Tupe stori za msanii uliesoma au kujuana nae kabla ya umaarufu

Tupe stori za msanii uliesoma au kujuana nae kabla ya umaarufu

100%
Nimesoma na Mheshimiwa Sugu shule ya Msingi Ligula,Mtwara.

Tukiwa darasa la pili tulikaa dawati moja na alikuwa ni rafiki yangu sana,tukitoka darasani muda wa saa tano tunakwenda nyumbani kwetu Ligula B tunachota korosho kwenye debe(korosho first grade za kutoka kiwanda cha korosho Likombe ambazo huwa zinauzwa nje ya nchi) tunaweka kwenye mifuko ya kaptura tunakula baadae anakwenda nyumbani kwao kiyangu.

Alikuwa anajulikana kwa jina la Joel.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kule wanafatiliana sana tabia, kusemana na kuonyana. Vichwa vilivyopinda hukimbia ili kukwepa usumbufu huo
Hlf sijui kwanini shuleni waislamu huwa hawapendi kuingia kwenye vipindi vyao vya dini
Hata shuleni kwetu wengi walikuwa wanaingia kwenye darasa la dini la kikristo,mpk shehe anashtaki kwa walimu

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
1. Bushoke tumecheza nae sana mpira makole pale, yeye alikua anadaka
2.voice wonder tulikua tukakutana kwenye mechi za kitaa, makole vs airport uwanja wa shule ya msingi makole. Mpira wa makaratas yan sembo.
3. Mswaki producer, huyu bwana mdogo alikua anakuja sana coco record studio ya kwanza pale Dodoma. Tulikua tunafanyia kazi kigamboni Karibu na magorofa mengi. Dogo hakua producer alikua msanii tena anaiga sauti ya ngwair sikuwahi kudhan anaweza kufika mbali
4.Moni central zone nilimkuta Dom sec, Mimi nikiwa nafundisha jioni darasa la watu wazima. Siku moja Moni alinifata na kunifananisha na producer flan wa pale pale Dom makole. Bahati nzuri yule producer nilishafanya nae kazi coco record hivyo nikamuunganisha nae.

Watu wengi maarufu hawana tabia ya kuringa ila watu wana inferiority complex juu yao. Unakuta mtu akipitwa bila kusalimiwa anasema jamaa anaringa wakati mtaani watu kibao wanampita bila kusalimia na hakuna shida. Mnapishana husalimii ukitegemea Kama atakusalimia, akiuchuna lawama tayar.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pale Morogoro Sec Sch kulikuwa na eneo maalum la kupaki Baiskeli za wanafunzi miaka hiyo. Enzi hizo Mji wa Morogoro ulikuwa na dala dala moja tu... lilikuwa basi moja tu la Mzee Chambo... na route ilikuwa ni Kihonda - Mjini. Kwa changamoto za usafiri, wazazi wengi waliwamilikisha Baiskeli watoto wao.

Miongoni mwetu wanafunzi wa Moro Sec tulikuwa na tabia, ukiwa na kijisafari chako cha fasta unamtafuta mwana mwenye Baiskeli.... Unamuazima.... kuepusha usumbufu huu... ilikuwa unaenda PARKING unaangalia Baiskeli isiyo na lock... unasepa kisha unairudisha kimya kimya kabla muda wa masomo haujaisha!

Hiki ni kipindi SQUEEZER alishaanza mziki na Mshkaji wake anaitwa Isaac .... (huyu Isaac sintamzungumzia). Squeezer alichukua Baiskeli ya Mwanafunzi mmoja mdada... yule mdada alikuwa mpole sana .... na Baiskeli yake ilikuwa nzuri tu... Squeezer aliichukua Baiskeli ile kwa dhamira akapige mishe zake kisha arudi shuleni!

