Tuweke kumbukumbu zetu sawa, huu ndo uchumi wa Magufuli aliouacha, all facts! - Sehemu ya kwanza

Tuweke kumbukumbu zetu sawa, huu ndo uchumi wa Magufuli aliouacha, all facts! - Sehemu ya kwanza

Hii ni sehemu ya kwanza, nta cover sekta ya biashara, uwekezaji wa nje, viwanda, na ntaelezea kwa kina kuusu madeni ya taifa..

Ila conclusion kabisa ni kwamba 'Magufuli alichofanya ni kukopa pesa nying nje na kufanya plundering ya pesa za wafanya biashara kupitia kodi za kidhalimu ili kujenga uchumi ambao ulielemea katika projects kubwa za miundo mbinu ambayo bado hatujajua itakamilika lini'
Naamini kabisa pamoja na kwamba upo Nje ya BUNGE mchango wakoo huu ulio uwakilisha hapa ni zaidi ya wabunge waliopo BUNGENI

Mungu akubariki
 
Hata kama sijui kuandika,ila ujumbe umefika, serikali ya Jk ilijaa majizi wapigaji,wala rushwa,na wauza madawa ya kurevya,inawezaka nawewe ulikuwa miongoni,eti mnajifanya wachambuzi wa uchumi, wakati WB walisema uchumi wa Tanzania umekua mpaka kupifiki wa kati na GDP imepanda,eti anatoka mtu ajiita Namtombe anasema Jpm amealibu uchumi,na kuna watu wanashangiria, ukiuliza kwa takwimu zipi!unaambiwa ukuna pesa mtaani,utafikiri pesa ni mabomba ya maji kupatika kila nyumba.
Nawashangaa wanaobishana na WB walio ona uchumi wa Tanzania unakua kwa kasi. Hadi tukapanda kuwa uchumi wa Kati. Watu wanakuja na takwimu zao za kishule shule hapa badala ya actual economy. Moja ya uchumi kukua ni uimarishaji wa huduma kwa wanannchi, hii ni pamoja na afya, Elimu, na miundo mbinu.
Watanzania baadhi walizoea ubadhirifu wa mali ya umma. Sekta binafsi ilitegemea michongo, kuonga na kujichukulia fedha ya serikali na kutoa huduma dhaifu. Mfano makandarasi wengi walijenga barabara au majengo ya serikali yasiyokuwa na kiwango huku wakiwa wamelipwa fedha nyingi. Hela iliyokuwa ikizagaa mtaani ilikuwa fedha ya dhuruma, madawa ya kulevya na ubadhirifu.

Nchi za Ulaya huwezi kuta fedha inazagaa mtaani. Sweden ni moja ya nchi ambayo ni wakali kwa kodi. Hawabembelezi mtu hata awe mfanya biashara mkubwa. Kuna baadhi ya mashirika makubwa ya biashara Sweden yamehama kwa kulalamikia kodi. Na utaratibu wa kulipia kodi Sweden ulianzishwa na kusisitizwa kwa lazima na aliekuwa mfalme wao Gustav, wanasema huyu watu walimchukia kwa ajili ya kuhimiza kodi. Lakini leo wanafurahi na kumkumbuka kuwa ameifanya Sweden kuwa kama leo ilivyo.
Katika serikali ya kikwete, kulikua na mambo mengi machafu, fedha ilichotwa. Hakukuwa na huduma kwa wananchi iliyowawezesha. Watu wa juu kimaisha waliendelea kuwajuu, na masikini aliendelea kuwa masikini.

Nakumbuka naanza kazi, ikaletwa orodha ya malipo ya mshahara, ambayo mimi na mwasibu wangu tulikuwa tunaipokea na kukagua kama wafanyakazi wote wamepata haki zao. Kilichokuwa kinanishangaza na ugeni wangu katika utumishi wa umma, katika orodha ya malipo ya mshahara kulikuwa na majina yapata kumi. Hawa watumishi sikuwajua na sijawahi waona ofisini. Nilimuuliza mhasibu kwani yeye alikuwa mtu mzima ambae kesha kaa katika utumishi yapata miaka 30. Akanambia aya majina hawa watu wengine walishafariki, na wengine kuacha kazi, lakini mishahara yao inaingia hiyo fedha ni ya wakubwa. Nilimwambia tuzuie. Akasema haiwezekani kwani huo ni mtandao mkubwa unaanzia juu. Hii niliiona kwa macho yangu na kushuhudia.

Utawala wa Kikwete posho zilikuwa nyingi. Mtu unaweza pokea posho mbili hadi Tatu wakati umeshalipwa kwa kazi husika. Watu hawakufanya kazi kilichotazamwa ni posho tu. Nilikuwa na ndugu yangu ambae yeye, alikuwa akiingia Bank kuu, anachota pesa huyu alikuwa na wakubwa fulani wa hii nchi. Aliweza ingiza watu weki bank kuu kufanya kazi na baadhi ya mashirika makubwa kama PSPF na kadhalika. Alikuwa na fedha haswa. Lakini baada ya Magufuli kuingia mirija yote ilikata.

Wakati wa Kikwete, wanafunzi wengi waliofahulu walishindwa kwenda shule, kwa kukoswa uniform, ada na michango ya madawati au mingineyo. Nakumbuka nikiwa mtumishi wa umma, ilinibidi kusomesha watoto 10. Pia niliongea na baadhi ya mashirka kuwasaidia baadhi ya wanafunzi wapatao 80 hawa walisomeshwa na hayo mashirika. Na hawa wanafunzi wengi wao walikuwa masikini wa kutupwa katika familia zao.

