Uchaguzi 2020 Tusemezane: Uhalisia wa matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa 2020

Uchaguzi 2020 Tusemezane: Uhalisia wa matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa 2020

kamwe mifumo ya kisiasa tulorithishwa na mabeberu haiendani na siasa japo tunalazimisha iwe ndo mifumo yetu rasmi, kuna haja ya kuunda mifumo ya kisiasa inayoendana nasi ili tuweze kupiga hatua mbele.
 
Jiandaeni kisaikolojia maana lissu ndiye ataapishwa baada ya October.

Wananchi wa Tanzania tegemeo lao ni mh Lissu.

Hutaki rudi kwenu Burundi.
Si unajua kiitikio chenu cha tumeibiwa×6
 
Nyani , kati siku akili zako zilipikurudia ni pamoja na post hii. Lakini nakuona kama msomi asiyependa nchi yake. Kasoro za ki muundo unaziona halafu lawama unawarushia wapinzani !!. Hii akili ya msomi wa aina gani ?!.

Kwamba wewe mamlaka zilizotakiwa kutoa haki kwa wananchi kujichagulia viongozi wao ni wapinzani ?!. Usomi huu mbona bure kabisa Ngabu ?!.

Nchi hii ni yetu sote. Tujiwekee utaratibu mzuri wa watu kuwaweka viongozi bora na wanaowataka. Si hii ya lazima utokane na chama cha ki communist cha Ccm !!. Usomi wako usaidie badala ya kuwazodoa wapinzani wanaopambana kupata haki hiyo [emoji120][emoji120]
Nimependa Sana ulivyomuelezea huyu jamaa,inaonesha Ana uelewa mdogo Sana wa mambo
Asante Sana kiongozi.
Una hekima kubwa Sana.
 
Mimi ni mmoja wa watu ambao wanaamini kwamba kama taifa, tulipaswa kuingia katika mfumo wa vyama vingi na katiba mpya pamoja na tume huru ya uchaguzi.

Sitazungumzia mambo ya kiufundi na ya kimuundo kuhusu hivyo vitu viwili. Lakini kimsingi, hivyo vitu ndo vilipaswa kufanyika kwanza kabla hatujarejea katika mfumo huo wa kiushindani.

Miaka yote hii tokea 1995, zoezi zima la kupiga kura katika uchaguzi mkuu limekuwa ni zoezi la kutimiza wajibu tu, ili nasi tuonekane tuna demokrasia ya kuchagua viongozi wetu ilhali uwanja wa ushindani haupo sawa baina ya washiriki wa mpambano.

Walio wahalisia wa mambo kama mimi, tayari ‘tunajua’ ni mgombea yupi kwenye ngazi ya urais atayetangazwa mshindi.

Mgombea huyo atayetangazwa kuwa ndo mshindi, ndo mtu huyo huyo aliyewateua kwenye hizo nafasi zao kwenye tume ya uchaguzi hao wataomtangaza yeye kuwa ndo mshindi.

Sasa nikiona jinsi ambavyo wanachama wa vyama vilivyo nje dola walivyo na hamu na hamasa ya uchaguzi mkuu, nashindwa kuelewa.

Nashindwa kuelewa kama ni wamejitoa tu fahamu kwa muda na kwamba kabla ya uchaguzi akili zitawarudia au wamejitoa kabisa fahamu na kusahau kabisa jinsi vile uwanja wa mapambano haupo sawa!

Kwa sababu, nikionacho hapa ni kwamba, baada ya tarehe 28 Oktoba, tutarudi kule kule tulikokuwa 2005, 2010, na 2015.

Baada ya ‘kushindwa’ watu ndo watagutuka tena kuwa kumbe tunahitaji katiba mpya. Kumbe tunahitaji tume huru ya uchaguzi. Kumbe tunahitaji uwanja ulio sawa kwa washiriki wote.

Siyo mmoja wa washiriki ndo anakuwa mchezaji yeye, refa yeye, kamisaa yeye, mwajiri yeye, na kila kitu kingine kihusianacho na uchaguzi anaoshiriki, yeye.

Sasa sijui kama kushiriki chaguzi ambazo mtu unajua una vikwazo vingi ni jambo la busara au la. Ingekuwa uamuzi ni wangu mimi binafsi, nisingeshiriki mchakato ambao ni wa maigizo.

Wengine wanaweza kuwa na mtazamo ulio tofauti. Hakuna ubaya kwenye hilo.

Ila kwa kadri mtu unapozidi kushiriki mchakato wa jambo ambalo unajua kabisa halitoi fursa sawa kwa wote, unapokosa kupata fursa uitakayo, unakuwa umejipunguzia mamlaka ya kimaadili ya kupinga na kulalamikia matokeo.

