Tuweke Historia Sawa. Tuwajadili Marais wa Tanzania tukianzia na Nyerere

Tuweke Historia Sawa. Tuwajadili Marais wa Tanzania tukianzia na Nyerere

Luna...
Hujafanya uungwana kutumia neno, "ujinga."

Kwa ufupi sana umetukana.

Ungeweza ukasema mathalan, "si kweli," au ukatumia neno lolote lile la kistaarabu.

Prof. Ali Mazrui si mjinga.

Prof. Mazrui katika kuchambua hali ya Tanzania wakati wa Mwalimu alitumia neno hili, "heroic failure," akiwa na maana "kushindwa kishujaa.'

Ninachokuomba usiondoke hapa bakia umsome Maalim Faiza upime "intellect," yake.

Utastarehe
Huyu ni "above average.''

Wewe kwa kuchangia tusi tayari wasomaji weshakupima na kutambua uwezo wako.

Mimi sitakuita mjinga nitasema una papara.

Wewe una haraka.
Hujui kufikiri.

Huna uwezo wa kupima.
Hakuna Cha maana mnachojadili zaidi ya UPUMBAVU tu.

Naona mmemiss sana kumtukana Nyerere.

Haya, Nyerere, Mkapa na Magufuli walikuwa Marais wabovu.

Mwinyi, Kikwete na Samia ni Marais BIRA KABISA.

Nimemaliza. Furahini sasa.
 
Gobole,
Usiguse suala la udini.

Tanganyika hapajukuwa na tatizo la ukabila wala udini wakati wa ukoloni.

Nyerere mwenyewe ni shahidi wa hili.

Kapokewa na Waislam katika mji wa Waislam wakamchagua kuwa kiongozi na wakaishi na yeye kwa salama na mapenzi makubwa hadi uhuru ulipopatikana.

Udini uliokuwapo wakati wa ukoloni ni wamishionari kutoa elimu kwa ubaguzi wakitumia shule zao kueneza Injili.

Mimi nakusihi hili suala tusiliguse.

Ama hili la kutuunganisha linahitaji maelezo.

Waafrika wa Tanganyika waliunganishwa na African Association toka mwaka wa 1929 na kutokana na chama hiki kikaundwa chama cha TANU 1954.

Kila palipokuwa na tawi la African Association pakawa na tawi la TANU.

Soma historia ya kweli ya TANU utawaona ni akina nani waliokuwa mbele ya chama hiki kuunganisha watu na nani walikuwa wanawatisha watu wasijiunge na TANU.

Kuhusu Kiswahili lugha hii imesemwa karne nyingi nyuma.

Nyerere hakuzaliwa anasema Kiswahili yeye lugha yake ni Kizanaki na wengi kutoka bara waliokuja pwani hali ni hii.
Udini mmeuchochea nyie vizee Kama wewe, kina sheikh Takadiri, Sheikh Ilunga Hussein, Sheikh Ponda.

Ndio maana enzi za zamani hata kina Bibi hawakuwa wakivaa Hijab, maana suala la dini halikuwahi kiwa Jambo serious sana Kama mlivyolifanya nyie takataka mliofuatia mpaka kuanza kuvalisha baraghashia, kanzu na hijab mashuleni na KUJENGA misikiti kwenye taasisi za umma.
 
Binafsi mimi Rais Shujaa wetu ni Nyerere

Na Rais fala kuliko wote ni mwendazake wa Chato. Tuendelee kumshukuru Mungu kwa kila jambo

Cc: mbunge wa chato MENGELENI KWETU
1. Julius Kambarage Nyerere
2. Samia Suluhu Hasan
3. Jakaya Mrisho Kikwete
4. Benjamin William Mkapa
5. Ally Hassan Mwinyi
6.. John Pombe Magufuli

Kila mtu ashinde mechi zake

You don’t get the drift, unatiririka tu, Wachaga wajinga sana kama Mbowe!

Hii ni divide et impera, amka!
 
Kama ni kwa mtazamo wako huo wa jina la Yesu, upo sahihi. Lakini kiuchumi naamini Nyerere alishindwa. Kwa Mkapa bado sijafika katika gumzo hili.
1. Nyerere
2. Mkapa
3. Kikwete
4. Samia
5. Mwinyi
6. Magufuli
 
Glenn,
Hapana udini hapa.