Naongea vitu ambavyo nilivishuhudia mwenyewe. Situmii theory ya kukariri darasani la asha. Nilishuhudia matajiri wakubwa wenye uwezo walivyokuwa wameiweka serikali mfukoni. Watumishi mbalimbali walionewa na kunyimwa haki zao hasa katika sekta binafsi. Kuna issue moja ya wahindi ambao baada ya kumsaidia mtumishi mmoja alodhulumiwa haki yake. Mmoja wa wahindi hao ambae ni mfanya biashara mkubwa linipigia simu na kunisihi niachane na hilo jambo. Nilipomkatalia alinitishia na kusema ataongea na Rais.
Nilimwambia ongea nae. Kipindi hicho kulijaa dhuruma na ufisadi wa hali ya juu. Wakubwa wengi walishiriki kuuza madawa ya kulevya na kujipatia mamilioni. Tunawajua!

Leo mnaanza mlaumu Magufuli, wengi wenu manaotoa hizo lawama ni wale mirija iliyokatwa. Ndo maana mnamchukia. Huwa najiuliza hivi Magufuli aliingia katika kila nyumba na kuchukua fedha zenu au mishahara yenu? Swala la kuongeza mishahara kwa kutangaza hilo ni lakizamani na limepitwa na wakati. Hakuna nchi duniani zilizoendelea zinazotangaza kuongeza mishahara. Nimebahatika kufanya kazi nje, sijawahi ona rais au waziri mkuu wa nchi akitangaza ongezeko la mishahara.

Mfano katika sehemu nayofanyia kazi. Wanatumia tathimini ya kazi. unapewa fomu unajikadilia utendaji wako wa kazi kwa kujipima. Baadae unakaa na Mkuu wako wa idara mnapitia kwa pamoja kile ulichojipima, mnajadiliana. Ile fomu itakwenda kwa jopo ya maafisa utumishi pamoja na mkuu wako wa idara kulingana na fomu ulojaza utapata ongezeko lako la mshahara. Hivyo mshahara unapandishwa kulingana na perfomance yako kazini.
Tanzania tunajaza hizo fomu lakini hakuna kinachofanyika hata cheo hupandishiwi. Mpaka mkuu wako atakapo jisikia.
Hongera Magufuli kwa ulipotumika. Pumzika kwa amani. Ila ipo siku watanzania watatamani wangekuona tena.
 
Hongera Sana Mkuu kwa uchambuzi wa Maana.

Suala la mifuko NSSF na PSSSF Ni nyeti, imeumiza Watanzania wengi.

Ikibidi, ufungulie thread yake, na ipewe uzito na mods ...ili Mh. Rais apate ujumbe.

Wafanyakazi wa NSSF wanapandisha mabega.

Pili wanakula Rushwa
Mkuu fungua tutakusapoti NSSF ni janga
 
Nawashangaa wanaobishana na WB walio ona uchumi wa Tanzania unakua kwa kasi. Hadi tukapanda kuwa uchumi wa Kati. Watu wanakuja na takwimu zao za kishule shule hapa badala ya actual economy. Moja ya uchumi kukua ni uimarishaji wa huduma kwa wanannchi, hii ni pamoja na afya, Elimu, na miundo mbinu.
Watanzania baadhi walizoea ubadhirifu wa mali ya umma. Sekta binafsi ilitegemea michongo, kuonga na kujichukulia fedha ya serikali na kutoa huduma dhaifu. Mfano makandarasi wengi walijenga barabara au majengo ya serikali yasiyokuwa na kiwango huku wakiwa wamelipwa fedha nyingi. Hela iliyokuwa ikizagaa mtaani ilikuwa fedha ya dhuruma, madawa ya kulevya na ubadhirifu.

Nchi za Ulaya huwezi kuta fedha inazagaa mtaani. Sweden ni moja ya nchi ambayo ni wakali kwa kodi. Hawabembelezi mtu hata awe mfanya biashara mkubwa. Kuna baadhi ya mashirika makubwa ya biashara Sweden yamehama kwa kulalamikia kodi. Na utaratibu wa kulipia kodi Sweden ulianzishwa na kusisitizwa kwa lazima na aliekuwa mfalme wao Gustav, wanasema huyu watu walimchukia kwa ajili ya kuhimiza kodi. Lakini leo wanafurahi na kumkumbuka kuwa ameifanya Sweden kuwa kama leo ilivyo.
Katika serikali ya kikwete, kulikua na mambo mengi machafu, fedha ilichotwa. Hakukuwa na huduma kwa wananchi iliyowawezesha. Watu wa juu kimaisha waliendelea kuwajuu, na masikini aliendelea kuwa masikini.

Nakumbuka naanza kazi, ikaletwa orodha ya malipo ya mshahara, ambayo mimi na mwasibu wangu tulikuwa tunaipokea na kukagua kama wafanyakazi wote wamepata haki zao. Kilichokuwa kinanishangaza na ugeni wangu katika utumishi wa umma, katika orodha ya malipo ya mshahara kulikuwa na majina yapata kumi. Hawa watumishi sikuwajua na sijawahi waona ofisini. Nilimuuliza mhasibu kwani yeye alikuwa mtu mzima ambae kesha kaa katika utumishi yapata miaka 30. Akanambia aya majina hawa watu wengine walishafariki, na wengine kuacha kazi, lakini mishahara yao inaingia hiyo fedha ni ya wakubwa. Nilimwambia tuzuie. Akasema haiwezekani kwani huo ni mtandao mkubwa unaanzia juu. Hii niliiona kwa macho yangu na kushuhudia.

Utawala wa Kikwete posho zilikuwa nyingi. Mtu unaweza pokea posho mbili hadi Tatu wakati umeshalipwa kwa kazi husika. Watu hawakufanya kazi kilichotazamwa ni posho tu. Nilikuwa na ndugu yangu ambae yeye, alikuwa akiingia Bank kuu, anachota pesa huyu alikuwa na wakubwa fulani wa hii nchi. Aliweza ingiza watu weki bank kuu kufanya kazi na baadhi ya mashirika makubwa kama PSPF na kadhalika. Alikuwa na fedha haswa. Lakini baada ya Magufuli kuingia mirija yote ilikata.

