Pre GE2025 Tundu Lissu: Wamepanga kuingiza kura feki uchaguzi wa ndani (CHADEMA)

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

mwanamwana

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2011
Posts
1,309
Reaction score
4,798
Tundu Lissu Makamu akizungumza kupitia clubhouse leo Desemba 23 amesema kuwa

"Nimepewa taarifa na mtu wa heshima sana kuhusu maandalizi ya vurugu kwenye uchaguzi.

Kuna watu wanaandaliwa waje waingie ukumbini kama wanachama, kumbe wapo kwa kazi maalum ya kutorosha masanduku ya kura, watakapogundua kwamba mambo ya upande wao hayako sawa na mhusika amenidokeza kwamba, vyovyote itakavyokuwa, tuhakikishe uchaguzi unafanyika wakati wa mchana na ameonya uchaguzi usifanyike usiku kwa sababu kuna possibility ya wenzetu kuzima taa zote ili kufanikisha utoroshaji wa kura ama kuingiza ndani kura feki.

Tafadhari hizi tumezipokea; lakini Katibu Mkuu wa Chama anapaswa kutoa ufafanuzi kuhusu huu mchakato wa uchaguzi utakavyokuwa ili kuhakikisha unakuwa huru na wa haki".
 
Lissu kila kitu kadokezwa na watu wakubwa itoshe kusema lissu ni muongo wa karne!
 
Mbowe mitano tena km hupendi nenda na ww kwny uchochoro wa kwenu ukaseme mama mitano tena
 
Tatizo umetumia codes sana, ndugu comrade. Lakini tumejitahidi kukuelewa. Ila nasikia wenyewe hawataki kushika dola. Eti wana malengo tofauti kabisa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…