Tuwakomalie Polisi kuwarejesha watuhumiwa wakiwa hai

Tuwakomalie Polisi kuwarejesha watuhumiwa wakiwa hai

Wakati panya road walipokuwa wanavamia nyumba za watu kuiba, kujeruhi na kuuwa raia wema wasiokuwa na hatia, mbona sikukuona ukija kutoa ushauri wa namna yoyote dhidi ya hao vijana wenu wa panya road?

Au wale waliokuwa wanavunjiwa nyumba zao, kuibiwa na kuuwawa hawakuwa na haki ya kutetewa mitandaoni kama mnavyowatetea panya road?
Tunajua wengi wa wale wanaowatetea panya road ni maboss wao au wanamtandao wenzao.

Sasa na sisi tutaanza kuwashauri polisi wawe wanakuja kufuatilia na kuwachunguza hawa wanaowatetea hawa panya road mitandaoni, kwamba wanawatetea kwa lengo zuri au na wao ni miongoni mwa wafaidika wa vitu vya wizi vinavyopatikana baada ya mwenye navyo kupigwa mapanga na kuuwawa bila sababu.
Wewe ni msukule proper
 
Tangu hii operation ya panya road ianze, umevurugika sana...lazma kila siku upost, kuna kitu sio bure!!

Utakuwa hukuwahi kunisikia tu mkuu.

Tofautisha kuvurugika na kuwapelekea wajinga wajinga moto.

IMG_20221001_023903_471.jpg


Au ni mapendekezo yako waonewe huruma hao ndugu?
 
Upo uhakia gani kuwa waliotolewa uhai na polisi waitoa uhai?

Kumbuka mfanya biashara wa madini Mtwara, wafanya biashara ya madini Ifakara. Hawa waliporwa fedha na kutolewaxuhai na polisi.

Usiwasahau Lissu, Lijenje, Ben, Azory. Hawa ni wahanga wa mamlaka kama navyo kumbushwa mara lukuki na bwana RNA kuwa kuna wavaa makoti marefu meusi.

Kumbuka wa kwenye viroba. Orodha haina mwisho.

NInakazia: ipo tofauti kubwa baina ya watoa uhai na washukiwa.
Washukiwa wote wafikishwe Mahakamani na Ukamataji ni baada ya Upelelezi kukamilika,mahabusu zinatumika kutesea wanaohusika na wasiohusika(Hawana hatia bado).
Siyo kazi ya POLISI kuua.TUKOMESHE UDHALIMU wa POLISI dhidi ya RAIA wenzetu-"STOP police BRUTALITY and KILLING innocent citizens until Proven Guilty by The Courts of The Law" period!
 
Issue hii inatuhusu sote,ukisema wahanga wakomalie ni pamoja nami na wewe.Jinsi ulivyoshauri ndivyo watesi wetu wapendavyo-Kutugawanya ili iwe rahisi kutushinda.Wanafahamu kwamba tukiunganisha Nguvu zetu pamoja tutawakomesha mazima.Asili ya mateso mengi wanayopitia wenyenchi hii ni Ukatili wa vyombo vya Dola na Watawala(CCM).
Kuna maandamano ya kupinga Ukatili/Unyama wa POLISI Duniani Jumatatu ya tarehe 03-10-2022.Tuanzie hapo.

Utakuwa hujanisoma kunielewa tu mkuu. Nikushauri kurejea kujridhisha.

Hakuna ninapo advocate utengano. Hata hivyo wakati hakuna la maana linaloendelea kila mtu anayo nafasi yake ya kulianzisha kivyake vyake justifiably kabisa.

Mangapi yamependekezwa? Nini kimetokea?

Si unawaona hawa kina Evelyn Salt wenye kuona tunaopaza sauti ati kuwa tumevurugika? Ni wa kutegemea hao kwenye kudai haki ipi?

Kumbuka kudai haki siyo kuchakata au kuchakatwa mbususu. Anasema Castro mtu 10 tunatosha sana.

