Tuweke kumbukumbu zetu sawa, huu ndo uchumi wa Magufuli aliouacha, all facts! - Sehemu ya kwanza

Tuweke kumbukumbu zetu sawa, huu ndo uchumi wa Magufuli aliouacha, all facts! - Sehemu ya kwanza

Naantombe Mushi
kwahiyo sasa ni kipi kifanyike ili mzunguko wa pesa uwe mkubwa kama enzi za kikwete?
Mama kaanza vizuri, sekta binafsi ilichokikosa kwa Magufuli ni confidence ambayo ilitokana na unyonywaji.. So confidence ikirejea, uwekezeja lazima utaimarika kwenye sekta binafsi, trust me, utaona mabadiliko ndugu yangu.

Wenye pesa hawahitaji bughudha, na Rais Samia ameshawahakikishia hilo, mambo yata improve, na mzunguko wa pesa utaanza kuongezeka, tuombe uzima baada ya miezi sita kutoka sasa... kutakuwa na improvement
 
Binafsi naona hizi ndiyo zile tunasema uchumi wa kwenye makaratasi ila kipindi cha JK tuseme tu ukweli fedha nyingi zilikuwa ni haram na hazikuwa zinaingia kwenye mzunguko ili lilipelekea mtaani hela kuzagaa kiasi ata laki ikaitwa si pesa ola sasa laki tunajua ni pesa.

Wafanyabiashara sikuzote wazo lao la kwanza kukwepa kodi, kipindi cha JK kuna meli 60 ziliwai kutia nanga pale bandarini Dar es Salaam na meli hizo zote hazikuwa recorded mahala popote na mwisho kontena zikapotea kusiko julikana, Zaman kipindi cha JK kontena kupotea huko bandarini kilikuwa kitu cha kawaida, Bandarini hapakuwa na scana ata ya kuscan vitu vinavyopita bandarini.

Nenda pale airport kipindi cha JK hakuna kikicho scsniwa ili kijulikane ni kitu gani...

Mwisho wa siku Magufuli alitamani kujenga Tanzania ya kesho, Magufuli hakuwa mwanasiasa ila alikuwa kiongozi, aliona bora aanze upya kuliko kuendelea na staili waliyotumia watangulizi wake.

Mwisho niseme tu huu wa kipindi cha Hayati ndo ulikuwa uchumi wetu halisi, huko nyuma kulikuwa na wajanja tu wenye kuchuma walivyotaka kuchuma lakini kwenye kujenga nchi hamna kitu.

Nakumbuka kipindi cha JK NGO zilopeta kweli lakini ki ukweli kabisa walikuwa hawalipi ata Tsh 150,000/= kwa mwaka wala hawapeleki ata hesabu zao za mwaka kwa msajili lakini alivyoingia Magufuli aligakikisha kila Wizara inayoona kuna sehemu inatakiwa ikusanye fedha inatakiwa kufanya hivo, hapo ukaanza utaratibu kama hupeleki hesabu zako kwa na hulipi ada shirika lako litafungwa na mengi yalifungwa maana yalikuwa hewa na hewa kweli cos ata mimi mwenyewe nishawah fanya kazi huko najua vyema na mpaka sasa mwenye NGO yake ninahakika anafanya kazi kwa unyofu mno.

Kiuweli tulichekea na tulipata mtu ambae alikuwa anatuambia ukweli, hizi habari za kulembeana na kupakana mafuta kwa mgongo wa chupa hakuwa nazo.
jamiiforums_1616781800713853.jpg
 
JPM ametwaliwa ili watanzania milioni 60 wapone imagine angeendelea kwa miaka mitano nchi ingekuwaje? Na wale wapuuzi wengine walitaka atawale miaka 20 zaidi Mungu akasema nitaliponya taifa langu Tanzania.
Kuna verse moja hivi ya hip hop inasema..

Hakuna nafsi inayoweza kuwa juu ya mungu, unaweza uka try na mwisho ukawa juu kizungu.../

Kuna nafsi zinajaribu kuwa juu kinguvu, mwisho wanabebwa kama nyanya iliyo juu ya fungu.../
 
Habarini wakuu…

Wakati bado tukiwa kwenye maombolezo, nimeona ni vema nifanye utafiti kidogo wa kumulika uchumi wa Hayati Magufuli, ili tuweke record zetu sawa, maana huku mtaani na kwenye vyombo vya habari kumekuwa na upotoshaji mkubwa sana.