Wakati wa Kikwete, wanafunzi wengi waliofahulu walishindwa kwenda shule, kwa kukoswa uniform, ada na michango ya madawati au mingineyo. Nakumbuka nikiwa mtumishi wa umma, ilinibidi kusomesha watoto 10. Pia niliongea na baadhi ya mashirka kuwasaidia baadhi ya wanafunzi wapatao 80 hawa walisomeshwa na hayo mashirika. Na hawa wanafunzi wengi wao walikuwa masikini wa kutupwa katika familia zao.

Naongea vitu ambavyo nilivishuhudia mwenyewe. Situmii theory ya kukariri darasani la asha. Nilishuhudia matajiri wakubwa wenye uwezo walivyokuwa wameiweka serikali mfukoni. Watumishi mbalimbali walionewa na kunyimwa haki zao hasa katika sekta binafsi. Kuna issue moja ya wahindi ambao baada ya kumsaidia mtumishi mmoja alodhulumiwa haki yake. Mmoja wa wahindi hao ambae ni mfanya biashara mkubwa linipigia simu na kunisihi niachane na hilo jambo. Nilipomkatalia alinitishia na kusema ataongea na Rais.
Nilimwambia ongea nae. Kipindi hicho kulijaa dhuruma na ufisadi wa hali ya juu. Wakubwa wengi walishiriki kuuza madawa ya kulevya na kujipatia mamilioni. Tunawajua!

Leo mnaanza mlaumu Magufuli, wengi wenu manaotoa hizo lawama ni wale mirija iliyokatwa. Ndo maana mnamchukia. Huwa najiuliza hivi Magufuli aliingia katika kila nyumba na kuchukua fedha zenu au mishahara yenu? Swala la kuongeza mishahara kwa kutangaza hilo ni lakizamani na limepitwa na wakati. Hakuna nchi duniani zilizoendelea zinazotangaza kuongeza mishahara. Nimebahatika kufanya kazi nje, sijawahi ona rais au waziri mkuu wa nchi akitangaza ongezeko la mishahara.

Mfano katika sehemu nayofanyia kazi. Wanatumia tathimini ya kazi. unapewa fomu unajikadilia utendaji wako wa kazi kwa kujipima. Baadae unakaa na Mkuu wako wa idara mnapitia kwa pamoja kile ulichojipima, mnajadiliana. Ile fomu itakwenda kwa jopo ya maafisa utumishi pamoja na mkuu wako wa idara kulingana na fomu ulojaza utapata ongezeko lako la mshahara. Hivyo mshahara unapandishwa kulingana na perfomance yako kazini.
Tanzania tunajaza hizo fomu lakini hakuna kinachofanyika hata cheo hupandishiwi. Mpaka mkuu wako atakapo jisikia.
Hongera Magufuli kwa ulipotumika. Pumzika kwa amani. Ila ipo siku watanzania watatamani wangekuona tena.
Dah..!! Mkuu umeongea ukweli mtupu.
 
Mtazamo wangu magufuli alifunga mikanda NA nilijua tutapita hapa NA kuumia ilikua ni lazma. Sasa ndio maana ya kuisoma namba. Ili kesho tuwe pazuri lzma kuumia leo
 
Ni bahati mbaya sana nchi kuongozwa na mtu asiyesikiliza wataalamu bali anaendeshwa na instinct zake mwenyewe.....watu wanaomshauri kinyume wanaonekana wapiga dili au wametumwa na mabeberu.
 
Mwendazake alikuwa anajiona yeye ana akili kuliko watanzania wote milioni 60. Mtu gani hataki ushauri anafanya kazi kwa mawazo yake peke yake. Nadhani ni ile PHD ndio ilikuwa inampa kibri.

Sasa sisi tunaostaafu miaka 20 ijayo lazima tujue kabisa Mwendazake hajaacha kitu kwenye mifuko ya pensheni. Tusije tukapeleka lawama kwa mama bure. Nchi hii haijawahi kupata kiongozi wa hovyo kama huyu mzee.
 
Sasa usilaumu wanaoweka thread usizopenda wakati wasipoweka hizo, ww/nyinyi mlio neutral hamtaweka kabisa. Hayo mengine kwenye post yako nimeshindwa kuyaelewa.
😂😂😂 dahhh ...
Mkuu nilitoa compliment tu na ningeomba yaishe haya maana hakuja haja ya kujibizana kwa kitu kilicho nje ya mada kwa sasa...

Pasaka njema in advance
 
Yeye ndie alikuwa anasema wamachinga wasisumbuliwe wafanye biashara popote. Watendaji wake unawaonea tu.
Kuwaacha machinga hakumaanisha wasitafute njia bora za kuwasaidia kuongeza tija badala ya hasara...Watendaji wengi walitoa majibu mepesi yasiyo na tija...Nikupe mfano waliwasaidiaje machinga kuunganisha mitaji yao ili kweli waweze kubaki kwenye complex yao badala ya kuwa wanatembeza bidhaa?

Kutembeza bidhaa pia ilikuwa market strategies za wafanya biashara wakubwa je walitumiaje hiyo mbinu ku improvise ili iongeze tija?

Wao walichokuwa wanajua ni kutumia mgambo tu na fimbo kuwafukuza machinga kama vibaka vile na siyo raia ambao waliwapa kura viongozi wa nchi; Magufuli kama mwanasiasa yeyote yule ambaye nafasi yake inahitaji kura asingekubali hilo na hapo alionyesha umahiri wake katika kuzilinda kura zake...Ila kama mwanasiasa yeyote asingekataa kupokea options zinazoongeza kodi na kuzilinda kura zake yaani machinga wakaendelea kumwona ndiyo mtetezi wao, huo ndiyo utaalamu ambao wataalamu wetu wengi wanaukosa na kubakia kulala kwamba wanasiasa wanawakwamisha...At the same time kwakukosa ubunifu huo hata uchumi unashindwa kuongezeka yet bado wanataka mishahara mikubwa...Haiji hiyo!
 