IMG_20220927_190940_421.jpg


Wazi wazi nimesema ole wao waguse kwetu, wewe je?
 
Polisi wanatuchukulia poa sana. Hawajui waajiri wao ni sisi.

Catherine Ruge anaeleweka vyema kuwa suala la kuzika halipo na halitakuwapo.

"Ingekuwa muafaka zaidi polisi kufahamishwa kuwarejesha watuhumiwa hai kama walivyowachukua."

Haiwezekani wajue kuuwa tu na si kurudisha uhai walioutoa kwa makusudi!

Ninakazia, wasije wakathubutu kwetu. Kwani kwa hakika patachimbika wala hakitakuwa cha mtoto.

Kwamba walimchukua mzima?Nakwenda vipi kulipa gharama zipi za "monchwari" (kama anavyokuita Abdul Nondo)? Monchwari ipi hiyo kwanza? Ninalipa vipi nauli ya polisi yupi?

NInamzika vipi marehemu aliyeuwawa na polisi kwenye mazingira haya?

Kwanini hatuwashauri wahanga kukomaa na polisi kuwarejeshea ndugu zao wakiwa hai?

Kwa nini badala yake tunageuka kuwa waandishi wa habari? Au ni yale ya kutajifutia mileage tu?

Nini mchango wetu kuona ubazazi huu kutoka kwa watu tuliowaajiri unakoma taslimu (forth with)?
Inaonesha nawe ni Panya Road, si bure
 
Utakuwa hujanisoma kunielewa tu mkuu. Nikushauri kurejea kujridhisha.

Hakuna ninapo advocate utengano. Hata hivyo wakati hakuna la maana linaloendelea kila mtu anayo nafasi yake ya kulianzisha kivyake vyake justifiably kabisa.

Mangapi yamependekezwa? Nini kimetokea?

Si unawaona Hawa kina Evelyn Salt wenye kuona tunaopaza Sauti ati kuwa tumevurugika? Ni wa kutegemea hao kwenye kudai haki ipi?

Kumbuka kudai haki siyo kuchakata au kuchakatwa mbususu. Anasema Castro mtu 10 tunatosha sana.

View attachment 2373859

Wazi wazi nimesema ole wao waguse kwetu wewe je?
Tupo pamoja sana Mtanzania wa Tanganyika mwenzangu.Nakubaliana kuwa Utengano ni Udhaifu na Umoja ni Nguvu.Vile vile utambue kwamba sikumaanisha kuwa haupendi Umoja.
Kwenye kulianzisha,wingi huanza na moja,tulianzishe Jumatatu kama inavyopendekezwa.Kila mmoja pale alipo afikishe Ujumbe wa "Komesha Udhalimu wa POLISI dhidi ya Raia wa Nchi yetu".
 
Washukiwa wote wafikishwe Mahakamani na Ukamataji ni baada ya Upelelezi kukamilika,mahabusu zinatumika kutesea wanaohusika na wasiohusika(Hawana hatia bado).
Siyo kazi ya POLISI kuua.TUKOMESHE UDHALIMU wa POLISI dhidi ya RAIA wenzetu-"STOP police BRUTALITY and KILLING innocent citizens until Proven Guilty by The Courts of The Law" period!

Uliyoyaandika hapa ni mema kabisa. Haya ndiyo tunayopigania watu wenye akili zetu. Nyuzi hizi hapa chini ni mfano wake:

Polisi wauwaji wafikishwe kunako stahili

Kusimama na Catherine Ruge ni Wajibu

Tutaendelea kupigania haki zetu zote bila kujali tu wangapi katika jitihada hizo.

Assets na liabilities katika jitihada zetu tunawajua.

NIsiache kusema Sexless, Evelyn Salt na wengine wenye mawazo hasi pumzikeni tu, msubiri matunda.

Tanzania yenye kuheshimu utawala wa sheria itakuwa ni tamu sana si kwetu tu bali hata nyie, watoto wenu na pia watoto wa watoto wenu.

IMG_20221001_162723_487.jpg
IMG_20221001_162723_487.jpg


Kwamba nyie hamuyataki haya? Na mngependa nani awe nanyi upande wenu?

