TZ Trends & Analysis: Hoja 30 za The Economist Kumhusu President Samia. Kuna za Kweli, za Uongo na Uzushi na Kutaka Kumpangia Watakacho Mabeberu, Jee?

TZ Trends & Analysis: Hoja 30 za The Economist Kumhusu President Samia. Kuna za Kweli, za Uongo na Uzushi na Kutaka Kumpangia Watakacho Mabeberu, Jee?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi,
Salaam,

Kati ya eneo gumu sana kwenye tasnia ya habari ni eneo la uchambuzi wa habari, news analysis. Japo Tanzania tuna vyombo vingi vya habari, na waandishi wengi wa habari, ni vyombo vichache ndio vina waandishi wenye uwezo wa kufanya news analysis.

Kwenye print media ndio angalau wanajitahidi kwenye editorial, lakini kwenye electronics main stream media, ukiondoa TBC ile segment ya Shabani Kisu, na Jicho Letu Ndani ya Habari cha Star TV, chini ya Mkongwe Dotto Emmanuel Bulendu, naweza kusema, Tanzania hatuna any serious news analysis na news analysts.

Hivyo kufuatia uzoefu wangu kwenye media wa miaka 30, sasa baada ya kustaafu, naendelea kuwatumikia Watanzania kwa kujitolea, kila nipatapo muda, nitakuwa nawapatia kitu kinachoitwa trends & analysis za mambo mbalimbali kwa kutanguliza mbele maslahi ya taifa.

Tukio la kifo cha ghafla cha Rais Magufuli, ni jambo ambalo halikuwahi kutokea, matokeo yake bado kuna trials na errors nyingi zitafanyika na serikali ya Samia hapa mwanzo mwanzo hadi itakapo stabilize, ambazo nyingine zitakwenda kinyume cha katiba, lakini kwa vile tukio hilo ni kama force majeure kwenye mikataba, tutavumiliana tuu.

Mfano kwa mujibu wa katiba, baada ya Ripoti ya CAG kukabidhiwa kwa rais, within the first 7 days, ilipaswa itue mezani kwa Spika. This is the most important report, katiba haikuweka mazingira yoyote ya ripoti hii kushindwa kuwasilishwa mezani kwa Spika within the prescribed time frame. Ila kiutu uzima tuu, ripoti hii ilibidi iwasilishwe jana saa 3 asubuhi. Very unfortunately jana hiyo Waziri wa Fedha alikuwa hajaapishwa hivyo hawawezi kuipokea. Natumaini itatinga Bungeni kati ya Jumanne na Alhamisi Ijayo.

Jingine ni ule waraka wa TLS kumtaka rais mpya Samia kulivunja Baraza la mawaziri la JPM na kuunda lake la Awamu ya Sita. Rais Samia kaamua kuanza Awamu yake ya 6, na mawaziri wachache wapya, na wengi ni mawaziri viporo wa Awamu ya Tano!, kwa hoja kuwa kile kiapo chao kwa utii kwa JPM, kinahuishwiwa kwake, kwa hoja kuwa kiapo ni kwa Taasisi ya Urais wa JMT na sio kwa mtu. Kwa maoni yangu, this is the first mistake ya rais Samia!, kwa executive appointees, hata rais akibadilika, wao wanaendelea, lakini kwa political appointees wote, hii ni serikali mpya ya awamu ya 6 na sio serikali ya muendelezo wa awamu ya 5!. Kiapo cha utii kwa Political appointees ni kiapo cha utii kwa rais aliye madarakani kwa awamu mpya, ndio maana hata Waziri Mkuu, hata kama ni yule yule, awamu ikibadilika, anateuliwa tena, anaidhinishwa tena na Bunge na kuapishwa upya!. Viapo vya utii kwa Political appointees ni non transferable!, JPM aliunda baraza lake, JPM kafa, Baraza lake lazima livunjwe ili Samia aanze na awamu mpya na Baraza jipya!. Hivyo ilibidi mawaziri wote wale kiapo kipya cha utii kwa Rais mpya Samia na sio kuhudumu kwa rais mpya kwa kiapo cha utii kwa rais aliyepita! JPM, ndio maana tukamshauri PM Majaliwa ange step down kumpa space Mama to start a fresh, na kama bado Samia anamuhitaji PM Majaliwa, ange m reappoint. Hivyo hii serikali ya Samia ya awamu ya 6, ni serikali ya awamu ya 6 ambayo pia ina muendelezo wa awamu ya 5!. Bila kulivunja Baraza la mawaziri la awamu ya 5, hii serikali ya Samia ni serikali ya awamu ya 5 ya 6!.

