Tusipotezeane muda! Ukweli ni kwamba 'Ulidanganywa' na 'Wanafiki' kuhusu Kabudi na Lukuvi, ila sasa 'Unatuzuga' na 'Kujikosha' tu Kwao

Kabudi iliyetolewa matopeni na kuketi pamoja na mtawala kwenye meza kuu,kamwe hawezi kukubali kurudi matopeni bora akale makombo ya kuokota chini ya meza ya malkia mtukufu.
 
Ni kwa sababu hawana elimu , vyeti vya kugaiwa makanisani vitaangamiza nchi
Wala sishangai kwa jibu hilo ila ukweli unaujua kwamba nchi yetu inanyemelewa na ubaguzi wa kiimani. Naomba Mungu atusaidie kama nchi tusifike huko.
 
Michezo ya siasa kwenye uongozi ni sawa na mchezo wa draft.
Kunawaka unalazimika kuiingiza kete ya adui king ili uiue la sivyo inaweza kukuhatarishia mchezo wako baadae.

Tulikua na magufuli mkiristo ,kule kuna mwinyi mwislam.
Tulitegemea akitoka magu huku yule wa kule labda angekava huku au angetafutwa mwislam mwingine kumpokea magu.
Bahat mbaya magu kajiondokea sasa Pende zote zina waislam kuanzia marais , makamu,hadi ma pm.

Sasa hapa je itawezekana kukaa kwenye sura hii kwa miaka 10 au 15?

Hapa wazee wsnaumiza vichwa sasa..!

Tukiangalia kwenye ukristo walioko pembeni tunawaona hawa kina lukuvi inawezekena washachunguzwa kuhisiwa kua na tamaa ya hizo sehemu.hivyo kunatishio kwa baaadae.

Hivyo kwenye mchezo wa draft tunaweka mtego.tunawaingiza kingi na kuziua kabisa.
 
Hivi yeye mwenyewe amekatazwa na nani kuwaza , kuona na kutafakari , hadi muanze kusingizia washauri wake ?

Mtu yuko ccm miaka yote toka utoto wake hadi anazeeka , kishakuwa kiongozi hadi kuwa makamu wa Rais , leo kawa Rais eti anashauriwa vibaya !

Hivi nyinyi mnadhani mtatuona mabwege hadi lini ?
 
Mhhhh! Mkuu umeenda kuanzia kwa father of the nation! Kama kungekuwa na opinion poll ndani ya CCM kabla ya March 17 2021 ya watu 10 bora, sidhani kama bi mkubwa angeingia kwenye 5 bora. Ndio ukweli wa dhahiri. Unachoongelea wewe ni mbeleko au mtu kurushiwa kamba ili aokolewe na kikundi kingine chenye nguvu, lakini yeye mwenyewe hana ubavu. CCM inawenyewe.

Kama alivyosema Generali Ulimwengu, bi mkubwa ni wa Kuja ndani ya CCM. Hana mizizi kama waliyonayo wapinzani wake. Na anajua hivyo. Lakini cha muhimu ni kwamba she was in the right place at the right time na ameukwaa Uraisi. Kwa haiba yake, hawezi kuapply siasa za Machiavelli zinazohalalisha rafu ili ushinde kwenye medani ya siasa. Lakini, ni lazima aimarishe ngome yake ya kisiasa kama anataka uongozi wake uendelee kwa amani. Vinginevyo atajuta. Usicheze na CCM political machine.

Angalia yaliyowakuta Edward Lowasa, Edward Membe na Frederick Sumaye ndipo utakapojua mziki wa CCM. Hao wote hapo juu walikuwa visiki ndani ya CCM. Walianzia Umoja wa Vijana mpaka wakaukwaa u PM, lakini mwisho wao tumeuona. Bi mkubwa hana japo nusu ya haiba ya hao makuhani hapo juu ndani ya Chama chake

Pona yake itategemea jinsi atakavyoboresha maisha ya walala hoi, kukuza uchumi, forming stronger alliance na mwisho kabisa ni kuuma na kupuliza ili watu ndani ya CCM watambue kwamba si wa kuchezewa.

Kwa kutegemea kurushiwa kamba ili uokolewe kila unapopata misukosuko hautafika mbali ndani ya siasa. Na uzuri wa bahati, yeye mwenyewe ameishaliona hilo jambo.
 

I am afraid, hapo hatuna Rais bali tuna kivuli cha Rais!

