Ubaguzi: Machotara Hizbu, Zanzibar ni nchi ya Waafrika

Ubaguzi: Machotara Hizbu, Zanzibar ni nchi ya Waafrika

Machotara tumepata ujumbe.Kumbuka Muhindi na Chotara ni watu wawili tofauti.Chotara amechangia damu ya Uafrika na mwenye asili ya weupe yaweza kuwa Muarabu,Muhindi au Mungu.
Hongereni CCM kwa double standard.Hope angekuwa aliye weka bango hilo ni mwanachama wa CUF au Chadema toka Jana angekuwa jela akisubiria kesi yake kutajwa kesho.
Lakini kesi ya jinai iwe ameua,ameiba,ametukana nk nk husihia kuwekea kwenye mitandao ikisema CCM wa naomba radhi kwa kosa lililofanywa na watu wasio julikana au na mwananchi mmoja.
Kwanini msiseme UVCCM? Mnahofu ya nini??Machotara tumepata ujumbe.
Marekebisho kidogo kwenye rangi isomeke mzungu nadhani.
 
Jaribu kuelewa ndugu, mimi nazungumzia tatizo la ubaguzi zanzibari na njia ya kulimaliza, na wala sitetei chama fulani cha siasa.

Kwasababu hata kikiingia chama kingine madarakani huu ubaguzi nilioueleza kua ni wa kihistoria na kijamii hauwezi kuisha.

Na hicho chama hakitaweza kulimaliza tatizo hilo bila kuwa na mikakati madhubuti ya kushiriki jamii nzima kama nilivyoeleza hapo juu.



Tinta wacha kuwa biased na unachoandika. Mbona suluhisho ya huo ubaguzi tayari lipo kikatiba. Katiba ya kuanzishwa kwa vyama vya siasa inatamka wazi kabisa Vyama vya kisiasa viwe vya kitaifa na visiwe na mlengo wa dini ama ubaguzi wa aina yoyote. Tatizo letu liko kwenye kufuata hiyo sheria na katiba yenyewe. Linapokuja suala la kufuata sheria CCM ndio mvunjaji mkubwa wa sheria za nchi. Shein kashindwa uchaguzi hataki kuachia madaraka! CCM inaendeleza ubaguzi kwa vitendo na maneno lakini hakuna wa kuweza kuwachukulia hatua kwa sababu wana nguvu za dola. Mimi nakushauri usianze kuzunguka mbuyu wala kutafuna maneno, Kikatiba basi CCM inapaswa kufutwa na msajili wa vyama. Ona hata yeye yuko kimya kwa jambo hili.
 
machotara hawahitajiki zanzibar. machotara hawatakiwi ccm. hata shein ni chotara. haa haa ubaguzi ni sumu mbaya sana. hiyo ndo ccm...
 
Nakubaliana nawe kwa asilimia 98 kuhusu vijana hao kuweka bango hilo. Lakini lazima pia tuwe wakweli. wale waarabu waliondoka Zanzibar baada ya mapinduzi au waarabu hao waliopinduliwa bado wanadai (siyo rasmi) kuwa Zanzibar ni yao na kwamba kwa kuwa waliondolewa kwa mtutu wa bunduki watarejea kupitia sanduku la kura. Sasa hapo ndipo tatizo. Kinachoonekana hapa ni kuwa waarabu hao wanatumia baadhi ya viongozi wa CUF kutaka kurejea Zanzibar kwa njia ya kura...
Uzushi mtupu, kwa nini mnakawaida ya kukimbilia kutumia karata hii mambo yanapo waendea ndio sivyo?

Sitashangaa kesho ukija na uzushi kwamba mna taarifa ya kuaminika kwamba Meli ya Sultani imetia nanga Ushelisheli ikiwa mbioni kuja Zanzibar kumrudisha madarakani Jamshed au mrithi wake.

Mtasema lolote lenye lengo la kudiscredit baadhi ya Raia wenzenu - kisa madaraka!!

Jaribu kurudia kusoma hoja zako hapo juu uone kama ninacho kisema hapa nakuonea.
 
Cha kushangaza hao viongozi wote wa CCM karibia wote wake zao ni machotora na watoto wa ni machotora.
Kama ilivyo hata huku bara viongozi wengi wa CCM wameoa wachagga kama sio Kaskazini lakini ndio wakwanza kuwapandikizia majungu na kuwabagua watu wa huko..
 