Hayo tuyaache yangu ya leo ni haya..
Baada ya kuisoma ile makala ya Jarida la Mabeberu la The Economist na hoja zake kumhusu Presidaa Samia, Nimekuja na hoja 30 kwa waliyoyasema kumhusu Samia. Kati ya hoja hizo, kuna za hoja za kweli, ni muhimu kutozipuuzia, kuna hoja za uongo na uzushi ni za kuzipuuza, lakini pia mabeberu hawa walivyo na akili, kuna hoja ambazo ni za kutaka kumpangia kazi kiana, rais wetu Mama Samia, ili afanye au atende kile mabeberu hawa wanacho kitaka!.

Nilisisitiza humu, kwa vile JPM hakupenda kupangiwa, na hatukumpangia, vivyo hivyo hata Samia, tusimpangie!, ila hakuna ubaya kumshauri na kumweleza jinsi mabeberu hawa wanavyo muona ni silaha muhimu sana ya kujiimarisha dhidi ya hila zozote za mabeberu hawa.

Ili uweze kulifaidi bandiko hili, anza na bandiko hili

Ukiona mabeberu wanaanza anza kuwasifu viongozi wazalendo wa bara la Afrika, ujue, wana lao jambo!.
Karibu kwenye hoja zangu...
    1. Hoping for change, Tanzania’s new president surely can’t be worse than the old one.-Hapa wanamsema JPM was worse president, hivyo sasa wana matumaini na Samia. Jee ni kweli JPM was worse president?.
    2. Tanzania’s new president, Samia Suluhu Hassan, vows to continue where her predecessor left off. –This is true.
    3. Pity the country if she keeps her promise. Hapa wanatuonea huruma kama atafuata nyayo za JPM. Jee ni kweli, Taifa la Tanzania, linahitaji kusikitikiwa iwapo Samia atafuata nyayo za JPM?.
    4. John Magufuli, was a covid-denying populist who ran a ruthless authoritarian regime. Jee ni kweli JPM run a ruthless authoritarian regime in Tanzania?.
    5. Many believe that the virus killed him. Hapa wana suggest JPM kaondolewa na covid!. Huu sio uongo?. Hao many who believes that ni wepi, wa wapi?!. Ili kuipush hii agenda ya covid, hawakuitangaza sababu ya kifo cha JPM iliyotangazwa na serikali yetu. Kumsingizia marehemu amekufa kwa kitu kingine chochote, zaidi ya kilichotangazwa rasmi ni kosa la consecration of the dead!, ni kutaka kumchafua marehemu na kuichafua nchi yetu kuwa watu wanakufa kwa covid, wakati reality wanakufa kwa magonjwa mengine!.
    6. For the moment liberal Tanzanians are surprisingly upbeat, in part because they do not take Ms Samia, the country’s first female leader, at her word.-Huu ni uongo!.
    7. She is a product of the ruling party, which has held power in different guises since independence from Britain in 1961. Hapa wanasema CCM inatawala toka uhuru kwa hadaa!-Huu pia ni uongo!.
    8. But she is no insider. She comes from the semi-autonomous archipelago of Zanzibar, not the Tanganyika mainland, which is the hub of power.-Huu ni uongo!. Samia ni CCM insider!, ila hana makundi!.
    9. Ms Samia was Mr Magufuli’s vice-president, but it is rumoured that she was foisted on him by CCM bigwigs. Hii sina uhakika, yaani JPM alilazimishwa kumchukua Samia na hao waitwao CCM bigwigs!.
    10. Foremost among these was Jakaya Kikwete, Tanzania’s president from 2005 to 2015, who is said to have admired her competent efficiency. –Hapa wamemsifu Samia ni efficient
    11. Mr Magufuli valued it less and she was excluded from his inner circle. Wanadai JPM hakumthamini Samia na hakuwa miongoni mwa watu wake wa karibu!. Huu ni uongo!.
    12. That is now seen as a reason for hope—as are the flashes of principle she has shown. Hapa wamemsifu Samia kuwa ni mtu wa principles na hapa ndipo matumaini na Samia yalipo lalia.
    13. In 2017, for example, she defied a presidential directive by visiting Tundu Lissu, a prominent opposition mp, as he recovered from being shot 16 times.Huu ni uongo!. JPM aliwa kuissue any directive Lissu asitembelewe?!, halafu eti Samia alimpuuza JPM akamtembelea Lissu kwa jeuri yake tuu!.
    14. Still, few are expecting a radical departure from her predecessor’s policies. –Hili lets wait and see, ila Samia tayari ameanza vizuri!.
