Tuwe objective: Mbowe ana sababu gani za kuendelea kuwa mwenyekiti wa CHADEMA

Tuwe objective: Mbowe ana sababu gani za kuendelea kuwa mwenyekiti wa CHADEMA

Its the right time chadema waka practice demokrasia wanayojinasabisha nayo. #Farewellfreeman
 
Mbowe must be respected, lakini hio haimanishi aendelee kuwa mgombea pekee wa uenyekiti, kwamba ndio anafaa pekee..ina mana miaka yote hii akiwa mwenyekiti chama hakijatengeneza wengine? Kama hakuna ina mana chama hiki bado hakiwezi aminiwa kuchukua hatamu za uongozi..ila kukiwa na wenye sifa zaidi ya mmoja hii ina manisha uhakika wa kuchukua madaraka ya nchi inawezekana. Chadema hebu ruhusuni wagombea wengine acheni uoga kwamba kama sio mbowe basi chama kitakufa au kukosa nguvu..
 
Mahitaji ya wakati kwa sasa ili upinzani uendelee kuwepo Tanzania unataka kiongozi mwenye sifa alizo nazo Mbowe..kuwa kiongozi wa chama cha upinzani Tanzania ni gharama kubwa, Lissu hawezi kubeba hiyo gharama hana energy za kufanya hivyo..hana!
Kwahiyo mpaka lini mfano? Yes the mana has energy..which energy? Ni udhaifu wa uongozi wa chadema kutoandaa competent candidates..wa kushika wadhifa huo kwakuwa ni mbowe pekee anatosha
 
Jana nimemsikia Mh. Lissu mwanzo mpaka mwisho
Nikiri kuwa sijasikia kama Freeman atagombea.
Nafahamu kwamba kwa heshima yake kama angekuwa hagombei anawaachia "vijana" basi angeshatoa taarifa mapema kidogo.
Kwa hiyo anaweza kugombea

Sasa nimekuwa najiuliza kama Mbowe ataamua kugombea uenyekiti atakuwa na sababu gani za kuamua kuendelea kuwa mwenyekiti kwa zaidi ya miaka 20.

Declaration of Interest
Namuunga mkono Lissu kuwa Mwenyekiti kwa sababu nzuri alizozitaja jana
Wachaga kuwatoa kwenye shamba la mgomba unataka vita nao
 
Kwahiyo mpaka lini mfano? Yes the mana has energy..which energy? Ni udhaifu wa uongozi wa chadema kutoandaa competent candidates..wa kushika wadhifa huo kwakuwa ni mbowe pekee anatosha
The way mnauliza ni km vile hali ya siasa za Tanzania ni plain kila kitu kiko sawa..unapofikiri nani anafaa kuwa kiongozi kwenye vyama vya upinzani, fikiri pia madhira na maumivu wanayopitia viongozi, utayari wa kubeba lawama, utayari wa kutumia rasilimali zako..fedha, muda, familia kutekeleza majukumu ili chama kisimame, kuangalia usalama na mahitaji ya wasaidizi wako na wanachama kwa ujumla, maumivu ya matukio ya kikatili kwa watu wa karibu.. km yale mauaji ya Mawazo kufariji familia zao na hata kuwasaidia binafsi, hii si nafasi ya kuikimbilia na kufanya ushabiki km wengi wanavyofanya!
Mpaka lini..inategemea aina ya watu chama kilio nao..uwezo na utayari kukipigania chama kulingana na nyakati, kuna nyakati chama kinahitaji kukua, kuna wakati kinahitaji kupambania uhai wake si kukua..kuna wakati kinahitaji maono mapya na watu wapya..hivyo si jambo la muda tu ndio factor ya kubadilisha uongozi wa chama!
Kuandaa competent candidates inawezekana, ndio maana wapo kina Mnyika, Heche, Sugu na wengine wenye msimamo waliokataa kucompromise! wakati wao utafika kulingana na mahitaji ya chama ya wakati huo..
 
Mbowe akigombea tena nitamuona yeye na kabila lake lote kama taka.taka
 
Mbowe must be respected, lakini hio haimanishi aendelee kuwa mgombea pekee wa uenyekiti, kwamba ndio anafaa pekee..ina mana miaka yote hii akiwa mwenyekiti chama hakijatengeneza wengine? Kama hakuna ina mana chama hiki bado hakiwezi aminiwa kuchukua hatamu za uongozi..ila kukiwa na wenye sifa zaidi ya mmoja hii ina manisha uhakika wa kuchukua madaraka ya nchi inawezekana. Chadema hebu ruhusuni wagombea wengine acheni uoga kwamba kama sio mbowe basi chama kitakufa au kukosa nguvu..
..unadhani hao wanaoshika hatamu za uongozi wa nchi wanakaa tu kutizama vyama pinzani wanaandaa successors kwenye uongozi wao..? weka listi mwenyewe ya waliomtangulia Msigwa kuhongwa vyeo wakasaliti chama Chao..chama kinafanya juhudi kuwa na successors wengi lkn binadamu tuna tofautiana..na sheria za kukataza wabunge kuhama chama huku wakiendelea kuwa wabunge zimewekwa makusudi kudhoofisha na kunyima vyama vya upinzani kukua!
 
Chadema ni chama kikuu Cha uponzani, Mimi sifikiri kuwa Lisu akigombea atakipasua chama Kwa kuwa kama jina la chama ni Chama Cha Demokrasia, sasa wakifanyie uchaguzi wa kidemokrasia na ili kudondoka utata na malalamiko,TLS wasimamie uchaguzi huo.
 