Mambo yakawa mengi.... Squeezer hakuweza kuwahi kurudi shule katika muda kabla ya masomo kuisha.... bint mwenye baiskeli yake alikuwa ameingia shift ya mchana (Moro Sec kulikuwa na shift enzi hizo, sijui sasa) ambao wanatoka saa 12 jioni.... bint katafuta Baiskeli mpaka Kiza... hola.... huku na huko .... baiskeli haionekani! Basi mwishowe wanafunzi wenzie wakamshauri aripot kwa walimu wachache waliopo kuwa 'kaibiwa baiskeli yake'.

Kuibiwa Baiskeli ndani ya shule lilikuwa ni tukio kubwa sana na si la kawaida.... mara chache sana kutokea.... So kwa kuwa ilikuwa jioni na kiza kishatanda, basi bint yule (F1 au F2, Squeezer alikuwa F3) ilibidi arudi home na wenzie kwa Miguu. Balaa ilikuwa asubuhi iliofuata.... kilinuka shule nzima.... bahati mbaya sana.... ktk main suspects... kura ikanidondokea mimi ...... sijawahi kujua mpk leo why (ukiacha utundu, sijawahi kuwa na records za matukio)!

Kwa kuwa kimeshanuka.... shule nzima walijua kwamba kuna baiskeli imeibwa.... na alieba baiskeli ni (niite Thom).... I see.... nilikuwa na wakati mgumu sana ..... kwanza ndio tunaelekea mwishoni mwa F4...... pia msala wa aina ile sio msala mdogo....nilijua hapa Polisi inanihusu.... tatu, nilikuwa sina namna yyt financially ya kulimaliza lile soo, ukijumlisha na aibu ya kujulikana shule nzima kuwa Thom ni kibaka...

wakati seke seke limepamba moto na tayari Mkuu wa Shule kashatuma watu, niitwe kwa Mahojiano ..... ndio akajitokeza Squeezer na kunipa full story kuhusu Baiskeli, na ukweli kwamba Baiskeli haijaibwa wala nini... Baiskeli alienda kupiga nayo mishe na akairudisha very late.... ipo safi kabisa.... na baiskeli iko chini ya mikono salama ya Mlinzi wa shule.... ambapo Mlinzi mwenyewe anakuja Shuleni kwenye lindo jioni kuanzia saa 12... lakini Mlinzi alimuambia Mwl mmoja tu kuwa Baiskeli ipo... yule Mwl hakuwepo wkt wa seke seke...

To shorten the story.... Squeezer alinipanga nipambane kivyangu mpk mwisho lkn endapo Maji yatazidi Unga, nimtose kwa kumtaja yeye.... amalizie Msala ili kuniokoa mimi .... pia nisalimike na kuwa ktk nafasi nzuri ya kumaliza F4 na kufanya ''pepa'' .... Mungu sio John.... niliumaliza ule msala bila kumtaja Squeezer, mwenye Baiskeli yake akakabidhiwa na mm shule ikaisha salama...!
 
Pale Morogoro Sec Sch kulikuwa na eneo maalum la kupaki Baiskeli za wanafunzi miaka hiyo. Enzi hizo Mji wa Morogoro ulikuwa na dala dala moja tu... lilikuwa basi moja tu la Mzee Chambo... na route ilikuwa ni Kihonda - Mjini. Kwa changamoto za usafiri, wazazi wengi waliwamilikisha Baiskeli watoto wao.

Miongoni mwetu wanafunzi wa Moro Sec tulikuwa na tabia, ukiwa na kijisafari chako cha fasta unamtafuta mwana mwenye Baiskeli.... Unamuazima.... kuepusha usumbufu huu... ilikuwa unaenda PARKING unaangalia Baiskeli isiyo na lock... unasepa kisha unairudisha kimya kimya kabla muda wa masomo haujaisha!

Hiki ni kipindi SQUEEZER alishaanza mziki na Mshkaji wake anaitwa Isaac .... (huyu Isaac sintamzungumzia). Squeezer alichukua Baiskeli ya Mwanafunzi mmoja mdada... yule mdada alikuwa mpole sana .... na Baiskeli yake ilikuwa nzuri tu... Squeezer aliichukua Baiskeli ile kwa dhamira akapige mishe zake kisha arudi shuleni!

