Tuwaelimishe vijana wanaoajiriwa sasa kwenye Utumishi wa Umma kuhusu haki na wajibu wao!

Tuwaelimishe vijana wanaoajiriwa sasa kwenye Utumishi wa Umma kuhusu haki na wajibu wao!

Kiwango cha posho ya kujikimu kilipanda kuanzia July 2022. Kiwango cha chini ambacho kicho waajiriwa wengi huangukia kilipanda toka sh 80,000/= hadi sh 100,000/=. Kwa hiyo stahiki ya mwajiriwa ni kupewa posho ya kujikimu kwa siku 14 kwa kiwango cha sh 100,000/= hivyo jumla ya posho ya kujikimu ni sh 1,400,000/==. Hii haipaswi kuwa na mjadala na inapaswa ilipwe fasta mara baada ya mwajiriwa kupewa barua ya ajira na kujaza mkataba wake wa kazi!!

Dkt. Ndumbaro amesema kutokana na kibali hicho cha Mhe. Rais, posho ya kujikimu ya safari za ndani ya nchi kwa Watumishi wa Umma kwa kiwango cha juu imepanda kutoka shilingi 120,000/= hadi 250,000/= na kiwango cha chini kutoka shilingi 80,000 hadi 100,000/=.

Sitaki nizungumzie sana stahiki ya mizigo kwa ajira ya kwanza, hapa naona maafisa utumishi watanuna sana!!
Nashauri mwajiriwa yeyote wa mara ya kwanza akilipwa posho ya kujikimu pungufu ya siku 14 na kwa kiwango pungufu ya sh 100,000/= kwa siku, tupia hapa wadau wataona jinsi ya kukushauri ili ulipwe stahiki yako!! Kumbuka wapo watumishi wa umma ambao kazi yao ni kuona tiu kuwa hakuna mwajiri au boss anayejifanya mungu mtu kuonea watu!!
 
Kwa kawaida Serikali huwa imejipanga vizuri sana inapokuwa imetoa kibali cha ajira kwenye utumishi wa umma kuhusu haki na stahiki za waajiliwa wapya. Lakini huwa kuna tatizo kubwa kwa watendaji watekelezaji wa adhima hiyo ya serikali hasa kuhusu eneo la haki na stahiki za waajiriwa wapya.

Mara nyingi watendaji hao hujikita katika kusisitiza wajibu tu wa waajiriwa hawa wapya bila kuwaelimisha pia kuhusa haki na stahiki zao kama waajiriwa wapya kwenye utumishi wa umma.

Ni kwa nadra sana utakuta maafisa utumishi wakiwaelekeza waajiriwa wapya kuhusu haki zao kama vile posho ya kujikimu kwa idadi ya siku zilizobainishwa kwenye miongozo ya serikali, haki ya kupewa fedha kwa ajili ya kusafirisha mizigo kwenye ajira (maana serikali inajuwa kuwa mtu aliyehama toka kwao alikokuwa anaishi na kuhamia kituo chake cha kazi lazima atakuwa na mizigo kama kitanda, nk).

Naomba tuutumie uzi huu:
1. Kuelimishana kuhusu haki na stahiki za waajiriwa wapya kwenye utumishi wa umma.
2. Kuelimishana kuhusu wajibu wa watumishi wa umma.
3. Kupashana uzoefu jinsi wanavyofanyiwa waajiriwa wapya hasa kushusiana na haki na stahiki zao.

Wenye utaalamu na uelewa katika mambo haya tafadhali karibuni sana hapa tujuzane!! Mimi wakati wangu wakati naajiriwa kwa mara ya kwanza (kwa sasa ni msaafu).

Nililipwa posho ya kujikimu siku 14, nililipiwa gharama ya kusafirisha mizigo (personal effects) tani moja na nusu (1,500kg), kwa parcel rate. Nililipiwa nauli first class (nikiwa graduate wa chuo kikuu) na posho ya kujikimu njiani.

