Tuzo ya Best African Act aliyopewa Wiz Kid imerudishwa kwa mshindi halali Ali Kiba

Punguzeni chumvi basi[emoji23][emoji23]..Ni tuzo ya BEST AFRICAN ACT tu na sio WORLWIDE ACT
wewe nawe kumbe akili ndogo, sasa wiz akipokwa best african act atakuwa na kigezo gani kushindania worldwide act
 
Asanteeee!! Taarifa tamu hii,,, haters wanajibalaguza!! Oooh hainaogi
Ushindi wa mezani
KAMA HAINOGI JUA TUU KUWA HUJAFURAHIA!!! Mana siye mashabiki tunajua utamu wake,, wewe usiye shabiki wake automatically utaiona chungu..
Tunawaruhusu mjibaraguze tuu
 
Msalimieni The bold jama...
Ujumbe
"Hatimaye imerudi "[emoji39]
Hiki kiuzi chenu nilikuwa nakipita tu, sasa ngoja niwatolee uvivu [emoji35] [emoji35]

Kwanza mimi ntabaki kuwa tomaso mpaka nikiona Kiba amekabidhiwa hiyo tuzo otherwise naona kelele za chura tu hizi.

Na endapo akikabidhiwa kweli hiyo tuzo hii nadhani ndio itakuwa tuzo yake ya kwanza ya kimataifa lakini naona ameanza kwa kujitilia nuksi! Tuzo gani unaipata kwa kung'ang'aniza?? Kuandika mibarua kama mwanasiasa?? Kutuma mashabiki wako wakatukane watoaji tuzo ili upewe wewe???
Hainogi, haisisimui, haina mvuto..

Hata kama tuzo ikitokea (nasisitiza kama ikitokea) akapewa hiyo tuzo hakuna ubishi kuwa Katika kile kinyang'anyiro hakukuwa na msanii aliyefanya vizuri kuliko Wizz, sasa unajisikiaje kutukana mitusi kumshutumu aliyepewa tuzo kwa kustahili kabisa anyang'anywe upewe wewe??? Hebu tuwe wa kweli, Africa yote hii ni moja wazungu ndio walituwekea hii mipaka hivyo hata wanaigeria ni ndugu zetu na ndugu yetu Wizz amefanya vizuri kuliko msanii yeyote yule mwaka huu. Mnaweza kuleta ubishi wa kupiga kura na mambo gani sijui lakini hamuwezi kubisha kuwa Wizz ni msanii bora mwaka huu kuliko msanii yeyeto yuke Afrika.

Naijua hulka ya Wizz na naijua hulka ya meneja wake Mr. Sande, inawezekana kabisa baada ya mashabiki wa kiba kufululiza kumtusi kwenye mitandao, labda wamesusa na wameamua wairudishe kwa hiari yao hiyo tuzo! Wizz sio mtu mwenye kukodolea macho tuzo, ni msanii anayejua thamani yake hata usipompa tuzo ndio maana kamwe huwezi kumkuta anahamasisha apigiwe kura. Ni mtu yuko bize na hustle zake, hanaga hizi drama za tuzo tuzo, binafsi kuna siku nimewahi kuongea na Ricardomomo yuke meneja wa WCB nikamshauri wamfanye Diamond kufuata mfano huu wa Wizz unaoonyesh ukomavu na kujitambua.

Mnasema kuwa mashabiki wa mondi walikuwa wanamtukana Davido na bado akapata collabo!! Aisee inamaana hamkumbuki au mnajisahaulisha makusudi??
Collabo ya Number 1 ilirekodiwa mwezi novemba 2013, video ikafanyika January 2014 na nyimbo ikatoka february mwaka huo. Bifu la mondi na davido lilianza mwezi wa 11 baada ya tuzo za channel O. Kwa ufupi bifu lao lilianza mwaka baada ya mwaka mmoja kupita toka collabo ifanyike..
Sasa juzi juzi Kiba amemgomea Wizz kupanda jukwaani mombasa kabla yake, leo mnawaandikia barua MTV wampokonye tuzo wampe yeye kiba.. Hivi mnadhani atawafikiriaje?? Akiwanyima collabo mtasema mondi kafanya figisu kwasababu ni maswahiba na Wizz?? Mnajiharibia wenyewe kila siku na mnakesha kutafuta mchawi wakati mnajiroga wenyewe!!

Kumbukeni Wizz ndiye mwanamziki mwenye mashabiki wengi zaidi huko west africa kwasasa, hivi vitendo mnavyomfanyia kumtukana na kumuandama kiasi hiki mnadhani mashabiki wake wataanza kumchukuliaje msanii wenu??? Kinyongo wanachokitengeneza dhidi ya msanini wenu itafanya iwe ngumu sana kwa Kiba kupenya west africa..

