Tuwafahamu Watu Maarufu waliokuwa wanatajwa sana na Wanamuziki wa Band nchini Tanzania

Tuwafahamu Watu Maarufu waliokuwa wanatajwa sana na Wanamuziki wa Band nchini Tanzania

Hahahaha umenikumbusha enzi za best angu Amos Makalla enzi hizo mweka hazina wa CCM!!

Makalla ana bahati ya kuzaliwa niishie hapo!!
Tofauti na watu wa kuja wanaomuona Makalla kama mtu wa kuja ,Makalla ni mtoto wa mujini kwelikweli namlinganisha tu na akina Borntown, mtu ukitamba vitongoji vya Mwanayamala basi wewe kidume. Kama wewe ni kijana wa jiji mpenda strehe wa miaka ile na humjui Makalla basi utakuwa ulikuwa unakuja jijini likizo na kufikia kwa kaka au mjomba
 
Kasema wapi? Jiulize kama huyo Hidaya alikuwa Arusha why kwenye wimbo amtafute iwapo alimuona Moro au Arusha, au Mwanza. Ilitengenezwa tu na wabongo.
tulisema huu uzi sio wa watoto wa 2000 tueleweke

KABASELE YAMPANYA aliahidi kuitungia NYIMBO YANGA akirudi CONGO
sasa kipindi anazungumza hayo maneno wewe ulikuwa na miaka mingapi
 
Young millionaire alikua DJ mzuri sana pale Kinondoni kwenye ukumbi wa Lang'ata social hall akisaidizana na Chriss Phabby,

Kama ni huyo ndio kaongelewa hapo.
Sio huyo Young Milionea DJ Lusungu yupo Mwanza miaka mingi kuna wakati alikuwa na studio ya kuuza kanda ,alwatani pale Mwanza,huyu Young Milionea mwingine ni Nshomile Muzamir Katunzi, alikuwa na kaka zake wawili mapacha wa kufanana na mmoja kesha tangulia mbele za haki,hawa mapacha walipata pesa nyingi sana miaka ile kupitia mambo ya kutoa mizigo bandarini, wao walikuwa kama GSM ta miaka ile.
 
Tofauti na watu wa kuja wanaomuona Makalla kama mtu wa kuja ,Makalla ni mtoto wa mujini kwelikweli namlinganisha tu na akina Borntown, mtu ukitamba vitongoji vya Mwanayamala basi wewe kidume. Kama wewe ni kijana wa jiji mpenda strehe wa miaka ile na humjui Makalla basi utakuwa ulikuwa unakuja jijini likizo na kufikia kwa kaka au mjomba
Haswaa umemqliza... nimekumbuka enzi za silentinn kwa Rwega...

Siku hizi tusioijua kidimbwi tunaambiwa wa kuja 😂😂
 
Mdogo wao mapacha kato na Kakuru ila huyu ni wa Juzi tu
Hao mapacha mmoja alishafariki na walikuwa na pesa kwelikweli,huyu mdogo wao alikuwa mjinga mjinga tu lakini nae akaja kuwa mjanja akapata pesa nyingi za utapeli, kwa siku hizi sijui kaishia wapi, matapeli wengi walisjamili enzi za Born town,lakini alipoingia Jiwe wengi wao waliishia lupango ma dili za bandarini au madini zikaisha
 
mziki wa dansi ulikuwa na mambo matatu

kwanza kulikuwa na mapedeshee hawa watuzaji
ndio hao aliowataja mtoa mada

halafu kulikuwa na mashabiki damu
kama hapo unemtaja
MAMA MINGOI CHESCO MAZEE WA MATUNDA kuna pia Kina MANKA MUSHI
ambao ndo waliikuwa navijiwe vyao au CAMP zao
karanga camp
HOME ALONE
VINGUNGUTI TIMBERLAND
DALADALA CAMP
SWAZI INTER
n CAMP nyingine nyingi sana
ambazo hizo CAMP zina mashabiki haswa na mapedeshee wajanjawajanja ndo zilikiwa maskani zao na watoto wa mjini na wakati mwingine hata wanamuziki wenyewe pia huweka vijiwe katika hizo CAMP
hizo CAMP kulikuwa na mashabiki WAZARENDO
nakumbuka kuna SHABIKI MMOJA wa VINGUNGUTI TIMBERLAND huyo Mdau alikuwa anaipenda sana TWANGA kiasi alikuwa mpk anapanda NDEGE kuifuata TWANGA ikiwa NJE ya MKOA haswa ARUSHA au MWANZA

halafu kundi Jingine sasa ni la wanaofanikisha BENDI kuwa na Mziki bora

mfano HUSSEIN MIUNDOMBINU
huyu alikuwa fundi mitambo(umeme)
Twanga popote itakapopiga huyu alikuwa anahakikisha mambo yote ya umeme yako sawa mziki unatoka vizuri

THABITI MTOTO ILALA huyu alikuwa mkali wa kucheza na Keyboad

lakini pia kulikuwa na mkali mwingine wa KEYBOAD
ukisikia PROFESHENARI TARIBONARI VIctor mkambi huyu mkali wa KEYBOAD hata kama akifa inapaswa TWANGA wamjengee Sanamu lake maana alikuwa PROFESHENO haswa kaipaisha sana twanaga na UFUNDI wake wa KEYBOAD


