umekurupuka.Umedanganya... Hujui vita ya ghuba ilikuaje. Lini Saddam Hussein aliwashinda Usa? Kuna uongo mwingine watu wanakugundua kirahisi tu.
umekurupuka.
tuliza akili, soma post kwa utulivu, digest kile ambacho umekisoma halafu changia maoni yako.
karibu tena ndg.
Haturuhusu uongohauna ulichokerekebisha kwenye uzi huu.
onyesha uongo.
Aisee... Kumbe ndo huyu mwamba.... Dadeki... Pedeshee haswaaakuna rhumba moja kali sana ya madilu system inaitwa vice versa.
ktk verse ya kwanza ya track hiyo, madilu anataja jina la Teodoro Obiang Nguema. huyu ni mtoto wa rais wa equatorial guinea, mzee Teodoro Obiang Nguema Mbasogo.
Teodoro au maarufu teddynguema kama anavyofahamika kwenye social media, kwa sasa ni makamu wa rais wa taifa hilo.
maisha anayoishi huyu teddy yanaakisi kwa kiwango kikubwa maisha halisi ya kipedeshee, ana pesa nyingi sana za kula bata.
anasafari maeneo mbalimbali duniani ktk kujipa raha na huwa hafichi kitu, picha zake za kula bata huwa anaziweka kwenye kurasa zake za social media.
baba yake yupo ktk orodha ya marais ambao wapo madarakani kwa mda mrefu duniani. yeye na baba yake wanaitawala equatorial guinea kwa mkono wa chuma kweli kweli.
View attachment 2279163View attachment 2279164View attachment 2279165View attachment 2279168
Hahahahaaa.. Mkuu!Nipo naisikiliza nyimbo hiyo, madilu kaua sana humo
Aisee.... Kama ndiye aliyenunua ile glove, basi jamaa ana ukwasi usiopimika...Nilisikia huyu mwamba mali zake zimekamatwa na serikali ya Marekani pamoja na Ufaransa na pia ni kama yupo kizuizini huko Ufaransa,huyu mwamba ndiye amasemekana alinunua ile glove maarufu yenye vimulimuli vya dhahabu aliyokuwa anaivaa Wacko Jacko.
Sawa Mkurugenzi...manuele samuele ni jina la mtu, madilu alilitumia kama title kwenye wimbo wake. binafsi sina information kuhusu profile yake
Ila hii ngoma FM Academia walitulia sana.... Wazee wa Bring Bring... Wazee wa Funika Bovu...Hatari sana mkuu, dunia kigeugeu hilooo....Jose Mara alitisha sana humo
hakika madilu aliuwa sana humu. rhumba moja tamu sana.Hahahahaaa.. Mkuu!
Emmanuele Sammuele... Bonge la songi....
Kuna mtu kama jina hili alinipigia simu siku chache zilizopita na akajitambulisha kwa jina hilo na akasema kama yupo Tanga na itakuwa yeye ananifahamu sema mie bado sijamkumbuka (Maongezi yetu ilikuwa ni kusaidia kusukuma gurudumu la maendeleo) hapo wakubwa mtakuwa mmeelewaHuyu abdalah nyumba nyingi,yeye alikua na mishe gani
aliyekupigia simu na kujitambulisha kwa hilo jina atakuwa amefanya hivyo ili kumu idolise the original Abdallah Nyumba Nyingi ambaye kwa sasa ni marehemu. alifariki miaka kadhaa iliyopita.Kuna mtu kama jina hili alinipigia simu siku chache zilizopita na akajitambulisha kwa jina hilo na akasema kama yupo Tanga na itakuwa yeye ananifahamu sema mie bado sijamkumbuka (Maongezi yetu ilikuwa ni kusaidia kusukuma gurudumu la maendeleo) hapo wakubwa mtakuwa mmeelewa
Naikumbuka hii kampuni ya Malai napokuja mjini ndo Mzee mwenyewe alikuwa ameisha fariki wapo wale wadogo zake ndo wanaiendesha nilipata kuwa karibu na baadhi ya staffs wa hapo nawajua baadhi wa miaka hiyo ambao wengine walikuwa wacheza basketball kuna wale kina Abeid alikuwa sana airport kuna kina mbaga,Otto,Mashele,mwamboma,Efreim,Mzee malay nlifanya kazi kwake
Za kutumwa hapa na pale upande wa dokomaa....enzi hzo nlikuwa dogo nasoma natafuta pesa
Umenikumbusha aise,alikuwa smart sana ila kuna wakat fulani nlimuona
Alikuwa tofauti nlijisikia vibaya sana
Ova
Nashukuru sana kwa kunifahamisha maana mtu kanipigia simu anajitambulisha kwa jina hilo na anasema yupo Tanga ni siku chache tu zimepita,nafikiri huyu alipachikwa jina hilo la huyo muhusika OG ,RIPhuyo aliyekupigia simu na kujitambulisha kwa hilo jina atakuwa amefanya hivyo ili kumu idolise the original Abdallah Nyumba Nyingi ambaye kwa sasa ni marehemu. alifariki miaka kadhaa iliyopita.
jina lake lilikuwa linaimbwa na bendi ya wana tamtam chini ya mwinyijuma muiminin na band ya twanga pepeta chini ya ally choki.
