Uchaguzi 2020 Tusemezane: Uhalisia wa matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa 2020

Uchaguzi 2020 Tusemezane: Uhalisia wa matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa 2020

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
94,296
Reaction score
122,540
Mimi ni mmoja wa watu ambao wanaamini kwamba kama taifa, tulipaswa kuingia katika mfumo wa vyama vingi na katiba mpya pamoja na tume huru ya uchaguzi.

Sitazungumzia mambo ya kiufundi na ya kimuundo kuhusu hivyo vitu viwili. Lakini kimsingi, hivyo vitu ndo vilipaswa kufanyika kwanza kabla hatujarejea katika mfumo huo wa kiushindani.

Miaka yote hii tokea 1995, zoezi zima la kupiga kura katika uchaguzi mkuu limekuwa ni zoezi la kutimiza wajibu tu, ili nasi tuonekane tuna demokrasia ya kuchagua viongozi wetu ilhali uwanja wa ushindani haupo sawa baina ya washiriki wa mpambano.

Walio wahalisia wa mambo kama mimi, tayari ‘tunajua’ ni mgombea yupi kwenye ngazi ya urais atayetangazwa mshindi.

Mgombea huyo atayetangazwa kuwa ndo mshindi, ndo mtu huyo huyo aliyewateua kwenye hizo nafasi zao kwenye tume ya uchaguzi hao wataomtangaza yeye kuwa ndo mshindi.

Sasa nikiona jinsi ambavyo wanachama wa vyama vilivyo nje dola walivyo na hamu na hamasa ya uchaguzi mkuu, nashindwa kuelewa.

Nashindwa kuelewa kama ni wamejitoa tu fahamu kwa muda na kwamba kabla ya uchaguzi akili zitawarudia au wamejitoa kabisa fahamu na kusahau kabisa jinsi vile uwanja wa mapambano haupo sawa!

Kwa sababu, nikionacho hapa ni kwamba, baada ya tarehe 28 Oktoba, tutarudi kule kule tulikokuwa 2005, 2010, na 2015.

Baada ya ‘kushindwa’ watu ndo watagutuka tena kuwa kumbe tunahitaji katiba mpya. Kumbe tunahitaji tume huru ya uchaguzi. Kumbe tunahitaji uwanja ulio sawa kwa washiriki wote.

Siyo mmoja wa washiriki ndo anakuwa mchezaji yeye, refa yeye, kamisaa yeye, mwajiri yeye, na kila kitu kingine kihusianacho na uchaguzi anaoshiriki, yeye.

Sasa sijui kama kushiriki chaguzi ambazo mtu unajua una vikwazo vingi ni jambo la busara au la. Ingekuwa uamuzi ni wangu mimi binafsi, nisingeshiriki mchakato ambao ni wa maigizo.

Wengine wanaweza kuwa na mtazamo ulio tofauti. Hakuna ubaya kwenye hilo.

Ila kwa kadri mtu unapozidi kushiriki mchakato wa jambo ambalo unajua kabisa halitoi fursa sawa kwa wote, unapokosa kupata fursa uitakayo, unakuwa umejipunguzia mamlaka ya kimaadili ya kupinga na kulalamikia matokeo.

Manake kama ulikuwa unajua kabla ya zoezi kuanza kuwa hakuna fursa sawa, kwa nini sasa ulishiriki? Si ungeligomea zoezi zima tu!

Kwa sasa endeleeni kufurahia maneno matamu ya Lissu. Sasa hivi anawapa nyie wapenzi na mashabiki wake kile kiitwacho ‘red meat’, yaani yale maneno mnayotaka kusikia na yanayoziamsha hisia zenu.

Naona na Bw. Membe naye anajitutumua kuwarushia mashabiki wake hizo nyama nyekundu lakini hamfikii Lissu.

Baada ya uchaguzi kuisha na Rais Magufuli kutangazwa mshindi, akili, kama mnazo, labda ndo zitawarudia na kutambua kuwa hamkuwa na lenu kwenye huo uchaguzi!

Kama mnabisha, siku ya siku ikifika tutakumbushana haya maneno yangu. Msije kununa tu.😁
 
Jaribu kuliona jambo moja, vyama makini vya upinzani kama Chadema, ACT na pengine NCCR vingeamua kutoshiriki lakini vibaraka wa CCM kama TLP, UDP nk vikaamua vinashiriki huoni kuwa dunia itatambua kuwa uchaguzi wa vyama vingi umefanyika?

Nini matokeo ya utendaji wa bunge litakalo fuatia? Hali itakuwa mbaya sana pengine kuliko Korea kaskazini. Njia INAYOBIDI kufuata ni ile aliyo shauri Lissu tuu, kutokubali wizi wa kura na kusema tunamwachia Mungu.
 
