Uchaguzi 2020 Tusemezane: Uhalisia wa matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa 2020

Uchaguzi 2020 Tusemezane: Uhalisia wa matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa 2020

Mimi hata siwaelewagi .... wanashangilia vijembe utafikiri vinageuka kura. Kwanza kwa hali iliyopo mwaka huu hata kama uchaguzi utasimamiwa na mabeberu CCM itashinda! Huko mitaani/vijijini Chadema imefutika, matawi yamefungwa mengi sana. Kabla hata ya issue za Katiba na tume chama hakina mizizi ya watu ngazi za chini kama CCM.
You wait..watakuja hapa kuanzia tarehe 29 na kuanza kulia lia tena.
 
Maneno meeeengi ilhali hoja yako ni kumpigia debe M-kanda ya Ziwa mwenzako. Kama wapinzani wanapoteza muda, why do you even care? Kama Magufuli unayempenda atashinda bila tatizo hapo Oktoba, why should you bother how Wapinzani watavyojiskia baada ya ushindi huo? 😡
Hakuna nayempigia debe!

Tatizo lenu nyie makamanda ni mko short-sighted sana.

Hamuwezi kuona hoja zaidi ya Magufuli.

Magufuli kwa sasa anazitawala fikra zenu.

Anaishi vichwani mwenu bure...halipi kodi ya pango wala nini.

Mtu akikosoa mfumo uliomuweka Magufuli madarakani, na ambao ndo uliwaweka Kikwete na Mkapa pia, nyie mnamwona Magufuli tu.

Na kama unadhani tatizo ni Magufuli na siyo mfumo mzima, basi subiri 2025 uone.
 
Niliona, ila sidhani kama Tanzania tutafikia huko. Hakuna lisilowezekana lakini sioni kama kuna uwezekano huo.
Mkuu mwenye kuepusha tusifike huko ni Magufuli na CCM yake, asiingilie utendaji wa Tume ya uchaguzi na asiibe kura. Ajinadi vizuri apewe kura halali basi, vinginevyo hayo mambo ya Misri au Sudan huwa yanahitaji mtu mmoja tuu kuleta hamasa na nchi ikaingia katika sintofahamu
 
Hata 2010 walikataa wizi wa kura.

2015 napo walikataa wizi wa kura na wakatishia kwenda sijui kwenye mahakama ya wapi wapi huko.

Hawakwenda. Yalikuwa ni maneno matupu tu.

2020 hao tena....wanashiriki tena chaguzi kwa sheria zile zile, tume ile ile, wakishindana na CCM ile ile.

Kila la kheri.
Mkuu mgombe wa 2015 na huyu wa 2020 nitofauti kubwa Sana huyu wa Sasa Ni jeuri kiburi asieogopa kitisho chochote naomba tushauriane kujitokeza kupiga kura kwa wingi ili hata kuzilinda tuwe wengi ili hao walinda chama wakiona uwingi wa walinda kura kila kituo kila kitongoji kila Kijiji kila wilaya kila mkoa na hata nchi nzima hawawezi kuwa na mabomu ya machozi ya kumwagia nchi nzima Kama unakumbuka 2015 wengi tulisubiria kauli moja ya bwana Edo ili tukinukishe kukaa kwake kimya ndicho kilichofanya tuvunjike moyo ila kwa bwana huyu mwanasheria Hatakubali kuwa mjinga Kama kura zitamtosha,, naomba ujue kuwa chama tawala waliweka masikio pamba kuhusu tume ya uchaguzi na wasimamizi wa uchaguzi mpaka Waka kata rufaa baada ya mahakama kutengu wakutugenzi kusimamia uchaguzi yote hayo ni ili vyama vikuu vya upinzani wasusie uchaguzi wabakize vibaraka wao tu! Sasa mtego umegoma kufyatuka na wagombea wamepitishwa hofu iko kwao, mkuu nakuomba kwa mara nyingine waeleze wananchi na wanajukwaa faida ya kupiga kura na sio hasara ya kufirika,, mungu anasaidia mwenye juhudi tujiandaeni kupiga kura ki halali kabisa Ni wajibu wetu ,, ikiwa kweli tutapiga kura kwa moyo mmoja mwaka huu itakuwa mara ya kwanza magazeti kuandika habari za chama tawala kuibiwa kura, na lugha tutakayoitumia ni kuwa Mwizi analalamika kaibiwa
 
Ukweli mtupu

Teali tupo kwenye mtindo mbovu wa maisha na lazma tukubali tu hakuna linalotokea kwa bahati mbaya
 
Ndiyo mazingira tuliyomo, hatuwezi kuukataa ukweli.