Tinta wacha kuwa biased na unachoandika. Mbona suluhisho ya huo ubaguzi tayari lipo kikatiba. Katiba ya kuanzishwa kwa vyama vya siasa inatamka wazi kabisa Vyama vya kisiasa viwe vya kitaifa na visiwe na mlengo wa dini ama ubaguzi wa aina yoyote. Tatizo letu liko kwenye kufuata hiyo sheria na katiba yenyewe. Linapokuja suala la kufuata sheria CCM ndio mvunjaji mkubwa wa sheria za nchi. Shein kashindwa uchaguzi hataki kuachia madaraka! CCM inaendeleza ubaguzi kwa vitendo na maneno lakini hakuna wa kuweza kuwachukulia hatua kwa sababu wana nguvu za dola. Mimi nakushauri usianze kuzunguka mbuyu wala kutafuna maneno, Kikatiba basi CCM inapaswa kufutwa na msajili wa vyama. Ona hata yeye yuko kimya kwa jambo hili.

Kwani wewe unadhani maalim sefu akipewa nchi ubaguzi zanzibar utakua umekwisha?

Na je ubaguzi zanzibari uko kwenye siasa tu?

Na je ni sababu gani ya msingi iliojenga misingi ya ubaguzi zanzibari hata kabla ya kuwepo ccm?

Na unasemaji ubaguzi ambao nimetaja kua kuna kundi kubwa la wazanzibar limeathirika nao? Ikafika hatua ya kuwabagua hata wabara leo hii na kuwaita watwana?

Je dawa ya ubaguzi wa kijamii utaisha tu pindi sefu akichukua nchi?


Tatizo lako wewe umeangalia athari ya ubaguzi kwenye siasa tu! Hilo ni dogo ndugu! Tatizo ni kubwa zaidi ya hapo mara elfu kumi!

Wanawajua na kuijua zanzibari vizuri wanafahamu.
 
Kwani wewe unadhani maalim sefu akipewa nchi ubaguzi zanzibar utakua umekwisha?

Na je ubaguzi zanzibari uko kwenye siasa tu?

Na je ni sababu gani ya msingi iliojenga misingi ya ubaguzi zanzibari hata kabla ya kuwepo ccm?

Na unasemaji ubaguzi ambao nimetaja kua kuna kundi kubwa la wazanzibar limeathirika nao? Ikafika hatua ya kuwabagua hata wabara leo hii na kuwaita watwana?

Je dawa ya ubaguzi wa kijamii utaisha tu pindi sefu akichukua nchi?


Tatizo lako wewe umeangalia athari ya ubaguzi kwenye siasa tu! Hilo ni dogo ndugu! Tatizo ni kubwa zaidi ya hapo mara elfu kumi!

Wanawajua na kuijua zanzibari vizuri wanafahamu.
Nafikiri linaweza kupunguza sana tu.Sababu nazijua siasa za Zenji
 
Hii ndo CCM ya sasa...... Si ajabu hakuna kiongozi wa CCM atakayekemea!!!
 
Kwa hali hii zenj sio shwali,kama dr.shein anataka madaraka kwa nguvu,tena kwa kutumia hoja za kibaguz,cc yetu macho.
 
Mohammed Said usiwe mnafiki.
Wewe ni mmoja wa watu humu mtandaoni mlioendeleza ubaguzi, kwako ulikuwa wa kidini.

Mwalimu aliwaonya, na sasa utabiri wake unatimia.
Mwalimu alisema,
"Zanzibar ikianza kujibagua toka Bara hawatabaki salama maana slama ya Zanzibar ni umoja na Bara.
Wakiisha kuwabagua Bara watakuwa wamefanya dhambi kama wachawi wanaokuka nyama ya watu.
Ulila nyama ya mtu utaendelea kula nyama ya mtu.
Mwalimu aliendelea kuwa, baadaye Wazanzibari wataendeleza dhambi ile ile ya ubaguxi na kugundua kua Zanzibar kuna Wazanzibari na Wazanzibara, na kuna Wapemba na Waunguja, hawatabaki salama hata kidogo"

Leo Mohammed Said, ukiwa mtu mzima mwenye akili yako washangaa nini, umeuendekeza sana ubaguzi wa kidini na makala zako za kuwa sifia na kuwaenzi "wazazi wako waislamu" humu mtandaoni, kwamba ndo walileta uhuru.
Ulihusika moja kwa moja kupanda mbegu za chuki katika jamii.

