Tuwafahamu Watu Maarufu waliokuwa wanatajwa sana na Wanamuziki wa Band nchini Tanzania

Tuwafahamu Watu Maarufu waliokuwa wanatajwa sana na Wanamuziki wa Band nchini Tanzania

Acha ubishi mzee mwenyeji wa Arusha wote hakuna asie mjua Hidaya tena alikua maarufu kwa jina la Hidaya Wa pepe kale kafariki mwaka jana , Hidaya ni miongon mwa wanawake matajiri wa Arusha enzi hizo, ameishi pia congo na amezaa na pepe kale wala hiyo siyo siri na ninavyo kueleza kafariki mwaka jana elewa hivyo
Alafu mi nazungumzia wimbo wa pepe kale Hidaya hiyo ya kwako ya Hedaya mimi siijui
Ni neno moja tu Hidaya na hedaya. Labda tusaidie huyo mtoto amezaa naye mwaka gani ili upewe full kisa ndipo ujue wabongo wanajua kuchangamkia fursa. Sikatai kwamba huyo Hidaya wa Pepe Kale kama mnavyomuita alikuwepo, ila kilichoimbwa kwenye wimbo sio Hidaya mwanamke. Ila wabongo kwa kuchangamkia fursa mko vizuri. Stori ndefu kidogo na muda hautoshi.
 
Kuna yule fundi wa makabureta haha
Naye alikuwa anapaishwa

Ova
Nadhan Hussein makabureta unamsema alianzia magomen wasanii walikuwa wanapeleka magar yao kwake enz hizo kutokana na kaz yake na kupenda ukitonga kwa wasanii wakaanza kumrusha kwenye nyimbo zao

Kuna car wash maarufu pale sinza kwa jina la MAN CITY CAR WASH Napo wasanii Kama akina Christian Bella huenda kuosha magari yao hapo Kuna wimbo kaitaja car wash hi i nadhan ule wimbo wa Rudi
 
umenikumbusha late 90s nimemaliza O-Level, nipo home idol nasubiri majibu yatoke. mshua akanitafutia temporary job mitaa ya mjini posta kwenye ofisi ya rafiki yake.

ofisi ilikuwa mtaa wa jamhuri jirani na ile round about ambayo inakutanisha india street na mkwepu street, almaarufu mitaa ya azam take away.

ilikuwa kila ikifika mida ya saa tatu mpaka saa nne asubuhi, lile eneo walikuwa wanatokea mabroo smart kwelikweli kimuonekano. mkononi wamebeba vi-diary.

walikuwa wanavaa mashati nadhifu, surauli za kadeti na viatu safi vya ngozi. kwa ujumla walikuwa wanapendeza sana, mimi mwenyewe nilikuwa nawa admire.

siku moja nikamuuliza broo mmoja ambaye tulikuwa tunafanya kazi pale, kwamba hawa jamaa ni akina nani,mbona mda mwingi wanautumia kakaa kwenye vijiwe vya shoe shiners, hawana kazi ya kufanya?.

akanijibu ukisikia mission town ndio hao, na hapo kwenye vijiwe vya shoeshiners ndio sehemu zao za kupanga mipango na kupeana deals mbalimbali.

akaniambia kile kipande chote cha mtaa wa mkwepu kinachokatiza club ya billicanas mpaka kule kwenye maungio ya samora avenue, ni territory ya ma-mission town.

hata papaa msofe alianza kujifunzia upigaji mitaa hiyo.
Papa msofe alikuwa sana salamander samora,alianzaga enzi zile za bandika
Bandua port
Hi michezo vijana wengi enzi zile walifanya na connection zote zilikuwa zinatoka kwa wafanyakazi wa hizo taasisi..kama tra,uhamiaji,ttcl nk
Wao ndy walikuwa wanawaletea watoto wa mjini wafanye alafu wao wanakula mgao....wao

Ova
 
Ni neno moja tu Hidaya na hedaya. Labda tusaidie huyo mtoto amezaa naye mwaka gani ili upewe full kisa ndipo ujue wabongo wanajua kuchangamkia fursa. Sikatai kwamba huyo Hidaya wa Pepe Kale kama mnavyomuita alikuwepo, ila kilichoimbwa kwenye wimbo sio Hidaya mwanamke. Ila wabongo kwa kuchangamkia fursa mko vizuri. Stori ndefu kidogo na muda hautoshi.
 
Ni neno moja tu Hidaya na hedaya. Labda tusaidie huyo mtoto amezaa naye mwaka gani ili upewe full kisa ndipo ujue wabongo wanajua kuchangamkia fursa. Sikatai kwamba huyo Hidaya wa Pepe Kale kama mnavyomuita alikuwepo, ila kilichoimbwa kwenye wimbo sio Hidaya mwanamke. Ila wabongo kwa kuchangamkia fursa mko vizuri. Stori ndefu kidogo na muda hautoshi.
 
