Tungekuwa wapi leo bila Rais Samia?

Tungekuwa wapi leo bila Rais Samia?

Amejitahidi.
Ana mapungufu yake.
Lakini ukinikumbusha yule Israel mla vichwa, Sina hamu!
Mleta mada hujakosea
 
Ni kweli kabisa Magufuli ndio kaharibu sana Bunge imefikia hatua Spika Ndugai akajiuzulu kipindi akiwa madarakani.
Unataka kumaanisha nini hapa? Kwamba hili nalo tuanze kubishana? Unamaanisha kuwa hujui udhaifu wa bunge ulianza lini na haya ya sasa ni matokeo tu? Enzi hizo CAG anakosoa udhaifu wa bunge mnamuita kamati ya maadili! Tunaposema kuharibu sana bunge unaelewa maana yake kwa upana?

Wewe na huyo Ndugai nyote ni wapuuzi tu kwa sababu mnayoyalalamikia msingi wake mlikuwa mkiushangilia sana.
 
Unaishi Dunia ipi?JPM alipoingia madarakani,Kikwete alishambuliwa sana!Mpaka watu wakasema utafikiri nchi haikuwa na Rais!
JPM hata yeye mwenyewe amemshambulia mtangukizi wake mara nyingi tu!
JPM ametokea,na yeye anashambuliwa japo ni marehemu,je angekuwa hai?
Nakuhakikishia,Samia akiondoka na yeye atageukwa na Hawa Hawa wanaomfagilia kwa Sasa!
Ila JPM ameshambuliwa sana sijawahi kuona marehemu anachukiwa vile
 
Ningekua hapahapa Tanzania nilipo sasa hivi ila haya yafuatayo yasingekuwepo.

Tusingekua tunatoa tozo.

Wanaomiliki nyumba wangeendelea kulipia kodi za majengo bila kuathiri bei ya umeme.

Tusingeona jinsi mhimili mmoja ulivyo dhaifu na wanaoutengeneza huo muhimili kuwa wanafiki na wanaojali matumbo yao zaidi kuliko kazi ya kuwakilisha wananchi.

Bei za vitu zisingeruka namna hii kama hali ilivyo sasa.
Kwenye bei ungefanya muujiza gani bei zisipande?
 
Wanambie hao Watanganyika kosa la mama ni Uzanzibar Uislamu na Ujanajike wake
Wana chuki kwa ajili ya hayo hapo lakini Takwimu za mama zinawaumbua.

Look at this

Screenshot_20220112-165049.png


Screenshot_20220112-164645.png


Screenshot_20220112-163818.png


Screenshot_20220112-161435.png
 
Sina cha kuongeza

R.I.P JPM
Ila udhaifu wa muhimili(BUNGE) haukuanza Leo wala Jana.

Nakumbuka 1993 kutokana na presha ya G55 chini ya Njelu Kasaka na Alipipi Kasyupa Bunge chini ya Spika Pius Msekwa lilipitisha Azimio la kuundwa kwa Serikali ya Tanganyika.

Lakini nini kilifuata?

Marehemu Kolimba na John Malechela wanafahamu vizuri.
 
Waachie kivipi? Kwani lini mfumko ulikua chini

Soma niliyekua namjibu aliuliza kitu gani kwanza mkuu.

Umefuatilia ongezeko la bei za vitu kwa kipindi cha miezi minne iliyopita?
 
Back
Top Bottom