Sina uhakika kwa sasa mambo yakoje au circulars/waraka husika wa serikali unasemaje kuhusu stahiki hizo. Japo hata huo wakati wetu kuna watu walikuwa wanapunjwa na kupewa posho ya kujikimu pungufu kwa kisingizio kuwa hakuna pesa, wakati Serikali huwa inafanya maandalizi kama ya kuruhusu ajira (maandalizi hayo ni pamoja na kuandaa posho zao). Karibuni.
Kutokana na teknolojia kukua utazijua nyingi hata ambazo waajili walitaka wakufiche usizijue.
 
Kwa kawaida Serikali huwa imejipanga vizuri sana inapokuwa imetoa kibali cha ajira kwenye utumishi wa umma kuhusu haki na stahiki za waajiliwa wapya. Lakini huwa kuna tatizo kubwa kwa watendaji watekelezaji wa adhima hiyo ya serikali hasa kuhusu eneo la haki na stahiki za waajiriwa wapya.

Mara nyingi watendaji hao hujikita katika kusisitiza wajibu tu wa waajiriwa hawa wapya bila kuwaelimisha pia kuhusa haki na stahiki zao kama waajiriwa wapya kwenye utumishi wa umma.

Ni kwa nadra sana utakuta maafisa utumishi wakiwaelekeza waajiriwa wapya kuhusu haki zao kama vile posho ya kujikimu kwa idadi ya siku zilizobainishwa kwenye miongozo ya serikali, haki ya kupewa fedha kwa ajili ya kusafirisha mizigo kwenye ajira (maana serikali inajuwa kuwa mtu aliyehama toka kwao alikokuwa anaishi na kuhamia kituo chake cha kazi lazima atakuwa na mizigo kama kitanda, nk).

Naomba tuutumie uzi huu:
1. Kuelimishana kuhusu haki na stahiki za waajiriwa wapya kwenye utumishi wa umma.
2. Kuelimishana kuhusu wajibu wa watumishi wa umma.
3. Kupashana uzoefu jinsi wanavyofanyiwa waajiriwa wapya hasa kushusiana na haki na stahiki zao.

Wenye utaalamu na uelewa katika mambo haya tafadhali karibuni sana hapa tujuzane!! Mimi wakati wangu wakati naajiriwa kwa mara ya kwanza (kwa sasa ni msaafu).

Nililipwa posho ya kujikimu siku 14, nililipiwa gharama ya kusafirisha mizigo (personal effects) tani moja na nusu (1,500kg), kwa parcel rate. Nililipiwa nauli first class (nikiwa graduate wa chuo kikuu) na posho ya kujikimu njiani.

Sina uhakika kwa sasa mambo yakoje au circulars/waraka husika wa serikali unasemaje kuhusu stahiki hizo. Japo hata huo wakati wetu kuna watu walikuwa wanapunjwa na kupewa posho ya kujikimu pungufu kwa kisingizio kuwa hakuna pesa, wakati Serikali huwa inafanya maandalizi kama ya kuruhusu ajira (maandalizi hayo ni pamoja na kuandaa posho zao). Karibuni.
Mkuu katika mchakato wa menejimenti ya rasilimali watu kuna kitu kinaitwa "orientation stage" na hii ni wakati mfanyakazi mpya katika ajira anapokasimiwa majukumu yake ya kazi kwa mara ya kwanza. Hapa huonyeshwa na wazoefu kuhusu mazingira yake halisi ya kazi kwa vitendo.

Tatizo huanzia kwa wale ambao humuelekeza afanye nini. Endapo hawatamsisitizia kuhusu masuala muhimu ya kuzingatia, mathalani uadilifu, utii wa maadili mema,, uwajibikaji n.k. naye atajikuta akiishi kwa mazoea kama vile ambavyo amewakuta wenyeji wake wakifanya hivyo.
 