Narudia tena na tena, kiba hana washauri, hana watu strategic, hana gret thinkers, watu wanaowaza kibiashara kuhusu mziki, hana watu mahiri wenye uwezo wa kunetwork, hana management yenye kufikiri nje ya boksi.

Umahiri pekee walionao ni kulalamika, kuongeza maadui kila uchwao, kutafuta sympath kwa jamii hata kwa kupotosha, kujihisi wanajua ilhali wana mengi bado ya kujifunza, kumpumbaza msanii wao kwa kumuwekea kioo mbele yake mfano wa hadubini ili ajione mkubwa kuliko uhalisia.. Hii itawagharimu sana.!
Kiba ni msanii mzuri na anakipaji kikubwa but he has a long way to go.


The Bold.
 
Povu linamtoka wiz hahaaa chezea kupokonywa tuzo [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
wabongo bhana sisi eti katuzo kenyewe kamoja, mara analinganishwa na chibu, chibu anaingiaje wakati habari ni ya kiba na wiz, btw umekubali kama kiba kachukua au?
Nimemjibu aliyeandika kua akawwwmbia dada zake wa madale tuzo iko kariakoo
Umeeelewa? Nona unadandia treni kwa mbele
 
i saw this coming, Mada ikibadilishwa,, tuzo ikionekana haimstahili alikiba,!! Anyway
Wizkid achukulie atakavyochukulia,, kwa hivyo mlitaka hatakama amepewa ushindi usio halali tusilalamike kisa atatunyima collabo???? Yaani alikiba ashinde halafu aache kupewa tuzo kisa kutafuta sympathy kwa wizkid???
 

Team kibakuli mzk hamjui alf washamba cjui mlizaliwa Enzi za pepe kale
 
Ali kiba kapewa ya best african act iyo ya worldwide act anabaki nayo wiz kid ndo maana hata kwny page ya mtv haijafutwa
 
wewe nawe kumbe akili ndogo, sasa wiz akipokwa best african act atakuwa na kigezo gani kushindania worldwide act
Sibishanagi na wasiojua kama wewe
Nani alikwambia kwamba ukishinda BEST AFRICAN ACT ndio unakuwa mshindi wa BEST WORLD WIDE ACT?!

Nenda kaangalie kama walioshinda kwenye mabara yao ndio wameshinda Worldwide?!hujui kubali tu
 
Mkuu Kiba na menejimenti yake wamefanya kitu cha aibu.. Watu waliopo kwenye industry watakuwa wananielewa!!

Watoaji tuzo sio malaika, hawawezi kufanya maamuzi ya kumridhisha kila mtu! Hivi unafahamu kuwa tuzo ya MTV MAMA kipengele cha Artist of the year mwaka jana hakupaswa kupewa Davido?? Ulimsikia Wizz kasema chochote?? Umejiuliza kwanini mwaka huu Wizz amepewa tuzo mbili za MAMA kitu ambacho hakijawahi kufanyika???

Kuna namna ya kuprotest pale ambapo unahisi haujatendewa haki kwa kunyimwa tuzo, sio hivi ambavyo kiba na timu yake walivyofanya!!
Mkuu naomba uikopi hii post na uihifadhi kwasababu nakuahidi kuwa hautakuja kumuona kiba akitajwa tena kuwania tuzo yoyote ya MTV.. Wamejiharibia sana
Mark my words, wameharibu! Uswahilini tunasema "Wamechinja kuku kwa njaa ya siku moja"

Nikupe mfano mwingine! Unakumbuka tuzo za MTV VMA mwaka 2009 kwenye kipengele cha Video of the year ambapo tuzo alipewa Taylor Swift wakati alistahili kupewa Beyonce video ya single ladies?? Kanye akaenda kuprotest jukwaani... Sasa kanye alikuwa sahihi kabisa but the way ambavyo aliprotest ndio akaharibu kabisa! Unakumbuka mwaka uliofuta MTV walifanya nini??

Kiba na menejimenti yake wameharibu, "wamechinja kuku kwa njaa ya siku moja"
 
Si ndo hapo sasa et collabo, kwani huyo wiz ndo nan mpaka ashobokewe mfyuu[emoji57] [emoji57] [emoji57]
 
Ali kiba hajalamika ametaka ufafanuzi kuhusu utaratibu wa ugawaji tuzo, na pia ni haki yake kujua na Kama tunzo ingekuwa sio yake wangetolea maelezo yanayoeleweka lakn kuirudisha tuzo kwa alikiba it means alideserve , na pia alikiba sio kwanza kulalamika ikumbukwe eddy kenzo pia alilalamikia mtvmama na yeye ni msanii mkubwa pia, kwahiyo ongeeni facts sio roho mbaya ziwasukume kuandika utumbo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…