Tuwafahamu Watu Maarufu waliokuwa wanatajwa sana na Wanamuziki wa Band nchini Tanzania

Tuwafahamu Watu Maarufu waliokuwa wanatajwa sana na Wanamuziki wa Band nchini Tanzania

Awali ya yote nitangulize angalizo kwa vijana ambao maturity stage imewakuta miaka hii ya mitandao ya kijamii. Itabidi msome kimyakimya huku mkiwa mmeshika peni na karatasi kuchukua notes.

Huu uzi ni wa sisi ma-seniors, maudhui yake yatagusa zaidi vijana wenzangu ambao maturity liwakuta kuanzia late 90s to early 2000s.

Mwaka 2002 mpaka 2012, mziki wa dansi ulikuwa upo kwenye prime time.

Kwa uchache tu, band zilizotamba ni FM Academia, Akudo Impact, Twanga Pepeta na Diamond Musica. Zingine zilikuwa zinaibuka na kupotea ndani ya muda mfupi.

Umaarufu wa hizi band ulienda sambamba na trend ya wanamuziki kutaja majina ya baadhi ya watu kwenye mashairi yao.

Majina ya hawa watu yalivuma na kuwa maarufu kuliko sura zao kwasababu miaka ile kulikuwa hakuna social platform za ku-share picha na video kama ilivyo hivi sasa.

Kutokana na kujichanganya kwangu ukijumlisha na ujanja wangu wa kimjini mjini wa miaka ile, nilifanikiwa kufahamiana na baadhi mapedeshee au wazee wa mujini ambao majina yao yalikuwa yanatajwa kwenye mziki wa dansi.

Nitataja ninaowakumbuka na wewe ongeza wa kwako.

Naandika majina yao kama yalivyokuwa yanatamkwa kwa mbwembwe na wanamuziki.

Kwa mfano kama mtu alikuwa anaitwa John, wanamuziki walikuwa wanatamka papaa John Young Millionaire Muzee ya ma-Range Rover[emoji3][emoji3].

Haya twende kazi:
Pedeshee Mychoice na kati ya Mbeya
:
huyu sijui alikuwa anapiga mishe gani huko Mbeya, watu wa Mbeya mtatusaidia.

Braza K na kati ya Tunduma:
Watu wa Tunduma mtatusaidia kutujuza kuhusu huyu jamaa, alivuma sana.

Mamaa Rukia Soloon:
Huyu bibie namfahamu, ana saloon yake ya kike mitaa ya Mikocheni barabara ya Rose Garden. Those days she was very pretty, kwa sasa utu uzima umemchukua.

Mamaa Dotnata Decoration:
Bila shaka wengi mnamkumbuka, aliwahi kuwa muigizaji maarufu kupitia ITV, baadae akaingia kwenye ujasiriamali wa kutoa huduma za decoration and catering. shughuli hizi zilimpatia mafanikio sana. sijui kwa sasa yupo wapi huyu mama. FM Academia waliwahi kumtungia wimbo wenye jina lake.

Mamaa Juddy Moshi:
Alikuwa mmiliki wa band ya Daimond Musica kwa financial support ya mshua mmoja ambaye alikuwa ni MD wa Yellow Pages, watu wa zamani wanaelewa. Juddy alikuwa mrembo si kitoto, kwa sasa umri wake umesonga mbele.

Pedeshee Akayesu Ndama Mutoto ya Ng'ombe:
Sina haja ya kumuelezea, ni mtu maarufu wa nyakati zote. Wajanja wa mujini watamuelezea zaidi. Jina lake lilitajwa sana kwenye nyimbo za dansi zilizovuma.

Young Millionaire Bill gate Muzamir Katunzi:
Christian Bella aliwahi kutunga mpaka wimbo wenye jina hilohilo la Muzamir Katunzi. I don't know him personally, but it's told he was financially successful.

Papaa Msofe Chuma cha Reli hakishiki Kutu.
Sina haja ya kuandika mengi kuhusu umaarufu wa Papaa Msofe. Itoshe tu kusema jina lake liliimbwa sana halafu ni wachache waliokuwa wanajua sura yake. Walianza kuiona kwenye media alipokuwa anahudhuria viunga vya mahakama kujibu kesi yake.

Papaa Martin Kasianju.
Ni marehemu kwa sasa, huyu mshua ndio alikuwa mmiliki wa Band ya FM Academia. Nilikuwa namfahamu personally. licha ya kwamba alikuwa ni mjasiriamali na muajirwa Serikalini, pia alikuwa ni Senior Officer wa Idara ya Usalama wa Taifa.