Japo mimi sijawahi kuwa mshabiki wa Hayati Magufuli, ila leo ntajaribu kuwa objective sana, kwa faida ya watu wa pande zote mbili, wale wanaoponda na wala wanaosifia. Nataka tufike kwenye mizania ya kujua ukweli wa Magufuli, ili kama mtu unasifia ujue unasifia kitu gani na kama unaponda ujue unaponda kitu gani.

Leo ntagusia viashiria vichache ambavyo vinanguvu katika uchumi wa nchi yeyote. Na viashiria hivo vina uhusiano wa viwakilishi kwenye kanuni ya kutafuta zao la nchi yaani GDP.

(GDP = Consumption + Investment + Government Spending + Net export)

Viashiria ambavyo ntaviangalia ni hivi vifuatavyo

1) Credit growth (Ukuaji wa mikopo inayotolewa na benki za kibiashara) – Hiki kiashiria kinawakilisha performance ya sekta binafsi kwenye uwekezaji, ukuaji wa mzunguko wa pesa, private sector confidence, performance ya mabenki ya kibiashara, na pia ni kiashiria cha consumption. Unapokuwa na declining trend, kwenye credit growth maana yake hayo mambo yote niliyoyataja lazima yawe negatively affected.

Ni nini kina determine credit growth? (Ama ni nini kisababishi cha ukuaji wa mikopo kwenye mabenki ya kibiashara kwa sekta binafsi?) – Nadhani hichi ni kitendawili ambacho Hayati Magufuli na wanaomzunguka wameshindwa kukijibu kwa miaka karibu sita aliyokuwa madarakani.

Asilimia karibu 65% mpaka 75% ya uchumi wa Tanzania upo determined na sekta binafsi, na hiyo inayobaki 25% mpaka 35% ndo sekta ambayo ni government nikimaanisha ile sekta inayohusu ukusanyaji wa mapato na bejeti ya nchi.

Utawala wa Magufuli, ulikuja na uwekezaji na matumizi makubwa kwenye projects kama Kununua Ndege, Ujenzi wa flyovers, Ujenzi wa Madaraja, Ujenzi wa Makao Makuu Dodoma, Ujezi wa Bwawa la Umeme, Ujenzi wa SGR na vinginevyo. Kwa ufupi naweza kukadiria kwamba, kwa miaka 6 iliyopita kuna Trillioni 40 mpaka 60 ambazo zilienda kwenye hizi projects za utawala Magufuli. Binafsi sina tatizo na hii approach ya Magufuli kwenye miundo mbinu, kwanza ntazidi kumsifu kwenye hili suala.

Tatizo kubwa ambalo nililiona na ambalo ndo kitendawili alichoshindwa kukijibu Magufuli na utawala wake ni kwamba, mipango ya kutekeleza hii miradi haikuangalia uwezo halisi wa nchi wa kutengeneza mapato ya ku finance hii miradi ambayo ilihitaj kiasi kikubwa cha pesa na rasilimali za viwandani.

Matokeo yake, serikali ya Magufuli ikajikuta ipo kwenye stress kubwa ya kupata pesa za ku finance hii miradi ya mapesa mengi. Kwa hiyo option zilikuwa ni mbili 1) Aaache kutekeleza hii miradi ya mepesa mengi au 2) Afanye kila njia kupata pesa.

Haiba ya Magufuli ilimfanya atumie njia namba mbili ‘Kutafuta pesa kwa gharama yeyote’. Nadhani hii njia ndo imefanya mpaka leo tuna vilio kwa wafanyabiashara, wawekezaji, wafanyakazi, mabenki, kwa sababu hii njia ilikuja na action zifuatazo za kutafuta pesa.

a) Kikosi kazi cha kukusanya kodi – Fairness kwenye mfumo wa kodi ilipotea, hakukua na logic tena, naweza sema kwa miaka sita iliyopita nchi ilikuwa kwenye ‘Unyang’anyi wa kodi’ na sio ‘Ukusanyaji wa kodi’. Madam President ameongea vema sana jana kuhusu hichi kitu. Hichi ndio kikubwa ambacho kimeua confidence ya sekta binafsi, matokeo yake ikaathiri mzunguko wa pesa kwenye uchumi, kwasababu kumbuka sekta binafsi ndio haswa wateja wa mabenki ya kibiashara. Kwa kuthibitisha hilo angalia trend ya utoaji mikopo kuanzia mwaka 2010 enzi ya kikwete mpaka 2020. Enzi ya Kikwete sekta binafsi ilikuwa inakuwa kwa kasi sana n ahata unaweza kuona trend ya utoaji wa mikopo ambayo ilikuwa ni kwa wastani wa asilimia Zaidi ya 13% wakati ukuaji wa mikopo kwenye utawala wa Magufuli ni wastani wa asilimia 5.6% kwa miaka mitano iliyopita. So unaweza kuona ni kwa namna gani sera ya Magufuli kwenye kodi ilivoua sekta binafsi na ukuaji wa mikopo.

