Kiwango cha posho ya kujikimu kilipanda kuanzia July 2022. Kiwango cha chini ambacho kicho waajiriwa wengi huangukia kilipanda toka sh 80,000/= hadi sh 100,000/=. Kwa hiyo stahiki ya mwajiriwa ni kupewa posho ya kujikimu kwa siku 14 kwa kiwango cha sh 100,000/= hivyo jumla ya posho ya kujikimu ni sh 1,400,000/==. Hii haipaswi kuwa na mjadala na inapaswa ilipwe fasta mara baada ya mwajiriwa kupewa barua ya ajira na kujaza mkataba wake wa kazi!!
Dkt. Ndumbaro amesema kutokana na kibali hicho cha Mhe. Rais, posho ya kujikimu ya safari za ndani ya nchi kwa Watumishi wa Umma kwa kiwango cha juu imepanda kutoka shilingi 120,000/= hadi 250,000/= na kiwango cha chini kutoka shilingi 80,000 hadi 100,000/=.
Sitaki nizungumzie sana stahiki ya mizigo kwa ajira ya kwanza, hapa naona maafisa utumishi watanuna sana!!