Tuweke Historia Sawa. Tuwajadili Marais wa Tanzania tukianzia na Nyerere

Tuweke Historia Sawa. Tuwajadili Marais wa Tanzania tukianzia na Nyerere

FaizaFoxy

Platinum Member
Joined
Apr 13, 2011
Posts
100,246
Reaction score
123,145
Mwaka huu wa 2022 unatuingiza mwaka wa 61 toka Tanganyika tupate Uhuru.

Kwanza na "declare interest", binafsi nimezaliwa Tanganyika, kwa maana nimezaliwa kabla ya Uhuru na kabla ya muungano. Namshukuru Mwenyezi Mungu nimezipitia awamu 7 za uongozi wa nchi yetu hii ambayo sasa inaitwa Tanzania. Nimepitia awamu ya utawala wa Muingereza kwa kuzaliwa kabla ya Uhuru na na nimepitia awamu zote zilizofatia baada ya Uhuru.

Nimeiishi historia yetu, mengi nayatazama kwa mtazamo wa 'nilikuwepo". Kwa kuwa historia ya nchi huhusisha mambo mengi na awamu nilizopitia zilipita kwenye aina nyingi za kisiasa, kiuchumi, kimichezo, kijamii na kimaisha kwa ujumla. Nafahamu uzi huu utaibua hisia na mitazamo tofauti. Tuujadili kiuungwana, kwa heshima na taadhima na tuvumiliane mitazamo yetu, kwani kila mmoja wetu anayo anayoyafahamu kwa mtazamo wake a kwa kusikia kwake au kwa kusomeshwa kwake.

Kuna yaliofurahisha na kuchukiza katika historia yetu kwa kila mmoja wetu kwa muono wake.

Kwa mtazamo wangu, Mwalimu Nyerere alifurahisha alipoongea, alikuwa ni muongeaji mzuri na mchekeshaji mzuri. Katika uongozi wa nchi, naamini kabisa Nyerere alishindwa kabisa katika mambo ya uchumi.

Tuendelee....
 
Uzi WA kijinga
Luna...
Hujafanya uungwana kutumia neno, "ujinga."
Kwa ufupi sana umetukana.

Ungeweza ukasema mathalan, "si kweli," au ukatumia neno lolote lile la kistaarabu.

Prof. Ali Mazrui si mjinga.

Prof. Mazrui katika kuchambua hali ya Tanzania wakati wa Mwalimu alitumia neno hili, "heroic failure," akiwa na maana "kushindwa kishujaa.'

Ninachokuomba usiondoke hapa bakia umsome Maalim Faiza upime "intellect," yake.

Utastarehe
Huyu ni "above average.''

Wewe kwa kuchangia tusi tayari wasomaji weshakupima na kutambua uwezo wako.

Mimi sitakuita mjinga nitasema una papara.

Wewe una haraka.
Hujui kufikiri.

Huna uwezo wa kupima.
 
Uzi WA kijinga
Umekosea sana!
Mada kama hizi ni maeneo adhimu ya kupata historia ya nchi yetu kwa walioiishi.Unapoteza nafasi muhimu sana nakusikitikia.
Dada FaizaFoxy kwanza shikamoo.
Pili nishike nafasi hapa jioni nipate wasaa wa kujadili hii mada murua.
Kiufupi nami nimepitia utawala wa Marais wote baada ya Uhuru,hakuna kipindi kilichoNITISHA kama awamu ya 5.
 
Mwaka huu wa 2022 unatuingiza mwaka wa 61 toka Tanganyika tupate Uhuru.

Kwanza na "declare interest", binafsi nimezaliwa Tanganyika, kwa maana nimezaliwa kabla ya Uhuru na kabla ya muungano. Namshukuru Mwenyezi Mungu nimezipitia awamu 7 za uongozi wa nchi yetu hii ambayo sasa inaitwa Tanzania. Nimepitia awamu ya utawala wa Muingereza kwa kuzaliwa kabla ya Uhuru na na nimepitia awamu zote zilizofatia baada ya Uhuru.

Nimeiishi historia yetu, mengi nayatazama kwa mtazamo wa 'nilikuwepo". Kwa kuwa historia ya nchi huhusisha mambo mengi na awamu nilizopitia zilipita kwenye aina nyingi za kisiasa, kiuchumi, kimichezo, kijamii na kimaisha kwa ujumla. Nafahamu uzi huu utaibua hisia na mitazamo tofauti. Tuujadili kiuungwana, kwa heshima na taadhima na tuvumiliane mitazamo yetu, kwani kila mmoja wetu anayo anayoyafahamu kwa mtazamo wake a kwa kusikia kwake au kwa kusomeshwa kwake.