Ukisikia MCD basi hapo anatajwa SUDI MOHAMED TIMBO(marehemu)
huyu alikuwa mpiga tumba matata sana

halafu ukisikia SHAKASHAKA SHAKUZURU hapa alikuwa anapaishwa MIRAJI SHAKASHIA huyu ni mpiga gitaa matata sana

halafu kulikuwa kulikuwa na mkung'uta DRUM hatari sana BABA DIANA BABAA SHARIFA BABAA ZAITUNI basi alikuuwa anatwaja ABUU SEMHANDO mpiga DRUM hatari

sasa utakuj kugundua kulikuwa na makundi matatu yalikuwa yanatwaja sana kwenye nyimbo
wngine walikuwa mashabiki damu wengine ndi hao watu wa wanamuziki wenyewe
[emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91]
 
umenikumbusha late 90s nimemaliza O-Level, nipo home idol nasubiri majibu yatoke. mshua akanitafutia temporary job mitaa ya mjini posta kwenye ofisi ya rafiki yake.

ofisi ilikuwa mtaa wa jamhuri jirani na ile round about ambayo inakutanisha india street na mkwepu street, almaarufu mitaa ya azam take away.

ilikuwa kila ikifika mida ya saa tatu mpaka saa nne asubuhi, lile eneo walikuwa wanatokea mabroo smart kwelikweli kimuonekano. mkononi wamebeba vi-diary.

walikuwa wanavaa mashati nadhifu, surauli za kadeti na viatu safi vya ngozi. kwa ujumla walikuwa wanapendeza sana, mimi mwenyewe nilikuwa nawa admire.

siku moja nikamuuliza broo mmoja ambaye tulikuwa tunafanya kazi pale, kwamba hawa jamaa ni akina nani,mbona mda mwingi wanautumia kakaa kwenye vijiwe vya shoe shiners, hawana kazi ya kufanya?.

akanijibu ukisikia mission town ndio hao, na hapo kwenye vijiwe vya shoeshiners ndio sehemu zao za kupanga mipango na kupeana deals mbalimbali.

akaniambia kile kipande chote cha mtaa wa mkwepu kinachokatiza club ya billicanas mpaka kule kwenye maungio ya samora avenue, ni territory ya ma-mission town.

hata papaa msofe alianza kujifunzia upigaji mitaa hiyo.
Papa Msofe alikuwa hachezi mbali ile mitaa wa iliyokuwa Salamander na benki ya Posta na alikuwa napenda kuvaa mashati meupe nadhifu sana na alikuwa na demu wake Benki ya Posta pale karibu na Posta ya zamani nasikia mwishowe alimuo yule mdada
 
Dj omyyyy mutoto wa mujiniiii mutoto wa mujini, Fikiri madinda mutoto wa mujiniii mutoto wa mujini...........
 
Umenikumbusha Haji Mbabe alitusumbuwa sana Sinza enzi hizo
Haji Mbabe mrundi alianzisha bendi yake chini ya gwiji Zahir Ally na haiukudumu alikuwa na kigari amazing ,bandarini kulimtajirisha akaenda Uingereza akajifanya mkimbizi alikuwa na kiofisi chake cha kutoa mizigo bandarini pale kariakoo kwenye nyumba ya mke wa marehemu Mbaraka Mwinshehe, alirudi tena Bongo baada ya kushindwa kubeba box Uingereza .
 
Mtawali-Yadi yake ya Magari inatazamana na Ostabay Police- alikuwa matata kwa totoz! Ila aliwai kutwa na skendo ya kufumaniwa na mke wa jamaa mmoja hivi ambae nae alikuwa mtoto wa Mujini .Ilimfanya siku moja anunue magazeti yote yaliokuwa na hii storyNchi nzima?? Ilikuwaje?? Siku nyingine[emoji23]
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kuna pedeshee Ndunguru na pedeshee Ndomba wa Makongo. Nteze wa Nteze mzee wa kifusi.... dah old good days. Kuna siku niko pale makumbusho, Papaa Msofe akanunua bia kwa kila mtu aliyekuwepo mle ndani nilichoka sana, anakujua hakujui unapewa bia 😅
 
Acha ubishi mzee mwenyeji wa Arusha wote hakuna asie mjua Hidaya tena alikua maarufu kwa jina la Hidaya Wa pepe kale kafariki mwaka jana , Hidaya ni miongon mwa wanawake matajiri wa Arusha enzi hizo, ameishi pia france ninavyo kueleza kafariki mwaka jana elewa hivyo
Alafu mi nazungumzia wimbo wa pepe kale Hidaya hiyo ya kwako ya Hedaya mimi siijui
Hidaya alikuwa ni mkaazi wa Arusha tena pale mjini karibu kabisa na Sheikh Amri stadium kwa nyuma ,mitaa ile kuna baa nyingi,nadhani allikuwa na kamadamu ya kisomali kwa mbali bonge la pisi amepanda juu na bonge la guu halafu mtoto wa mjini, udongo huu umechukua wengi zamani kulikuwa na pisi kali kwelikweli.
 
Back
Top Bottom