Ni neno moja tu Hidaya na hedaya. Labda tusaidie huyo mtoto amezaa naye mwaka gani ili upewe full kisa ndipo ujue wabongo wanajua kuchangamkia fursa. Sikatai kwamba huyo Hidaya wa Pepe Kale kama mnavyomuita alikuwepo, ila kilichoimbwa kwenye wimbo sio Hidaya mwanamke. Ila wabongo kwa kuchangamkia fursa mko vizuri. Stori ndefu kidogo na muda hautoshi.
Soma huo uzi jamaa amekuquote hapo juu utamjua vizuri huyo Hidaya
 
Huu uzi mwandishi atakuwa na IQ nzuri.

Hapa jf unatakiwa upewe hata mji kama ile mitaa ya nape.


Papaa Mutarika Mzee wa Mambo mengi:

Huyu brother wa umri wa akina papaa msofe.

Ni wa tunduma alikuwa mwajiriwa wa tra na mke wake fundi cherehani.

Upapaa wake ni kama uliisha baada ya ajira ile kukomeshwa, umaarufu ulimponza.

Uzi mzuri sana huu.
Yupo masasi choka mbaya
 
Zamani mziki ulikuwa zamu kwa zamu, Kuna muda Taarabu ilishika Kasi balaa, Kuna muda miduara ilibamba kinoma, Kuna wakati bongofleva zilikamata kisawasawa, Kuna muda muziki wa dansi asili ya Kongo ulikamata nchi nzima, Ila Kuna kipindi muziki wa dansi wa msondo na sikinde ilishika nchi ikatikisika Sana, Hasa kipindi kile msondo waliposhusha Kilio Cha mtu mzima utunzi wake John Jambele msondo ulikuwa Moto Sana. Chenja alitajwa Sana msondo Hadi wakamuimbia wimbo. Zamani ulikuwa balaa na nusu
Ni kweli mkuu, miaka ya 90 na mwanzo wa miaka ya 2000 muziki wa Congo ulisumbua sana. Shukrani za pekee ni kwa Mulumba Kashama na bendi yake kipindi hicho akighani "mwenge mwenge daladala shilingi mia... " na kibinda nkoi yake, iliwaamsha akina Banza stone na Ali Choki (kisa cha mpemba) kuja na muziki wa dansi wa kizazi kipya.
Nao Clouds Fm wakaifufua taarabu iliyo kuwa imezimia... Kwa mbaali unakasikia kakionjo ka Onyango "wewe mambo iko huku... " huku kamsemo ka "taarabu imo humo?" kakivuma kuchagiza utamu wa taarabu.
Nashindwa kuisahau siku niliyo tembea kwa mguu kutoka Msasani club hadi Temeke mwisho, huku tukiimba wimbo wa Profesa Jay,kwa mara ya kwanza amepafomu pale beach, muandaaji Taji Liundi.
Miaka imeenda sana.
 
awali ya yote nitangulize angalizo kwa vijana ambao maturity stage imewakuta miaka hii ya mitandao ya kijamii. itabidi msome kimya kimya huku mkiwa mmeshika peni na karatasi kuchukua notes.

huu uzi ni wa sisi ma-seniors, maudhui yake yatagusa zaidi vijana wenzangu ambao maturity liwakuta kuanzia late 90s to early 2000s.

mwaka 2002 mpaka 2012, mziki wa dansi ulikuwa upo kwenye prime time.

kwa uchache tu, band zilizotamba ni fm academia, akudo impact, twanga pepeta na diamond musica. zingine zilikuwa zinaibuka na kupotea ndani ya muda mfupi.

umuarufu wa hizi band ulienda sambamba na trend ya wanamuziki kutaja majina ya baadhi ya watu kwenye mashairi yao.

majina ya hawa watu yalivuma na kuwa maarufu kuliko sura zao kwasababu miaka ile kulikuwa hakuna social platform za ku-share picha na video kama ilivyo hivi sasa.

kutokana na kujichanganya kwangu ukijumlisha na ujanja wangu wa kimjini mjini wa miaka ile, nilifanikiwa kufahamiana na baadhi mapedeshee au wazee wa mujini ambao majina yao yalikuwa yanatajwa kwenye mziki wa dansi.

nitataja ninaowakumbuka na wewe ongeza wa kwako.

naandika majina yao kama yalivyokuwa yanatamkwa kwa mbwembwe na wanamuziki.
kwa mfano kama mtu alikuwa anaitwa John, wanamuziki walikuwa wanatamka papaa john young millionaire muzee ya range rover[emoji3][emoji3].

haya twende kazi:
Pedeshee Mychoisi na Mbeya
:
huyu sijui alikuwa anapiga mishe gani huko mbeya, watu wa mbeya mtatusaidia.