Katiba haipo, tume huru pia haipo, lakini uchaguzi upo tufanyeje?!
Tujitokeze kwa wingi kuchagua viongozi tunaowataka halafu tusimame imara katika kutetea haki yetu viongozi ni wachache wananchi ni wengi mara dufu tuwe bega kwa bega kupata haki zetu kwa kusaidiana na viongozi wetu lissu amejiamini kwa sababu anaamini wananchi tupo tunaemkubali na kumuamini
 
Mimi hata siwaelewagi .... wanashangilia vijembe utafikiri vinageuka kura. Kwanza kwa hali iliyopo mwaka huu hata kama uchaguzi utasimamiwa na mabeberu CCM itashinda! Huko mitaani/vijijini Chadema imefutika, matawi yamefungwa mengi sana. Kabla hata ya issue za Katiba na tume chama hakina mizizi ya watu ngazi za chini kama CCM.
Aisee wewe huijui Tanzania kabisa. Mie nakuambia sasa hivi Chadema iko imara sana mikoani kuliko ilivyokuwa awali pamoja na kuzuiwa kufanya siasa.
Ndio sababu ya hofu iliyonayo CCM kama chama.
 
Magu ataapishwa kama atashinda kihalali. Lakini muonekano wa sasa ni kuwa kama hatachanga karata zake vyema wakati wa kampeni na kudhani kuwatumia kina Diamond na TOT watapumbaza watu na yeye atalazimisha Tume kumuibia kura hapo ametafuta matatizo makubwa.
Katika hali halisi ya maisha ya Watanzania kuwaimbia nyimbo za ndege, SGR, Ujenzi wa bwawa nk ni ngumu sana kuwashawishi kukupa kura mbele ya yule anaye wapa matumaini ya kuboresha maisha yao na Uhuru zaidi.
Kila mmoja na mtizamo wake
 
Mmeanza kuweweseka sasa, tulieni dawa iwangieni vizuri dadeeeki
Mimi ni mmoja wa watu ambao wanaamini kwamba kama taifa, tulipaswa kuingia katika mfumo wa vyama vingi na katiba mpya pamoja na tume huru ya uchaguzi.

Sitazungumzia mambo ya kiufundi na ya kimuundo kuhusu hivyo vitu viwili. Lakini kimsingi, hivyo vitu ndo vilipaswa kufanyika kwanza kabla hatujarejea katika mfumo huo wa kiushindani.

Miaka yote hii tokea 1995, zoezi zima la kupiga kura katika uchaguzi mkuu limekuwa ni zoezi la kutimiza wajibu tu, ili nasi tuonekane tuna demokrasia ya kuchagua viongozi wetu ilhali uwanja wa ushindani haupo sawa baina ya washiriki wa mpambano.

Walio wahalisia wa mambo kama mimi, tayari ‘tunajua’ ni mgombea yupi kwenye ngazi ya urais atayetangazwa mshindi.

Mgombea huyo atayetangazwa kuwa ndo mshindi, ndo mtu huyo huyo aliyewateua kwenye hizo nafasi zao kwenye tume ya uchaguzi hao wataomtangaza yeye kuwa ndo mshindi.

Sasa nikiona jinsi ambavyo wanachama wa vyama vilivyo nje dola walivyo na hamu na hamasa ya uchaguzi mkuu, nashindwa kuelewa.

Nashindwa kuelewa kama ni wamejitoa tu fahamu kwa muda na kwamba kabla ya uchaguzi akili zitawarudia au wamejitoa kabisa fahamu na kusahau kabisa jinsi vile uwanja wa mapambano haupo sawa!

Kwa sababu, nikionacho hapa ni kwamba, baada ya tarehe 28 Oktoba, tutarudi kule kule tulikokuwa 2005, 2010, na 2015.

Baada ya ‘kushindwa’ watu ndo watagutuka tena kuwa kumbe tunahitaji katiba mpya. Kumbe tunahitaji tume huru ya uchaguzi. Kumbe tunahitaji uwanja ulio sawa kwa washiriki wote.

Siyo mmoja wa washiriki ndo anakuwa mchezaji yeye, refa yeye, kamisaa yeye, mwajiri yeye, na kila kitu kingine kihusianacho na uchaguzi anaoshiriki, yeye.

Sasa sijui kama kushiriki chaguzi ambazo mtu unajua una vikwazo vingi ni jambo la busara au la. Ingekuwa uamuzi ni wangu mimi binafsi, nisingeshiriki mchakato ambao ni wa maigizo.

Wengine wanaweza kuwa na mtazamo ulio tofauti. Hakuna ubaya kwenye hilo.

