Tuwafahamu Watu Maarufu waliokuwa wanatajwa sana na Wanamuziki wa Band nchini Tanzania

Tuwafahamu Watu Maarufu waliokuwa wanatajwa sana na Wanamuziki wa Band nchini Tanzania

Reila hajachuana na hadija kopa...maana nafikiri reila ameimba taarab akiwa na mzee yusuf labda ungesema nasma khamis kidogodogo
reilah khatibu( RIP),hakuwahi kuimba taarabu na mzee yusufu. unless unamzungumzia reilah mwingine, naruhusu kusahihishwa.
 
Nimekulia Sinza ile ya akina Remi ndio wanatamba na Volkswagen imeandikwa.''mambo kwa soksi'' tulikuwa tunajua karibu vijana wote, hivi sasa Sinza imebadirika ni Sinza ya magorofa,mahoteli,vijana wote wa zamani ama wamerudisha namba kwa Sir God ama wamehamia sehemu nyingine nje ya mji,nyumba nyingi tulizokuwa tunapanga chumba kimoja kimoja zimebomolewa na kujengwa mahekalu, nakumbuka pale sinza madukani kulikuwa na mbabe wa kikurya Lucky baba yake alikuwa usalama wa Taifa,namkubuka bibi Uliye alikuwa na mabinti kama 10 hatari sana, nakumbuka akina Banza stone wakiwa wadogo wakicheza disco mtaani, nakumbuka Vatican City ikiwa hotel kumbwa Sinza na Simba walikuwa wakiweka kambi hapo, namkumbuka Fred Mwalasha akiwa ametoka Ulaya na mke wa kizungu ikawa yeye ni bangi na bangi na yeye hadi mwanamke wa kizungu akamkimbia, siku hizi sinza yamejaa madangulo na wazee wale waliokuwa na nyumba ambazo tulikuwa tumepanga nao hatunao duniani ila zile nyumba walizoacha watoto wao wameziuza kwa matajiri na kwenda kunywea pombe na kula sembe. Sinza ya sasa si ile tuliyokuwa tunaitimba, ama kweli siku hazigandi.
[emoji91][emoji91][emoji91][emoji91]
 
Reila hajachuana na hadija kopa...maana nafikiri reila ameimba taarab akiwa na mzee yusuf labda ungesema nasma khamis kidogodogo
Mjuu wa bi nasma ni Doctor turkey ila kwake maisha ya kawaida mno
 
Umemsahau Papaa Shabani Ngalawa (R.I.P). Huyu alikua mwalimu mzuri wa tution miaka ya 1995-2001 hizi za shule ya msingi. Miaka ambayo mtaa mzima unakuta waliofaulu la saba ni wawili au hakuna na katika hao waliofaulu wote walisoma tution kwa huyu mwalimu shabani..

Nakumbuka alichukuaga mkopo wa milioni 200 lengo likiwa kujenga shule yake binafsi maeneo ya kibamba. Akaweka rehani nyumba na shamba lake. Mwisho wa siku pesa zote zikaishia kuwatunza akina ally choki na mwinjuma muumini ktk mabendi na nyingine akanunulia toyota baloon. Benki ikaja ikapiga mnada nyumba na shamba wakamfilisi mazima.

Alitajwa sana kwenye nyimbo za Mwinjuma hasa ile ya Kilio cha Yatima. Alikuja kuugua mda mrefu na aliisha akawa kama mtoto. Amefariki akiwa hana hata pa kulala. Sad!
Shaban Ngalawa nilisomava tuition kwake wiki moja tu.

Pale mitaa ya kimara resort (vidudu)na tulikuwa tunafanya mitihani kwake enzi hizo.

Alikuwa mfupi hivi anapiga panki kifuani anaacha vishikizo viwili juu wazi na cheni inabembea na bonge la mustache.
 
Hakua na issue yoyote aliku anakaa kwao kota mpk anazeeka..
Nakumbuka alipigwa ridandasi nbc ela za mafao ndio akaweka heshima bar.
Shabiki kindakindaki wa wajelajela gwa
Kuba mwana mmoja alikuwa jirani yetu hapo dar somewhere alikuwa anatupa stori kuwa jimmy chocolate alikuwa anawambato sana maduu wa kino enzi zake.
 
