Tunduru: Mama aua mtoto wake kwa sumu ya panya kwa masharti ya kupata kazi za ndani Arusha

Tunduru: Mama aua mtoto wake kwa sumu ya panya kwa masharti ya kupata kazi za ndani Arusha

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
MKAZI wa Kijiji cha Mwenge, Kata ya Mtina wilayani Tunduru, mkoani Ruvuma, Neema Athumani (24), anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za mauaji ya mtoto wake kwa kumwekea sumu ya panya kwenye soda.

Taarifa za tukio hilo zinadai kuwa mwanamke huyo alitekeleza mauaji hayo Desemba 24, mwaka huu, baada ya kuweka sumu ya panya kwenye soda na kumnywesha mtoto wake Rashfod Tariq, mwenye umri wa miaka minne.

Mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa baada ya mtuhumiwa huyo kutekeleza unyama huo, alichimba shimo na kwenda kumzika na baadaye kutoroka kijijini hapo.

Kwa mujibu wa taarifa hizo mtuhumiwa alikamatwa akiwa safarini kuelekea mkoani Arusha alikodai kuwa alikuwa anaenda kwa ajili ya kufanyakazi za dani kutokana na ugumu wa maisha, baada ya mzazi mwenzake kumtelekeza na kukataa kumhudumia mtoto.

Akiwa chini ya ulinzi wa polisi, mtuhumiwa huyo alikiri kufanya tukio hilo baada ya kupewa masharti na mwajiri wake wa mkoani Arusha kuwa kama anahitaji kazi aende bila mtoto.

Nipashe
 
Tunduma ndio ngome ya ACT wazalendo .wacha waone unyama wao
 
Kwanini umuue mtoto kwa ukali wa maisha si uende nyumba ya ibada na uingie zako mitini? Tutamlea sisi na kamwe usigeuke nyuma.
 
Shetani anakuanzishia kisanga, anakutengenezea dili la kujinasua halafu anatengeneza tena back-up la kukumaliza mazima. Wanaofanya urafiki wowote na dubwana hilo jahili wakapimwe akili Mirembe ya India.
Alimwambia Hawa: "Hutakufa, utakuwa sawa na Mungu". Mtu akifa: "Aaa!! Mungu amempenda zaidi, inabidi amchukue, msilie. Mnamchukiza sana Mungu mnapolialia, msipoangalia atamtupa motoni".
 
MKAZI wa Kijiji cha Mwenge, Kata ya Mtina wilayani Tunduru, mkoani Ruvuma, Neema Athumani (24), anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za mauaji ya mtoto wake kwa kumwekea sumu ya panya kwenye soda.

Taarifa za tukio hilo zinadai kuwa mwanamke huyo alitekeleza mauaji hayo Desemba 24, mwaka huu, baada ya kuweka sumu ya panya kwenye soda na kumnywesha mtoto wake Rashfod Tariq, mwenye umri wa miaka minne.

Mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa baada ya mtuhumiwa huyo kutekeleza unyama huo, alichimba shimo na kwenda kumzika na baadaye kutoroka kijijini hapo.

Kwa mujibu wa taarifa hizo mtuhumiwa alikamatwa akiwa safarini kuelekea mkoani Arusha alikodai kuwa alikuwa anaenda kwa ajili ya kufanyakazi za dani kutokana na ugumu wa maisha, baada ya mzazi mwenzake kumtelekeza na kukataa kumhudumia mtoto.

Akiwa chini ya ulinzi wa polisi, mtuhumiwa huyo alikiri kufanya tukio hilo baada ya kupewa masharti na mwajiri wake wa mkoani Arusha kuwa kama anahitaji kazi aende bila mtoto.

Nipashe
wanawake tangu siku wameongea na nyoka kisichojulikana sio wa kuwaamini.hata uzao wao wanaua
 
Huyo nae fala, yani kalea mtoto mpaka kufikia miaka mi4, alafu anamuua.???

Ila na sisi akina baba tulee watoto jamani..
 
Too sad...
May his soul rest in paradise little Angel
 
Back
Top Bottom