    15. Not yet, anyway. Lacking a base within the party, Ms Samia will be concentrating on surviving the early stages of her presidency (inherited in accordance with the constitution), when she will be weakest. Huu ni uongo!. Wanadai Samia hana mimizi na Chama hivyo siku za mwanzo atakuwa dhaifu!. Kwenye hili tayari Samia has proved them wrong!, she is very strong woman!. Ile kuanza na kuanza, ameanza kwa kumgoa Dr. Bashiru pale Ikulu na kumtupia Bungeni as nobody!. Mtu alikuwa KM wa chama chake, then CS, alafu unamgoa na hata uwaziri hakustahili?!. It takes a very very strong man to do this!, sasa kama aliyefanya hili is a woman, then she is dam strong woman!. (Tanzania tutashuhudia “strength of a woman” (emphasize mine)
    16. Mr Magufuli’s faction still holds dominant positions in the cabinet and the party. (that was then, hii topic imekuwa overtaken by events)
    17. She is not totally helpless, however. She may not have a base of her own, but she does have potential allies. –Hapa wanasema Samia is helpless, ila atasaidiwa na wanaomuunga mkono ndio anawategemea!- Hapa pia they are wrong!. Wame mu under estimates Samia!. (Samia is a woman with streghth of a woman).
    18. With the support of Mr Kikwete’s previously sidelined faction, she was able to resist pressure to appoint Bashiru Ally, a Magufuli acolyte, as her deputy. Haya ni yale mauongo ya Twittwer!. Eti kulikuwa na pressure Dr. Bashiru ndio awe VP!. Eti kundi la JK waliokuwa sidelined na JPM ndio wamemsaidia Samia!.
    19. Instead she tapped Philip Mpango, the finance minister, pleasing international donors. – Huu pia uongo, ati chaguo la Dr. Mpango as VP ni ili to please mabeberu waitwao international donors!. Sababu za why Dr. Mpango, Samia amezitaja na sio hizo!.
    20. Still, she will have to avoid becoming too reliant on Mr Kikwete. –Hapa pia ni waongo!. Eti Samia anamtegemea sana JK kusimama!. Samia amethibitisha kwa kauli, maneno na matendo kuwa anasimama yeye kama yeye!.
    21. While foreign investors, often the butt of Mr Magufuli’s nativist policies, would welcome a return to the easy-going pro-market internationalism that marked the Kikwete years, many Tanzanians remember it as an era when corrupt patronage networks flourished. –Hapa mabeberu wanalaani sera za JPM za kutanguliza maslahi ya taifa kwa kuziita “nativist policies”, sasa wana matumaini kuwa Tanzania will return to the easy-going pro-market internationalism, kama cha JK ambapo rushwa na ufisadi vilitamalaki.
    22. Kikwete factions “smell blood and sense a comeback”, says Thabit Jacob of Roskilde University. It would be sensible to look to the former president for cover rather than guidance.-Hii pia sio kweli!.
    23. Ms Samia’s first challenge will be to reverse one of the most self-defeating coronavirus policies in the world. –Hapa ni kuichafua nchi yetu!. Jee kweli msimamo wa JPM on Corona ndio “self-defeating coronavirus policies in the world”.
    24. Mr Magufuli responded to the pandemic with a blend of quackery and denialism. –hii ni kweli
    25. Turning his back on science, despite having a phd in chemistry, he prescribed God, communion wafers and steam baths as prophylaxes. Hii ni kweli
    26. Unsurprisingly, the virus spread unchecked through the population. –Huu ni uongo wa kutaka kuichafua nchi yetu, etu kusema Corona imeenea sana Tanzania!.
    27. A more sensible approach is desperately needed. Hapa wanataka kutuingilia kwa kudai hatua za JPM ku deal na Corona sio sensible, sasa hatua sensible zinatakiwa kuchukuliwa kwa haraka.
    28. Diplomats and the World Health Organisation hope the new president will again start publishing official data on the virus (after a year-long pause), sack the anti-vaxxer health minister and sign Tanzania up to the covax vaccine-sharing programme. –Hapa wanataka kumpangia kazi Samia, walitaka Waziri wa Afya, atimuliwe, wanamuita anti-vaxxer, wakitumai President Samia sasa atakumbatia chanjo ya corona.
    29. Continuing to deny Tanzanians the jab would stain her reputation from the outset. –Hapa wanatutisha, eti Tanzania kuendelea kugomea chanjo ya Corona, kutapelekea sisi kutengwa na jumuiya ya kimataifa.
    30. Whether Ms Samia is for making such changes remains to be seen. In her first public appearances as president, she did not deign to wear a mask. –Hapa wana mashaka kama Samia ataleta mabadiliko tarajiwa kwenye vita vya Corona kwasababu hajaonekana kuvaa barakoa.
Hitimisho.
Swali ni Jee President Samia, atakubali kupangiwa kazi na mabeberu?.
Jibu ni only time will tell.