Braza K na Tunduma:
watu wa tunduma mtatusaidia kutujuza kuhusu huyu jamaa, alivuma sana.

Mamaa Rukia Soloon:
huyu bibie namfahamu, ana saloon yake ya kike mitaa ya mikocheni barabara ya rose garden. those days she was very pretty. kwa sasa utu uzima umemchukua.

Mamaa Dotnana:
bila shaka wengi mnamkumbuka, aliwahi kuwa muigizaji maarufu kupitia ITV. baadae akaingia kwenye ujasiriamali wa kutoa huduma za catering. shughuli hizi zilimpatia mafanikio sana.sijui kwa sasa yupo wapi huyu mama. fm academia waliwahi kumtungia wimbo wenye jina lake.

Mamaa Juddy Moshi:
alikuwa mmiliki wa band ya daimond musica kwa kuwezeshwa na mshua mmoja ambaye alikuwa ni MD wa Yellow Pages. watu wa zamani wanaelewa. juddy alikuwa mrembo si kitoto. kwa sasa umri wake umesonga mbele.

Pedeshee Akayesu Ndama Mutoto ya Ng'ombe:
sina haja ya kumuelezea , ni mtu maarufu wa nyakati zote. wajanja wa mujini watamuelezea zaidi. jina lake lilitajwa sana kwenye nyimbo za dansi zilizovuma.

Young Millionaire Billgate Muzamil Katunzi:
Christian bella aliwahi kutunga mpaka wimbo wenye jina hilohilo la muzamir katunzi. i don't know him personally, but it's told he was financially very successful.

Papaa Msofe Chuma cha Reli hakishiki Kutu.
sina haja ya kuandika mengi kuhusu umaarufu wa papaa msofe. itoshe tu kusema jina lake liliimbwa sana. halafu ni wachache waliokuwa wanajua sura yake. walianza kuiona kwenye media alipokuwa anahudhuria viunga vya mahakama kujibu kesi yake.

Papaa Martin Kasianju.
ni marehemu kwa sasa. huyu mshua ndio alikuwa mmiliki wa Band ya Fm Academia. nilikuwa namfahamu personally.licha ya kwamba alikuwa ni mjasiriamali na muajirwa serikalini, pia alikuwa ni Senior Officer ktk Idara ya Usalama wa Taifa.

Andrew Traders na Kariakoo Big Supply: jamaa alikuwa ni mfanyabiashara wa kuuza tairi mpya za gari mtaa wa agrey kariakoo huku akipiga michongo yake ya "general supply". watu wa mujini wa zamani wanaelewa vizuri maana ya kampuni kusajiriwa kwa jina la general supply. ktk biashara ya kuuza tairi, alishirikiana na kaka yake, ila yeye akawa maarufu zaidi na akaaminika na wadau.

Kinje Mutoto wa Mujini:
najua wengi mnamfahamu na zile deal zake alizokuwa anapiga. sina haja ya kumuelezea zaidi.

pedeshee David Kabunga:
sifahamu alikuwa ni nani. jina lake lilikuwa linatajwa sana.

Papaa Ali Kileo:
he was a prominent lawyer in town, jina lake lilikuwa linatajwa sana kwenye nyimbo za dansi.

Papaa Mutarika Mzee wa Mambo mengi:
binafsi simfahamu, wajanja wa mujini wa zamani watajazia nyama kumuelezea.

Chef Justice Rugaibura:
binafsi simfahamu, wajanja wa mujini wa miaka ile watajazia nyama kumuelezea.

Chief Kiumbe Big Boss:
anafahamika vizuri. jina lake lilitajwa na kuimbwa sana na wanamuziki wa band. wajanja wa zamani wa mujini watajazia nyama kumuelezea

Papaa Amos Makalla mzee wa Mvomero:
kwa sasa ni RC wa dar. jina lake lilianza kuvuma kitambo sana kabla hata hajaingia kwenye siasa.

Fikiri Madinda Mukuu wa kazi: anafahamika vizuri, wajanja wa wa zamani wa mujini watajazia nyama kumuelezea

Pedeshee Abdul Mkeketa:
huyu wakati fulani aliwahi kuwa mbunge ktk mkoa wa morogoro. sikumbuki ni jimbo gani. kwa sasa ni marehemu.

Charles Mutawali Muzee ya Magari.
binafsi simfahamu, wajanja wa zamani wa mujini watajazia nyama kumuelezea.

Saidi Mukuu wa lumumba:
jamaa alikuwa dalali wa kuuza magari pande za lumumba.

