tuna akili timamu za kuamua kumpigia burna boy kijana wa njombe
 
Na Diamond atashinda hii tuzo asubuhi na mapema.

Nyumbu hawawezi kumzuia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…