Nawatakia Ijumaa Kuu Njema

Paskali
 
Summarization nacho ni kipaji..., hususan karne hii ya SMS na watu wapo buzy kama unaweza ukasema / ukafikisha ujumbe kwa maneno mawili usitumi manne... au andika long article alafu summarize kwa wanaotaka maelezo zaidi wayapate huko...
 
Summarization nacho ni kipaji..., hususan karne hii ya SMS na watu wapo buzy kama unaweza ukasema / ukafikisha ujumbe kwa maneno mawili usitumi manne... au andika long article alafu summarize kwa wanaotaka maelezo zaidi wayapate huko...
Hawezi maana amekopi kama ilivyo
 
Hapo kwenye executive appointees na political appointees ndipo penye patashika.

Kusema kwamba executive appointees hawatakiwi kuapa ila political appointees ndio wanatakiwa kuapa nachanganyikiwa kwasababu nijuavyo hata hao wasiotakiwa kuapa bado wanatoka chama kile kile ambapo walishaapa mwanzo wakiwa political appointees kabla ya kupewa majukumu mengine ya kiserikali.

Hapo nahitaji msaada wako kidogo.
 
Wanabodi,
Salaam,

Kati ya eneo gumu sana kwenye tasnia ya habari ni eneo la uchambuzi wa habari, news analysis. Japo Tanzania tuna vyombo vingi vya habari, na waandishi wengi wa habari, ni vyombo vichache ndio vina waandishi wenye uwezo wa kufanya news analysis.