Manake kama ulikuwa unajua kabla ya zoezi kuanza kuwa hakuna fursa sawa, kwa nini sasa ulishiriki? Si ungeligomea zoezi zima tu!

Kwa sasa endeleeni kufurahia maneno matamu ya Lissu. Sasa hivi anawapa nyie wapenzi na mashabiki wake kile kiitwacho ‘red meat’, yaani yale maneno mnayotaka kusikia na yanayoziamsha hisia zenu.

Naona na Bw. Membe naye anajitutumua kuwarushia mashabiki wake hizo nyama nyekundu lakini hamfikii Lissu.

Baada ya uchaguzi kuisha na Rais Magufuli kutangazwa mshindi, akili, kama mnazo, labda ndo zitawarudia na kutambua kuwa hamkuwa na lenu kwenye huo uchaguzi!

Kama mnabisha, siku ya siku ikifika nitawakumbusha haya maneno yangu. Msije kununa tu.[emoji16]
mkuu nyani, nakuomba uondoe aya ya mwisho kabisa maana hakuna timamu anayeweza kubishana na wewe katika haya uliyoandika!


nadhani kinachotafutwa ni idadi ya wabunge plus ruzuku, maana wabunge kushinda ni rahisi sana hasa mkikomaa!


shida yetu kelele za hitaji la tume huru huwa linaanza mwaka mmoja kabla ya uchaguzi, kitu ambacho kimsingi haisadii!
 
Kuna siku unachangia kama mtu kabisa. Wakati mwingine unajitoaga ufahamu..., Kwa leo umeongea Jambo la maana.

Kwa mtazamo wangu, Sisi wananchi tuna mahitaji yetu mengi saana, siyo tu kuitoa CCM madarakani bhaaaas, yapo mengi Sana. Kwa hiyo basic need siyo kuitoa CCM madarakani Tu.

Kati ya vitu vya hatari tangu dunia iumbwe ni power, yaan mtu akishakuwa nayo hiyo anafanya kila awezalo isitoke kwake, Kama watu walikuwa wanaua watoto wote wa kiume kuzaliwa kisa Tu kaambiwa kuna mfalme atazaliwa, enzi hizo, itakuwa leo Kwa urais? Kwa maana hiyo, sitegemei kutawahi kuwa na mazingira rahisi and fair ya mtu/chama kujishindia Tu dola kirahisi.

Sasa basi, lazima tushiriki uchaguzi, tuambizane Sera, tukosoane kila mmoja anapokesea, tukosane kosane kutoana madarakani...., Chama kilichopo madarakani kiendelee kujirekebisha wananchi wakipende, kikijisahau watu watakuja kuchagua upinzani 80% Kwa 20% itakuwa ngumu kuchakachua.

Note: kuna maeneo ya ubunge na udiwani, upinzani wanatangazwa na the same system, si Kwa kupenda Bali inawabidi kufanya hivyo.

#HapaKaziTu
#NiYeye
 
Nimependa Sana ulivyomuelezea huyu jamaa,inaonesha Ana uelewa mdogo Sana wa mambo
Asante Sana kiongozi.
Una hekima kubwa Sana.
Kwa ujumla WaTz ni wanafki. Na Nyani Ngabu anauwakilisha unafki huo. Kasoro anaziona kwenye katiba na tume , halafu pa kurushia taka ni kwa wapinzani !!! Ajabu na kweli
 
Kwa sasa busara ni kushiriki. Na kisha kukusanya nguvu ya wananchi kuhakikisha Tume ziziso huru zinalazimishwa kuwa huru. Na wakati wote wa kampeni, wagombea wa vyama vya upinzani wapige kampeni kubwa ya kuwaandaa watu katika kuilazimisha Tume isiyo huru iwe huru, katiba inayolinda chama tawala iwasaliti watawala.

Wajati muda mzuri wa kuwaandaa watu kwa hilo kama wakati wa kipindi cha kampeni.

Tunataka CCM wajutie kwa nini waliamua kuingia kwenye uchaguzi kukiwa na Tume isiyiaminika, na katiba mbaya.

Wapinzani siyo wajinga. CCM watajutia ujinga wao wa kuamini watu ni wajinga wakati wote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kususia uchaguzi inaweza kuwa wazo baya kuliko yote,,ili upate tume huru au hata katiba mpya unahitaji jukwaa la "kupambania" huwezi kudai mambo hayo ukiwa sebuleni kwako.Isitoshe "umma" haujaiva kiasi cha kutosha "kuingia barabararani" kudai haki za kijamii.Kwahiyo nilazima kukubali hali hii iendelee kwa mda hadi hapo "umma" utakapokuwa tayari kubadili hali ya mambo.
 
Back
Top Bottom