Naeleza historia ya uhuru wa Tanganyika na mchango wa Waislam katika kupambana na ukoloni.

Mimi sioni kama ni udini.

Ukiwa unataka tujadili udini nina mengi tofauti kabisa na haya unayosoma hapa.

Fungua uzi mpya utahakikisha ninayokueleza kuwa hii ni historia ya mchango wa Waislam katika kuunda TANU - 'a field of enquiry.''

Kwa nini niliamua kufanya utafiti na kuandika kitabu ni kuwa hii ni historia yangu ya wazee wangu na jamii yangu iliyofutika au kufutwa kwa kudhamiria.

Hii ni historia ya vizazi vitatu iliyokuwa hadi 1998 imeandikwa popote historia inayoanza mwishoni mwa 1800.

Historia hii inamuhusu sana babu yangu Salum Abdallah.

Yeye alikuwapo African Association ilipoundwa na alikuwapo TANU ilipoasisiwa na kashiriki kwa hali na mali kupigania uhuru wa Tanganyika.

View attachment 2252696
View attachment 2252700View attachment 2252703
Huyu Selemani Mamba alikuwa 'chief' wa eneo lolote hapa Tanganyika? Au ni mmoja wa wafusi wa Kinjekitile ?

Ile 'dawa' ya Kinjekitile ilikuwa na ukweli wowote au ilikuwa mbinu tu ya kuwahamasisha raia kupinga ukoloni ?....
 
Huu mjadala sasa hivi utabadilika kwenye udini watu wa Msikiti wataanza kupambana na ndugu zao wa Kanisani.
 
Si tatizo la kutumia au kutokutumia mtaji.

Kumbuka kuwa Nyerere aliichukua nchi ikiwa ni msafirishaji wa kwanza wa mazao ya mashamba katika Afrika, nchi yenye rasilimali tele, yenye miundombinu inayojitosheleza kwa wakati huo.
Unajua marginalization of the poor nations...., waliokuwa wanasafirisha kipindi hicho ndio wanunuzi washika mpini sasa unadhani baada ya hapo wangeendelea kununua kama kuna alternative ?, Pili unadhani waliondoka sababu walituonea huruma au it was no more profitable to run colonies...

Pili unadhani revampment ni kitu rahisi..., alivyorithi hio miundombinu n.k. alirithi wataalamu wangapi wenye technical know how..., pili bila kutaifisha baadhi ya shule n.k. na kulazimisha kwamba watu wote waweze kupata elimu angalau kidogo unadhani baadhi ya hawa waliopo hata wangesoma au wangeendelea kuwa watwana wa mabwana ?
Matokeao ndani ya miaka 10 tukawa masikini wa mwisho na omba omba wa kwanza katika Afrika. Hadi hii leo, kwa maneno ya "Bwana Mapesa - "Nchi omba omba". Haujatuishia licha ya jitoihada za Kikwete kutuonodoa katika kuomba bajeti yetu toka asilimia zaidi ya 60 mpaka kutufikisha chini ya asilimia 40.
Kwamba aliondoka na rutuba na rasilimali zote hadi leo karne kadhaa mazao hayawezi kuota tena ?, At the time alikuwa na excuse ya vitendea kazi vibovu kama vile pilau na sasa hivi tuna matractor na combined harvester still watu wana njaa !! (Kweli tunahitaji emancipation from mental slavery)
Katuachia misingi mibovu ya uchumi ambayo itatuchukuwa muda mrefu sana kujing'atua kutoka kwenye umasikini.

Nadiriki kusema, misingi mibovu aliyotuachia inatupelekea hadi leo hii hatupo huru kiuchumi kama nchi.
Hio misingi aliyotuachia ni kwamba alituroga ?!!! Narudia tena ni kama mzazi mmoja ameacha mashamba mtoto analia mzazi hakuuza hilo shamba ili aweze kusoma na mwingine kauza hayo mashamba ili mtoto aweze kujipatia vijipipi kwa muda mfupi alafu tunamsifu huyo mzazi aliyeuza badala ya kumlaumu huyo mtoto kwanini hilo shamba ambalo mzee hakuliuza kwanini hajaliendeleza !!!!

Africans problems are more mentally than physically.... And with such thinking which majority of us have..., am a afraid we have still got a long way to go...
 
