Tuwatembelee Mapolisi wetu katika vituo vyao kuonesha Upendo

Polisi kabla hajavaa Gwanda ni binadamu.
Akitia gwanda mwilini tu, anabadilika kabisa na kuwa ibilisi.
 
Mtazamo ni kitu hatari sana...

kuna siku niliwahi kujiuliza, kwamba kwanini askari ukikutana naye mahali na ukamsalimia, wengi wao hujibu kwa ukali au kama hajapendezwa na salamu yako hivi.

Nikagundua kuwa kumbe kimachowatesa wao ni mtazamo ambao wamejiwekea kana kwamba mwananchi ni mkosaji hivi au ni mtu anayevunja sheria za nchi kitu ambacho si kweli.

Kitu cha kufurahisha zaidi ni kwamba polisi wote wanakili kuwa kazi yao ni kulinda raia na mali zao, sasa unajiuliza, unawezaje kumlinda mtu na mali zake ambaye unamuona ni kama adui hivi?

Bado kuna mambo tunatakiwa kujifunza..wenzetu walioendelea kwenye viwango vya ustaarabu, raia hata akiwa polisi anajiona yuko salama kwani kila kitu ni friendly, kimbembe ni huku kwenye ngozi nyeusi.
 
Hahahahahah Nenda wakupe kesi ya Ugaidi hahahaha
 
Anza wewe tuwekee na selfie ya mfano
 
Hawa Hawa polisccm. Aisee hapana. Na tatzo linaanzia kipewa hizi nafasi kwa wengi kua na uelewa mfogo. Make wengi ni la Saba na 4m fail.
 
Umefikiria nini! Au ulitaka kumaanisha tutembelee wafungwa!??
Enewei we ni polisi wa kituo gani kwani!?

KiChwa BoX
 

Inawezekana kabisa hongera kwa fikra pevu, fundamentally sisi sote ni polisi sema grassroots meaning na role yake imepuuzwa, raia ndio polisi namba moja
 
Mleta mada una kichaa wahitaji tiba, upendo upi tuwaonyeshe wakati wao hawana upendo na sisi, unaweza ukawatembelea kwa nia nzuri ukajikuta umepewa kesi ya uhujumu uchumi

Hebu tuache sisi
 
Mimi nina mpango wa kuwatembelea ila bado mzigo wangu haujafika,nimeagiza kutoka somalia.siku si nyingi nitaenda kuwatembelea nikiwa na mkanda wangu kwenye kindoo
 
Bora kutembelea kambi ya majambazi kuliko hao jamaa
 
Yani unataka kusema tuwatembelee wauwaji,majambazi,wala lushwa wenye uniform tena kwenye himaya yao aisee tunaishi nao lakini sio kuwaamini
 
Wao kwa wao tu hawaaminiani, sembuse wewe na saba juu (7up) yako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…