Tusipotoshane, ajira ina nafuu na uhakika zaidi kuliko kujiajiri

Tusipotoshane, ajira ina nafuu na uhakika zaidi kuliko kujiajiri

Kwani kazini huwezi kufukuzwa
Ni nadra sana, nadra mnoooo!!! Labda uwe mlevi sana, unadokoa sana bila tahadhari, n.k wengi wakikosea sana sana huamishwa vituo cya kazi kushushwa daraja, n.k. Hii ni tofauti na kwenye biashara, upepo wa kisuli suli ukikupata ndio unaweza kuharibu maisha moja kwa moja, ila kwa watu kama wahindi, waarabu, wapemba, wakinga kwa kuwa wanabebana hata upepo ukipiga kidogo kuna kuinuliwa, Sasa unakuta mtu kabila au ukoo wake hawanaga mambo ya kuinuana, huyu akipigwa na upepo lazima aisome namba.
 
Sawa umeajiliwa na mfanya biashara pia! ambaye ndo huyo serikali au mtu Binafsi kama Mo Dewji! Bakhresa nk ! sasa kwa nini wewe usiwe na hamu ya kuwa km yeye??! au mfanye Partiner wako ktk Biashara?

Mfano unaweza gundua pale kazini kwako Boss wako anapata shida ya kupata viroba vya kuhifadhia unga! sasa weye tengeneza viroba vizuri na vya Bei rahisi mpelekee ! anunue! bila yeye kujua kuwa vile viroba vinatoka kwako! au

kuwa juu zaidi yake?! yaani uajili km yeye? ukiajiliwa unaenda kuvumbua Fursa pale! Ilimu, ujuzi, maarifa ya kujiendesha, management style! badala yake unatamani uwe chini yake miaka nenda rudi!! weweeeee!! ungekuwa karibu ningekuzaba kibao!

Siku akifilisika na wewe Dororo!!....... RTC, NMC, TRC Kamata! nk! zooote zile zilikuwa kampuni za serikali lkn siku ziliyumba kiuchumi au zilifilisika mazima wengi humu hamzijui, wewe utaenda wapi? na huna akili ya Biashara? ufe au......

sawa labda weye ni Dr Hospitali ya Serikali huna Biashara siku wakikubana tu! utanyea wapi? kwa mfano watakubana hivi

umeenda shule bila rukhsa!, posho yako inapigwa pin! utasimamia wapi? na biashara huna? yaani kma una kijiwe chako sehemu huko Mabwe, au Namanga, sinza.. wakikupiga pin unawaona Mafara tu! shule unaenda ki ubwete, maisha yanaenda, na unajilipia shule mwenyewe, Ngoma drooo!!

na hao walio kufanyia figisu! wanakuona ndo kwanzaa unaagiza ndinga Mpyaaa! tena sasa kwa jeuri unaenda soma nje kabisaaa!! somea sector nyeti inayo husu afya na kijiwe chako unakisomea pia!! ukirudi unashtua! kwanza part time palee Agakhani!!

kwa sababu tu una Elimu kubwa unaomba sector ya juu wizarani yaani zaidi ya pale walipofikia wale mafara wale ! we ndo unakuwa top Boss wao! inafika mahali wanakunyenyekea unajifanya km huwajui vile! na

usisahau kuimarish kijiwe kwanza ndo kimekuokoa na kitakuokoa! huko masomoni wewe jali sana utaalamu wa kijiwe chako pia km kuongeza mazaga zaga! ya mitumba! kukipendezesha, kiwe na kazi nyingi nzuri pia zaidi!

kama kawa! ukitoka Mzigoni mzee uko kijiweni kwako hakutishi mtu!! tena kwa sababu una Ilimu kubwa unafungua kijiwe nje ya nchi kabisaa kuwamwaga nyaa!! na Mikopo yako Weye unakopea WORLD BANK huko!

Mpaka Unadhamini Taasisi nyingi za ki- Africa, Marais wa nchi husika wanakuita wao ukawekeze kwao km Naniliu yule Mooo! je hapo Boss wako gani atakugusa?? kwanza watakujua tena? ukipita wanajisemea kimoyo!moyo Nyarusare huyooo!!ooooo!!ooooooo!!!oooooooooo!!!
 
Mawazo yako yanaweza kuonekana finyu kwa mtu ambaye ameshaingia kwenye biashara na kufanikiwa pakubwa.

Ni ngumu sana kumshawishi mtoto wa Bhakressa ambaye amekulia kwenye mazingira ya biashara na kuona hizi 500M-1B figures kama mauzo ya kila siku kwamba ajira ya kumlipa million 25 kwa mwezi ni bora kuliko biashara!

Ila ukija kwa mtu ambaye baba yake anaendesha duka ambalo faida zake ni kati ya 9000-12,000 kwa siku ni ngumu sana kumshawishi kuwa biashara ni bora kuliko kulipwa 2.5 millions per each month!

