Tuwafahamu Watu Maarufu waliokuwa wanatajwa sana na Wanamuziki wa Band nchini Tanzania

Tuwafahamu Watu Maarufu waliokuwa wanatajwa sana na Wanamuziki wa Band nchini Tanzania

hapana sio kweli, tusichanganye madesa. jose kongolo na sadam hussein ni watu wawili tofauti.

Najikita kumuelezea zaidi Jose Kongolo.
Jose Kongolo ni mwanamama maarufu wa kicongo na mfanyabiashara anayemiliki mgahawa mkubwa na lounge jijini paris, pia ni mdau mkubwa wa mziki wa rhumba.

jina lake limetajwa sana na wanamuziki wa kicongo wakitamka "JOSÉ KONGOLO FBI MIBEKO LA LOI".

wengi kwa kutokujua wemekuwa wanachanganya jina lake na jina la Kongulu Mobutu "Sadam Hussein", ambaye alikuwa mtoto wa Mobutu Sese Seko.

mgahawa anaoumiliki huyu mama umekuwa ni meeting point ya wacongo wengi ndani ya ufaransa.

kwanini wanamuita FBI mibeko la loi au kwa kiswahili FBI wa Yesu?(wanaojua kikongo vizuri watasaidia kutafsiri). ni kwasababu Jose Kongolo ni born again christian au tuseme mlokole.

licha ya kwamba ni mfanyabiashara, pia ana miliki kanisa lake pale paris. kanisa hili limekuwa msaada mkubwa kwa vijana wa kicongo waliopoteza matumaini ya kimaisha ndani ya ufaransa na nchi nyingine za europe.

yeye huwapokea, huwafanyia counseling, huwapa chakula,maradhi, hawachangia michango mbalimbali ya kibinadamu na baadae huwashawishi waokoke.

baadhi ya wanamuziki wameokoka baada ya kushawishiwa na huyu mama. wengine huwa wanaendelea na career yao ya mziki huku yeye akiendelea kuwapa support.

hapo ndio umaarufu wake unapokuja na ndio maana jina lake linatajwa sana na wanamuziki wa rhumba

kuhusu Kongulu Mobutu "Sadam Hussein".
Kongulu Mobutu almaarufu sadam hussein, huyu sitaki kumuelezea kwasababu hapa JF zipo nyuzi kadhaa ambazo amezungumziwa kiundani. ni wewe tu kuzipitia ili kuongeza knowledge.

nakuwekea link hapa chini:
Mjue Saddam Hussein wa Zaire

Fahamu machache kuhusu special presidential division: Kikosi maalumu kilichomlinda Mobutu Seseseko enzi za utawala wake

katika picha huyu ndio mamaa JOSÉ KONGOLO FBI MIBEKO LA LOI.
View attachment 2280509
josee kongolo[emoji1489][emoji1489]
 
Hao Wanamuziki wa Congo wote break yao kuna Don wa Ki Ivory coast anaishi Paris anaitwa Hemed Bakayoko, huyu ndio funga kazi, hii treasure.

Huyu ndio hakauki mdomoni mwa Boss ya Mboka Koffi Ollomide then ndio anakula shavu Samuel Etoo, hizi ni international level.
Brother hemed bakayoko haishi ufaransa huyu Kwa sasa ni maremu alishawahi kua waziri mkuu ivory coast na kama unafatilia vizuri nyimbo za fally ipupa hivi karibuni , huyu Mzee mpaka alikua anapanda jukwaani kucheza fally akiperform.
anamtaja kabisa na analiza na rip
 
Brother hemed bakayoko haishi ufaransa huyu Kwa sasa ni maremu alishawahi kua waziri mkuu ivory coast na kama unafatilia vizuri nyimbo za fally ipupa hivi karibuni , huyu Mzee mpaka alikua anapanda jukwaani kucheza fally akiperform.
anamtaja kabisa na analiza na rip
Usichokijuwa hao viongozi wa hizo Francophone Kwa Mwaka muda mwingi wanakuwa Ufaransa.

Kuna Rais hapo anaongoza nchi akiwa Ufaransa, issue ya kufariki na Corona Hemmed Bakayoko niliisikia.
 
Ni marehemu kwa sasa.Alikuwa waziri mkuu wa Ivory coast.Alikufa huko Ujerumani akiwa kwenye matibabu ,aliugua Ini.Ilisemekana alipewa sumu maana alikuwa na ndoto ya kugombea Urais.
[emoji24][emoji24][emoji24][emoji134]
 
R.I.P Patrick Kessy (Kilimo Kwanza)

Mdau alikuwa kwa kipindi hiki anasapoti sana muziki wa dance

Patrick Matolo Felician Kessy

Bilionea umeenda kama maskhara vile
Mungu akulipe mema mzee wangu
Kwa hakika wema hautofutika moyoni mwetu
Mpaka leo napata ridhki kwa kile kidogo ulichotuachia tutaendelea kukuenzi mzee wetu upumzike pahala pema
 
Kiongozi utakua umesikia vibaya ni Didi stone mtoto wa kike wa Koffi ni model anaishi france
Didie kinwani (inaandikwa Kinuani) ni pedeshee drc..kama sikosei ni rais wa kampuni.....didistone ni mtoto wa Koraman grand mopao koffi.

Huyo hapo kwenye picha.
Screenshot_20240110_191259_Google.jpg
 
wengi kwa kutokujua hufananisha jina lake na jina la marehemu Kongulu Mobutu aka Sadam Hussein(mtoto mtukutu wa rais wa zamani wa zaire Mobutu Seseseko).

Ninayemzungumzia hapa ni mwanamama Jose Kongolo FBI Mibeko la loi ambaye jina lake linatajwa sana na wanamuziki wakubwa wa Congo DR kwa level ileile ambayo marehemu Kongulu Mobutu aka Sadam Hussein alikuwa anatajwa.

nilishawahi kuandika wasifu wa huyu mama ndani ya uzi huu. pitia post zilizopita.
 

Attachments

  • TikTok_7310695281497066785 (1).mp4
    1.9 MB
nimesoma uzi na kupitia comments zote, sijaona sehemu katajwa,

pedeshee akanyambasira mutu ya watu.

nimesikitika sana.
mimi kama author wa uzi huu na wadau wenzangu wengine wa masuala ya celebrities and powerful public figures wa bara hili la africa hatumfahamu mtu huyo na wala hatujawahi kusikia jina lake.

umaarufu na upedeshee wake bila shaka unaushia kwenye familia yake na kijijini alichozaliwa. karibu tena ndg.
 
mimi kama author wa uzi huu na wadau wenzangu wengine wa masuala ya celebrities and powerful public figures wa bara hili la africa hatumfahamu mtu huyo na wala hatujawahi kusikia jina lake.

umaarufu na upedeshee wake bila shaka unaushia kwenye familia yake na kijijini alichozaliwa. karibu tena ndg.
Alooo, kwa hyo masikitiko yaendelee siyo?
 
wengi kwa kutokujua hufananisha jina lake na jina la marehemu Kongulu Mobutu aka Sadam Hussein(mtoto mtukutu wa rais wa zamani wa zaire Mobutu Seseseko).

Ninayemzungumzia hapa ni mwanamama Jose Kongolo FBI Mibeko la loi ambaye jina lake linatajwa sana na wanamuziki wakubwa wa Congo DR kwa level ileile ambayo marehemu Kongulu Mobutu aka Sadam Hussein alikuwa anatajwa.

nilishawahi kuandika wasifu wa huyu mama ndani ya uzi huu. pitia post zilizopita.
Duuuh katisha huyo mama
 
Back
Top Bottom