Mambo yakawa mengi.... Squeezer hakuweza kuwahi kurudi shule katika muda kabla ya masomo kuisha.... bint mwenye baiskeli yake alikuwa ameingia shift ya mchana (Moro Sec kulikuwa na shift enzi hizo, sijui sasa) ambao wanatoka saa 12 jioni.... bint katafuta Baiskeli mpaka Kiza... hola.... huku na huko .... baiskeli haionekani! Basi mwishowe wanafunzi wenzie wakamshauri aripot kwa walimu wachache waliopo kuwa 'kaibiwa baiskeli yake'.

Kuibiwa Baiskeli ndani ya shule lilikuwa ni tukio kubwa sana na si la kawaida.... mara chache sana kutokea.... So kwa kuwa ilikuwa jioni na kiza kishatanda, basi bint yule (F1 au F2, Squeezer alikuwa F3) ilibidi arudi home na wenzie kwa Miguu. Balaa ilikuwa asubuhi iliofuata.... kilinuka shule nzima.... bahati mbaya sana.... ktk main suspects... kura ikanidondokea mimi ...... sijawahi kujua mpk leo why (ukiacha utundu, sijawahi kuwa na records za matukio)!

Kwa kuwa kimeshanuka.... shule nzima walijua kwamba kuna baiskeli imeibwa.... na alieba baiskeli ni (niite Thom).... I see.... nilikuwa na wakati mgumu sana ..... kwanza ndio tunaelekea mwishoni mwa F4...... pia msala wa aina ile sio msala mdogo....nilijua hapa Polisi inanihusu.... tatu, nilikuwa sina namna yyt financially ya kulimaliza lile soo, ukijumlisha na aibu ya kujulikana shule nzima kuwa Thom ni kibaka...

wakati seke seke limepamba moto na tayari Mkuu wa Shule kashatuma watu, niitwe kwa Mahojiano ..... ndio akajitokeza Squeezer na kunipa full story kuhusu Baiskeli, na ukweli kwamba Baiskeli haijaibwa wala nini... Baiskeli alienda kupiga nayo mishe na akairudisha very late.... ipo safi kabisa.... na baiskeli iko chini ya mikono salama ya Mlinzi wa shule.... ambapo Mlinzi mwenyewe anakuja Shuleni kwenye lindo jioni kuanzia saa 12... lakini Mlinzi alimuambia Mwl mmoja tu kuwa Baiskeli ipo... yule Mwl hakuwepo wkt wa seke seke...

To shorten the story.... Squeezer alinipanga nipambane kivyangu mpk mwisho lkn endapo Maji yatazidi Unga, nimtose kwa kumtaja yeye.... amalizie Msala ili kuniokoa mimi .... pia nisalimike na kuwa ktk nafasi nzuri ya kumaliza F4 na kufanya ''pepa'' .... Mungu sio John.... niliumaliza ule msala bila kumtaja Squeezer, mwenye Baiskeli yake akakabidhiwa na mm shule ikaisha salama...!
Umenikumbusha mbali sana.
Sasa hivi hakuna shift, iliisha baada ya Kihonda secondary kufunguliwa.
 
Nimesoma na comedian TR PAUL advanced level KAHORORO HIGH SCHOOL BUKOBA ,alikuwa anasoma EGM mie PCM ,kiuweli jamaa alikuwa comic sn hasa tulikuwa tunakutana kwenye kipindi cha PURE mathematics na GS,
bandicam%202019-09-10%2021-16-54-290.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Meja kunta mzee siamini mpaka kesho imekuaje kuaje umewaka hivyo.lile jino lako la mbere Nina historia take nilipatwa na misara kupiti lile jino lake lilo vunjika
 
Back
Top Bottom