NInakazia: Tanzania hiyo haiwezi kupiganiwa na cowards.
 
Sina muda wa kubishana na chawa wa Catherine Ruge

Mkuu siyo kuwa utakuwa umejichanganya vilivyo? Catherine Ruge hawezi kuwa na chawa huyo mbona ni underdog mno?

Chawa huwa wapo kwa watu na majina yao mkuu Mfano mwendazake, Mama, na kina Mbowe mbowe huko.

Kama Lissu, Zitto, Lipumba, Mbatia, Cheyo, Rungwe nk hawana chawa itakuwa Catherine Ruge ndugu policeman?

Tunajua kuwa mnapitia wakati mgumu sana. Kwamba mlipo ni kujikaza kisabuni tu.

Kwa hakika mngejua msingekuwa mmeyakanyaga.

Hiiiii bagosha!
 
Uliyoyaandika hapa ni mema kabisa. Haya ndiyo tunayopigania watu wenye akili zetu. Nyuzi huu hapa chini ni mfano wake:

Polisi wauwaji wafikishwe kunako stahili

Kusimama na Catherine Ruge ni Wajibu

Tutaendelea kupigania haki zetu zote bila kujali tu wangapi katika jitihada hizo.

Assets na liabilities katika jitihada zetu tunawajua.

NIsiache kusema Sexless, Evelyn Salt na wengine wenye mawazo hasi pumzikeni tu, msubiri matunda.

Tanzania yenye kuheshimu utawala wa sheria itakuwa ni tamu sana si kwetu tu bali hata nyie, watoto wenu na pia watoto wa watoto wenu.

View attachment 2373882View attachment 2373882

Kwamba nyie hamuyataki haya? Na mngependa nani awe nanyi upande wenu?

NInakazia: Tanzania hiyo haiwezi kupiganiwa na cowards.
You nailed it nicely.We want ourFreedom,Rights and Peace in the country.
 
Sina muda wa kubishana na chawa wa Catherine Ruge
Umejipiga picha na kututumia huku?Catherine hana chawa maana siyo mCCM.
Usichanganye mafaili chawa,kunguni,viroboto au Jiggers wapo CCM,don't forget that.
 
Mkuu siyo kuwa utakuwa umejichanganya vilivyo? Catherine Ruge hawezi kuwa na chawa huyo mbona ni underdog mno?

Chawa huwa wapo kwa watu na majina yao mkuu Mfano mwendazake, Mama, na kina Mbowe huko.

Kama Lissu, Zitto, Lipumba, Mbatia, Cheyo, Rungwe nk hawana chawa itakuwa Catherine Ruge ndugu policeman?

Tunajua kuwa mnapitia wakati mgumu sana. Kwamba mlipo ni kujikaza kisabuni tu.

Kwa hakika mngejua msingekuwa mmeyakanyaga.

Hiiiii bagosha!
Wayaogee maana wamechojoa wenyewe,tuliwaonya hawakutaka kusikia.Wameukalia na Tutaelewana tu.
 
You nailed it nicely.We want ourFreedom,Rights and Peace in the country.

Katika nchi watu wa aina zote wapo. Wapo wajinga, werevu, wapumbavu, opportunists, nk. Anaimba Sam wa Ukweli:

"Wapenda ngono na wachawi siyo kwenu tu, hata kwetu wapo."

Ukisubiri Kila mtu kuelewa hakuna la maana litafanyika.

1. Kwamba tatizo linajulikana?
2. Kwamba namna ya kulitanzua inajulikana?
3. Ya nini kupoteza muda kurumbana na watu?

Anasema Museveni:

"Maendeleo ya Uganda hayawezi kuwasubiri wa Karamojong wajue kuvaa suruali."

Tutakutana mbele kwa mbele.
 