Tatizo la wengi huwa ni kwamba kabla hajafanikiwa kupata ajira na hana pesa zimekuwa adimu kwake, mara nyingi hutumia nguvu na muda mwingi sana kupata hata hicho kidogo anachofanikiwa kupata. Tumeshuhudia graduates wengi wakibembeleza kazi hata kwa mshahara wa 200,000/= tu.
Akipata kazi ghafla ataanza kuona mshahara wake ni mdogo sana!! haukidhi kabisa haja na matarajio yake! Hilo huwafanya wasiwe na tija mahali pa kazi. Ushauri: Chapa kazi kwa bidii sana na usitarajie mafanikio ya haraka. Viongozi wako watakuona lakini zaidi sana Mungu atakuona na atakubariki. Mafanikio na kupanda kutakuja tu ukiwa mchapa kazi. Ni kweli miaka ya kuvumilia ni lazima itakuwepo lakini kaza uzi, Mungu ni mwaminifu. Usikubali kabisa njia za mkato kama wizi na ufisadi, huo utakuharibia kabisa maisha yako. Lakini pia jifunze kuweka akiba hata kama ni kidogo!! Kinachoitafutwa hapa ni TABIA ya kujuwekea akiba.
 
Waajiriwa wapya sikieni, kujiwekea akiba ni tabia na siyo kuwa kujiwekea akiba ni kwa sababu ya kipato kikubwa. Tabia hujengwa ili iwe endelevu. Usipojijengea tabia ya kujiwekea akiba wakati una kipato kidogo hutaweza kujiwekea akiba hata kama kipato kitakuwa kikubwa!! Hakikisha kila mwezi unajiwekea akiba hata kama ni sh 5,000/= tu kwa mwezi. Ukifanikiwa hapo utahamasika kujiwekea akiba kubwa kipato kikiongezeka maana tayari ulishajijengea tabia ya kujiwekea akiba!
 
Karibuni wenye uelewa na wazoefu wa mambo ya kazini tuwajenge vizuri waajiriwa wapya kwenye utumishi!!
 
Uaminifu kazini unalipa sana hata kama itachukua muda kuona malipo ya uaminifu wako. Mungu ni mwaminifu lazima utafanikiwa kazini ukiwa mwaminifu, mtiifu na mchapa kazi!! Usijiunge na makundi ya walalamishi!!
 
Government Standing Orders inayotumika hadi sasa ni ile ya mwaka 2009. Kinachobadilika mara kwa mara ni kiwango cha subsistance allowance/posho ya kujikimu lakini utaratibu na idadi ya siku anazostahili kulipwa mwajiriwa kwa mara ya kwanza zimebaki kuwa siku 14. Hii ni kwa mujibu wa standing order section L.6.

L.6 Subsistence Allowance on arrival on first appointment:
A public servant on arrival on first appointment within Tanzania shall be paid subsistence allowance on the journey from his home or place of engagement to his duty station; and for the first 14 days at his duty station.

Hii iko wazi kabisa! Lakini utakuta kuna maafisa utumishi wengine wanakuambia jaza siku tatu tu maana hakuna fedha, au anakuambia hata mimi nililipwa siku tatu tu. Cha msingi hapa mwajiriwa mpya hahitaji kujadiliana na afisa utumishi ila anahitaji kuandika barua tu ya kuomba hiyo posho ya kujikimu kwa siku 14 halafu unaikabidhi barua masjala ianze kutembea hadi kwa mtendaji mkuu wa ofisi. WAkikujibu kwa mdomo tofauti na malipo ya siku 14 unawaambia wakujibu kwa maandishi. Hapo hawatothubutu kukujibun kwa maandishi kama walipanga kukupunja, vinginevyo watakuwa hawajitaki!!
Mkuu kama una pdf ya Standing Order nitumie.
 
Ukisoma standing order utashangaa sana. Wakubwa hujinufaisha sana kwa kuitumia hii standing order, lakini kwa wengine kwa kiasi kikubwa huwa haitekelezwi. Kwa mfano mwajiriwa wa kwanza ambaye huanzia TGS D anapaswa alipwe pesa ya mizigo tani 5 wakati anaripoti kituoni kwake kwa mara ya kwanza. Mtoto wa mkubwa atafanyiwa hivyo kihalali kabisa lakini kwa wengine haiingii akilini kuwa unaweza kulipwa pesa za mizigo tani tano wakati wa kuajiriwa. Japo wakati wa kustaafu huwa wanalipwa.
 