Ajira inategemea unaingalia in which dimensions! Kwa maisha ya sasa na uchumi wetu ulivyodorora mtu anayepata ajira ya kumlipa 3.5-5m ana unafuu mkubwa kuliko wafanyabiashara wengi wadogo wadogo wenye mitaji chini ya million 3!
Umemaliza mkuuu...
 
Nikki wa Pili kazi kaikubali kwa moyo mkunjufu 😅 amna biashara ya kukulipa 6m kila mwezi na kukuwekea mafuta ya gari na bima ya afya 😅
Unasema?! Hivi nyie watu mnaishi wapi? Tokeni ndani ya maboksi hayo. Mshahara wa 6m kila mwezi ni hela ya kubeza biashara? Be serious man! Nilitaka nipite kimya ila uzalendo umenishinda.
 
Unasema?! Hivi nyie watu mnaishi wapi? Tokeni ndani ya maboksi hayo. Mshahara wa 6m kila mwezi ni hela ya kubeza biashara? Be serious man! Nilitaka nipite kimya ila uzalendo umenishinda.
what about the power? its far more superior
 
Hiyo ya kuponda ajira ni sizitaki mbichi hizi tu yaani ni kwa vile bongo ajira hazipo ila zingekuwepo hata hao waliojiajiri wangezikimbilia! Kuna watu wengi tu wana miaka 30 wameajiriwa wanakunja salary zaidi ya 3M monthly jiulize je ni vijana wangapi wa huo umri waliojiajiri wanakunja profit zaidi ya 3M monthly?
Kwahio unafikiri waliojiajiri wengi wamejiajiri kwasababu ya kukosa ajira?! 3m profit per month nayo hela? Pita kariakoo Tafuta unao wajua wakwambie mshiko unaotembea kwenye biashara. Tatizo mnaposema biashara mnaanza kuzungumzia maduka ya Mangi mtaani.
 
Kwahio unafikiri waliojiajiri wengi wamejiajiri kwasababu ya kukosa ajira?! 3m profit per month nayo hela? Pita kariakoo Tafuta unao wajua wakwambie mshiko unaotembea kwenye biashara. Tatizo mnaposema biashara mnaanza kuzungumzia maduka ya Mangi mtaani.
Kariakoo imemezwa na wakinga mkuu, soma paragraph ya mwisho kwenye post, nimewagusia hawa, wapo next level
 
Mtu anaamka kila siku miaka nenda rudi anafungua duka alafajiri mpaka usiku na faida yenyewe haizidi hata elf 30 kwa siku, Ni wapi anapata confidence ya kusema ajira ni utumwa kwa mwenzake anaeiingiza milioni 2 kila mwezi, siku 150 za kupumzika kila mwaka, akiumwa bado anapata mshahara, anaingia kazini saa 2 anatoka saa 11 jioni, kuna posho, n.k, Ni wapi anatoa hii confidence.
Hongera kwa mtazamo wako ila hizo 2m utazikwa nazo? Wanao watarithi mini? Ukifika miaka 60 utapewa mfano 150,000,000 utazifanyia kitu gani?

Kwangu Mimi ajira ni nzuri kama uko narrow minded na unawaza Leo na sio kesho.

Hawa walioko kwenye ajira ndio wakopaji wakubwa kila siku, wengine wanavizia chai za ofisini....sisemi kwa nia mbaya ila kwangu Mimi hakuna ajira inayokupa Uhuru.

Naishia hapa maana Leo tumepigwa vitatu kavu
 
Power ndo mpango mzima 😂 kamata huyo weka ndani, wafanya biashara full kujikomba kwa mwenye power,😂
Wewe Baki kwenye ajira. Pia endelea kujipa moyo uko vizuri Kwa kujilingaanisha na Mangi shop mtaani kwenu. ILA utakapokutana na wenzako ambao mshahara wako wa mwezi wanaingiza siku moja utaelewa kujiajiri sio duka la Mangi tu
 
Kwahio unafikiri waliojiajiri wengi wamejiajiri kwasababu ya kukosa ajira?! 3m profit per month nayo hela? Pita kariakoo Tafuta unao wajua wakwambie mshiko unaotembea kwenye biashara. Tatizo mnaposema biashara mnaanza kuzungumzia maduka ya Mangi mtaani.
Sawa mkuu. Nasi tutajitahidi kidogo kidogo tufike huko.

But as far as i know watu wengi waliofanikiwa kibiashara walianzia kwenye ajira wakapata mitaji mikubwa ya biashara. Na siyo kwamba tunasema eti mtu akae ameajiriwa tu miaka yote no ila kusema kuwa ajira haifai kabisa kwamba eti kila mtu akianzia kwenye biashara ndiyo guarantee ya kutoboa si kweli kwa 100%.
 
Back
Top Bottom