paul sylvester
JF-Expert Member
- Mar 18, 2020
- 3,503
- 3,499
Sahihisha paragraph ya 2 iwe Machi 1, 2021.Wizara ya Afya imebaini upotevu wa Sh26.7 bilioni za dawa uliosababishwa na uzembe, kutojali katika usimamizi wa mfumo wa ugavi wa bidhaa za afya, viashiria vya hujuma, wizi na udokozi wa bidhaa za dawa.
Hayo yamesemwa leo Machi Mosi, 2020 na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk Doroth Gwajima wakati akitoa tamko kwa vyombo vya habari kuhusu matokeo ya ufuatiliaji huo.
“Nimekuwa nikipokea malalamiko mengi kutoka kwa wananchi kuhusu kukosa huduma ya dawa na vipimo katika vituo vya kutolea huduma katika ngazi zote kinyume na matarajio, jumla ya thamani ya fedha ambayo imethaminishwa kwa upungufu huu inakadiriwa kuwa siyo chini ya Sh26.7 kwa kipindi cha Julai 2019 hadi Desemba 2020,” amesema Dk Gwajima.
Amesema kufuatia malalamiko hayo, wizara iliunda kamati ya wataalamu kutoka Wizara na taasisi za sekta mbalimbali ili kufanya ufuatiliaji katika hospitali 28 za rufaa za mikoa kwa kipindi cha miezi 18.
“Lengo ilikuwa kubaini changamoto zinazochangia upatikanaji duni wa dawa na vipimo licha ya kuongezeka kwa mtaji wa dawa,
Jumla ya bidhaa za dawa na vipimo 20 hadi 30 tu kati ya nyingi zilizo kwenye orodha ya bidhaa za afya kwa kituo husika ndiyo zilifanyiwa ufuatiliaji kuanzia ununuzi, mapokezi na matumizi,” amesema Dk Gwajima.
Mwananchi
Mbali ya kuibwa na kuuzwa nchi jirani zingine zimekuwa zikiozea Bohari ya Dawa - MSD na badae kuharibiwa na kuchomwa kwa maana ya expires!!!!!!.Wizi wa dawa ni biashara kubwa sana kuna kipindi Marekani kupitia usaid ilikuwa inatoa msaada wa dawa za malaria Tanzania lakini dawa hizo zilikuwa zinakutwa zinauzwa Angola walipoamua kufatilia qakakuta kontena likifika airport linapotea
Ni kweli kabisa!!!!Sahihisha paragraph ya 2 iwe Machi 1, 2021.
Katika hili yule mtu ambaye anashtakiwa Mahakamani na TAKUKURU ndiye mhusika Mkuu ambaye amepelekea upotevu wa Tsh 26 Bilioni. Huyu ni Laurean BWANAKUNU Rugambwa ambaye kwenda kwake MSD kuligubikwa na mizengwe.
Na akiwa Mkurugenzi Mkuu MSD alijenga mtandao wa yeye, Waziri Ummy Mwalimu, supplier wa dawa Bahari Pharmacy na baadhi ya watu wa TISS katika kuhujumu MSD.
Sasa ni wakati mwafaka wa kuboresha mashataka yake ili upotevvu huu uweze kuwa accounted
Kwa nchi hii mtu hawezi kujificha!!Sahihisha paragraph ya 2 iwe Machi 1, 2021.
Katika hili yule mtu ambaye anashtakiwa Mahakamani na TAKUKURU ndiye mhusika Mkuu ambaye amepelekea upotevu wa Tsh 26 Bilioni. Huyu ni Laurean BWANAKUNU Rugambwa ambaye kwenda kwake MSD kuligubikwa na mizengwe.
Na akiwa Mkurugenzi Mkuu MSD alijenga mtandao wa yeye, Waziri Ummy Mwalimu, supplier wa dawa Bahari Pharmacy na baadhi ya watu wa TISS katika kuhujumu MSD.