Andrew Traders na Kariakoo Big Supply: Jamaa alikuwa ni mfanyabiashara wa kuuza tairi za gari Mtaa wa Agrey Kariakoo huku akipiga michongo yake ya "general supply". Watu wa mujini wa zamani wanaelewa vizuri maana ya kampuni kusajiliwa kwa jina la general supply. Katika biashara ya kuuza tairi, alishirikiana na kaka yake, ila yeye akawa maarufu zaidi na akaaminika na wadau.

Kinje Mutoto wa Mujini:
Najua wengi mnamfahamu na zile deal zake alizokuwa anapiga. sina haja ya kumuelezea zaidi.

Pedeshee David Kabunga:
Sifahamu alikuwa ni nani, jina lake lilikuwa linatajwa sana.

Papaa Ally Kileo:
He was a prominent lawyer in town, jina lake lilikuwa linatajwa sana kwenye nyimbo za dansi.

Papaa Mutarika Mzee wa Mambo mengi:
Binafsi simfahamu, wajanja wa mujini wa zamani watajazia nyama kumuelezea.

Chef Justice Rugaibura:
Binafsi simfahamu, wajanja wa mujini wa miaka ile watajazia nyama kumuelezea.

Chief Kiumbe le Big Boss:
Anafahamika vizuri, jina lake lilitajwa na kuimbwa sana na wanamuziki wa band. wajanja wa zamani wa mujini watajazia nyama kumuelezea

Papaa Amos Makalla mzee wa Mvomero, Babaa na Gabriele:
Kwa sasa ni RC wa Dar, jina lake lilianza kuvuma kitambo sana kabla hata hajaingia kwenye siasa.

Fikiri Madinda Mukuu wa kazi: Anafahamika vizuri, wajanja wa zamani wa mujini watajazia nyama kumuelezea

Pedeshee Abdul Mkeketa:
Huyu wakati fulani aliwahi kuwa mbunge ktk Mkoa wa Morogoro, sikumbuki ni jimbo gani. kwa sasa ni marehemu.

Charles Mutawali Muzee ya Magari.
Binafsi simfahamu, wajanja wa zamani wa mujini watajazia nyama kumuelezea.

Saidi Mukuu wa lumumba:
Jamaa alikuwa dalali wa kuuza magari pande za Lumumba.

Meddy Kitendawili....?
Ben Mulokozi....?
Salim Chicago Matelefone...?
Kizaizai....?
Omary Tolu...?
Abduli Tolu...?
Joshua Limited...?
Muddy Nyamalonda mzee wa Pamba...?
China wa China...?
Shaibu Mapajero....?
Moris Mariaga Rais wa Sinza...?
Nteze wa Nteze....?
John Nzenze....?
Papaa Madenge....?
Muddy Nyambi....?
Jimmy Chokolete....?


Note of Appreciation
.
sikujua kama huu uzi ungewavutia watu wengi kiasi hiki. niwashukuru wote mnaoufatilia na mnaochangia maoni yenu. asanteni sana wadau.[emoji1431][emoji1431][emoji1431][emoji1431]
Daaah,kipindi cha Magu walipoteana hao hakukuwa na kutajana tena 🤣🤣🤣

Kila mtu alipambania hali yake hakuna cha papaa msofe, wala papaa nani 🤣🤣🤣
 
Naikumbuka hii kampuni ya Malai napokuja mjini ndo Mzee mwenyewe alikuwa ameisha fariki wapo wale wadogo zake ndo wanaiendesha nilipata kuwa karibu na baadhi ya staffs wa hapo nawajua baadhi wa miaka hiyo ambao wengine walikuwa wacheza basketball kuna wale kina Abeid alikuwa sana airport kuna kina mbaga,Otto,Mashele,mwamboma,Efreim,

Mie nikiwa bwana mdogo tu nafundishwa fundishwa mambo ya C&f na jamaa zangu nimetoka kwetu unyamwezini tukiwa kijiwe chetu hapo kwenye hilo jengo lililokuwa linauza vyombo sijui jina Hosco House ,Samora Ave , hapo ni shift tu natumwa tumwa kwenda 'Long room' mara kukagua gari/containers bandarini na kurudi kujibanza hapo 'Hosco House' ndo kuna mihuri ya kugonga ya C&F na kampuni ilikuwa ya mzee wa Kichaga Mzee Mushi jamaa zangu wanakamata kazi lkn mihuri tunatumia ya huyo Mzee ,nae kajaza vijana wake toka Moshi, kina Basil,Frank,Peter Kipara NK

