Twende mbele, turudi nyuma: Nchi za wenzetu zilizoendelea wanapiga kazi


Kwa huku Africa secta Binafsi wanaojitahidi kidogo kwa kuwa wanalipwa kwa kazi wanayofanya
Ila huko kwingine ambapa hata ukisabisha loss mshahara unaingia ndiko kuna shida kubwa!
 
Hili la kukosa uaminifu linatugharimu sana kama taifa. Yaani leo hii uwe na unaishi dar halafu uwe na biashara mbeya ni jambo ambalo haliwezekani kibongobongo
Ni masikitiko makubwa sana kwa kweli
Huwa naona watu wanavyolalamika humu kutafuta ajira na wengine wataalamu na wafanisi wakubwa
Nawaza na kusema kwa kweli kama wangekuwa na sifa za uaminifu
Ningewekeza vingi na kuwaacha wanizalishie huko ila tatizo mswahili ukimwachia mali au biashara anaifanya ya mama yake

Wanakera sana kwa kweli yaani kutwa unaangalia saa ngapi wataiba
Niwaze kuibiwa au kuongeza biashara
Mungu awasaidie kwa kweli
 
"Halafu jumapili wakajazane makanisani wakipayuka kama mbayuwayu kumuomba Mungu wapate mafanikio."

Napigilia msumari hapa! Kwa ufupi (kama ni shetani, basi shetani kakaa mazima kwenye nyumba za ibada). Hizi dini hizi! Inasikitisha maana ndo chanzo cha UMASIKINI!
 
Watu mbona wanapiga kazi saa 11 asubuhi wapo barabarani mpka saa4 za usiku 😀
Bize for nothing! Ni kama mtu akikuambia usukume hukuta wa nyumba yako, utausukumua asubuhi hadi jioni utatokwa jasho na kuchoka lakini hakuna kipato utarudi nyumbani mikono mitupu! Ndo wabongo walivyo
 
Jaribu kutudadavulia kwanini unaona wana moyo wa kuchapa kazi ni kitu kinawamotivate?
Je uzalendo halisi au maslahi yako vizuri?
 
Bize for nothing! Ni kama mtu akikuambia usukume hukuta wa nyumba yako, utausukumua asubuhi hadi jioni utatokwa jasho na kuchoka lakini hakuna kipato utarudi nyumbani mikono mitupu! Ndo wabongo walivyo
Kama mfumo ndio umemsukuma kwenye kazi hizo mtu afanyaje sasa
Mtu kasoma ajira hakuna anaamua kuuza mitumba alafu unasema busy for nothing 😀
 
Ndio aisee, huko mtu kupiga kazi masaa 15 kwa siku kawaida, na wanajituma haswaaaa
Ni kweli mkuu na ni hakika ukisemacho ila na mfumo ama mifumo waliyoiweka iko imara kaka tofauti na huku kwetu africa mtu anafanya kazi kimazoea tena umkute kaaajiriwa na umma ndio kasheshe tupu. Ukitoka hapo uje kwa raia mmoja mmoja ndio shida kijana akipata nyumba na ka IST kimkoko kimoja ndio baasi ameridhika ni mwendo wa viwanja vya starehe.
 
Unaongelea efficiency; effectiveness au kupiga kazi ? Kwamba waafrica ni wazee wa kukaa vijwieni ? Nadhani pitia madesa yako upya.... Hard work does not Necessary Pay; Especially hii dunia ya Kilaghai...

View attachment 2964659
Uko sahihi.

Lakini mleta mada yuko sahihi pia. Sana.

Swali la kujiuliza ni ubora na utendaji wa watu wa huko ndio umewapa Mfumo thabiti unaowalinda wote kwa usawa ule ule kiasi kwamba matokeo mwisho wa siku ni almost sawa kwa wote kwa mujibu wa hiyo willingness ya kulipa gharama yoyote ili mradi kupata wanachohitaji?…ie Maisha mazuri…etc?

Je, sisi kinachotufanya tukwame ama kwenda mwendo wa kobe katika ujenzi mzima wa maisha yetu ni Mfumo ambao tumewekewa tu hata hatujui muwekaji ni nani na madhumuni ni Yapi? Kutunyonya?

Ama sisi ndio adui zetu kwa sisi wenyewe?

Kwamba tunahusika na aina ya Mfumo unaoendesha maisha yetu kiasi kwamba tuko katika mkwamo kwa sababu hakuna wa kumfunga paka kengele?

Kuna jambo lipo hapo kati linalosababisha utofauti huu mkubwa uliopo haswa ikizingatiwa kimaumbile tu ni wazi race ipi imependelewa kwa kiasi zaidi ya zingine katika kuendana na mazingira ya Dunia hii.

Je, hilo jambo ni makusudi na uumbaji wa binaadam mwenyewe? Ama ni natural force at work?

Tunaweza kulibadili na kupindua meza ama kuliondosha na kutengeneza usawa kati ya wote? Wa kule na wa huku?
 
Kazi inatakiwa ulipwe, sasa kubeba kuni za kupikia nyumbani kwako nani atakulipa?
Ama utendaji ulio bora zaidi ni pamoja na kutumia rasilimali ya bure ya uwezo wa kuakili kubuni/ kutengeneza nyenzo za kukuwezesha kukabiliana/kuishi ndani ya mazingira yako?

Utendaji wa subjects wa mleta mada ni pamoja na kuthubutu na kuweza kutumia akili/bongo zao effectively.

Hoja ipo.
 
Sasa bongo kazi zenyewe ziko wapi? Watu tuko iddle sana, tunatamani hata tufanye kazi tatu tati ila hata hiyo moja ni mtihani!
Kweli?

Unataka kusema mtaa/jamii unaoishi wewe kila mmoja yuko na anachohitaji kwa asilimia 100?

Hakuna kabisa chochote unachoweza wewe kuwa chanzo chake ndani ya jamii/mtaa wako? Kabisa?
 
Uko sahihi kabisa. Sisi mwanaume anatoka kazini na ni lazima apitie bar anywe na kesho yake anakwenda tena kazini. Majuu ukitoka kazini hata hiyo nguvu ya kupitia bar kunywa huna, na ukilazimisha kesho yake kazi huwezi kufanya. Wenzetu wanakunywa weekend tu au wakati wa likizo.
 
Ulieleta uzi huu Mungu akubiriki aise..Hakuna Mafanikio katika nchi yatakuja Bila kufanya kazi Kwa bidii Kwa bidii, weledi na utu. Niwe mkweli Kipindi naanza kuishi na hawa watu nilihisi ni mateso. These people work so hard, sijawai ona. Utakuta MTU 24 hours anfikiria kazi yake. Na wakipata time ya kuenjoy life eg weekend wanafanya kweli. Africa tusijidanye, hatutatoka kwa njia za uongo uongo,never.
 
Hayo ni matokeo ya kupenda unachokifanya.
 
Sasa bongo kazi zenyewe ziko wapi? Watu tuko iddle sana, tunatamani hata tufanye kazi tatu tati ila hata hiyo moja ni mtihani!
Mkuu kazi zipo nyingi Sana..sema ndoo hivyo..mentality zetu tayari zilijengwa kuajiliwa. Mfano hata kama umesoma Kiswahili..eg We need a lot Swahili novels, translators vitabu and any resources for Swahili speakers etc. Ni mfano,kuna mambo mengi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…