Kwenye print media wanajitahidi kwenye editorial, lakini kwenye electronics main stream media, ukiondoa TBC ile segment ya Shabani Kisu, na Jicho Letu Ndani ya Habari cha Star TV, chini ya Mkongwe Dotto Bulendu, naweza kusema, Tanzania hatuna any serious news analysis na news analysts.

Hivyo kufuatia uzoefu wangu kwenye media wa miaka 30, sasa baada ya kustaafu, naendelea kuwatumikia Watanzania kwa kujitolea, kila nipatapo muda, nitakuwa nawapatia kitu kinachoitwa trends & analysis za mambo mbalimbali kwa kutanguliza mbele maslahi ya taifa.

Tukio la kifo cha ghafla cha Rais Magufuli, ni jambo ambalo halikuwahi kutokea, matokeo yake bado kuna trials na errors nyingi zitafanyika na serikali ya Samia hapa mwanzo mwanzo, ambazo nyingine zitakwenda kinyume cha katiba, lakini kwa vile tukio hilo ni kama force majeure kwenye mikataba, tutavumiliana tuu.

Mfano kwa mujibu wa katiba, baada ya Ripoti ya CAG kukabidhiwa kwa rais, within the first 7 days, ilipaswa itue mezani kwa Spika. This is the most important report, katiba haikuweka mazingira yoyote ya ripoti hii kushindwa kuwasilishwa mezani kwa Spika within the prescribed time frame. Ila kiutu uzima tuu, ripoti hii ilibidi iwasilishwe jana saa 3 asubuhi. Very unfortunately jana hiyo Waziri wa Fedha alikuwa hajaapishwa hivyo hawawezi kuipokea. Natumaini itatinga Bungeni kati ya Jumanne na Alhamisi Ijayo.

Jingine ni ule waraka wa TLS kumtaka rais mpya Samia kulivunja Baraza la mawaziri la JK na kuunda lake la Awamu ya Sita. Rais Samia kaamua kuanza Awamu yake ya 6, na wachache wapya, na wengi ni mawaziri viporo wa Awamu ya Tano, kwa hoja kuwa kile kiapo chao kwa utii kwa JPM, kinahuishwiwa kwake, kwa hoja kuwa kiapo ni kwa Taasisi ya Urais wa JMT na sio kwa mtu. Kwa maoni yangu, kwa executive appointees, hata rais akibadilika, wao wanaendelea, lakini kwa political appointees wote ilibidi wale kiapo kimya kwa Rais Samia na sio kiapo cha utii kwa JPM, lakini kumtumikia Samia, ndio maana tukamshauri PM Majaliwa ange step down kumpa mama space to start a fresh, na kama bado anamuhitaji PM Majaliwa, ange m reappoint.

Hayo tuyaache yangu ya leo ni haya..
Baada ya kuisoma ile makala ya Jarida la Mabeberu la The Economist na hoja zake kumhusu Presidaa Samia, Nimekuja na hoja 30 kwa waliyasema kuhusu Samia. Kati ya hoja hizo, kuna za hoja za kweli, ni muhimu kutozipuuzia, Luna hoja za uongo na uzushi ni za kuzipuuza, lakini mabeberu hawa walivyo na akili, kuna hoja ambazo ni za kutaka kumpangia kazi kiana, rais wetu ili afanye au atende kile mabeberu hawa wanacho kitaka.

Nilisisitiza humu, kwa vile JPM hakupenda kupangiwa, na hatukumpangia, vivyo hivyo kwa Samia, tusimpangie, lakini kumshauri na kumweleza jinsi mabeberu hawa wanavyo muona ni silaha muhimu sana ya kujiimarisha dhidi ya hila zozote za mabeberu hawa.

Ili uweze kulifaidi bandiko hili, anza na bandiko hili

Ukiona mabeberu wanaanza anza kuwasifu viongozi wazalendo wa bara la Afrika, ujue, wana lao jambo!.
Karibu kwenye hoja zangu...
Hitimisho.
Swali ni Jee President Samia, atakubali kupangiwa kazi na mabeberu?.
Jibu ni only time will tell.

