Tuwafahamu Watu Maarufu waliokuwa wanatajwa sana na Wanamuziki wa Band nchini Tanzania

Yamkini na wewe ulikuwa mmoja wa watajwa !!!!!!!!!!!!!!!!😀 which is no bad at ll.
hapana ndg yangu, mimi kipindi hicho watu kama akina msofe wana run the town, sikuwa na umaarufu wowote.

nilikuwa bado chalii "nikijitafuta". ktk safari yangu ya kujitafuta nilikuwa mtu wa kujichanganya sana, nikajikuta nawafahamu baadhi ya wajanja wa town wa miaka hiyo.

alhamdulillah baada ya kujitafuta kwa mda mrefu, sasa "nimejipata" na maisha yanasonga.
 
Enzi hizo msofe yuko pande za salamnda Ana deal na pport za bandika bandua [emoji1]
Aise watu wanatoka mbali

Ova
 
kiukweli mitaa yetu ya katikati ya jiji imepoa siku hizi.

last weekend nilipita mitaa ya samora, mkwepu,makunganya na azikiwe, kulikuwa na utulivu usio wa kawaida mpaka nikaingiwa na unyonge.

nikawa navuta hisia zile pilikapilika za vijana wa zamani walivyokuwa wanakumbizana huku na kule kukamilisha michongo yao.

nikapita kwenye maskani ya azam take away pale round about, napo nikakuta pamepoa sana.
 
Siku hizi mambo ya mitandao wasap n.k kukutana mara chache
Sisi tuko wadogo tunaskia hizo vitu tuu na hao watu
hii mitandao japo inafaida ila imekuja na hasara zake. moja wapo ni "kuleta utengano".

mfano siku hizi unaweza kupanga miadi na rafiki zako mkutane jioni sehemu flani kupata kinywaji na kula nyama choma.

halafu mkikutana mnasilimiana, baada ya hapo hakuna story, ukimya unatawala, kila mtu anahamia kwenye simu yake.

zamani marafiki mkikutana kweye starehe ilikuwa ni full kupiga story, kufurahi na kukumbushana mambo mbalimbali.
 
Yule polisi koba kimanga wa Central tulikuwa tunamchangamsha kweri kweri,maana haipiti siku bila kuletewa misala yetu [emoji1] Town hapo
Kuna wakati watu waliasafiri mjini kukapoa koba,akawa anazimiss pilika
Pilika
Mara ya mwisho kuonana naye nakumbuka nlimpelekea zawadi za gloves za ngumi maana alikuwa anapenda sana ngumi....na alikuwa anacheza....
Akaomba sparing nkamchomeleaaa
[emoji1]

Ova
 
Koba KIMANGA sio KABANDA[emoji28][emoji28]
 
[emoji23] [emoji23]
 
Ila wakati huo kulikua na ule Ukimwi grade one ay Juliana. Bora hizi zama zetu za Arv
ukimwi wa miaka ile usikie tu kwenye story watu wakisimuliana.

mwaka 1997 nilishuhudia anko wangu(RIP) akipigania uhai wake kutokana na maradhi ya huo ugonjwa. mwili wake ulijaa vipele vikubwa mithiri ya majipu.

alikonda sana, ilifika wakati chumba alichokuwa analala kilikuwa kinatoa harufu mbaya unaweza sema ndani kuna mzoga.
 
Mkuu @ Smarte, nimeona nyuzi online yule jamaa umemtaja sana kwenye huu uzi ambae amemuoa aliekua mke wa JB Mpiana, akiitwa Vital Karmehe kateuliwa na rais Tshisekedi kua waziri wa uchumi .Naona hapo JB ndio hawezi hata kumgusa tena huyo ex wake.

Vital Kamerhe, ni mwanasiasa mwenye influence kubwa congo mashariki hususani mji wa bukavu.

ni kweli jina lake huwa linatajwa sana na wanamuziki wa congo. sio koffi, fally, ferre, jb mpiana nk, wote hao hawawezi kukwepa kuimba jina la huyo jamaa.

majuzi nikiwa nasikiliza taarifa ya habari kupitia idhaa ya kiswahili ya DW, wafuasi wake kule bukavu walikuwa wanalalamika kutoridhishwa na nafasi ya uwaziri wa uchumi ambayo ameteuliwa hivi karibuni.

wanadai rais tshisekedi alipaswa kumpa nafasi ya juu zaidi.
 
YOU ARE SMART INDEED!!!!!!!!! Ujue unaweza kuwa unajichanganya na watu maarufu kama hao na ukatumia hiyo fursa vizuri UKATUSUA !!!!!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…