Mkuu FaizaFoxy , kwanza asante sana kwa uzi huu, pili nikupongeze as you grow older, you transforms as an old wine, as old as it's gets, the better it becomes, you are wiser and more objective, nimefurahi leo umemuanzishia Mwalimu Nyerere, a positive thread bila kulitumia lile neno lako la laanatulah kila ukimtaja Mwalimu Nyerere. Thanks for this. Nasubiria kwa makini to get the real motive behind this thread. All the best.

P
Aaah peleka pumba zako kwengine, usinipake mafuta kwa mgongo wa chupa.

Punguani wahed.
 
Aaah peleka pumba zako kwengine, usinipake mafuta kwa mgongo wa chupa.

Punguani wahed.
I thought you have grown into a wise old lady as you grow older, you become wiser..., kumbe I was wrong!. Zamani kila ukimtaja Mwalimu Nyerere, ulikuwa ukimtukana laanatulah, kitendo tuu cha kumtaja Mwalimu Nyerere this time bila kumtukana, it's a good start ya kuzeeka vizuri maana...
P
 
Safi kabisa mkuu umenena vilivyo
Faana...
Sina maana kuwa halifai kujadiliwa ila ni jambo ambalo mimi nina taarifa ambazo naona vibaya kuziweka hapa.

Lakini kwa anaetaka kusoma historia hiyo asome kitabu cha Abdul Sykes nimeandika kila kitu.
 
Faana...
Sina maana kuwa halifai kujadiliwa ila ni jambo ambalo mimi nina taarifa ambazo naona vibaya kuziweka hapa.

Lakini kwa anaetaka kusoma historia hiyo asome kitabu cha Abdul Sykes nimeandika kila kitu.

🙏
 
I thought you have grown into a wise old lady as you grow older, you become wiser..., kumbe I was wrong!. Zamani kila ukimtaja Mwalimu Nyerere, ulikuwa ukimtukana laanatulah, kitendo tuu cha kumtaja Mwalimu Nyerere this time bila kumtukana, it's a good start ya kuzeeka vizuri maana...
P
Weka ushahidi.
 
Bila maelezo ya ziada uzi wako hauna nia njema
 
I thought you have grown into a wise old lady as you grow older, you become wiser..., kumbe I was wrong!. Zamani kila ukimtaja Mwalimu Nyerere, ulikuwa ukimtukana laanatulah, kitendo tuu cha kumtaja Mwalimu Nyerere this time bila kumtukana, it's a good start ya kuzeeka vizuri maana...
P
Pascal,
Kuna mambo yanasikitisha yanapotokea.

Mwaka wa 1995 nilialikwa na jumuia moja kuzungumza Mnazi Mmoja katika muhadhara.

Wazungumzaji walikuwa wengi na mimi nilipangiwa kuzungumza baada ya Isha.

Msikiti wa Manyema ni jirani sana na Viwanja Vya Mnazi Mmoja na pia Ofisi Ndogo ya CCM Lumumba Avenue.

Baada ya sala natoka nje niende Mnazi Mmoja nikakutana na marehemu Sheikh Aboud Maalim, mmoja wa masheikh wenye kuheshimika sana.

Nikamwambia, ''Sheikh nimepangwa kuzungumza hapo Mnazi Mmoja na hivi ndiyo nakwenda lakini naogopa sana.''

Sheikh akanijibu, ''Unawaogopa watu au unaogopa mada yako?''
Shekh akaniombea dua nikaondoka.

Nilikuwa naogopa kwa sababu nilikuwa sijapata kuzungumza katika uwanja wa wazi na umma ulikuwa umefurika.

Miaka ile Waislam walikuwa wamekuja juu sana wanauliza mengi serikalini.
Mada yangu ilikuwa ''Historia ya Uhuru wa Tanganyika.''

Katikati ya mhadhara nikataja jina.
Nikapokelewa na kibwagizo.

Nilipigwa na mshangao kama nimesikia sawasawa au vipi.

Hii ilikuwa mara yangu ya kwanza kusikia kibwagizo hicho lakini nikawa kama vile akili yangu inakataa kuamini kama kweli nimesikia sawasawa.

Nikakisikia tena kibwagizo kile.
Niliingiwa na hofu na njia pekee kwangu ikawa ni kuacha kulitaja jina lile.