Kuna yaliofurahisha na kuchukiza katika historia yetu kwa kila mmoja wetu kwa muono wake.

Kwa mtazamo wangu, Mwalimu Nyerere alifurahisha alipoongea, alikuwa ni muongeaji mzuri na mchekeshaji mzuri. Katika uongozi wa nchi, naamini kabisa Nyerere alishindwa kabisa katika mambo ya uchumi.

Tuendelee....
Kwa hiyo mama yangu hapa tunajadili umahiri wa kuongea au uwajibikaji wa marais wetu.kama ni kuongea nchi ina wasanii sana hii zilongwa mbali zitendwa mbali,tuwajadili kwa vitu vizito na sio blabla zao nyerere hakushindwa kiuchumi,alijenga viwanda vingi na pesa ilikuwa na thamani sema idea ya ujamaa ilisalitiwa na wahuni wachache pia vita vya Idi Amini Dada vilimuangusha
 
Alishindwa kwenye mambo ya uchumi !

Alitumia mtaji kiasi gani na alizalisha kiasi gani..., Inabidi tupime input na output pia

Sasa hivi unaweza kudhani watu wamefaulu kwenye uchumi kwa watu kupata vijipesa ila at what cost (kuna tofauti kati ya kutokuzalisha mali zaidi bali kuitunza wakati ukifika iweze kuzalishwa... na kuamua yote kuiuza / kuigawa ili upate short term gains)

Kwahio at least hakufuja mtaji kuliko waliofuata mtaji wanafuja with nothing to show for it, apart from their own bellies...
 
Kwa hiyo mama yangu hapa tunajadili umahiri wa kuongea au uwajibikaji wa marais wetu.kama ni kuongea nchi ina wasanii sana hii zilongwa mbali zitendwa mbali,tuwajadili kwa vitu vizito na sio blabla zao nyerere hakushindwa kiuchumi,alijenga viwanda vingi na pesa ilikuwa na thamani sema idea ya ujamaa ilisalitiwa na wahuni wachache pia vita vya Idi Amini Dada vilimuangusha
Sera zake za kiuchumi hazikufanikiwa kutokana na kuwa baadhi ya maamuzi yalikuwa ni 'one man show'. Kuna mzungu mmoja (Canadian) miaka mingi aliniambia dalili za kuanguka kwa uchumi wa Tanzania zilianza kujitokeza tangu mwaka 1974 na alinipa sababu kadhaa (yeye alikuwa ni economist). Lakini hasa la kutaifisha viwanda na mashamba yaliyumbisha sana uchumi wa nchi kwani waliokabidhiwa hivo vitu hawakuwa na uzoefu wa kuviendesha.

Hata hivyo kila utawala ulikuwa na mema yake na yasiyo mema pia kwani changamoto zilikuwa tafauti. Mfano katika kipindi cha Nyerere ndiyo tuliona vijana 'wateka nyara' walijitokeza mara mbili, pia tuliona majaribio ya kutaka kupindua serikali mara mbili. Hizi changamoto hazikuwepo katika awamu nyingine.
 
Nyerere aliendesha inchi ktk kipindi kigumu sana. Inchi haikua na infastructures wala wasomi. And the most important alijua athari za kutumia resources zilizipo ardhini, yumkini tungalikua km congo ya leo km angetuonjesha asali na level ile ya illeterate.

Bt he laid the foundation ambayo viongozi waliomfuata wanapita, thus why we call him a founding father.
Ukitaka tuwalinganishe ki uchumi then inabidi managerial position ziongozwe na form4, stnd 7, 6 kwa mbaaali na chuo wa kuhesabu and waachane na madini or gas then waendeshe inchi kwa Kilimo na viwanda.
All in all alituleta pamoja, kiswahili kikatuunganisha,akapunguza gape la wenye nacho na wasio nacho(bila hili tungekua km kenya or sa), ukabila na udini ukapotea angawa time to time kuna watu hua wanaurudisha and for that we thank him maana ktk nyumba kitu cha msingi kuliko vyote ni msingi na alitujengea msingi imara.
 