Jaribu kuliona jambo moja, vyama makini vya upinzani kama Chadema, ACT na pengine NCCR vingeamua kutoshiriki lakini vibaraka wa CCM kama TLP, UDP nk vikaamua vinashiriki huoni kuwa dunia itatambua kuwa uchaguzi wa vyama vingi umefanyika?

Nini matokeo ya utendaji wa bunge litakalo fuatia? Hali itakuwa mbaya sana pengine kuliko Korea kaskazini. Njia INAYOBIDI kufuata ni ile aliyo shauri Lissu tu, kutokubali wizi wa kura na kusema tunamwachia Mungu.
Hata 2010 walikataa wizi wa kura.

2015 napo walikataa wizi wa kura na wakatishia kwenda sijui kwenye mahakama ya wapi wapi huko.

Hawakwenda. Yalikuwa ni maneno matupu tu.

2020 hao tena, wanashiriki tena chaguzi kwa sheria zile zile, tume ile ile, wakishindana na CCM ile ile.

Kila la kheri.
 
Hakuna jinsi ya kuzuia uchaguzi usifanyike October 2020, na hakuna jinsi wala namna watanzania watapata tume huru kesho au mwezi ujao, na hakuna jinsi wa namna kuipata katiba mpya kabla ya uchaguzi mkuu October 2020.

Hivyo walivyoamua kushiriki ni sahihi kabisa kwasababu ni bora washiriki kisha walalamike kuliko kutoshiriki wakose na wasiwe na hoja ya kuongea.

Humo walimo ndio mwake, wacheze humo humo na malalamiko yao yakiwa yanaendelea.

Uchaguzi serikali za mitaa ulikiukwa na ccm walifurahia kujipa ushindi, kwasababu tu walishiriki. Kila aliyeshiriki alishinda by default.

Huu wa mwaka huu isiwe hivyo, wapambane tu chochote watakachoambulia ni sawa, kuliko kukosa kabisa.
 
Miezi miwili nyuma walikuwa na akili lakini ujuo wa Membe nyumba ile na ujio wa aliyekwenda kutibiwa ughaibuni umewatowa akili zitawaruxia baada ya october Magu atakapokuwa anaapishwa!
Magu ataapishwa kama atashinda kihalali. Lakini muonekano wa sasa ni kuwa kama hatachanga karata zake vyema wakati wa kampeni na kudhani kuwatumia kina Diamond na TOT watapumbaza watu na yeye atalazimisha Tume kumuibia kura hapo ametafuta matatizo makubwa.
Katika hali halisi ya maisha ya Watanzania kuwaimbia nyimbo za ndege, SGR, Ujenzi wa bwawa nk ni ngumu sana kuwashawishi kukupa kura mbele ya yule anaye wapa matumaini ya kuboresha maisha yao na Uhuru zaidi.
 
Hakuna jinsi ya kuzuia uchaguzi usifanyike October 2020, na hakuna jinsi wala namna watanzania watapata tume huru kesho au mwezi ujao, na hakuna jinsi wa namna kuipata katiba mpya kabla ya uchaguzi mkuu October 2020.

Hivyo walivyoamua kushiriki ni sahihi kabisa kwasababu ni bora washiriki kisha walalamike kuliko kutoshiriki wakose na wasiwe na hoja ya kuongea.

Humo walimo ndio mwake, wacheze humo humo na malalamiko yao yakiwa yanaendelea.

Uchaguzi serikali za mitaa ulikiukwa na ccm walifurahia kujipa ushindi, kwasababu tu walishiriki. Kila aliyeshiriki alishinda by default.

Huu wa mwaka huu isiwe hivyo, wapambane tu chochote watakachoambulia ni sawa, kuliko kukosa kabisa.
Defeatist attitude yako inatia simanzi.
 
Huu ujio wa vyama vingi CCM wenyewe walilazimishwa na Nyerere, wengi wao walipigia kura mfumo wa chama kimoja uendelee.

Hili linaonesha wazi hao jamaa wamegoma kubadilisha katiba ili waendelee kuwabana wapinzani kwa kutumia hii katiba iliyopo sasa iliyoasisiwa toka kwa mkoloni, kwasababu wanajua ndio inayowabeba waendelee kutawala kwasababu hawakubaliki kwa wengi.

Hata ukiwalaumu wapinzani kwenye hili ni sawa na kuwaonea, wao kwa uchache wao kule bungeni hawawezi kufanya lolote kubadilisha hiyo hali, vinginevyo labda watumie njia nyingine mbali na zile zilizozoeleka ambazo zinaonesha zimeshindwa.
 
Huu ujio wa vyama vingi CCM wenyewe walilazimishwa na Nyerere, wengi wao walipigia kura mfumo wa chama kimoja uendelee.

Hili linaonesha wazi hao jamaa wamegoma kubadilisha katiba ili waendelee kuwabana wapinzani kwa kutumia hii katiba iliyopo sasa iliyoasisiwa toka kwa mkoloni, kwasababu wanajua ndio inayowabeba waendelee kutawala kwasababu hawakubaliki kwa wengi.
Mbona inasemwa kuwa asilimia 80 ya Watanzania walikataa mfumo wa vyama vingi lakini Nyerere ndo akaupigia debe...uongo?
 