Habarini wakuu…

Wakati bado tukiwa kwenye maombolezo, nimeona ni vema nifanye utafiti kidogo wa kumulika uchumi wa Hayati Magufuli, ili tuweke record zetu sawa, maana huku mtaani na kwenye vyombo vya habari kumekuwa na upotoshaji mkubwa sana.

Japo mimi sijawahi kuwa mshabiki wa Hayati Magufuli, ila leo ntajaribu kuwa objective sana, kwa faida ya watu wa pande zote mbili, wale wanaoponda na wala wanaosifia. Nataka tufike kwenye mizania ya kujua ukweli wa Magufuli, ili kama mtu unasifia ujue unasifia kitu gani na kama unaponda ujue unaponda kitu gani.

Leo ntagusia viashiria vichache ambavyo vinanguvu katika uchumi wa nchi yeyote. Na viashiria hivo vina uhusiano wa viwakilishi kwenye kanuni ya kutafuta zao la nchi yaani GDP.

(GDP = Consumption + Investment + Government Spending + Net export)

Viashiria ambavyo ntaviangalia ni hivi vifuatavyo

1) Credit growth (Ukuaji wa mikopo inayotolewa na benki za kibiashara) – Hiki kiashiria kinawakilisha performance ya sekta binafsi kwenye uwekezaji, ukuaji wa mzunguko wa pesa, private sector confidence, performance ya mabenki ya kibiashara, na pia ni kiashiria cha consumption. Unapokuwa na declining trend, kwenye credit growth maana yake hayo mambo yote niliyoyataja lazima yawe negatively affected.

Ni nini kina determine credit growth? (Ama ni nini kisababishi cha ukuaji wa mikopo kwenye mabenki ya kibiashara kwa sekta binafsi?) – Nadhani hichi ni kitendawili ambacho Hayati Magufuli na wanaomzunguka wameshindwa kukijibu kwa miaka karibu sita aliyokuwa madarakani.

Asilimia karibu 65% mpaka 75% ya uchumi wa Tanzania upo determined na sekta binafsi, na hiyo inayobaki 25% mpaka 35% ndo sekta ambayo ni government nikimaanisha ile sekta inayohusu ukusanyaji wa mapato na bejeti ya nchi.

Utawala wa Magufuli, ulikuja na uwekezaji na matumizi makubwa kwenye projects kama Kununua Ndege, Ujenzi wa flyovers, Ujenzi wa Madaraja, Ujenzi wa Makao Makuu Dodoma, Ujezi wa Bwawa la Umeme, Ujenzi wa SGR na vinginevyo. Kwa ufupi naweza kukadiria kwamba, kwa miaka 6 iliyopita kuna Trillioni 40 mpaka 60 ambazo zilienda kwenye hizi projects za utawala Magufuli. Binafsi sina tatizo na hii approach ya Magufuli kwenye miundo mbinu, kwanza ntazidi kumsifu kwenye hili suala.

Tatizo kubwa ambalo nililiona na ambalo ndo kitendawili alichoshindwa kukijibu Magufuli na utawala wake ni kwamba, mipango ya kutekeleza hii miradi haikuangalia uwezo halisi wa nchi wa kutengeneza mapato ya ku finance hii miradi ambayo ilihitaj kiasi kikubwa cha pesa na rasilimali za viwandani.

Matokeo yake, serikali ya Magufuli ikajikuta ipo kwenye stress kubwa ya kupata pesa za ku finance hii miradi ya mapesa mengi. Kwa hiyo option zilikuwa ni mbili 1) Aaache kutekeleza hii miradi ya mepesa mengi au 2) Afanye kila njia kupata pesa.

Haiba ya Magufuli ilimfanya atumie njia namba mbili ‘Kutafuta pesa kwa gharama yeyote’. Nadhani hii njia ndo imefanya mpaka leo tuna vilio kwa wafanyabiashara, wawekezaji, wafanyakazi, mabenki, kwa sababu hii njia ilikuja na action zifuatazo za kutafuta pesa.

a) Kikosi kazi cha kukusanya kodi – Fairness kwenye mfumo wa kodi ilipotea, hakukua na logic tena, naweza sema kwa miaka sita iliyopita nchi ilikuwa kwenye ‘Unyang’anyi wa kodi’ na sio ‘Ukusanyaji wa kodi’. Madam President ameongea vema sana jana kuhusu hichi kitu. Hichi ndio kikubwa ambacho kimeua confidence ya sekta binafsi, matokeo yake ikaathiri mzunguko wa pesa kwenye uchumi, kwasababu kumbuka sekta binafsi ndio haswa wateja wa mabenki ya kibiashara. Kwa kuthibitisha hilo angalia trend ya utoaji mikopo kuanzia mwaka 2010 enzi ya kikwete mpaka 2020. Enzi ya Kikwete sekta binafsi ilikuwa inakuwa kwa kasi sana n ahata unaweza kuona trend ya utoaji wa mikopo ambayo ilikuwa ni kwa wastani wa asilimia Zaidi ya 13% wakati ukuaji wa mikopo kwenye utawala wa Magufuli ni wastani wa asilimia 5.6% kwa miaka mitano iliyopita. So unaweza kuona ni kwa namna gani sera ya Magufuli kwenye kodi ilivoua sekta binafsi na ukuaji wa mikopo.