Nyerere aliendesha inchi ktk kipindi kigumu sana. Inchi haikua na infastructures wala wasomi. And the most important alijua athari za kutumia resources zilizipo ardhini, yumkini tungalikua km congo ya leo km angetuonjesha asali na level ile ya illeterate.

Bt he laid the foundation ambayo viongozi waliomfuata wanapita, thus why we call him a founding father.
Ukitaka tuwalinganishe ki uchumi then inabidi managerial position ziongozwe na form4, stnd 7, 6 kwa mbaaali na chuo wa kuhesabu and waachane na madini or gas then waendeshe inchi kwa Kilimo na viwanda.
All in all alituleta pamoja, kiswahili kikatuunganisha,akapunguza gape la wenye nacho na wasio nacho(bila hili tungekua km kenya or sa), ukabila na udini ukapotea angawa time to time kuna watu hua wanaurudisha and for that we thank him maana ktk nyumba kitu cha msingi kuliko vyote ni msingi na alitujengea msingi imara.
Gobole,
Usiguse suala la udini.

Tanganyika hapajukuwa na tatizo la ukabila wala udini wakati wa ukoloni.

Nyerere mwenyewe ni shahidi wa hili.

Kapokewa na Waislam katika mji wa Waislam wakamchagua kuwa kiongozi na wakaishi na yeye kwa salama na mapenzi makubwa hadi uhuru ulipopatikana.

Udini uliokuwapo wakati wa ukoloni ni wamishionari kutoa elimu kwa ubaguzi wakitumia shule zao kueneza Injili.

Mimi nakusihi hili suala tusiliguse.

Ama hili la kutuunganisha linahitaji maelezo.

Waafrika wa Tanganyika waliunganishwa na African Association toka mwaka wa 1929 na kutokana na chama hiki kikaundwa chama cha TANU 1954.

Kila palipokuwa na tawi la African Association pakawa na tawi la TANU.

Soma historia ya kweli ya TANU utawaona ni akina nani waliokuwa mbele ya chama hiki kuunganisha watu na nani walikuwa wanawatisha watu wasijiunge na TANU.

Kuhusu Kiswahili lugha hii imesemwa karne nyingi nyuma.

Nyerere hakuzaliwa anasema Kiswahili yeye lugha yake ni Kizanaki na wengi kutoka bara waliokuja pwani hali ni hii.
 
Gobole,
Usiguse suala la udini.

Tanganyika hapajukuwa na tatizo la ukabila wala udini wakati wa ukoloni.

Nyerere mwenyewe ni shahidi wa hili.
Kapokewa na Waislam katika mji wa Waislam wakamchagua kuwa kiongozi na wakaishi na yeye kwa salama na mapenzi makubwa hadi uhuru ulipopatikana.

Udini uliokuwapo wakati wa ukoloni ni wamishionari kutoa elimu kwa ubaguzi wakitumia shule zao kueneza Injili.

Mimi nakusihi hili suala tusiliguse.
Mchango mzima umeona issue ya udini tu?
Mzee kuna sehemu kuna tatzo.
And why do keep reminding us kua Nyerere alipokelewa na waislamu?almost 90% ya michango yako humu JF unagusia hili?cant you find something new to inform us?
 
Mchango mzima umeona issue ya udini tu?
Mzee kuna sehemu kuna tatzo.
And why do keep reminding us kua Nyerere alipokelewa na waislamu?almost 90% ya michango yako humu JF unagusia hili?cant you find something new to inform us?
Goble,
Hukupenda mimi kueleza niyajuayo kwenye nukta hii muhimu ya udini uliyoileta?

Michango yangu si 90% udini ni 100% kuhusu Waislam na Uislam na sijaelezwa kuwa hairuhusiwi.

Hili ndilo jipya ambalo wengi hamkuwa mnalifahamu.

Kuna yeyote hapa aliyekuwa anajua mchango wa Waislam katika kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika?

Ushakaa kitako ukajiuliza kwa nini hamkuwa mnaijua historia hii?

Kama yupo aliyekuwa anaijua aonyeshe kidole.
 
Goble,
Hukupenda mimi kueleza niyajuayo kwenye nukta hii muhimu ya udini uliyoileta?

Michango yangu si 90% udini ni 100% kuhusu Waislam na Uislam na sijaelezwa kuwa hairuhusiwi.

Hili ndilo jipya ambalo wengi hamkuwa mnalifahamu.

Kuna yeyote hapa aliyekuwa anajua mchango wa Waislam katika kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika?