Mimi ni mmoja wa watu ambao wanaamini kwamba kama taifa, tulipaswa kuingia katika mfumo wa vyama vingi na katiba mpya pamoja na tume huru ya uchaguzi.

Sitazungumzia mambo ya kiufundi na ya kimuundo kuhusu hivyo vitu viwili. Lakini kimsingi, hivyo vitu ndo vilipaswa kufanyika kwanza kabla hatujarejea katika mfumo huo wa kiushindani.

Miaka yote hii tokea 1995, zoezi zima la kupiga kura katika uchaguzi mkuu limekuwa ni zoezi la kutimiza wajibu tu, ili nasi tuonekane tuna demokrasia ya kuchagua viongozi wetu ilhali uwanja wa ushindani haupo sawa baina ya washiriki wa mpambano.

Walio wahalisia wa mambo kama mimi, tayari ‘tunajua’ ni mgombea yupi kwenye ngazi ya urais atayetangazwa mshindi.

Mgombea huyo atayetangazwa kuwa ndo mshindi, ndo mtu huyo huyo aliyewateua kwenye hizo nafasi zao kwenye tume ya uchaguzi hao wataomtangaza yeye kuwa ndo mshindi.

Sasa nikiona jinsi ambavyo wanachama wa vyama vilivyo nje dola walivyo na hamu na hamasa ya uchaguzi mkuu, nashindwa kuelewa.

Nashindwa kuelewa kama ni wamejitoa tu fahamu kwa muda na kwamba kabla ya uchaguzi akili zitawarudia au wamejitoa kabisa fahamu na kusahau kabisa jinsi vile uwanja wa mapambano haupo sawa!

Kwa sababu, nikionacho hapa ni kwamba, baada ya tarehe 28 Oktoba, tutarudi kule kule tulikokuwa 2005, 2010, na 2015.

Baada ya ‘kushindwa’ watu ndo watagutuka tena kuwa kumbe tunahitaji katiba mpya. Kumbe tunahitaji tume huru ya uchaguzi. Kumbe tunahitaji uwanja ulio sawa kwa washiriki wote.

Siyo mmoja wa washiriki ndo anakuwa mchezaji yeye, refa yeye, kamisaa yeye, mwajiri yeye, na kila kitu kingine kihusianacho na uchaguzi anaoshiriki, yeye.

Sasa sijui kama kushiriki chaguzi ambazo mtu unajua una vikwazo vingi ni jambo la busara au la. Ingekuwa uamuzi ni wangu mimi binafsi, nisingeshiriki mchakato ambao ni wa maigizo.

Wengine wanaweza kuwa na mtazamo ulio tofauti. Hakuna ubaya kwenye hilo.

Ila kwa kadri mtu unapozidi kushiriki mchakato wa jambo ambalo unajua kabisa halitoi fursa sawa kwa wote, unapokosa kupata fursa uitakayo, unakuwa umejipunguzia mamlaka ya kimaadili ya kupinga na kulalamikia matokeo.

Manake kama ulikuwa unajua kabla ya zoezi kuanza kuwa hakuna fursa sawa, kwa nini sasa ulishiriki? Si ungeligomea zoezi zima tu!

Kwa sasa endeleeni kufurahia maneno matamu ya Lissu. Sasa hivi anawapa nyie wapenzi na mashabiki wake kile kiitwacho ‘red meat’, yaani yale maneno mnayotaka kusikia na yanayoziamsha hisia zenu.

Naona na Bw. Membe naye anajitutumua kuwarushia mashabiki wake hizo nyama nyekundu lakini hamfikii Lissu.

Baada ya uchaguzi kuisha na Rais Magufuli kutangazwa mshindi, akili, kama mnazo, labda ndo zitawarudia na kutambua kuwa hamkuwa na lenu kwenye huo uchaguzi!

Kama mnabisha, siku ya siku ikifika nitawakumbusha haya maneno yangu. Msije kununa tu...😁

Maneno meeeengi ilhali hoja yako ni kumpigia debe M-kanda ya Ziwa mwenzako. Kama wapinzani wanapoteza muda, why do you even care? Kama Magufuli unayempenda atashinda bila tatizo hapo Oktoba, why should you bother how Wapinzani watavyojiskia baada ya ushindi huo? 😡
 
Mimi hata siwaelewagi .... wanashangilia vijembe utafikiri vinageuka kura. Kwanza kwa hali iliyopo mwaka huu hata kama uchaguzi utasimamiwa na mabeberu CCM itashinda! Huko mitaani/vijijini Chadema imefutika, matawi yamefungwa mengi sana. Kabla hata ya issue za Katiba na tume chama hakina mizizi ya watu ngazi za chini kama CCM.
 
Back
Top Bottom