Haya ndiyo masaibu na matatizo wanayokutana waajiriwa wapya: Mtu anapewa barua ya uthibitisho kutoka sekretarieti ya ajira kuwa amefaulu usaili na kupangiwa kituo cha kazi. Barua inamtaka aripoti kwa mwajiri wake ndani ya siku 14 toka kupokea barua hiyo. Hii inatoa picha kuwa mwajiriwa akisharipoti kwa mwajiri wake basi tangu hapo atakuwa mikononi mwa mwajiri huyo. Lakini nhaiko hivyo!!!

Niwape mfano hai: Mwajiriwa mpya anasafiri toka Dar hadi dodoma kufuata barua yake ya kupangiwa kituo. Amepangiwa kuripoti Halmashauri mojawapo ya mkoa wa Tabora. Kijana fasta akaenda kuripoti. Alipofika huko akapokelewa na kuonesha vyeti vyake original na kuambiwa " Subiri tutakapokuwa tumejiridhisha na usahihi wa vyeti vyako tutakupigia simu ili uje upewe sasa barua ya ajira"!! Hakurudishiwa nauli aliyotumia kusafiri toka Dar hadi Tabora, hakupewa pesa yoyote ya kumsaidia kujikimu maana bado hajaajiriwa rasmi kwa maana ya kupewa barua ya ajira! Kwa kuwa kijana hana namna ya kuishi tabora wakati anasubiria kupigiwa simu ili kuitwa kazini na mwajiri wake, akalazimika arudi tena nyumbani Dar!! Hao ndio miungu watu wanavyosumbua waajiriwa wapya!

Sasa najiuliza, wakati wa usaili aliwasilisha vyeti vyake halisi vikahakikiwa tena mara mbili maana usaili upo mara mbili! Kwa kuchaguliwa kwake maana yake sekretarieti ya ajira imejiridhisha na vipengele vyote ikiwemo uhalali wa vyeti vyake! Kwa nini usumbufu wote huo!! Kwa nini mwajiri asigharimie malazi na chakula cha huyu mwajiriwa mpya wakati wanafanya mchakato wa kujiridhisha maana ni wao walimwita tena kwa kitisho cha kuripoti ndani ya siku 14 vinginevyo atapoteza nafasi yake!!

Kuna mwingine ameripoti hivi majuzi kwenye manispaa mojawapo ya jiji la Dar es salaam. Naye amerudishwa nyumbani asubiri kuitwa tena kwa simu na hakupewa pesa yoyote! Je huo ndio utaratibu uliokubalika rasmi?
 
Nashauri mwajiriwa yeyote wa mara ya kwanza akilipwa posho ya kujikimu pungufu ya siku 14 na kwa kiwango pungufu ya sh 100,000/= kwa siku, tupia hapa wadau wataona jinsi ya kukushauri ili ulipwe stahiki yako!! Kumbuka wapo watumishi wa umma ambao kazi yao ni kuona tiu kuwa hakuna mwajiri au boss anayejifanya mungu mtu kuonea watu!!
Duhhh! Mimi mwaka wa 6 huu sijalipwa hata mia. Nilidai hadi nikachoka
 
Kuna maafisa utumishi wengine usiombe!! bUtafikiri pesa anayolulipa anaitoa mfukoni mwake wakati kuna bajeti kabisa kwa ajili ya waajiriwa wapya. Jamani acheni nyongo!!
Kuna watu wana roho mbaya ajabu!
 
Wadau naomba msahada Kwa hili jamani,sisi tumepewa laki tatu tu ela ya kujikimu,tumeripoti kazini Mwezi wa 01/09/2023.leo ndo tumelipwa Tena laki tatu jamani ndugu zangu tusaidie I kama Utumishi upo ivi ,hali hii siyo nzuri Kwa waajiriwa, hapa bariadi dc ndo ela tuliopokea Leo,Kwa Mwenye kutusemea juu ,maana hatuna hata namba za viongozi tusaidieni.tumesaini milioni alafu unapewa laki tatu kweli inauma Tena sana.naomba msahada
 
Back
Top Bottom