View attachment 1741641

View attachment 1741642

Kwa kuangalia data za ongezeko la ukusanyaji wa mapato kwa miaka 10 iliyopita pamoja na ongezeko la utoaji mikopo kwa sekta binafsi kama zilivo hapo juu, tunaweza kuwa na conclusion zifuatazo kuhusu uchumi wa Magufuli dhidi ya watangulizi wake.

  • Kwa miaka mitano ya mwisho ya utawala wa Kikwete, kwa ujumla aliweza kuongeza kodi kwa karibu asilimia 88% kwa kuangalia kodi iliyokusanywa 2011 na ile iliyokusanywa 2015, wakati huo huo, sekta binafsi ilikuwa ikifanya vizuri kwa kuangalia uwiano wa mikopo na zao ghafi la ndani, ilikuwa ikipanda kutoka 12.21% mwaka 2011 mpaka 14.47% mwaka 2015 alipotoka madarakani. (Key note: Utawala wa Kikwete uliweza kuongeza makusanyo ya kodi mwaka hadi mwaka, na wakati huo huo sekta binafsi ilikuwa inamea mwaka hadi mwaka – Economically hii ndio tunaiita positive
  • Kwa miaka mine ya Magufuli 2016 – 2019 (sikuweza kupata data za 2020), kwa ujumla aliweza kuongeza makusanyo ya kodi kwa asilimia 56% ndani ya miaka minne 2016 -2019, wakati huo huo mikopo kwa sekta binafsi ilianza kudorora kwa kuangalia uwiano wa mikopo na GDP ambao kwa miaka hiyo minne imekuwa ikienda chini kutoka ile peak iliyofikiwa na utawala wa kikwete ya 14.47% mwaka 2015 mpaka 12.05% mwaka 2019. Hii ki uchumi tunaiita growth ambayo ni negative, yaani GDP inakuwa lakini sekta ya mikopo inadorora, na unaweza kuona ni kipindi hichi hichi nchi ilikuwa na sera za kodi za unyang’anyi.

b) Kutokuongeza mishahara ya watumishi wa umma – ilikuwa pia ni lazima utawala wa Magufuli ufanye hichi kitu ambacho is unfair, kwa minajili ya kulinda pesa za kufanya miradi. Kwa miaka sita iliyopita, kipato cha mfanyakazi kimeporomoka karibu kwa asilimia 18% kutokana na kupanda kwa gharama za maisha na serikali kushindwa kuongeza mishahara.

c) Kuzuia fao la kujitoa kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii – ambacho wengi hawajui ni kwamba katika harakati za kutafuta pesa za miradi, utawala wa magufuli ndani ya miaka 6, wamekopa Zaidi ya Trillioni 12 kwenye hii mifuko ya hifadhi ya jamii, kitu ambacho kimepelekea hii mifuko kuwa ni kama imefilisika na ndio maana ikabidi wazuie fao la kujitoa kwasababu mifuko imekaushwa na serikali.

d) Kukua kwa haraka kwa deni la serikali (madeni ya nje na ndani) – Hii ndo ilikuwa karata ya mwisho ya kupata pesa, kwa sababu njia zote tatu hapo juu ni kama hazikuzaa matunda. (Ntaelezea kwa mapana hichi kitu nyuzi zinazofuata)

Hayo ni baadhi ya mambo yaliyotokea kama sera za uchumi wa Magufuli ambao ntaendelea kuuchambua, ila kwanza nataka mnielewe taratibu ili tuweze kwenda sawa.

Kwa wale ambao wana mashaka na uchambuzi wangu kuhusu masuala ya kiuchumi naomba mpitie baadhi ya nyuzi zangu ambazo niliwahi kuandika kipindi cha nyuma na ambazo zitahusika moja kwa moja na uchambuzi kuhusu uchumi wa Magufuli. Naahidi kuwaletea vipande vipande na hoja chache chache ili msije kuchanganyikiwa na rundo la taarifa.

-----------------------------------------------------------------------------------------------------
1. Ukali wa maisha kwa watanzania - Serikali tafakarini kuongeza mishahara ya Watumishi wa Umma, ukali wa maisha ni bomu linaloua taratibu!

2. Kuadimika kwa saruji nchini - Serikali haiwezi kukwepa lawama ya kuadimika na kupanda kwa bei ya Saruji nchini. Waziri wa Viwanda ana kazi sana, kuna janga linatunyemelea

3. Uchumi bado upo kwenye mkwamo - ‘Namba zinanuka’ – kwanini nasema bado uchumi wetu upo kwenye mkwamo?

4. Serikali imedumaza mifuko ya hifadhi ya jamii - ‘Namba zinanuka’ – Serikali imechangia kudumaza mifuko ya Hifadhi ya Jamii

5. Uchumi wetu ni dhaifu - USHAHIDI: IMF hawajakosea, Uchumi wetu ni ‘DHAIFU’
It is an excellent piece of information. Continue producing more facts. I remain your keen consumer.
 
Amekuza sana pia tabaka la wanyonge. Mama ntilie, wamachinga na boda boda.
 
Ila mimi nimemuelewa Magufuli kwenye baadhi ya mambo baada ya kufariki.

Kuna vitu nimekua exposed kwake kwa hivi karibuni kwa siku za mwisho mwisho za uhai wake, ndio nikaja kujua alikua na nia gani.

Kwenye ujenzi wa bwawa la umeme, nilikua nampinga tu Magufuli kwa kufuata mkumbo lakini baada ya kupata facts kuhusu gharama za uendeshaji wa mitambo ya gesi na mafuta kwa tanesco, nikajua kabisa Magufuli aliona mbali na alikua na nia njema kabisa kuhusu uchumi wa nchi yetu.

Sasa naamini ukiona mtu anapinga jambo flani inaweza kua halijui vizuri, ana maslahi binafsi, hajalielewa ama anafuata tu mkumbo au ameamua tu, maana watu wengine wanaweza kuamua tu kua dogma, akapewa undeniable facts na bado akaamua tu kutokuelewa.