Sasa ni wakati mwafaka wa kuboresha mashataka yake ili upotevvu huu uweze kuwa accounted
Tukiishi Kwa kufumbiana macho hakuna kitakachofanyikaNi kweli kabisa!!!!
Na manunuzi ya hizo dawa zilikuwa zinanunuliwa kiholela sana pale MSD wakati wa uongozi wa huyo Laurian Ruganbwa Bwanakunu. Ni kweli kabisa kulikuwa na syndicate kubwa na hatari sana kwenye suala la manunuzi ya dawa pale MSD hadi kwenye Tender Board ambapo Bwanakunu alihakikisha anaweka team yake kwa mfano; Abdul Mwanja - Katibu wa Tender Board, Victoria Mwanri Elangwa - Mwenyekiti wa Tender Board, hii combination ilikuwa ni hatari sana kwa ustawi wa Bohari ya Dawa - MSD!!
Kwa vile huna unalolijua, una haki ya kubwabwaja namna hii.Haya mambo Ndiyo yamelifanya bara la Africa kuwa na watu wachache wanaoshika Uchumi wake na wengine wengi kuwa masikini wa kutupwa
Wizara iwachukulie hatua Kali hawa majambazi wasiotosheka na haki ya jasho Lao
JPM na Serikali yake wanahaha Ni Kwa kiasi gani maji yawafikie kila mwananchi, umeme na huduma Bora za kiafya, halafu watu wachache tu wawe sehemu ya mamilioni ya Watanzania kukosa haki zao na saa nyingine kupoteza maisha Kwa sababu Yao!!
Wakamatwe na Sheria ifuate mkondo wake
mum onee kwa kuwa dada wa watu mpole. Yule mjeshi nadhani anafaa aendelee tu.Tureteeni cheupe.
Walaji na wapigaji ni watumishi wa hiyo wizara,hakuna mtu anayeweza kutoka kubeba zege akaenda kuhujumu hospitalTimu ya ukaguzi maalumu kutoka Wizara ya Afya imegundundua ubadhirifu huo wa dawa na vifaa tiba kutoka hospitali hizo za rufaa za mikoa kwa kipindi cha miezi 18 kuanzia Kula 2019 hadi Desemba 2020. Hayo yametangazwa leo na Waziri wa Afya Dr Dorothy Gwajima wakati akitoa taarifa ya uchuguzi huo uliotokana na malalamiko ya wananchi ya kukosa dawa mara kwa mara kila wakienda kutibiwa kwenye hospitali hizo. Taarifa kamili soma kiambatanisho hapo chini
Nasikia alipigwa beat na stone juu ya kufanya mbwembwe mitandaoni kujitafutia umaarufu kuliko mwenye nyumbaSiasa bana mama kaona hii ndo kiki ya kumrudishabkwenye raman
Hakuna Aliye SalamaHapo wafamasia wanaenda kukalia kuti kavu
Duuh!Mfumo wa afya wa nchi hii lazima ubadilike kinyume na apo mtakuwa mnawaonea watumishi kila siku kuwa wanawaibia dawa.
Hospital na na vituo vya afya vilivyochin ya serikali huduma za misamahaa ziko juu kuliko wanaolipia so kujiendesha n kaz
Kama nchii tuamue if tunatoa huduma za afya kama sehemu ya kusaidia wanachi au tuiendeshe sekta ya afya kama private sekta kina aga khan.
Nb wananchi wasifurahie iyo kashfa anayoieneza Mama coz kinachofuata n maumivu kwao maaana sasa huduma zinaenda kuwa ghali kwao kwa lengo la hospital kupata faida na kujiendesha kama taasisi binafsi
Wanaowalipa hukata malipo kwa visingizio mbalimbali ikiwemo dawa ni nyingi sana au ghali kuliko kawaida.Mlungula kivipi mkuu? Fafanua tujifunze wengi hapa