mbingunikwetu
JF-Expert Member
- Feb 17, 2015
- 13,897
- 18,477
Kwa kawaida Serikali huwa imejipanga vizuri sana inapokuwa imetoa kibali cha ajira kwenye utumishi wa umma kuhusu haki na stahiki za waajiliwa wapya. Lakini huwa kuna tatizo kubwa kwa watendaji watekelezaji wa adhima hiyo ya serikali hasa kuhusu eneo la haki na stahiki za waajiriwa wapya.
Mara nyingi watendaji hao hujikita katika kusisitiza wajibu tu wa waajiriwa hawa wapya bila kuwaelimisha pia kuhusa haki na stahiki zao kama waajiriwa wapya kwenye utumishi wa umma.
Ni kwa nadra sana utakuta maafisa utumishi wakiwaelekeza waajiriwa wapya kuhusu haki zao kama vile posho ya kujikimu kwa idadi ya siku zilizobainishwa kwenye miongozo ya serikali, haki ya kupewa fedha kwa ajili ya kusafirisha mizigo kwenye ajira (maana serikali inajuwa kuwa mtu aliyehama toka kwao alikokuwa anaishi na kuhamia kituo chake cha kazi lazima atakuwa na mizigo kama kitanda, nk).
Naomba tuutumie uzi huu:
1. Kuelimishana kuhusu haki na stahiki za waajiriwa wapya kwenye utumishi wa umma.
2. Kuelimishana kuhusu wajibu wa watumishi wa umma.
3. Kupashana uzoefu jinsi wanavyofanyiwa waajiriwa wapya hasa kushusiana na haki na stahiki zao.
Wenye utaalamu na uelewa katika mambo haya tafadhali karibuni sana hapa tujuzane!! Mimi wakati wangu wakati naajiriwa kwa mara ya kwanza (kwa sasa ni msaafu).
Nililipwa posho ya kujikimu siku 14, nililipiwa gharama ya kusafirisha mizigo (personal effects) tani moja na nusu (1,500kg), kwa parcel rate. Nililipiwa nauli first class (nikiwa graduate wa chuo kikuu) na posho ya kujikimu njiani.
Sina uhakika kwa sasa mambo yakoje au circulars/waraka husika wa serikali unasemaje kuhusu stahiki hizo. Japo hata huo wakati wetu kuna watu walikuwa wanapunjwa na kupewa posho ya kujikimu pungufu kwa kisingizio kuwa hakuna pesa, wakati Serikali huwa inafanya maandalizi kama ya kuruhusu ajira (maandalizi hayo ni pamoja na kuandaa posho zao). Karibuni.
Mara nyingi watendaji hao hujikita katika kusisitiza wajibu tu wa waajiriwa hawa wapya bila kuwaelimisha pia kuhusa haki na stahiki zao kama waajiriwa wapya kwenye utumishi wa umma.
Ni kwa nadra sana utakuta maafisa utumishi wakiwaelekeza waajiriwa wapya kuhusu haki zao kama vile posho ya kujikimu kwa idadi ya siku zilizobainishwa kwenye miongozo ya serikali, haki ya kupewa fedha kwa ajili ya kusafirisha mizigo kwenye ajira (maana serikali inajuwa kuwa mtu aliyehama toka kwao alikokuwa anaishi na kuhamia kituo chake cha kazi lazima atakuwa na mizigo kama kitanda, nk).
Naomba tuutumie uzi huu:
1. Kuelimishana kuhusu haki na stahiki za waajiriwa wapya kwenye utumishi wa umma.
2. Kuelimishana kuhusu wajibu wa watumishi wa umma.
3. Kupashana uzoefu jinsi wanavyofanyiwa waajiriwa wapya hasa kushusiana na haki na stahiki zao.
Wenye utaalamu na uelewa katika mambo haya tafadhali karibuni sana hapa tujuzane!! Mimi wakati wangu wakati naajiriwa kwa mara ya kwanza (kwa sasa ni msaafu).
Nililipwa posho ya kujikimu siku 14, nililipiwa gharama ya kusafirisha mizigo (personal effects) tani moja na nusu (1,500kg), kwa parcel rate. Nililipiwa nauli first class (nikiwa graduate wa chuo kikuu) na posho ya kujikimu njiani.
Sina uhakika kwa sasa mambo yakoje au circulars/waraka husika wa serikali unasemaje kuhusu stahiki hizo. Japo hata huo wakati wetu kuna watu walikuwa wanapunjwa na kupewa posho ya kujikimu pungufu kwa kisingizio kuwa hakuna pesa, wakati Serikali huwa inafanya maandalizi kama ya kuruhusu ajira (maandalizi hayo ni pamoja na kuandaa posho zao). Karibuni.