Mfano mzuri watu dogma ni kama Magufuli mwenyewe juu ya covid 19, aliamua tu kua dogma juu ya corona na bahati mbaya udogmatic wake umegharimu maisha yake.

Ukweli ni kwamba uzalishaji wa umeme kutumia maji ni way cheaper kuliko sources nyingine zote za nishati, ni kati ya shilingi za kitanzania 60 hadi 90 kwa unit. Lakini pia maintanance ya mitambo yake ni baada ya muda mrefu sana, zaidi ya miaka 15 na hata gharama za utengenezaji wake sio kubwa.

Ukija kwenye gas, uzalishaji wa unit moja ni mara 2.5 ya uzalishaji wa maji, lakini pia mitambo ya gesi inahitaji overhaul maintenance kila baada ya miaka 2 na ni billion of money, hao ABB ya Uingereza, Siemens ya Sweden, General Electric ya Marekani, Wartisila na wengine hela wanazofyonza pale Tanesco sio za kitoto, sio za kitoto. Hawa hawataki kusikia tunakua na chanzo kingine cha umeme zaidi ya gasi ama mafuta mazito maana ulaji wao pale Tanesco utakata.
Cost accountants and economists bail us out of this calamity: Which is a cheaper and reliable source of electric power in the TZ environment? Please come up with quantified argument.
 
Kuwaacha machinga hakumaanisha wasitafute njia bora za kuwasaidia kuongeza tija badala ya hasara...Watendaji wengi walitoa majibu mepesi yasiyo na tija...Nikupe mfano waliwasaidiaje machinga kuunganisha mitaji yao ili kweli waweze kubaki kwenye complex yao badala ya kuwa wanatembeza bidhaa?

Kutembeza bidhaa pia ilikuwa market strategies za wafanya biashara wakubwa je walitumiaje hiyo mbinu ku improvise ili iongeze tija?

Wao walichokuwa wanajua ni kutumia mgambo tu na fimbo kuwafukuza machinga kama vibaka vile na siyo raia ambao waliwapa kura viongozi wa nchi; Magufuli kama mwanasiasa yeyote yule ambaye nafasi yake inahitaji kura asingekubali hilo na hapo alionyesha umahiri wake katika kuzilinda kura zake...Ila kama mwanasiasa yeyote asingekataa kupokea options zinazoongeza kodi na kuzilinda kura zake yaani machinga wakaendelea kumwona ndiyo mtetezi wao, huo ndiyo utaalamu ambao wataalamu wetu wengi wanaukosa na kubakia kulala kwamba wanasiasa wanawakwamisha...At the same time kwakukosa ubunifu huo hata uchumi unashindwa kuongezeka yet bado wanataka mishahara mikubwa...Haiji hiyo!

Maelezo yako ni mengi, lakini naomba nikusaidieje kitu, Magufuli hakuwa anategemea kura hata moja ya mpiga kura kuwa rais. Hivyo wakati unaendelea na hizi hekaya zako, achana kabisa na upotoshaji kuwa Magufuli alitegemea kura ya mpiga kura nje ya vyombo vya dola.
 
Sekta ya gesi zaidi ya kuzalisha umeme ingezalisha maelfu ya biashara za bidhaa, huduma na ajira za moja kwa moja mara nyingi zaidi ya zitakazozalishwa na huo mradi wa umeme wa maji.

Umeme ambao ungezalishwa na gesi ingekuwa pesa za uwekezaji na sio hii mikopo,kutopanda mishahara,ubabaishaji wa pensheni na kodi wanazokamuliwa wananchi hadi wanakonda.
Ila mimi nimemuelewa Magufuli kwenye baadhi ya mambo baada ya kufariki.

Kuna vitu nimekua exposed kwake kwa hivi karibuni kwa siku za mwisho mwisho za uhai wake, ndio nikaja kujua alikua na nia gani.

Kwenye ujenzi wa bwawa la umeme, nilikua nampinga tu Magufuli kwa kufuata mkumbo lakini baada ya kupata facts kuhusu gharama za uendeshaji wa mitambo ya gesi na mafuta kwa tanesco, nikajua kabisa Magufuli aliona mbali na alikua na nia njema kabisa kuhusu uchumi wa nchi yetu.

Sasa naamini ukiona mtu anapinga jambo flani inaweza kua halijui vizuri, ana maslahi binafsi, hajalielewa ama anafuata tu mkumbo au ameamua tu, maana watu wengine wanaweza kuamua tu kua dogma, akapewa undeniable facts na bado akaamua tu kutokuelewa.

Mfano mzuri watu dogma ni kama Magufuli mwenyewe juu ya covid 19, aliamua tu kua dogma juu ya corona na bahati mbaya udogmatic wake umegharimu maisha yake.

Ukweli ni kwamba uzalishaji wa umeme kutumia maji ni way cheaper kuliko sources nyingine zote za nishati, ni kati ya shilingi za kitanzania 60 hadi 90 kwa unit. Lakini pia maintanance ya mitambo yake ni baada ya muda mrefu sana, zaidi ya miaka 15 na hata gharama za utengenezaji wake sio kubwa.

Ukija kwenye gas, uzalishaji wa unit moja ni mara 2.5 ya uzalishaji wa maji, lakini pia mitambo ya gesi inahitaji overhaul maintenance kila baada ya miaka 2 na ni billion of money, hao ABB ya Uingereza, Siemens ya Sweden, General Electric ya Marekani, Wartisila na wengine hela wanazofyonza pale Tanesco sio za kitoto, sio za kitoto. Hawa hawataki kusikia tunakua na chanzo kingine cha umeme zaidi ya gasi ama mafuta mazito maana ulaji wao pale Tanesco utakata.
 
Mkuu usiziamini takwimu za Magu hata kidogo hazikuwa na uhalisia ndio maana alipiga marufuku kutoa takwimu.