View attachment 1741641

View attachment 1741642

Kwa kuangalia data za ongezeko la ukusanyaji wa mapato kwa miaka 10 iliyopita pamoja na ongezeko la utoaji mikopo kwa sekta binafsi kama zilivo hapo juu, tunaweza kuwa na conclusion zifuatazo kuhusu uchumi wa Magufuli dhidi ya watangulizi wake.

  • Kwa miaka mitano ya mwisho ya utawala wa Kikwete, kwa ujumla aliweza kuongeza kodi kwa karibu asilimia 88% kwa kuangalia kodi iliyokusanywa 2011 na ile iliyokusanywa 2015, wakati huo huo, sekta binafsi ilikuwa ikifanya vizuri kwa kuangalia uwiano wa mikopo na zao ghafi la ndani, ilikuwa ikipanda kutoka 12.21% mwaka 2011 mpaka 14.47% mwaka 2015 alipotoka madarakani. (Key note: Utawala wa Kikwete uliweza kuongeza makusanyo ya kodi mwaka hadi mwaka, na wakati huo huo sekta binafsi ilikuwa inamea mwaka hadi mwaka – Economically hii ndio tunaiita positive
  • Kwa miaka mine ya Magufuli 2016 – 2019 (sikuweza kupata data za 2020), kwa ujumla aliweza kuongeza makusanyo ya kodi kwa asilimia 56% ndani ya miaka minne 2016 -2019, wakati huo huo mikopo kwa sekta binafsi ilianza kudorora kwa kuangalia uwiano wa mikopo na GDP ambao kwa miaka hiyo minne imekuwa ikienda chini kutoka ile peak iliyofikiwa na utawala wa kikwete ya 14.47% mwaka 2015 mpaka 12.05% mwaka 2019. Hii ki uchumi tunaiita growth ambayo ni negative, yaani GDP inakuwa lakini sekta ya mikopo inadorora, na unaweza kuona ni kipindi hichi hichi nchi ilikuwa na sera za kodi za unyang’anyi.

b) Kutokuongeza mishahara ya watumishi wa umma – ilikuwa pia ni lazima utawala wa Magufuli ufanye hichi kitu ambacho is unfair, kwa minajili ya kulinda pesa za kufanya miradi. Kwa miaka sita iliyopita, kipato cha mfanyakazi kimeporomoka karibu kwa asilimia 18% kutokana na kupanda kwa gharama za maisha na serikali kushindwa kuongeza mishahara.

c) Kuzuia fao la kujitoa kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii – ambacho wengi hawajui ni kwamba katika harakati za kutafuta pesa za miradi, utawala wa magufuli ndani ya miaka 6, wamekopa Zaidi ya Trillioni 12 kwenye hii mifuko ya hifadhi ya jamii, kitu ambacho kimepelekea hii mifuko kuwa ni kama imefilisika na ndio maana ikabidi wazuie fao la kujitoa kwasababu mifuko imekaushwa na serikali.

d) Kukua kwa haraka kwa deni la serikali (madeni ya nje na ndani) – Hii ndo ilikuwa karata ya mwisho ya kupata pesa, kwa sababu njia zote tatu hapo juu ni kama hazikuzaa matunda. (Ntaelezea kwa mapana hichi kitu nyuzi zinazofuata)

Hayo ni baadhi ya mambo yaliyotokea kama sera za uchumi wa Magufuli ambao ntaendelea kuuchambua, ila kwanza nataka mnielewe taratibu ili tuweze kwenda sawa.

Kwa wale ambao wana mashaka na uchambuzi wangu kuhusu masuala ya kiuchumi naomba mpitie baadhi ya nyuzi zangu ambazo niliwahi kuandika kipindi cha nyuma na ambazo zitahusika moja kwa moja na uchambuzi kuhusu uchumi wa Magufuli. Naahidi kuwaletea vipande vipande na hoja chache chache ili msije kuchanganyikiwa na rundo la taarifa.

-----------------------------------------------------------------------------------------------------
1. Ukali wa maisha kwa watanzania - Serikali tafakarini kuongeza mishahara ya Watumishi wa Umma, ukali wa maisha ni bomu linaloua taratibu!