Kwa hiyo katiba yao wanavyoitii inahalalisha wao kubaki kutawala? Wewe umesema Mbowe ana muda mrefu, nimekuuliza ccm je mbona husemi wao pia wapumzike..unarukia katiba, katiba ndio zinapiga kura..
CCM wapumzike wapi na kivipi?

Kuhusu suala la ukomo wa Mwenyekiti na Uenyekiti wake ndani ya Chama na nchi kwa ujumla liko wazi kwa upande wao na wamekua wakiletekeleza bila kuacha. Kwa mujibu wa katiba yao ya Chama.

Why the comparisons?
 
Kusema Mbowe ana mafanikio gani wakati unafahamu fika vyama vyote vilivyowahi kuwa na mafanikio km chadema mf. Kuwa na idadi ya wabunge wengi wa kuchaguliwa..CUF, NCCR hata UDP vimebaki majina tu..lkn Chadema bado ipo..hayo ni mafanikio makubwa km unafahamu siasa za Tanzania..
Niseme kitu kimoja..hamsemi sifa gani zinafanya Lisu aaminiwe kuongoza chama..Lisu amedhulumiwa stahiki zake za ubunge, hadi Leo hajalipwa..hili ni jambo binafsi, pamoja na kuwa lawyer kitu gani kinafanya asidai stahiki zake km yeye ni jasiri..! Waliojaribu kuondoa uhai wake hadi Leo hakuna uchunguzi umefanyika..nini kinamzuia Lissu kupigania haki zake..na nyinyi mnaomsapoti mbona hatusikii mkisema mko nae kumsaidia apate haki zake? Anashindwa kutetea haki zake mwenyewe, hizo za chama ataweza? Wanaoshikilia haki zake ni wale wale wananyima haki za kufanya siasa kwa uhuru..kipi kinafanya aaminiwe kuongoza chama..!
Nasisitiza muda wa Mbowe kuendelea kuwa mwenyekiti umeshapita. Hayo mafanikio yake ni historia. Kuhusu Lisu kudai stahiki zake hilo amefanya, ila sio yeye mtoa haki, bali ni mifumo ya kutoa haki imeoza. Unataka Lisu aache kuleta mabadaliko ndani ya cdm kisa mifumo ya nchi ya kutoa haki imeoza? Sisi tuna muamini maana ameahidi kuleta mabadiliko ndani ya cdm, huku Mbowe akiwa hana jipya la kuipatia cdm.
 
Bila Mbowe hakuna CHADEMA, mwamba ndio mbeba maono
 
Muacheni Mbowe na Chadema yake, wasiompenda waende kwa Mutungi wakasajiri chama wamkabidhi Lisu.
 
Jana nimemsikia Mh. Lissu mwanzo mpaka mwisho
Nikiri kuwa sijasikia kama Freeman atagombea.
Nafahamu kwamba kwa heshima yake kama angekuwa hagombei anawaachia "vijana" basi angeshatoa taarifa mapema kidogo.
Kwa hiyo anaweza kugombea

Sasa nimekuwa najiuliza kama Mbowe ataamua kugombea uenyekiti atakuwa na sababu gani za kuamua kuendelea kuwa mwenyekiti kwa zaidi ya miaka 20.

Declaration of Interest
Namuunga mkono Lissu kuwa Mwenyekiti kwa sababu nzuri alizozitaja jana
Lissu hawezi kuendesha CDM kidiplomasia baba yeye ni activist anahitaji ukomavu zaidi.
 
Sifa alizotaja Lissu jana..ni sifa gani hakuwa nayo wakati Mbowe anagombea uenyekiti mara ya kwanza? Km vile viungo vya mwili vinavyohitajiana na uongozi kwenye kundi ni hivyo hivyo, mkono hauwezi kufanya kazi za kichwa..Lissu hawezi kazi/majukumu ya kuwa Mwenyekiti..anaweza kuwa msaidizi..ukizitambua kazi za kichwa cha mnyama, hizo ndio sifa za Mbowe kuwa Mwenyekiti Chadema..tujifunze kujua vyama vina maelekezo ya waliobeba maono wakati kinaanzishwa vzr kuyazingatia kuliko jazba za ujana..kwa anayesoma vitabu pekee vyenye umri mrefu kupita vitabu vingine vyote..vina mifano ya kutahadhalisha jamii kufuata msimamo wa vijana au kusikiliza maneno yao..9 kati ya 10 yana mwelekeo wa uharibifu na si kujenga.
Mbowe hana jipya na uzee wake hauna msaada kwa CHADEMA na kwa upinzani na muelekeo wake kwa ujumla.

Uanaharakati wake hauna ubunifu wowote wenye kuendana na mahitaji ya kisiasa, miaka ile ya 2004-2005 alikuja na sera za kuandika makala kwenye gazeti la Tanzania Daima na haya anayoyaongea majukwaani hayana tofauti na zile makala zake zenye nia ya kuamsha mapambano miongoni mwa vijana.

Alichotaka kitokee September 23 mwaka huu hakina tofauti na yote aliyokuwa akiyaandika miaka ile, kwa ufupi hana jipya kwa kulinganisha na namna ilani ya uchaguzi ya CCM inavyoweza kukamilishwa ukurasa mmoja hadi mwingine..
 
Back
Top Bottom