Vijana wa Clearing & Forwarding walipata pesa sana miaka hiyo ya 90+ , namkumbuka kijana mmoja wa kinondoni alikuwa maarufu sana hapo 'long room' anaitwa Ally Kilinda RIP kama sijakosea jina na girlfriend wake Fatuma RIP bila kumsahau Swetu Fundikira RIP na akiniona lazima aniulizie salamu za jamaa zake wa unyamwezini kina Adam

Nakumbuka pia na ushamba wangu huu kuna mzee wangu alitoka nje ya nchi akaja na simu (Alcatel) ya hizi chip/simcard za siku hizi hapo kabla ilikuwa bado hazijaanza kutumika nchini lkn ndo kipindi tunakaribia kutoka analogue kuja digital, mzee wangu akaniambia nikauze hiyo simu nilikuwa nawajua jua vijana baadhi pale Azam kama yule half caste muhindi na muhaya kama sikosei anaitwa Rajesh ndo walikuwa wana zungusha hapo vijiwe vya Azam na vijana wa mjini wengine kina Ukwaju,Dan,Joel,Kinje (siyo yule maarufu zaidi huyu ni ndugu yao alikuwa sana hapo Azam miaka hiyo) dah kweli miaka imeenda

Sema namshukuru Mungu mie nilitaka kuwa maisha yangu yawe ya kawaida 'low key' toka kitambo japokuwa ningetaka kuwa tofauti labda na kuwa hata na ka jina jina hapa mjini fursa zilikuwepo lkn haikuwa kipaumbele changu na hasa kujua wapi nilipotoka na kubwa toka kijana mdogo nilianza kuheshimu kitu kinachoitwa 'Karma' kwa kila ulitendalo ndo utavuna/utalipwa , naingia utu uzima kwa amani tele naomba na mwisho wangu uwe wa amani

Sorry kwa mtoa mada nimeweka yasiyo husiana na mada haha
wee jamaa takuwa nakufahamu hio miaka na hao watu uliowataja karibu wote nawafamu, hivi mzee Mushi yupo?? ulivyomtaja Swetu Fundikira-rip ukamsahau na aliemfundisha kazi ya C&F jamaa akiitwa Charles Sanga - rip. wakati huo long room tunaondoka na mifuko ya rambo imejaa pesa zingine tunapitia kitumbini kwa mzee Zakaria-rip. Wakati huo Kinondoni inawaka moto haswaa haswa hapo kwa manyanya na PR Camp. maisha hayaaaa...
 
umetema madini ya zamani sana. mimesoma kwa utulivu mno huku niki recall mitkasi yetu ya azam take away.

nimewakumbuka mabroo wa wakati ule na viofisi vyao vya kupiga mishe za ujanja-ujanja nyuma ya club billcanas(siku hizi mitaa ya jengo la Rita).kule nyuma kulikuwa na vijiofisi vingi vya wapigaji.

huyo Ukwaju uliyemtaja kwenye post yako ndio yule jamaa mmoja hivi mfupi mnene kiasi aliyekuwa shabiki mkubwa wa kilimanjaro band(wana njenje)?.
Kijiwe cha azam kuna jamaa mmoja akiitwa Peter alikua sana pale na kina Amani, huyu Peter alikua mwajiriwa wa bima halafu akapigwa redanduncy akawa mission town hapo kijiweni. ulevi wake ulikua pale kontena opposite na soko la ma TX. kitambo sana hio.
 
wee jamaa takuwa nakufahamu hio miaka na hao watu uliowataja karibu wote nawafamu, hivi mzee Mushi yupo?? ulivyomtaja Swetu Fundikira-rip ukamsahau na aliemfundisha kazi ya C&F jamaa akiitwa Charles Sanga - rip. wakati huo long room tunaondoka na mifuko ya rambo imejaa pesa zingine tunapitia kitumbini kwa mzee Zakaria-rip. Wakati huo Kinondoni inawaka moto haswaa haswa hapo kwa manyanya na PR Camp. maisha hayaaaa...
Charles sanga alifariki nakumbuka tulikuwa tunapiga mvinyo hapo kwa ashura macheni,usiku mnene
Kama pumzi ikambana....
Ila mpaka naondoka hapo Charles nlimuacha...badaye nasikia jamaa ntolee
Office yake ilikuwaga nyuma ya shule ya forodhani pale