Abdallah Nyumba Nyingi alikuwa ni mtoto wa mjini aliyekulia mitaa ya temeke na pia alikuwa mtu wa karibu sana na marehemu Meddy Mpakanjia.
nakumbuka nilihudhuria sherehe ya harusi yake iliyofanyika ktk ukumbi wa chuo cha IFM mjini posta, hiyo ilikuwa mwanzoni miaka ya 2000.
sherehe ilifana sana, ukumbini alikuwepo meddy mpakanjia na rafiki zake. kipindi hicho meddy yupo kwenye ubora wake, pesa anayo halafu ana date na binti maarufu wakati huo, marehemu amina chifupa.
kwa sasa wote ni marehemu. may their souls continue to rest in peace.
[emoji1431][emoji1431][emoji1431][emoji1431]Nashukuru sana kwa kunifahamisha maana mtu kanipigia simu anajitambulisha kwa jina hilo na anasema yupo Tanga ni siku chache tu zimepita,nafikiri huyu alipachikwa jina hilo la huyo muhusika OG ,RIP
Naikumbuka hii kampuni ya Malai napokuja mjini ndo Mzee mwenyewe alikuwa ameisha fariki wapo wale wadogo zake ndo wanaiendesha nilipata kuwa karibu na baadhi ya staffs wa hapo nawajua baadhi wa miaka hiyo ambao wengine walikuwa wacheza basketball kuna wale kina Abeid alikuwa sana airport kuna kina mbaga,Otto,Mashele,mwamboma,Efreim,
Mie nikiwa bwana mdogo tu nafundishwa fundishwa mambo ya C&f na jamaa zangu nimetoka kwetu unyamwezini tukiwa kijiwe chetu hapo kwenye hilo jengo lililokuwa linauza vyombo sijui jina Hosco House ,Samora Ave , hapo ni shift tu natumwa tumwa kwenda 'Long room' mara kukagua gari/containers bandarini na kurudi kujibanza hapo 'Hosco House' ndo kuna mihuri ya kugonga ya C&F na kampuni ilikuwa ya mzee wa Kichaga Mzee Mushi jamaa zangu wanakamata kazi lkn mihuri tunatumia ya huyo Mzee ,nae kajaza vijana wake toka Moshi, kina Basil,Frank,Peter Kipara NK
Vijana wa Clearing & Forwarding walipata pesa sana miaka hiyo ya 90+ , namkumbuka kijana mmoja wa kinondoni alikuwa maarufu sana hapo 'long room' anaitwa Ally Kilinda RIP kama sijakosea jina na girlfriend wake Fatuma RIP bila kumsahau Swetu Fundikira RIP na akiniona lazima aniulizie salamu za jamaa zake wa unyamwezini kina Adam
Nakumbuka pia na ushamba wangu huu kuna mzee wangu alitoka nje ya nchi akaja na simu (Alcatel) ya hizi chip/simcard za siku hizi hapo kabla ilikuwa bado hazijaanza kutumika nchini lkn ndo kipindi tunakaribia kutoka analogue kuja digital, mzee wangu akaniambia nikauze hiyo simu nilikuwa nawajua jua vijana baadhi pale Azam kama yule half caste muhindi na muhaya kama sikosei anaitwa Rajesh ndo walikuwa wana zungusha hapo vijiwe vya Azam na vijana wa mjini wengine kina Ukwaju,Dan,Joel,Kinje (siyo yule maarufu zaidi huyu ni ndugu yao alikuwa sana hapo Azam miaka hiyo) dah kweli miaka imeenda
Sema namshukuru Mungu mie nilitaka kuwa maisha yangu yawe ya kawaida 'low key' toka kitambo japokuwa ningetaka kuwa tofauti labda na kuwa hata na ka jina jina hapa mjini fursa zilikuwepo lkn haikuwa kipaumbele changu na hasa kujua wapi nilipotoka na kubwa toka kijana mdogo nilianza kuheshimu kitu kinachoitwa 'Karma' kwa kila ulitendalo ndo utavuna/utalipwa , naingia utu uzima kwa amani tele naomba na mwisho wangu uwe wa amani
Sorry kwa mtoa mada nimeweka yasiyo husiana na mada haha