Hivi ile kauli ya Mkuu wa Mkoa ya kuwaambia wazazi wasipowaona watoto wao nyumbani wakawatafute hospitali isipotenguliwa maana yake inaendelea kutumika mpaka sasa, hii maana yake tujiandae kusikia taarifa zaidi za watuhumiwa kuuliwa wakiwa mikononi mwa polisi.

Kiongozi mwenye dhamana kubwa kwa mkoa wako, kuamua kuwaua kinyume cha sheria wale uliotakiwa kuwaongoza, hili halikubaliki, huyu alitakiwa kujiuzulu au kuondolewa kabisa ofisini na mkuu wake, bahati mbaya hakuna kinachofanyika na maumivu kwa watuhumiwa yatazidi.

Mkuu hayupo mwenye mnofu mdomoni anayeweza kuutema mwenyewe kwa Raha zake. Labda uwe wa mto au atemeshwe kwa nguvu.

Kutokupoa kwetu kuhusiana dhuluma zao chafu hizi ndiyo njia pekee kuwatia adabu na hata kuwatemesha minofu iliyowajaa midomoni.

Kumbuka hao wote lao moja. Hufarakana tu moto wetu unapokuwa hauna dalili ya kupungua.

IMG_20221001_023903_471.jpg


Hapa walipo wanasali na kuswali swala 5 kuomba tukio jingine kubwa Ili tuachane na hili.

Dawa pekee ni kutokupoa.
 
Hivi Polisi wakiwachukulia Wahalifu kama wateja wanaosafiri na ndege na Wageni KWENYE Gest wanavyopokelewa Kwa Ukarimu halafu Wahalifu wakashamiri nani hasa atapata hasara. Hivi unafikiri walioporwa Mali na kuuwa na Ponya rod ni familia za askari

Kwa Nini watu walikua wanapiga kelele kuwa Polisi wapambane na Panya rod lakini Sasa Jiji limetulia na watu wanaweza hata kukaa vibarazani halafu Kuna matako yanaleta mada za kipumbavu hapa.


Yani watu wanatengengeza vikundi vya kigaidi na kupora Mali za watu Kwa mapanga na nondo Halafu mbwa wa kisasa wanakuja kuwauunga mkono hapa.

Nyie mnawasikiliza wale mazezeta akina Abduli Nondo bila kujaua kuwa yule Kuna mikono na harakati za kigaidi nyuma yake. Mbona hakuchunguta akajua kuwa TV zilizokuwa zinaibiwa zinauzwa wapi?

Hawa wanaoleta harakati za hovyo kuhatarisha usalama na amani ya nchi ni Moja wapo ya washenzi wanaopaswa kupigwa risasi mchana kweupe .

Serikali ya CCM isitishwe na hizi takataka ambazo hata miaka mia hawatakuja kuingia Ikulu . Nyerere alijua kuwa Tanzania Ina historia ya kuwa naachifu waliokua wanapigania mgawanyiko wa kikabila na kidini Ndio maana akaunda Chama imara sana na kuweka mifumo imara ili Taifa hili liwe Moja lisiloyumbishwa na wanasiasa Malaya Malaya kama akina Abdul Nondo na wapuuzi WENGINE.

Hii inchi Ina watu wabinafsi sana hawajali mateso ya wengine wanaangalia maslahi ya Leo TU. Bora CCM utawale milele kuliko Hawa wapinzani wanaohamasisha ugaidi.

ACT imeshaanza harakati za kigaidi kama Ile Ngangari ya zamani. Na upenyo wa Magaidi siku zote ni kudhoofisha Polisi kwanza. Pumba kabisa.

Yaani ACT badala ya kupigania katiba mpya wao wanahamasisha uhalifu.
 
Wakati panya road walipokuwa wanavamia nyumba za watu kuiba, kujeruhi na kuuwa raia wema wasiokuwa na hatia, mbona sikukuona ukija kutoa ushauri wa namna yoyote dhidi ya hao vijana wenu wa panya road?

Au wale waliokuwa wanavunjiwa nyumba zao, kuibiwa na kuuwawa hawakuwa na haki ya kutetewa mitandaoni kama mnavyowatetea panya road?
Tunajua wengi wa wale wanaowatetea panya road ni maboss wao au wanamtandao wenzao.