2. Kuadimika kwa saruji nchini - Serikali haiwezi kukwepa lawama ya kuadimika na kupanda kwa bei ya Saruji nchini. Waziri wa Viwanda ana kazi sana, kuna janga linatunyemelea

3. Uchumi bado upo kwenye mkwamo - ‘Namba zinanuka’ – kwanini nasema bado uchumi wetu upo kwenye mkwamo?

4. Serikali imedumaza mifuko ya hifadhi ya jamii - ‘Namba zinanuka’ – Serikali imechangia kudumaza mifuko ya Hifadhi ya Jamii

5. Uchumi wetu ni dhaifu - USHAHIDI: IMF hawajakosea, Uchumi wetu ni ‘DHAIFU’
Wengine mkisoma mnakuwa msaada sana kwa wale mliowaacha vijijini, well done guy.
 
Hii ni sehemu ya kwanza, nta cover sekta ya biashara, uwekezaji wa nje, viwanda, na ntaelezea kwa kina kuusu madeni ya taifa..

Ila conclusion kabisa ni kwamba 'Magufuli alichofanya ni kukopa pesa nying nje na kufanya plundering ya pesa za wafanya biashara kupitia kodi za kidhalimu ili kujenga uchumi ambao ulielemea katika projects kubwa za miundo mbinu ambayo bado hatujajua itakamilika lini'
Mzee alikuwa mpuuzi sana yule! Halafu kuna mataahira yalikuwa yanataka atawale milele!
 
Mkuu umenikosha Kwa uchambuzi huu. Kiukweli tumelia mara nying na kusisitiza kuwa nchi yetu haina uwezo wa kutekeleza miradi ya matrilioni Kwa wakati mmoja lakin Mwendazake akawaamimisha wajinga kuwa sis sio wazalendo.
 
Binafsi naona hizi ndiyo zile tunasema uchumi wa kwenye makaratasi ila kipindi cha JK tuseme tu ukweli fedha nyingi zilikuwa ni haram na hazikuwa zinaingia kwenye mzunguko ili lilipelekea mtaani hela kuzagaa kiasi ata laki ikaitwa si pesa ola sasa laki tunajua ni pesa.

Wafanyabiashara sikuzote wazo lao la kwanza kukwepa kodi, kipindi cha JK kuna meli 60 ziliwai kutia nanga pale bandarini Dar es Salaam na meli hizo zote hazikuwa recorded mahala popote na mwisho kontena zikapotea kusiko julikana, Zaman kipindi cha JK kontena kupotea huko bandarini kilikuwa kitu cha kawaida, Bandarini hapakuwa na scana ata ya kuscan vitu vinavyopita bandarini.

Nenda pale airport kipindi cha JK hakuna kikicho scsniwa ili kijulikane ni kitu gani...

Mwisho wa siku Magufuli alitamani kujenga Tanzania ya kesho, Magufuli hakuwa mwanasiasa ila alikuwa kiongozi, aliona bora aanze upya kuliko kuendelea na staili waliyotumia watangulizi wake.

Mwisho niseme tu huu wa kipindi cha Hayati ndo ulikuwa uchumi wetu halisi, huko nyuma kulikuwa na wajanja tu wenye kuchuma walivyotaka kuchuma lakini kwenye kujenga nchi hamna kitu.

Nakumbuka kipindi cha JK NGO zilopeta kweli lakini ki ukweli kabisa walikuwa hawalipi ata Tsh 150,000/= kwa mwaka wala hawapeleki ata hesabu zao za mwaka kwa msajili lakini alivyoingia Magufuli aligakikisha kila Wizara inayoona kuna sehemu inatakiwa ikusanye fedha inatakiwa kufanya hivo, hapo ukaanza utaratibu kama hupeleki hesabu zako kwa na hulipi ada shirika lako litafungwa na mengi yalifungwa maana yalikuwa hewa na hewa kweli cos ata mimi mwenyewe nishawah fanya kazi huko najua vyema na mpaka sasa mwenye NGO yake ninahakika anafanya kazi kwa unyofu mno.

Kiuweli tulichekea na tulipata mtu ambae alikuwa anatuambia ukweli, hizi habari za kulembeana na kupakana mafuta kwa mgongo wa chupa hakuwa nazo.View attachment 1741699
Fungua macho utazame,

1. Unasema enzi ya JK pesa ilikuwa ni haramu, naomba ufafanue kivipi? wakati watu walikuwa wanafanya kazi na kupata pesa, kwani kipindi cha JK pesa zilikuwa zinagawiwa bure? Kwanini useme eti zilikuwa za haramu?