Nawatakia Ijumaa Kuu Njema

Paskali
Ndio maana magufuli alikua anaamua yeye mwenyewe aendeshaje nchi,ukisikiliza sana watu watakuendesha kila mtu anataka umtimizie hitaji lake na makala zao za ajabu ajabu.
Hakuna binadamu mwenye shukrani dunia hii na huwezi pendwa na watu wote
Siku si nyingi wataanza kumropokea na mama samia na kumpangia aongozaje nchi
Hii nchi inabidi iendeshwe kimagufuli magufuli ttu.Ndio itaenda vizuri
 
Ndio maana magufuli alikua anaamua yeye mwenyewe aendeshaje nchi,ukisikiliza sana watu watakuendesha kila mtu anataka umtimizie hitaji lake na makala zao za ajabu ajabu.
Hakuna binadamu mwenye shukrani dunia hii na huwezi pendwa na watu wote
Hakuna mtu anataka fulani apendwe (unless otherwise ni kwenye michakato ya kutafuta life partner) kinachoongelewa na inachobidi kitazamwe ni kama anafuata haki, utaratibu na sheria..., hayo mengine ni ziada....

Sasa cha kujiulize Bwana yule alifuata hayo..., na yaliyosemwa alisingiziwa au yalikuwa kweli (Kama mtu unazo akili za kusoma na macho ya kuangalia unasoma na una-draw your own conclusion sio usubiri upewe na conclusion) Sasa bwana yule kuzima midomo ya wasiokubaliana na yeye na kutumia hoja za nguvu na sio nguvu za hoja...., hapo nadhani alipwaya....
 
Hakuna mtu anataka fulani apendwe (unless otherwise ni kwenye michakato ya kutafuta life partner) kinachoongelewa na inachobidi kitazamwe ni kama anafuata haki, utaratibu na sheria..., hayo mengine ni ziada....

Sasa cha kujiulize Bwana yule alifuata hayo..., na yaliyosemwa alisingiziwa au yalikuwa kweli (Kama mtu unazo akili za kusoma na macho ya kuangalia unasoma na una-draw your own conclusion sio usubiri upewe na conclusion) Sasa bwana yule kuzima midomo ya wasiokubaliana na yeye na kutumia hoja za nguvu na sio nguvu za hoja...., hapo nadhani alipwaya....
Kila utawala una strength na weakness yake. Hio ilikua weakness yake mlibidi mjue jinsi ya kwenda nae maisha yaende.
 
Hilo gazeti lilipigwa marufuku Tanzania wenzetu mnalipata wapi wakati serikali ilishalipiga pini marufuku Tanzania?

Mna quote toka gazeti lililopigwa marufuku?
 
Kila utawala una strength na weakness yake. Hio ilikua weakness yake mlibidi mjue jinsi ya kwenda nae maisha yaende.
Kwahio hao walioongea walikuwa wanaoongelea weakness zake au walikuwa wanatunga vitu ambavyo havipo...,

Na ndio maana binafsi ni vigumu kupinga / kulalamika kazi zake akiwa waziri, huenda hizo strength zake zilifaa akiwa mtendaji na sio kiongozi wa kuongoza na kuunganisha watu...., Mtu anaweza akawa bondia mzuri ila sababu ni mwanamichezo sio necessarily akawa mwanasoka mzuri pia...
 
Naona mzee wa makala ndefu umerudi tena kwa kasi baada ya kupigwa pin.

Sie tupo,karibu sana kwenye jukwaa letu huru ingawa sio tu zati eksitenti.
 
umeanza kujipendekeza na kwa mama samia? wewe uko kwenye black list ya hao watu, concentrate kwenye kazi zako mkuu, hakuna appointment utapata hata lusiku na lumwe.
 
Back
Top Bottom