Meddy Kitendawili....?
Ben Mulokozi....?
Salim Chicago Matelefone...?
Kizaizai....?
Omary Tolu...?
Abduli Tolu...?
Joshua Limited...?
Muddy Nyamalonda mzee wa Pamba Kali...
?
China wa China...?
Shaibu Mapajero....?
Moris Mariaga Rais wa Sinza...?
Ntenze wa Ntenze....?
Hawa wote waliimbwa na akina Nyoshi, Patcho Mwamba, Bela baada ya kutupiwa buku 10 wanapokuwa stejini si unajua njaa za wakongoman ,na wote hao waliotajwa wengi wao walikuwa matapeli enzi za mzee wa Msoga, huyu Ali Kileo alikuwa mwajiriwa wa uhamiaji na ndie alikuwa msemaji wa idara ya uhamiaji nadhani alipigwa chini baada ya kulewa sifa na kuwa na ukwasi ambao haukuwa unalingana na ajira yake.
 
Enzi hizo hawa ndo walishika pesa za kufadhili mtandao... Amos alikua ukipiga simu moja tu umejaa. Now umri umeenda tu...bado yupo njema.
Bado kijana sana ila noti zilimtembelea haraka. Salome alikuwa nyodo sana pia
 
kulikua na wadau wengine sio mapedeshee lakini walipaishwa sana.

Chesco mzee wa matunda.
mama Mingoi.
Meja matunda.
Hassan Miundombinu R.I.P.
Swetu Fundikila R.I.P.
daladala camp.

mrangi ngoja niwa tag wakali wa donta.


mziki wa dansi ulikuwa na mambo matatu

kwanza kulikuwa na mapedeshee hawa watuzaji
ndio hao aliowataja mtoa mada

halafu kulikuwa na mashabiki damu
kama hapo unemtaja
MAMA MINGOI CHESCO MAZEE WA MATUNDA kuna pia Kina MANKA MUSHI
ambao ndo waliikuwa navijiwe vyao au CAMP zao
karanga camp
HOME ALONE
VINGUNGUTI TIMBERLAND
DALADALA CAMP
SWAZI INTER
n CAMP nyingine nyingi sana
ambazo hizo CAMP zina mashabiki haswa na mapedeshee wajanjawajanja ndo zilikiwa maskani zao na watoto wa mjini na wakati mwingine hata wanamuziki wenyewe pia huweka vijiwe katika hizo CAMP
hizo CAMP kulikuwa na mashabiki WAZARENDO
nakumbuka kuna SHABIKI MMOJA wa VINGUNGUTI TIMBERLAND huyo Mdau alikuwa anaipenda sana TWANGA kiasi alikuwa mpk anapanda NDEGE kuifuata TWANGA ikiwa NJE ya MKOA haswa ARUSHA au MWANZA

halafu kundi Jingine sasa ni la wanaofanikisha BENDI kuwa na Mziki bora

mfano HUSSEIN MIUNDOMBINU
huyu alikuwa fundi mitambo(umeme)
Twanga popote itakapopiga huyu alikuwa anahakikisha mambo yote ya umeme yako sawa mziki unatoka vizuri

THABITI MTOTO ILALA huyu alikuwa mkali wa kucheza na Keyboad

lakini pia kulikuwa na mkali mwingine wa KEYBOAD
ukisikia PROFESHENARI TARIBONARI VIctor mkambi huyu mkali wa KEYBOAD hata kama akifa inapaswa TWANGA wamjengee Sanamu lake maana alikuwa PROFESHENO haswa kaipaisha sana twanaga na UFUNDI wake wa KEYBOAD


Ukisikia MCD basi hapo anatajwa SUDI MOHAMED TIMBO(marehemu)
huyu alikuwa mpiga tumba matata sana

halafu ukisikia SHAKASHAKA SHAKUZURU hapa alikuwa anapaishwa MIRAJI SHAKASHIA huyu ni mpiga gitaa matata sana

halafu kulikuwa kulikuwa na mkung'uta DRUM hatari sana BABA DIANA BABAA SHARIFA BABAA ZAITUNI basi alikuuwa anatwaja ABUU SEMHANDO mpiga DRUM hatari

sasa utakuj kugundua kulikuwa na makundi matatu yalikuwa yanatwaja sana kwenye nyimbo ndio hao mapedeshee
wngine walikuwa mashabiki damu wa dansi
wengine ndio hao wenyewe wa wanamuziki
 
Wakati Mustahiki Meya wa Jiji Allan Mulumba Kashama anatuchezesha Dar es salaam kibinda nkoyi ndani ya Silent in Mwenge ulikuwa darasa la ngapi?

Unamjuwa Joseph Rwegasira?
Mzee wa Rwegasira alikuwa muumini wa Mlima wa Moto baada ya ikibinda nkoi kufa kifo cha mende, unawakumbuka akina Jesus Ibonga, binti wa Lovy Longomba akitwa jinala stage Sungura, Elyston Angai na wengineo wengi,Mwenge ilikuwa inasimama ikfika Jumamosi.
 
Back
Top Bottom