Tunamkumbuka kama Shujaa wetu na mtu mwenye mapenzi ya kweli na kisarawe alikuwa mkurugenzi wa Bandarini ila Faida yake mpk Leo baadhi vizazi bado ipo sio yule bwana waziri anafaida yeyote zaidi ya kuongeza wake... Tunamsubiri kwa Hamu 2025...
Nilishaona mzee Mohamed said akimsfia kwenye moja ya nyuzi zake huku.

Pamoja na yule dr dau wa nssf ambaye alianzia huko bandarini.

Uliposema mtoto wa mzee janguo yuko Nssf leo

Yes the dot is connected.

Kwaheri[emoji2]
 
Shaban Ngalawa nilisomava tuition kwake wiki moja tu.

Pale mitaa ya kimara resort (vidudu)na tulikuwa tunafanya mitihani kwake enzi hizo.

Alikuwa mfupi hivi anapiga panki kifuani anaacha vishikizo viwili juu wazi na cheni inabembea na bonge la mustache.
Mzee inawezekana tulikulia mtaa mmoja.

Yeah Shaban Ngalawa alikua mfupi haswa, enzi zile wanafunzi tulimpaga jina la utani "Mwalimu Kiroba"

Mda unaenda kwa kasi sana...
 
ninachoupendea huu uzi tangu nilipoupandisha haujawahi kupoa. kila ikifika mida ya jioni(east african time)mida ya ku relax na kupata moja moto moja baridi, uzi unaamka upya. mnanipa faraja sana wadau.

nipo zangu hapa arusha ktk bar moja maarufu nalainisha koo huku napitia comment zenu na kusikiliza rhumba kali zilizotamba miaka ya 2000-2010, honestly it's 100% a vibe.

halafu ninachojifunza ktk huu uzi, wote wanaozungumziwa walitafuta pesa kwa nguvu zao legally and illegally, hakuna uchawa. hii ichukuliewe kama lesson kwa nyinyi vijana wa generation ya instagram, tiktok na platform zingine za kijamii.

ma-senior wenzangu, mmesikia kwamba wenge bcgb ile ya Werrason na JB mpiana inarudi tena?. binafsi nawasubiri kwa hamu kubwa hawa magwiji. wapo studio kurecord nyimbo zao mpya. haya wenye mziki wao wa rhumba na seben wanarudi upya. i can't wait.
 
Sikujua kuwa pacha mmoja alishatutoka! Maskini
Toka 2019.

Alifariki kwa ajali ya gali hapo Mbezi, usiku anaingia barabara kuu akiwa maji kidogo kumbe kuna fuso imejaa nyanya inatokea Afrikana ikamvaa kuja mjini, biashara ikaishia hapo.
 
Hem
Hao Wanamuziki wa Congo wote break yao kuna Don wa Ki Ivory coast anaishi Paris anaitwa Hemed Bakayoko, huyu ndio funga kazi, hii treasure.

Huyu ndio hakauki mdomoni mwa Boss ya Mboka Koffi Ollomide then ndio anakula shavu Samuel Etoo, hizi ni international level.
Hemedi Bakayoko alikua waziri mkuu wa Ivory Coast na alifariki mwaka jana kwa Kansa.

Kabla ya kua waziri mkuu alikua meya wa Mji wa Abijan kwa muda mrefu na ni alikua mpenzi sana wa muziki wa kongo toka Extra Musica wanamuiba akiwa kijana mdogo miaka ya 90.

Ni mtu alikua na mpunga mkubwa miaka mingi tu.

Amefariki mwaka jana akiwa na miaka 55.
 
Kweli huyu bakayoko kwnye twanga fotoo nimesikia jina lake
Amefariki mwaka jana alikua waziri Mkuu wa Ivory Coast.

Ni mdau wa muziki wa Congo miaka mingi sana.

Amefariki akiwa na miaka 55. Alikua meya wa Abijan kwa miaka mingi na pia waziri.

Ukisikiliza hata extra Musica walikuimba miaka ya 1998.
 
Kilivyoingia chuma pale Ikulu ndio ikawa mwisho wa hao watu. Huku ikisemekana walijipatia ukwasi nje ya mstari sahihi.

Na ndio ikawa mwisho wa mziki wa dance hapa nchini hadi sasa. Maana walitegemea udhamini wa hao watu.
Jiwe aliua mziki wa dansi,
mapedeshee walimwaga pesa Sana mtaani[emoji4]
 
Back
Top Bottom