Ova
 
wee jamaa takuwa nakufahamu hio miaka na hao watu uliowataja karibu wote nawafamu, hivi mzee Mushi yupo?? ulivyomtaja Swetu Fundikira-rip ukamsahau na aliemfundisha kazi ya C&F jamaa akiitwa Charles Sanga - rip. wakati huo long room tunaondoka na mifuko ya rambo imejaa pesa zingine tunapitia kitumbini kwa mzee Zakaria-rip. Wakati huo Kinondoni inawaka moto haswaa haswa hapo kwa manyanya na PR Camp. maisha hayaaaa...
Alikuwepo omary urembo naye clearing agent,ma clearing wengi walikuwa wazushi wazushi tu
Ila omary urembo naye alivuta miaka kama 7, hv nyuma

Ova
 
Kijiwe cha azam kuna jamaa mmoja akiitwa Peter alikua sana pale na kina Amani, huyu Peter alikua mwajiriwa wa bima halafu akapigwa redanduncy akawa mission town hapo kijiweni. ulevi wake ulikua pale kontena opposite na soko la ma TX. kitambo sana hio.
Kontena pale kwa mama propser
Kilikuwa kijiwe haswa...
Support asubuhi watu wote wanajaa opposite na kinondoni makaburini
Watu wanapiga supu wanaenda mzigoni

Ova
 
Naikumbuka hii kampuni ya Malai napokuja mjini ndo Mzee mwenyewe alikuwa ameisha fariki wapo wale wadogo zake ndo wanaiendesha nilipata kuwa karibu na baadhi ya staffs wa hapo nawajua baadhi wa miaka hiyo ambao wengine walikuwa wacheza basketball kuna wale kina Abeid alikuwa sana airport kuna kina mbaga,Otto,Mashele,mwamboma,Efreim,

Mie nikiwa bwana mdogo tu nafundishwa fundishwa mambo ya C&f na jamaa zangu nimetoka kwetu unyamwezini tukiwa kijiwe chetu hapo kwenye hilo jengo lililokuwa linauza vyombo sijui jina Hosco House ,Samora Ave , hapo ni shift tu natumwa tumwa kwenda 'Long room' mara kukagua gari/containers bandarini na kurudi kujibanza hapo 'Hosco House' ndo kuna mihuri ya kugonga ya C&F na kampuni ilikuwa ya mzee wa Kichaga Mzee Mushi jamaa zangu wanakamata kazi lkn mihuri tunatumia ya huyo Mzee ,nae kajaza vijana wake toka Moshi, kina Basil,Frank,Peter Kipara NK

Vijana wa Clearing & Forwarding walipata pesa sana miaka hiyo ya 90+ , namkumbuka kijana mmoja wa kinondoni alikuwa maarufu sana hapo 'long room' anaitwa Ally Kilinda RIP kama sijakosea jina na girlfriend wake Fatuma RIP bila kumsahau Swetu Fundikira RIP na akiniona lazima aniulizie salamu za jamaa zake wa unyamwezini kina Adam

Nakumbuka pia na ushamba wangu huu kuna mzee wangu alitoka nje ya nchi akaja na simu (Alcatel) ya hizi chip/simcard za siku hizi hapo kabla ilikuwa bado hazijaanza kutumika nchini lkn ndo kipindi tunakaribia kutoka analogue kuja digital, mzee wangu akaniambia nikauze hiyo simu nilikuwa nawajua jua vijana baadhi pale Azam kama yule half caste muhindi na muhaya kama sikosei anaitwa Rajesh ndo walikuwa wana zungusha hapo vijiwe vya Azam na vijana wa mjini wengine kina Ukwaju,Dan,Joel,Kinje (siyo yule maarufu zaidi huyu ni ndugu yao alikuwa sana hapo Azam miaka hiyo) dah kweli miaka imeenda

Sema namshukuru Mungu mie nilitaka kuwa maisha yangu yawe ya kawaida 'low key' toka kitambo japokuwa ningetaka kuwa tofauti labda na kuwa hata na ka jina jina hapa mjini fursa zilikuwepo lkn haikuwa kipaumbele changu na hasa kujua wapi nilipotoka na kubwa toka kijana mdogo nilianza kuheshimu kitu kinachoitwa 'Karma' kwa kila ulitendalo ndo utavuna/utalipwa , naingia utu uzima kwa amani tele naomba na mwisho wangu uwe wa amani

Sorry kwa mtoa mada nimeweka yasiyo husiana na mada haha
Dah wakina kilinda nawajua wote
Familia yao pia nko nayo karibu tu
Nimeishi pia mitaa ya kule kwao sana

Yah,malay alikuwa na office kubwa na wakat ule watu walipiga hela maana mteja hajui chochote kilichopo kwenye system,anakadiria malipo tu na agent....
Malay vijana wengi enzi hizo aliwaingiza kazini,jamaa hakuwa mchoyo wa kutoa fursa
Sema wakat ule sisi ule utoto,ujana sana ulitusumbua wengine maana kutulia ilikuwa 0

Ova
 
Manka mushi alikuwa ni shabiki tu wa mziki wa dansi. alitokea kuupenda mziki kiasi kila band zilipokuwa zinatuambuiza kwenye kumbi za dar, yeye alikuwa anahudhuria. na alikuwa anaingia bure kwasababu tayari alishakuwa mdau.