Kiuhalisia inflation imepanda hii haitaji resaerch ya mbobezi
Kwa hili nitakubali kama layman, lakini inflation ni below 5%. Jee umeona, mchele, ndizi, maharagwe ama mazao yamepanda?

Ni bidhaa za viwandani tuu. Kwa hali ambavyo raia wamepigika, hali mbaya, jee unapandisha bei bidhaa nani anunue ?
 
Bahati mbaya sana "wanyonge" ambao ndio kundi kubwa kabisa katika nchi yetu kwa sasa hawawezi kuelewa huu uchambuzi wako makini sana. Kila nikiongea na dereva boda boda anasema kile kilikuwa ni Chuma na wana shaka kama mkuu mpya wa nyumba ataweza kuendeleza uchuma ule.
Hii ni sehemu ya kwanza, nta cover sekta ya biashara, uwekezaji wa nje, viwanda, na ntaelezea kwa kina kuusu madeni ya taifa..

Ila conclusion kabisa ni kwamba 'Magufuli alichofanya ni kukopa pesa nying nje na kufanya plundering ya pesa za wafanya biashara kupitia kodi za kidhalimu ili kujenga uchumi ambao ulielemea katika projects kubwa za miundo mbinu ambayo bado hatujajua itakamilika lini'
 
Habarini wakuu…

Wakati bado tukiwa kwenye maombolezo, nimeona ni vema nifanye utafiti kidogo wa kumulika uchumi wa Hayati Magufuli, ili tuweke record zetu sawa, maana huku mtaani na kwenye vyombo vya habari kumekuwa na upotoshaji mkubwa sana.

Japo mimi sijawahi kuwa mshabiki wa Hayati Magufuli, ila leo ntajaribu kuwa objective sana, kwa faida ya watu wa pande zote mbili, wale wanaoponda na wala wanaosifia. Nataka tufike kwenye mizania ya kujua ukweli wa Magufuli, ili kama mtu unasifia ujue unasifia kitu gani na kama unaponda ujue unaponda kitu gani.

Leo ntagusia viashiria vichache ambavyo vinanguvu katika uchumi wa nchi yeyote. Na viashiria hivo vina uhusiano wa viwakilishi kwenye kanuni ya kutafuta zao la nchi yaani GDP.

(GDP = Consumption + Investment + Government Spending + Net export)

Viashiria ambavyo ntaviangalia ni hivi vifuatavyo

1) Credit growth (Ukuaji wa mikopo inayotolewa na benki za kibiashara) – Hiki kiashiria kinawakilisha performance ya sekta binafsi kwenye uwekezaji, ukuaji wa mzunguko wa pesa, private sector confidence, performance ya mabenki ya kibiashara, na pia ni kiashiria cha consumption. Unapokuwa na declining trend, kwenye credit growth maana yake hayo mambo yote niliyoyataja lazima yawe negatively affected.

Ni nini kina determine credit growth? (Ama ni nini kisababishi cha ukuaji wa mikopo kwenye mabenki ya kibiashara kwa sekta binafsi?) – Nadhani hichi ni kitendawili ambacho Hayati Magufuli na wanaomzunguka wameshindwa kukijibu kwa miaka karibu sita aliyokuwa madarakani.

Asilimia karibu 65% mpaka 75% ya uchumi wa Tanzania upo determined na sekta binafsi, na hiyo inayobaki 25% mpaka 35% ndo sekta ambayo ni government nikimaanisha ile sekta inayohusu ukusanyaji wa mapato na bejeti ya nchi.

Utawala wa Magufuli, ulikuja na uwekezaji na matumizi makubwa kwenye projects kama Kununua Ndege, Ujenzi wa flyovers, Ujenzi wa Madaraja, Ujenzi wa Makao Makuu Dodoma, Ujezi wa Bwawa la Umeme, Ujenzi wa SGR na vinginevyo. Kwa ufupi naweza kukadiria kwamba, kwa miaka 6 iliyopita kuna Trillioni 40 mpaka 60 ambazo zilienda kwenye hizi projects za utawala Magufuli. Binafsi sina tatizo na hii approach ya Magufuli kwenye miundo mbinu, kwanza ntazidi kumsifu kwenye hili suala.

Tatizo kubwa ambalo nililiona na ambalo ndo kitendawili alichoshindwa kukijibu Magufuli na utawala wake ni kwamba, mipango ya kutekeleza hii miradi haikuangalia uwezo halisi wa nchi wa kutengeneza mapato ya ku finance hii miradi ambayo ilihitaj kiasi kikubwa cha pesa na rasilimali za viwandani.

Matokeo yake, serikali ya Magufuli ikajikuta ipo kwenye stress kubwa ya kupata pesa za ku finance hii miradi ya mapesa mengi. Kwa hiyo option zilikuwa ni mbili 1) Aaache kutekeleza hii miradi ya mepesa mengi au 2) Afanye kila njia kupata pesa.

Haiba ya Magufuli ilimfanya atumie njia namba mbili ‘Kutafuta pesa kwa gharama yeyote’. Nadhani hii njia ndo imefanya mpaka leo tuna vilio kwa wafanyabiashara, wawekezaji, wafanyakazi, mabenki, kwa sababu hii njia ilikuja na action zifuatazo za kutafuta pesa.

a) Kikosi kazi cha kukusanya kodi – Fairness kwenye mfumo wa kodi ilipotea, hakukua na logic tena, naweza sema kwa miaka sita iliyopita nchi ilikuwa kwenye ‘Unyang’anyi wa kodi’ na sio ‘Ukusanyaji wa kodi’. Madam President ameongea vema sana jana kuhusu hichi kitu. Hichi ndio kikubwa ambacho kimeua confidence ya sekta binafsi, matokeo yake ikaathiri mzunguko wa pesa kwenye uchumi, kwasababu kumbuka sekta binafsi ndio haswa wateja wa mabenki ya kibiashara. Kwa kuthibitisha hilo angalia trend ya utoaji mikopo kuanzia mwaka 2010 enzi ya kikwete mpaka 2020. Enzi ya Kikwete sekta binafsi ilikuwa inakuwa kwa kasi sana n ahata unaweza kuona trend ya utoaji wa mikopo ambayo ilikuwa ni kwa wastani wa asilimia Zaidi ya 13% wakati ukuaji wa mikopo kwenye utawala wa Magufuli ni wastani wa asilimia 5.6% kwa miaka mitano iliyopita. So unaweza kuona ni kwa namna gani sera ya Magufuli kwenye kodi ilivoua sekta binafsi na ukuaji wa mikopo.

