Tusio na adui wa kudumu tunasimama na Dkt. Slaa

Siwajibiki kumuunga mkono yoyote, lakini nikiona anasimamia ninachoamini sitampinga, na hiyo hainilazimishi kumuamini. Na sina popote ninapopinga anachopigania Slaa kwa sasa, lakini haki yangu ya kutokuwa na imani naye iheshimiwe. Kuna shida kwenye hilo?
 
Mwabukusi Jembe apewe kadi ya CHADEMA kama hana tunamuhitaji sana kuliko Dk Cassava
 
Upo sahihi, wala haujaweka ushahidi ila umebisha ila mimi nakupa usahihi kwamba upo sahihi.
Mtazamo wako kwangu kama nipo wrong just clap for yourself, maana sitakukatalia wala kujaribu ku prove anything.
 
Unapoandika kwamba una ushahidi wa matendo ya Slaa kutokana na aliyowahi kufanya siku zilizopita, huoni kama unajichanganya unapoleta hii dhana yako ya Dr. Slaa kutaka kuanzisha chama kitakachokuwa rafiki wa CCM?

Nijuavyo, huko nyuma hakuwahi kujiunga na chama chochote cha siasa, licha ya kuondoka Chadema, iweje sasa umtilie shaka kwa jambo ambalo hakuwahi kulifanya kabla?
 
Upo sahihi, wala haujaweka ushahidi ila umebisha ila mimi nakupa usahihi kwamba upo sahihi.
Mtazamo wako kwangu kama nipo wrong just clap for yourself, maana sitakukatalia wala kujaribu ku prove anything.
Sijabisha, he who alledges must prove, nimekubana hapo tu kwenye hiyo dhana.
 

Hayupo anayekuwajibisha wala kuwa hata na nia ya kukuaminisha kwenye lolote. Kichwa cha uzi kipo wazi kuliko maelezo:

Tusio na adui wa kudumu tunasimama na Dkt. Slaa

Tunajua CCM na washirika wao wengine kwa umburura wao au kutokujitambua tu wako dhidi yetu.
 
Mwabukusi Jembe apewe kadi ya CHADEMA kama hana tunamuhitaji sana kuliko Dk Cassava

Kazi ni pale akina Mwabukusi wanapokuwa wanaongea lugha moja na akina Slaa.

Ushauri wa bure: Hamia CCM ndugu, huko hawana haja na Slaa au Mwabukusi au wa aina zao au hoja zao.

Hudhani utakuwa na amani zaidi huko?
 
Sijabisha, he who alledges must prove, nimekubana hapo tu kwenye hiyo dhana.
Unazidi kuleta hisia zake, kwa akili yako unavyojipima unajiona kabisa kuwa you anywhere close kuweza kunibana mimi?

Kwa ushauri tu, Msiwe mnakariri misemo bila kujua inatumikaje. Unapotakiwa ku prove ni pale panapokuwepo na upande wa tatu ambao utakua huru ambao kazi yake ni kupima. Sasa kwenye pande mbili unauleta huo msema, nyie watu mnaonekana wa ajabu sana na hiyo misemo ya kizungu. Ndiyo nyie mara ooh, "no research no right to speak", ni full vituko.
 
Ni bora nibaki bila Chama

Ninakazia:

Bravo: Dkt. Slaa, Dkt. Nshala, Mwabukusi, Kamanda Mdude na wa namna hiyo.

Mlipo tupo!

Pole yenu mlio na marafiki na maadui wa kudumu.

Ushauri wa bure: kwa Mwamposa, Lusekelo au Mwaipopo kunaweza kuwafaa zaidi. Siyo huku kwenye ukombozi ambako akili zenu za kushikiwa ni mzigo usiovumilika.
 
Usingeniquote mimi msimamo wangu nilishauweka wazi kuhusu Dokta Cassava
 
Wala tusiparurane wenyewe kwa wenyewe ktk hili. Haya ni maoni ya mtoa mada. Mm nafahamu brazaj, Tindo, denooJ, Kalamu n.k wote ninyi ni wanamageuzi wazuri tu.

Tusisahau Dr. Slaa alipoondoka chadema alisepa na wafuasi wengi. Kuna waliosepa kimoyomoyo lkn kimwili bado wako chadema. Na Kuna walioondoka mazima. Hivyo tunapomjadili Dr. Slaa haya muyaweke kichwani.
 

Usalama wetu katika hili ni huu hapa:

Hatuwezi kuwa na rafiki au adui wa kudumu bali agenda.

Awaye yote akighairi agenda yetu tutamtupia virago. Atakayesema agenda yetu hata kama ni CCM yenyewe, tutakuwa naye.

Tatizo liko wapi hapo?
 
Huo ni mtizamo wako

Huo si mtizamo wangu tu bali ndiyo ulio ukweli:

1. Unakereka na Dr. Slaa.
2. Lucas mwashambwa anakereka na Dr. Slaa
3. CCM wanakereka na Dr. Slaa
4. Watatu hapo juu mko pamoja.

Mtizamo wangu hapo ni upi kama si kuwa huo ndiyo ulio ukweli?
 
Huo si mtizamo wangu tu bali ndiyo ulio ukweli:

1. Unakereka na Dr. Slaa.
2. Lucas mwashambwa anakereka na Dr. Slaa
3. CCM wanakereka na Dr. Slaa
4. Watatu hapo juu mko pamoja.

Mtizamo wangu hapo ni upi kama si kuwa huo ndiyo ulio ukweli?
Naona wacha nilale alamsiki ndugu.
 
Muda wote alipoondoka CDM hasa kipindi cha Magufuli hakuwahi kuguswa na maswahiba ya CDM, hata kwa mambo yaliyokuwa dhahiri. Ni kweli hakujiunga na chama chochote cha siasa, lakini hakuwahi kuongea chochote kuonyesha wapinzani hawatendewi haki hasa CDM, japo aliona dhahiri nini kiliendelea.

Ndio maana nasema sipingi msimamo wake wa sasa, lakini siwajibiki kumuuamini Slaa. Na huu ni msimamo wangu binafsi. Ama nimekosea kwenye hili?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…