Nilishangaa kuwa hapo ndipo tulipofika.

Asubuhi hata saa nne haijafika cassettes za ule muhadha wangu ziko mitaani zinauzwa na zinanunuliwa kama vitumbua vya moto.

Nilialikwa Zentrum Moderner Orient (ZMO) Berlin kufanya mhadhara na mada yangu ilikuwa historia ya uhuru wa Tanganyika na mashujaa wake waliosahauliwa.

ZMO ni taasisi kubwa sana katika utafiti wa historia.

Katika mhadhara wangu nilieleza jinsi Tanzania ilivyobadilika na nikaeleza yale yaliyonifika Mnazi Mmoja.

Mhadhara wangu uliwafadhaisha wengi katika yale waliyosikia kutoka kwangu na wakaniambia kuwa wamepita wahadhiri wengi kutoka Tanzania na wamezungumza historia ya uhuru lakini yale waliyosikia kutoka kwangu yalikuwa mageni masikioni mwao.

Siku ya kuagana Mkurugenzi wa ZMO aliniita ofisini kwake na kuniuliza maswali mengi lakini swali moja ambalo lilinigusa sana ni pale alipotaka kujua nini kimesababisha hali ile?

Wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika mama zetu katika mikutano ya TANU walikuwa wakitengewa sehemu maalum wasichanganyike na wanaume.

Akina mama hawa walikuwa na wimbo wakiimba katika mikutano ile ubeti wa mwisho ulikuwa unasema hivi., ''In Shaa Allah Mungu yupo Tanganyika tutajitawala.

Naweka picha moja ya mikutano ya TANU ya mwanzo na tazama kushoto utaona weusi hayo ni mabaibui waliyokuwa wanavaa mama na shangazi zetu.

Pascal.
Ulikuwa unaujua wimbo huu au historia hii?
Umepata kujiuliza kwa nii leo imekuwa hivi?

Chuki hizi nini sababu yake?

1654630537156.jpeg

Picha kwa hisani ya watoto wa Mohamed Shebe aliyekuwa mpiga picha wa TANU kwa kujitolea.
 
Hapo kwenye kufeli kwa uchumi nakuunga mkono.
Ishu ya ujamaa haikuwa sahihi kabisa. Ilileta uvivu sana. Ona wenzetu Kenya.
Kimlolongo wa madaraka Mkapa alitakiwa awe Rais wa kwanza
Sera za Magufuli ndio alitakiwa awe rais wa kwanza au wa pili.
Kikwete angefuata then hao waliobakia walitakiwa waje mwaka 2355
Mwaka huu wa 2022 unatuingiza mwaka wa 61 toka Tanganyika tupate Uhuru.

Kwanza na "declare interest", binafsi nimezaliwa Tanganyika, kwa maana nimezaliwa kabla ya Uhuru na kabla ya muungano. Namshukuru Mwenyezi Mungu nimezipitia awamu 7 za uongozi wa nchi yetu hii ambayo sasa inaitwa Tanzania. Nimepitia awamu ya utawala wa Muingereza kwa kuzaliwa kabla ya Uhuru na na nimepitia awamu zote zilizofatia baada ya Uhuru.

Nimeiishi historia yetu, mengi nayatazama kwa mtazamo wa 'nilikuwepo". Kwa kuwa historia ya nchi huhusisha mambo mengi na awamu nilizopitia zilipita kwenye aina nyingi za kisiasa, kiuchumi, kimichezo, kijamii na kimaisha kwa ujumla. Nafahamu uzi huu utaibua hisia na mitazamo tofauti. Tuujadili kiuungwana, kwa heshima na taadhima na tuvumiliane mitazamo yetu, kwani kila mmoja wetu anayo anayoyafahamu kwa mtazamo wake a kwa kusikia kwake au kwa kusomeshwa kwake.

Kuna yaliofurahisha na kuchukiza katika historia yetu kwa kila mmoja wetu kwa muono wake.

Kwa mtazamo wangu, Mwalimu Nyerere alifurahisha alipoongea, alikuwa ni muongeaji mzuri na mchekeshaji mzuri. Katika uongozi wa nchi, naamini kabisa Nyerere alishindwa kabisa katika mambo ya uchumi.

Tuendelee...
 
Back
Top Bottom