View attachment 1741641

View attachment 1741642

Kwa kuangalia data za ongezeko la ukusanyaji wa mapato kwa miaka 10 iliyopita pamoja na ongezeko la utoaji mikopo kwa sekta binafsi kama zilivo hapo juu, tunaweza kuwa na conclusion zifuatazo kuhusu uchumi wa Magufuli dhidi ya watangulizi wake.

  • Kwa miaka mitano ya mwisho ya utawala wa Kikwete, kwa ujumla aliweza kuongeza kodi kwa karibu asilimia 88% kwa kuangalia kodi iliyokusanywa 2011 na ile iliyokusanywa 2015, wakati huo huo, sekta binafsi ilikuwa ikifanya vizuri kwa kuangalia uwiano wa mikopo na zao ghafi la ndani, ilikuwa ikipanda kutoka 12.21% mwaka 2011 mpaka 14.47% mwaka 2015 alipotoka madarakani. (Key note: Utawala wa Kikwete uliweza kuongeza makusanyo ya kodi mwaka hadi mwaka, na wakati huo huo sekta binafsi ilikuwa inamea mwaka hadi mwaka – Economically hii ndio tunaiita positive
  • Kwa miaka mine ya Magufuli 2016 – 2019 (sikuweza kupata data za 2020), kwa ujumla aliweza kuongeza makusanyo ya kodi kwa asilimia 56% ndani ya miaka minne 2016 -2019, wakati huo huo mikopo kwa sekta binafsi ilianza kudorora kwa kuangalia uwiano wa mikopo na GDP ambao kwa miaka hiyo minne imekuwa ikienda chini kutoka ile peak iliyofikiwa na utawala wa kikwete ya 14.47% mwaka 2015 mpaka 12.05% mwaka 2019. Hii ki uchumi tunaiita growth ambayo ni negative, yaani GDP inakuwa lakini sekta ya mikopo inadorora, na unaweza kuona ni kipindi hichi hichi nchi ilikuwa na sera za kodi za unyang’anyi.

b) Kutokuongeza mishahara ya watumishi wa umma – ilikuwa pia ni lazima utawala wa Magufuli ufanye hichi kitu ambacho is unfair, kwa minajili ya kulinda pesa za kufanya miradi. Kwa miaka sita iliyopita, kipato cha mfanyakazi kimeporomoka karibu kwa asilimia 18% kutokana na kupanda kwa gharama za maisha na serikali kushindwa kuongeza mishahara.

c) Kuzuia fao la kujitoa kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii – ambacho wengi hawajui ni kwamba katika harakati za kutafuta pesa za miradi, utawala wa magufuli ndani ya miaka 6, wamekopa Zaidi ya Trillioni 12 kwenye hii mifuko ya hifadhi ya jamii, kitu ambacho kimepelekea hii mifuko kuwa ni kama imefilisika na ndio maana ikabidi wazuie fao la kujitoa kwasababu mifuko imekaushwa na serikali.

d) Kukua kwa haraka kwa deni la serikali (madeni ya nje na ndani) – Hii ndo ilikuwa karata ya mwisho ya kupata pesa, kwa sababu njia zote tatu hapo juu ni kama hazikuzaa matunda. (Ntaelezea kwa mapana hichi kitu nyuzi zinazofuata)

Hayo ni baadhi ya mambo yaliyotokea kama sera za uchumi wa Magufuli ambao ntaendelea kuuchambua, ila kwanza nataka mnielewe taratibu ili tuweze kwenda sawa.

Kwa wale ambao wana mashaka na uchambuzi wangu kuhusu masuala ya kiuchumi naomba mpitie baadhi ya nyuzi zangu ambazo niliwahi kuandika kipindi cha nyuma na ambazo zitahusika moja kwa moja na uchambuzi kuhusu uchumi wa Magufuli. Naahidi kuwaletea vipande vipande na hoja chache chache ili msije kuchanganyikiwa na rundo la taarifa.

-----------------------------------------------------------------------------------------------------
1. Ukali wa maisha kwa watanzania - Serikali tafakarini kuongeza mishahara ya Watumishi wa Umma, ukali wa maisha ni bomu linaloua taratibu!

2. Kuadimika kwa saruji nchini - Serikali haiwezi kukwepa lawama ya kuadimika na kupanda kwa bei ya Saruji nchini. Waziri wa Viwanda ana kazi sana, kuna janga linatunyemelea

3. Uchumi bado upo kwenye mkwamo - ‘Namba zinanuka’ – kwanini nasema bado uchumi wetu upo kwenye mkwamo?

4. Serikali imedumaza mifuko ya hifadhi ya jamii - ‘Namba zinanuka’ – Serikali imechangia kudumaza mifuko ya Hifadhi ya Jamii

5. Uchumi wetu ni dhaifu - USHAHIDI: IMF hawajakosea, Uchumi wetu ni ‘DHAIFU’
Bora haujaandika huu uzi kwa kizungu tungetoka hapa 🤭😂😂
 
Back
Top Bottom