Angekuwa hakuyasema aliyoyasema siku alipokuwa akimzodoa Speaker Ndugai, ningekuwa sina sababu ya kutoamini kauli yake ya sasa. Siku ile alisema clearly kwamba kuna watu kwenye BW lake hawakuwa na yeye na kwamba angewaondoa ili abaki na wale ambao aliamini walikuwa naye. Kama alivyoahidi, alifanya mabadiliko aliyotaka na sisi hatuna tafisiri nyingine tofauti na kusema Kabudi na Lukuvi ni miongoni mwa wale ambao walilengwa na hayo madai ya kwamba kwenye BW kulikuwa na watu ambao hawakuwa naye!
 
Kwanza hii nchi inaongozwa na mama??Mana anapewa order tu yeye mwenyewe mama aliona watu walivyomuondoa Magufuli so order zote anapata kutoka kwao...Serikali nzima mpaka watoto zao wameshaanza kurudi kwenye vyeo vikubwa vikubwa....hii nchi ina watu wao wanaoingoza mama yupp hapo kama kibendera tu cha fata upepo....
 
Sawa ndugu, Samia anafanya kazi kubwa ya kubomoa hasa swala la ardhi ambazo watu fulani walizihodhi na zikachukuliwa na serikali ya JPM Samia anatakiwa azirudishe kwao na ili kufanikisha hilo ilibid awaondoe waziri, makamu kupandishwa na kubadilisha katibu wa wizara ambaye alikuwa ndiye mtendaji mkuu
Na kwa Kabudi vilevile ni juu ya kutengua na kubadilisha mikataba yote ambayo JPM aliishughulikia kwa manufaa ya nchi sasa Samia anataka kuibadilisha iwe kwa ajili ya manufaa ya mabeberu,,,, Oneni ati mshauri wake ni Tony Blair ex PM wa UK ambaye huku UK watu wanasaini petion avuliwe tuzo aliyopewa na Queen ambapo imechukua miaka takribani 20 kutokana na uhalifu alioufanya wa kuanzisha vita vilivyoua watu zaidi ya milion 10 duniani huko Iraqi, Afghanstan, Syria na Arab revolution ya 2010-2011,,leo ati huyo ndiyo mshauri wa Samia
Samia ana kazi moja pia kubwa ya kuondoa na kufuta legacy ya JPM kwa kuchelewesha miradi aliyoiaanzisha ili apewe sifa yeye akimalizia wakati siyo akili yake wala ya huyo Kikwete anayemuelekeza upuuzi wa kuzuga watz akizani ni wajinga kumbe wanamuona anachofanya,,,Samia atadumu na wajinga watamchagua 2025 kwani wema hawadumu bali wabaya huishi milele
 
Ni mawazo yako ila yana nadharia nyingi, sidhani kama ukiambiwa uthibitishe hayo utaweza. Kwani ha ki Lukuvi hizo nafasi walikua wafe nazo?
 
Na kama kweli alikuwa na kazi nao maalum kwann haukusema siku ya utenguzi badala yake akasubiri maoni ya mitandao.
 
Na kama kweli alikuwa na kazi nao maalum kwann haukusema siku ya utenguzi badala yake akasubiri maoni ya mitandao.
Anahangaika kujadili viongozi mazuzu hapa! Ogopa sana mtu asiyejitambua mwenyewe! Huwa kama mabua yapeperushwayo na upepo huku na kule!
 
Genta unaweza kuzunguka sana, ila chuki zako juu ya Samia hazifichiki, Why unamchukia Madam President?
 
Ni mawazo yako ila yana nadharia nyingi, sidhani kama ukiambiwa uthibitishe hayo utaweza. Kwani ha ki Lukuvi hizo nafasi walikua wafe nazo?
Hivi unahitaji kuthibitisha vitu vinavyoonekana wazi wazi kweli?? Ona RUFIJI DAM ilikuwa ijazwe maji last November leo hii hata sehemu iliyotakiwa kujaza maji haijajengwa kazi iliyotakiwa ifanyike miezi mitatu,, wakaja na porojo za crane crane wakati kazi wamesimamisha na hawaonyeshi maendeleo yake tena kwani hakuna kinachoendelea,, wakati wa JPM TBC walifunga kambi kule kutuonyesha maendeleo deilee,,, leo ati waziri Makamba kaleta kampuni ya kihindi ati iuze umeme na unakatika ile mbaya,,,mtoeni huyo binti hapo nchi isonge siyo kuwateua Ridhiwani na Nape ni kuturudisha nyuma
Kiufupi Samia kawatoa waliokuwa wakichapa kazi kizalendo,, Kalemani, Chamriho, Lukuvi na Kabudi siyo kama wangekaa kwenye hizo wizara mpake wafe hapana,,,mteteeni Samia ila uhalifu anaoufanya mnauona
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…