Sasa na sisi tutaanza kuwashauri polisi wawe wanakuja kufuatilia na kuwachunguza hawa wanaowatetea hawa panya road mitandaoni, kwamba wanawatetea kwa lengo zuri au na wao ni miongoni mwa wafaidika wa vitu vya wizi vinavyopatikana baada ya mwenye navyo kupigwa mapanga na kuuwawa bila sababu.
Ni kweli Kuna maduka Mengi sana wanauza TV za wizi na spea za magari ya wizi. Na wengi wao ni wanachama wa ACT kule Temeke na Tandika na Ilala. ndio maana hayo maduka Mengi yapo kwenye maeneo yenye wanachama wengi wa ACT Panya rodi.

Polisi ianze kuchunguza kwenye maduka yote yaliyopo hayo maeneo ya ACT na washirikishe wadau wengine kama TRA na Bandari. Waonyeshe vielelezo kuwa bidhaa zao ziliingia nchini lini na zilitokea wapi na zilipiwa Kodi au laa.
Tutajua mbivu na mbichi
 
Rejea kuona unaniwekea maneno mdomoni mwoga mkubwa wee!

Nimekupa tathmini ya miye kama mimi nini nitafanya. Nimekupa tathmini ya Catherine Ruge kama yeye nini amefanya.

Nimekupa tathmini ya Abdul Nondo kama yeye nini amefanya. Huyu karipoti kama mwandishi wa habari.

Nimekupa tathmini yangu ya nini wengine wanaweza kufanya kwa ndugu wa wahanga, kikaleta tija.

Cha kwako wewe kiko wapi?

Wewe si uko kwenye rekodi ukisema hauko tayari kukabiliana na polisi kwa kuwa unaogopa kufa? Sasa hilo tatizo unalotaka kudai linaanzia hapo, hapo wapi? Pakufikirika?

Weka mkakati wako hapa ulio tayari wewe kuusimamia kuumaliza uovu huu wa polisi.

Ya nini kuandikia mate?
Kumbuka Polisi hawatetei Mali zao wanatetea Mali za watu wengine.
Kuua mtu Kwa ajili ya Mali ya mtu Mwingine sio jambo Dogo.

Panya rodi ni kikundi kilichoundwa na haliwezi kikawa kimeundwa na wajinga wanaotoka mate mdomoni. Kuna watu nyuma yake . Kama Wewe kweli ni raia mwema usishabikie Hawa wahalifu wanaotengenezwa kimkakati. Kumbuka kabla ya JPM kuingia madarakani Nini kilikua kimeanza. Watu walianza kuandamana kutoa watu kwenye vituo vya polisi.baadae wakaanza kuchoma vituo moto then wakanza kupora polisi silaha, mwishowe wakawa wanaua polisi .Kwa Siku Moja polisi wanauawa wanne. Walianza Kwa kujifanya wanatetea Haki za binadamu lakini nyuma palikua na agenda za kigaidi na kudhoofisha serikali Kwa kulidhoofisha Jeshi la polisi na kuwatia hofu. Wanaoumia no Raia wema wasiojihusisha na mambo ya madaraka na Siasa za madaraka.

Hakuna Nchi iliyoko serious kulinda amani na usalama wake inawaza kuwaangalia watu wanaunda vikundi vya kihalifu Kwa kutumia silaha. Majeshi YETU yanawajibu Wa kulinda amani na usalama Wa watu Kwa namna yoyote Ile. Ndio MAANA Dunia kote bajeti Kubwa ni za Majeshi na ni Kwa ajili ya kununua silaha za kuua watu wanaojaribu kuvuruga amani na usalama Wa Nchi husika .

Rwanda hakuna mchezo na Wahalifu ,na wanasiasa wanaoleta chokochoko ni kufutilia MBALI . Nchi imetulia kama Uswisi.
 