2. Yaani wewe uchumi kudorora, mzunguko wa pesa haupo ndo unasema huo kwako ndo uchumi halisi? Kuwa serious mkuu.. fungua macho utazame tena kauli yako.
 
Nyie unaosema hamna vyama, huwa hamuwezi kuanzisha uzi zenu mpaka msubiri wenye vyama waanzishe? Sasa hapo tatizo ni hao wenye vyama kuanzisha nyuzi zinazobeba vyama vyao, au nyie msio na vyama lakini hamuwawez kujianzishia uzi zenu?


wengine utatuonea tu,
specialization yetu ni kusoma na kuchangia tu

kuhusu hao waanzisha thread zenye nondo, itabidi tuwaeleweshe tu kuwa hata darasa lenye watoto watukutu wasiojali kuhusu shule zaidi ya kupenda ubishi wa Diamond Vs Ali kiba ,
bado huwa wana waalimu wanaomaliza syllabus kwa kutimiza wajibu tu

ijapokuwa huwa wanajua wanapanda maharage wakitegemea kuvuna mahindi..
"wasted energy"
 
Mkuu umenikosha Kwa uchambuzi huu. Kiukweli tumelia mara nying na kusisitiza kuwa nchi yetu haina uwezo wa kutekeleza miradi ya matrilioni Kwa wakati mmoja lakin Mwendazake akawaamimisha wajinga kuwa sis sio wazalendo.
Na hii ndo point kubwa, sio kwamba tulikuwa tunapinga miundo mbinu, ila tulikuwa tunataka serikali iifanye kwa step ili isiparalse uchumi.. umenipata vema hapo
 
Hizi ndio aina za thread zinazotakiwa kuwepo jukwaa la siasa 👏👏👏,
at least watu wasio na interest ya vyama nao wapate kutoa mawazo yao pasipo kuwekwa katika ligi za kutetea vyama badala ya maslahi ya kitaifa ..
Ubarikiwe kwa muda wako mkuu
Asante mkuu,
 
Binafsi naona hizi ndiyo zile tunasema uchumi wa kwenye makaratasi ila kipindi cha JK tuseme tu ukweli fedha nyingi zilikuwa ni haram na hazikuwa zinaingia kwenye mzunguko ili lilipelekea mtaani hela kuzagaa kiasi ata laki ikaitwa si pesa ola sasa laki tunajua ni pesa.

Wafanyabiashara sikuzote wazo lao la kwanza kukwepa kodi, kipindi cha JK kuna meli 60 ziliwai kutia nanga pale bandarini Dar es Salaam na meli hizo zote hazikuwa recorded mahala popote na mwisho kontena zikapotea kusiko julikana, Zaman kipindi cha JK kontena kupotea huko bandarini kilikuwa kitu cha kawaida, Bandarini hapakuwa na scana ata ya kuscan vitu vinavyopita bandarini.

Nenda pale airport kipindi cha JK hakuna kikicho scsniwa ili kijulikane ni kitu gani...

Mwisho wa siku Magufuli alitamani kujenga Tanzania ya kesho, Magufuli hakuwa mwanasiasa ila alikuwa kiongozi, aliona bora aanze upya kuliko kuendelea na staili waliyotumia watangulizi wake.

Mwisho niseme tu huu wa kipindi cha Hayati ndo ulikuwa uchumi wetu halisi, huko nyuma kulikuwa na wajanja tu wenye kuchuma walivyotaka kuchuma lakini kwenye kujenga nchi hamna kitu.

Nakumbuka kipindi cha JK NGO zilopeta kweli lakini ki ukweli kabisa walikuwa hawalipi ata Tsh 150,000/= kwa mwaka wala hawapeleki ata hesabu zao za mwaka kwa msajili lakini alivyoingia Magufuli aligakikisha kila Wizara inayoona kuna sehemu inatakiwa ikusanye fedha inatakiwa kufanya hivo, hapo ukaanza utaratibu kama hupeleki hesabu zako kwa na hulipi ada shirika lako litafungwa na mengi yalifungwa maana yalikuwa hewa na hewa kweli cos ata mimi mwenyewe nishawah fanya kazi huko najua vyema na mpaka sasa mwenye NGO yake ninahakika anafanya kazi kwa unyofu mno.

Kiuweli tulichekea na tulipata mtu ambae alikuwa anatuambia ukweli, hizi habari za kulembeana na kupakana mafuta kwa mgongo wa chupa hakuwa nazo.View attachment 1741699
Waambie wakipata muda wapite na hapa ili waelewe vizuri [emoji116][emoji116]

 
Back
Top Bottom