Twitter wamesema wameshuhudia mtandao wao ukiminywa nchini Tanzania

Kazi gani majizi tu
Hata mimi kila nikisikia MATAGA wanasifia kazi za magufuli huwa nazitafuta sizioni. Sana sana kuteua na kutumbua kila kukicha (ushahidi wa kutokujua kanuni za utawala bora). Barabara zilizompa jina na kumpenyeza kufikiriwa kuwa rais, nyingi zilijengwa na mtangulizi wake. Ndege alizonunua, amewabebesha walipa kodi mzigo wa kutoa ruzuku kuendesha shirika kwa sifa tu. Chato bado wanakunywa maji ya vidimbwi pamoja na kuwa na uwanka wa ndege.
 
Twitter nao hawachelewi jamani!!! Yaani nanyi mnawapiga spana ma CCM?
 
Uchaguzi ni tukio mhimu Sana katika kulinda au kuvuruga amani ya nchi

Hivyo Basi ni jukumu la serikali kuhakikisha Taifa linakuwa salama wakati huu wa uchaguzi. Na kwa Dunia Hii ya leo Internet ndio sehemu ya kuangalia zaidi kuliko hata huku kwenye maisha ya kawaida.
 
Hofu ya nini wakati uchaguz ni wa huru na haki?
 
CDM walikuwa wamejiandaa kwa disinformation ili kuleta taharuki na machafuko, vyombo vya usalama vimeona isiwe tabu, mtu anawekwa kibra kimya kimya saivi hadi j2 au j3 social media ikirudi kazi imeisha.
Wao wanadhani wangetumia tu mitandao kufanya upotoshaji wao wa kila siku.

Safari hii mazee wamejipanga kwelikweli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…