Ila kwa kadri mtu unapozidi kushiriki mchakato wa jambo ambalo unajua kabisa halitoi fursa sawa kwa wote, unapokosa kupata fursa uitakayo, unakuwa umejipunguzia mamlaka ya kimaadili ya kupinga na kulalamikia matokeo.

Manake kama ulikuwa unajua kabla ya zoezi kuanza kuwa hakuna fursa sawa, kwa nini sasa ulishiriki? Si ungeligomea zoezi zima tu!

Kwa sasa endeleeni kufurahia maneno matamu ya Lissu. Sasa hivi anawapa nyie wapenzi na mashabiki wake kile kiitwacho ‘red meat’, yaani yale maneno mnayotaka kusikia na yanayoziamsha hisia zenu.

Naona na Bw. Membe naye anajitutumua kuwarushia mashabiki wake hizo nyama nyekundu lakini hamfikii Lissu.

Baada ya uchaguzi kuisha na Rais Magufuli kutangazwa mshindi, akili, kama mnazo, labda ndo zitawarudia na kutambua kuwa hamkuwa na lenu kwenye huo uchaguzi!

Kama mnabisha, siku ya siku ikifika nitawakumbusha haya maneno yangu. Msije kununa tu...[emoji16]
 
Jiandaeni kisaikolojia maana lissu ndiye ataapishwa baada ya October.

Wananchi wa Tanzania tegemeo lao ni mh Lissu.

Hutaki rudi kwenu Burundi.
Miezi miwili nyuma walikuwa na akili lakini ujuo wa Membe nyumba ile na ujio wa aliyekwenda kutibiwa ughaibuni umewatowa akili zitawaruxia baada ya october Magu atakapokuwa anaapishwa!
 
Hao Upinzani Uchwara wakijitahidi sana
Watapata 15%
Hiyo Wajione washindi
 
Mkuu hapo unapoteza nguvu zako kwa kumpigia mbuzi gitaa.

Hao unao waelimisha hawana chochote wajuacho zaidi ya kutetea, kuramba miguu na kupongeza.
Jaribu kuliona jambo moja, vyama makini vya upinzani kama Chadema, ACT na pengine NCCR vingeamua kutoshiriki lakini vibaraka wa CCM kama TLP, UDP nk vikaamua vinashiriki huoni kuwa dunia itatambua kuwa uchaguzi wa vyama vingi umefanyika?
Nini matokeo ya utendaji wa bunge litakalo fuatia? Hali itakuwa mbaya sana pengine kuliko Korea kaskazini.
Njia INAYOBIDI kufuata ni ile aliyo shauri Lissu tuu, kutokubali wizi wa kura na kusema tunamwachia Mungu
 
Magu ataapishwa kama atashinda kihalali. Lakini muonekano wa sasa ni kuwa kama hatachanga karata zake vyema wakati wa kampeni na kudhani kuwatumia kina Diamond na TOT watapumbaza watu na yeye atalazimisha Tume kumuibia kura hapo ametafuta matatizo makubwa.
Katika hali halisi ya maisha ya Watanzania kuwaimbia nyimbo za ndege, SGR, Ujenzi wa bwawa nk ni ngumu sana kuwashawishi kukupa kura mbele ya yule anaye wapa matumaini ya kuboresha maisha yao na Uhuru zaidi.
Magufuli lazima ashinde
Hasiposhinda tutampa ushindi wa lazima halafu tunabadili katiba awe rais wa kudumu
 
Mbona husemi mlivyompiga mh Lissu pyuuuu pyuuuu?
Hata 2010 walikataa wizi wa kura.

2015 napo walikataa wizi wa kura na wakatishia kwenda sijui kwenye mahakama ya wapi wapi huko.

Hawakwenda. Yalikuwa ni maneno matupu tu.

2020 hao tena....wanashiriki tena chaguzi kwa sheria zile zile, tume ile ile, wakishindana na CCM ile ile.

Kila la kheri.
 
Hakika mkuu
Magu ataapishwa kama atashinda kihalali. Lakini muonekano wa sasa ni kuwa kama hatachanga karata zake vyema wakati wa kampeni na kudhani kuwatumia kina Diamond na TOT watapumbaza watu na yeye atalazimisha Tume kumuibia kura hapo ametafuta matatizo makubwa.
Katika hali halisi ya maisha ya Watanzania kuwaimbia nyimbo za ndege, SGR, Ujenzi wa bwawa nk ni ngumu sana kuwashawishi kukupa kura mbele ya yule anaye wapa matumaini ya kuboresha maisha yao na Uhuru zaidi.
 
Back
Top Bottom