Ushakaa kitako ukajiuliza kwa nini hamkuwa mnaijua historia hii?

Kama yupo aliyekuwa anaijua aonyeshe kidole.
Hili jambo unalolizingumzia halina upya wowote, kila siku unaliongelea, labda km ni jipya ktk uzi huu ila kwa sisi tunaokufahamu humu ndani hakuna jipya...its too boring, plz tuambie kitu kipya ambacho hujawahi kukisema kt nyuzi nyingine.
 
Michango yangu si 90% udini ni 100% kuhusu Waislam na Uislam na sijaelezwa kuwa hairuhusiwi.
Mzee wangu, ingawa mada imeanzishwa na muumini mwenzio, sidhani kama alikusudia kuzungumzia Uislamu katika mada yake hata kama ungehamasishwa vipi, ungejikita kwenye mada tu ili sisi tuliozaliwa kipindi cha Ari mpya tupate madini na kupima wenyewe, nani ni nani!

Mji wa waislamu, wakristo, wapagani, n.k ni upi, kuanzia kipindi gani? Waliupataje, wakajimikishaje? Hii nchi iliyoitwa Tanganyika, ilianza kuitwa lini Tanganyika? Kipindi hicho, hizi imani zilikuwepo? Kabla ya hizo vamizi, kulikuaje? n.k

Hiyo pia ni mada tofauti ambayo pengine wewe na mtoa mada kwa pamoja, kwa hadhina ya umri mliyonayo, bila kuwa biased mnaweza kutujaza madini pia.

Leo tujikite kwenye mada iliyopo mezani mzee.
 
Kwa mtazamo wangu, Mwalimu Nyerere alifurahisha alipoongea, alikuwa ni muongeaji mzuri na mchekeshaji mzuri. Katika uongozi wa nchi, naamini kabisa Nyerere alishindwa kabisa katika mambo ya uchumi.

Tuendelee....
Mkuu FaizaFoxy , kwanza asante sana kwa uzi huu, pili nikupongeze as you grow older, you transforms as an old wine, as old as it's gets, the better it becomes, you are wiser and more objective, nimefurahi leo umemuanzishia Mwalimu Nyerere, a positive thread bila kulitumia lile neno lako la laanatulah kila ukimtaja Mwalimu Nyerere. Thanks for this. Nasubiria kwa makini to get the real motive behind this thread. All the best.

P
 
Goble,
Hukupenda mimi kueleza niyajuayo kwenye nukta hii muhimu ya udini uliyoileta?

Michango yangu si 90% udini ni 100% kuhusu Waislam na Uislam na sijaelezwa kuwa hairuhusiwi.

Hili ndilo jipya ambalo wengi hamkuwa mnalifahamu.

Kuna yeyote hapa aliyekuwa anajua mchango wa Waislam katika kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika?

Ushakaa kitako ukajiuliza kwa nini hamkuwa mnaijua historia hii?

Kama yupo aliyekuwa anaijua aonyeshe kidole.
Mzee wangu naomba niseme kidogo juu yako.
Unajua sumu ya udini huanza na mtu mmoja hatimaye huenea.
Unaonaje uanze kubadilika kidogokidogo kuhusu udini?
Mafikiri hao wazee wa kiislam unaweza kuwatazama kama Watanganyika wakazi wa Pwani kuliko kila wakati unawarejea kwa imani zao?
 
Mkuu FaizaFoxy , kwanza asante sana kwa uzi huu, pili nikupongeze as you grow older, you transforms as an old wine, as old as it's gets, the better it becomes, you are wiser and more objective, nimefurahi leo umemuanzishia Mwalimu Nyerere, a positive thread bila kulitumia lile neno lako la laanatulah kila ukimtaja Mwalimu Nyerere. Thanks for this. Nasubiria kwa makini to get the real motive behind this thread. All the best.

P
Mkuu FaizaFoxy , wakati nikichangia uzi huu, nilikuwa nimesoma post no. 1 tuu ya thread starter, ya Dada Mtu, kumbe post number 3, Kaka Mtu, tayari ametia timu!. More and more concern about the motive behind!. Let me sit front seat and watch haswa kwa kuzingatia the equation is now balance, 3 X 3. Its very unfortunatey our 3 are all down, 6ft under, and the other 3, are still up!. Naendelea kusubiria the motive behind!.
P
 
Back
Top Bottom