#COVID19 Tuwatambue wanaohujumu vita dhidi ya Covid-19 nchini

#COVID19 Tuwatambue wanaohujumu vita dhidi ya Covid-19 nchini

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Hatimaye serikali ya awamu ya sita ilitangaza rasmi uwepo wa ugonjwa hatari wa Corona hapa nchini. Hii ikienda sambamba na kutolewa kwa maelekezo thabiti ya hatua gani za kuchukuliwa tunaposubiria kuwasili kwa chanjo.

Hatua hii ni njema kabisa ya kupongezwa na kila mzalendo na hasa kila muelewa.

Hata hivyo wamekuwapo wanaoendelea kushikilia misimamo isiyokuwa na mashiko kutokea awamu ile kuhusiana na huu ugonjwa. Wakihusianisha hatua hizi mpya za serikali na kiu tu cha mikopo kutoka kwa mabeberu.

Matokeo yake, hadi sasa takwimu za ugonjwa hazitolewi na mwitikio mzima wa hatua za tahadhari ni mdogo mno.

Tathmini ya kawaida inaonyesha kuwa asilimia kubwa ya watu wanaopinga mtizamo huu mpya wa serikali, ni wale wale ambao pia wanapinga kurejelewa kwa mchakato wa kupatikana kwa katiba mpya.

Wakati wanaounga mkono msimamo huu wa serikali, pia ndiyo wale wale wenye kuhitaji kurejelewa kwa mchakato wa kupatikana kwa katiba mpya.

Kuna elements za wazi za ujinga kwenye kupinga hatua hizi dhidi ya Corona. Wakati kuna elements za ujinga na ubinafsi uliopitiliza kwenye kupinga suala la mchakato wa katiba mpya.

Bila shaka habari za kuanzishwa kwa kiwanda cha kutengeneza chanjo za Corona nchini, ni namna ya kujaribu kuwapaka mafuta kwa mgongo wa chupa wajinga hao.

Ushauri wa bure kwa serikali inapohangaika kuwashawishi ndugu zetu hawa dhidi ya gonjwa hili:

"Serikali itangaze rasmi kusitisha jitihada zote za kupata mkopo wowote kuhusiana na ugonjwa huu au labda hata na kwa shughuli nyingine zozote ikibidi."

Ndugu zetu hawa hawaelewi kuwa mikopo huombwa tena kwa kunyenyekea. Ni fikra potofu kudhani kuwa pana mikopo mahali bwerere inayohitaji wakopaji."

Ni vyema serikali ikafanya hivyo huku ikitambua pia kwanini si sahihi sana nchi kuendekeza agenda zinazosukumwa na watu wenye uelewa mdogo (yaani wajinga).

Ninawasilisha.
 
Mkuu lazima wakupe medal kwa jinsi unavyolipigania swala la corona 😊😊🏃‍♀️

Uzuri ni kuwa hata recognition tu sihitaji.

Ila siyo siri: "ujinga unaudhi." Hasa hao wanapotaka kutuamulia hatma za maisha yetu.

Angalia wamekufa watu wangapi tokea March 2020 huku wakipigishwa nyungu, kulishwa malimao, michai chai au kupigishwa maombi?

Kama taifa - degeneration ya kiwango gani hii?
 
Uzuri wa corona inapita nao wale wanaoidharau, yenyewe haina shida hata kidogo ukiiheshimu.

Usisahau kuwa wanaokufa wasio na majina ni wengi zaidi.

Kwani hata hao wenye majina yupi waliyeridhia kuwa ni Corona?

Labda ungesema - uzuri ni kuwa tunapukutika sote!
 
Uzuri ni kuwa hata recognition tu sihitaji.

Ila siyo siri: "ujinga unaudhi." Hasa hao wanapotaka kutuamulia hatma za maisha yetu.

Angalia wamekufa watu wangapi tokea March 2020 huku wakipigishwa nyungu, kulishwa malimao, michai chai au kupigishwa maombi?

Kama taifa - degeneration ya kiwango gani hii?
Ni kweli unayosema Mkuu, Kama kuna mistake iliyofanywa na Tanzania dhidi ya mapambano dhidi ya corona , ni Rais kupiga siku tatu za maombi na ku declare hakuna corona, worse ni kuonyesha suspicions kwenye Chanjo,,,, aisee hii effect yake ni ngumu to mitigate!
 
Waziri wa Afya

Waziri wa afya alisongwa na jiwe. Kwa njaa zake akaukumbatia ujinga.

Hii ni sawa na wale wanaopinga katiba mpya kwa njaa zao tu: wakiwamo kina Pole pole, mparamagamba, bashiri, na wengi wa namna hiyo.

Tofautisha hapa na wale wanyonge, the brainwashed. Yaani wapiga debe, sungu sungu, boda boda, machinga nk.
 
Makuwadi na vibaraka wa mabeberu, unateseka sana.

Anayetaka mkopo ni kuwadi. Asiyetaka mkopo ni kuwadi. Huo ndiyo urithi wa sera za kijinga za jiwe:

IMG_20210706_203616_157.jpg


Bila shaka wewe hata katiba mpya hutaki wewe.

Hatuwezi kuwaachia mamburula nyie kuamua hatma za maisha yetu.
 
Nyie ndio mada inawahusu, kila jema hamlitaki, sijui nyie ni viumbe wa aina gani.
Huyo mrundi hajitambui. Imagine watu mnataka ati katiba mpya as if katiba ni finished product ipo mahali. Baadala ya kusema mnataka katiba mpya iwe na yafuatayo. Kwa sasa kuna version mbili za katiba ujue ya Warioba na ile ya kifisadi ya JK.

Katika duniani ya leo hakuna katiba iliyotungwa na interested parties ikawa kwa manufaa ya Umma. Lazima kuwepo na kifungu ambacho kitakataza mtu yeyote atakayejihusisha na katiba asigombee uongozi kwa muda kama miaka 20. Ref katiba ya Libya etc. Umesahau kuwa version ya Warioba ilikuwa safi maana Warioba hakuwa na tamaa ya kuwania madaraka. Umesahau JK aliuliza nyie wabunge hamtaki kuwa mawaziri? Kitu cha maana ni kufumua kwanza sheria.
 
Huyu jamaa anaipambania Corona sijapata kuona,ikitokea dunia nzima Corona iishe,itamuuma Sana,maana post zake nyingine ni corona.
Na bahati mbaya anachokitamani kitokee Tanzania kamwe hakitatokea.

Ndiyo maana akiandika anahimiza tahadhari kuchukuliwa?

Kuna kitu kimoja common kati ya wapinga tahadhari za ugonjwa huu na wapinga katiba kama wewe:

IMG_20210707_205907_958.jpg


Hicho kitu common kipo kwenye mada.

Utakuwa na wewe unapinga ujio wa katiba mpya.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Back
Top Bottom