Hivi Polisi wakiwachukulia Wahalifu kama wateja wanaosafiri na ndege na Wageni KWENYE Gest wanavyopokelewa Kwa Ukarimu halafu Wahalifu wakashamiri nani hasa atapata hasara. Hivi unafikiri walioporwa Mali na kuuwa na Ponya rod ni familia za askari

Kwa Nini watu walikua wanapiga kelele kuwa Polisi wapambane na Panya rod lakini Sasa Jiji limetulia na watu wanaweza hata kukaa vibarazani halafu Kuna matako yanaleta mada za kipumbavu hapa.


Yani watu wanatengengeza vikundi vya kigaidi na kupora Mali za watu Kwa mapanga na nondo Halafu mbwa wa kisasa wanakuja kuwauunga mkono hapa.

Nyie mnawasikiliza wale mazezeta akina Abduli Nondo bila kujaua kuwa yule Kuna mikono na harakati za kigaidi nyuma yake. Mbona hakuchunguta akajua kuwa TV zilizokuwa zinaibiwa zinauzwa wapi?

Hawa wanaoleta harakati za hovyo kuhatarisha usalama na amani ya nchi ni Moja wapo ya washenzi wanaopaswa kupigwa risasi mchana kweupe .

Serikali ya CCM isitishwe na hizi takataka ambazo hata miaka mia hawatakuja kuingia Ikulu . Nyerere alijua kuwa Tanzania Ina historia ya kuwa naachifu waliokua wanapigania mgawanyiko wa kikabila na kidini Ndio maana akaunda Chama imara sana na kuweka mifumo imara ili Taifa hili liwe Moja lisiloyumbishwa na wanasiasa Malaya Malaya kama akina Abdul Nondo na wapuuzi WENGINE.

Hii inchi Ina watu wabinafsi sana hawajali mateso ya wengine wanaangalia maslahi ya Leo TU. Bora CCM utawale milele kuliko Hawa wapinzani wanaohamasisha ugaidi.

ACT imeshaanza harakati za kigaidi kama Ile Ngangari ya zamani. Na upenyo wa Magaidi siku zote ni kudhoofisha Polisi kwanza. Pumba kabisa.

Yaani ACT badala ya kupigania katiba mpya wao wanahamasisha uhalifu.

Utakuwa umeguswa vilivyo si kwa makasiriko haya.

Si mara moja nimeweka wazi kuwa, ni mhanga wa panya road lakini si mhanga wa washukiwa wa panya road. Ninawachukia panya road lakini siwachukii watuhumiwa wa panya road.

Huna kisichohitajika kukufanya kuwa mshukiwa wa panya road labda kama wewe ni polisi. Polisi wanaotaka kuwaaminisha wengine kuwa wao siyo panya road ndiyo hao hao waliopora na kuuwa Mtwara na kwingi kwingineko ikiwemo yaliyowahusu wale marehemu wafanyabishara wa Ifakara.

Mifano Iko mingi mno na orodha haina mwisho.

Mauaji ya Polisi dhidi watuhumiwa na hata wasiokuwa na hatia, hakuna asiyeyajua labda wewe nyuma ya wheel barrow hapo:

IMG_20220928_112538_686.jpg


Polisi kufanya kazi yake kwa mujibu wa sheria yaani kuzuia uhalifu, kupeleleza, kukamata baada ya upelelezi na kufikisha watuhumiwa mahakamani hakuna maana yako duni kabisa ya kuwa:

"Polisi kuwachukulia wahalifu kama wateja wanaosafiri na ndege na wageni KWENYE Gest .. au upuuzi zaidi ulioendelea kuandika."

Mada hii haina cha kufanya na ACT wala Abdul Nondo ambaye pia ajabu yake kaandika kama reporter tu.

Ni kwamba ndugu policeman:

IMG_20221001_234759_452.jpg


Mikono yenye damu ya awaye yote hatuitaki. Na hasa ya hawa tunaowaajiri, kupitia uharamia wao au mauaji kinyume cha sheria.

Upuusi mwingine ulioandika nadhani unaweza kwenda kuwaambia ndege.
 
Back
Top Bottom