Hii ikamfanya kuwa karibu na baadhi ya wanamuziki hususani Mwinyjuma muumini wakati ule akiwa na tamtam band.
Tam tam band ilimtaja Papa Alex Massawe A.M
 
Alikuwepo omary urembo naye clearing agent,ma clearing wengi walikuwa wazushi wazushi tu
Ila omary urembo naye alivuta miaka kama 7, hv nyuma

Ova
Daaah na wewe takua nakujua maana hio mitaa ya kinondoni ndio ilikua yetu enzi, Omary Urembo nafikiri ndio yule tulikua tukimuita Omari kichwa nasikia na yeye alivuta pia, Sanga nae story yake nilisikia hivyo hivyo ulivosema. Mie nilivoona bongo miyeyusho mpunga niliovuta long room nikaona nitambae kwa Joe Biden mpaka leo nikija huko ni vacation tu week 2/3 narudi zangu. bongo ya sasa imejaa waturutumbi wengi haisomeki.Huyo Peter ndio simsikii kabisa. Kinondoni ilikua motoooo.
 
Daaah na wewe takua nakujua maana hio mitaa ya kinondoni ndio ilikua yetu enzi, Omary Urembo nafikiri ndio yule tulikua tukimuita Omari kichwa nasikia na yeye alivuta pia, Sanga nae story yake nilisikia hivyo hivyo ulivosema. Mie nilivoona bongo miyeyusho mpunga niliovuta long room nikaona nitambae kwa Joe Biden mpaka leo nikija huko ni vacation tu week 2/3 narudi zangu. bongo ya sasa imejaa waturutumbi wengi haisomeki.Huyo Peter ndio simsikii kabisa. Kinondoni ilikua motoooo.
Hahaha kinondoni ilikuwa moto
Sema si haba angalau wengine tumeacha legacy tu [emoji1]
Makazi ya kudumu +nlihamia madale
Ila bado kinondoni nai respect maana
Ilitujengaaa sana,kutupa uthubutu

Yah omary urembo alivuta alienda kenya huko akaugua gafla, alikuwa mtu wa kamali sana na starehe
Ukimpa kazi lazima kuwe na maneno maneno kalenda nyingi...
Ile kutokuwa mwaminifu inakuaribia soko mwisho wa siku wateja wote wanakukimbia
Ma clearing wengi walikuwa wanavimba na hela za wateja wao tu
Huo ndy ukweli
Ndomana miaka ilivyokuwa inaenda wakaingia watu wa kazi kweli kwenye field hyo na kuwaulia soko lao

Ova
 
Ruge na kusaga walishiriki kikamilifu kuua mziki wa dansi tena kwa fitina za wazi, kama mradi wa kujiongezea kipato kibwanyenye.
Ruge alitoka USA na maono hayo.
Mziki ni kama chakula, unawalisha watu unachotaka tu hadi wanaamin ndo kitamu.
Pia kuliibuka saikolojia ya mziki mfupi dk 4 ndo upigwe radio na tv wakat kwa dansi unaua utam wote.
Pia gharama za kuendesha dansi kwa faida zikawa juu kuliko bongo fleva, ikampa standing point mfitini wa dansi.
Umarekan na uniga wa akina sugu, na prof j, nature, sele n.k nao ukachukua hatam.
Lakin ukiachilia mbali suala la gharama bado dansi ndo mziki kabsa kabsa kwa walio wengi. Bas tu, tunalishwa tunachopikiwa bila menu!
Ndo maana likipigwa sebene hata nikki wa pili atajitingisha tu!
Exactly [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
John Cheyo ni wa masaki Dar, nyumbani kwake si mbali sana na ubalozi wa South Africa au sea cliff apartments, huko Bariadi makolo wake alikuwa akiwatumia tu kupata ubunge, hadi Magu wameshawahi kumpa Ubunge, ana mdogo wake anaitwa Isaack Cheyo pia alikuwa anapewa ubunge wa Bariadi Magharibi naye ni mtu wa Dar maskani yake Kinyerezi tulikuwa tuna kijiwe chetu enzi hizo tunapiga lager za kutosha.
Ubalozi wa south uko mjini Kati kabisa sheikh,sio masaki
 
Back
Top Bottom