Zanzibar walipoanza na sera za kujibagua, ili wapate kujitambulisha nani ni mzanzibari(kwa kuwabagua wabara) sikuwahi kuona makala zako za kuonya juu ya ubaguzi huu.
Wengi tulilaumu hili, lakini kwa vile wazanzibari kupitia Baraza La Wawilishi, ndo liliendeleza ubaguzi huu hadi kufikia hatua ya kumpiga mrufuku ya kukanyaga Zanzibara Waziri Mkuu Pinda, wengi walishangaa ubaguzi na umoja wa kibaguzi wa wazanzibari.
Lakini hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa kuonya juu ya hili.

Leo mbele ya kadamnasi u Hizbu na u ASP unaonyeshwa hadharani- tofauti zilizokuwepo hata kabla ya uhuru.
Halafu mtu mwenye akili unailaumu CCM.

HUU NI UNAFIKI MKUBWA.
Mnavuna mlichopanda, na Mwalimu was right, salama ya Zanzibar ni Tanganyika.
Mohamed Said has never and will never be consistent in his arguments.
 
UBAGUZI! UBAGUZI! UBAGUZI!
 

Attachments

  • 1452613504013.jpg
    1452613504013.jpg
    26.8 KB · Views: 30
Tofauti kati yu huyo kijana na Mtoto wa Mfalme Rizi yeye aliandika kwenye Ukurasa wake wa Facebook na pia alitamka maneno ya kibaguzi kwenye mkutano wa UVCCM wakati huyu kijana yeye ametembea na ilo bango kwenye sherehe ya kitaifa...

Tukumbuke tu Rizi alisema "Kamwe yeye akiwa hai Mkaskazini hatakaa atawale hii nchi" ina maana hao Wakaskazini si Watanzania.. Dhambi hii itawatafuna tu, sasa mmejidhihirisha huko Zanzibar pia...
 
Kwani wewe unadhani maalim sefu akipewa nchi ubaguzi zanzibar utakua umekwisha?

Na je ubaguzi zanzibari uko kwenye siasa tu?

Na je ni sababu gani ya msingi iliojenga misingi ya ubaguzi zanzibari hata kabla ya kuwepo ccm?

Na unasemaji ubaguzi ambao nimetaja kua kuna kundi kubwa la wazanzibar limeathirika nao? Ikafika hatua ya kuwabagua hata wabara leo hii na kuwaita watwana?

Je dawa ya ubaguzi wa kijamii utaisha tu pindi sefu akichukua nchi?


Tatizo lako wewe umeangalia athari ya ubaguzi kwenye siasa tu! Hilo ni dogo ndugu! Tatizo ni kubwa zaidi ya hapo mara elfu kumi!

Wanawajua na kuijua zanzibari vizuri wanafahamu.




1.Kwani wewe unadhani maalim sefu akipewa nchi ubaguzi zanzibar utakua umekwisha?

jibu: Kwa vile Seif yeye ni mwathirika wa ubaguzi atakuwa anamajibu ya hilo. Tizama mfano wa Mandela na South Africa. maamuzi ya wazanzibari yaheshimiwe! Tukitaka tusitake katiba ya nchi inampa rais wa nchi mamlaka ya zaidi ya Utume. Asipoliondio hilo tatizo wazanzibari watamuondoa madarakani kama walivyomuondoa Shein kwenye kura. nadhani Seif analijua hilo!

2. Na je ubaguzi zanzibari uko kwenye siasa tu?
Jibu: ubaguzi Zanzibar hauko kwenye siasa tu. uko hata kwenye michezo, elimu hata maofisini. Kati ya hizo siasa ina asilimia zaidi ya 90 kwenye ubaguzi. Watawala wa Zenji (ambao ni CCM) ndio wanaendeleza huo ubaguzi kwa kisingizio cha Mapinduzi. dawa ni kuiondoa CCM zanzibar madarakani .


3. Na je ni sababu gani ya msingi iliojenga misingi ya ubaguzi zanzibari hata kabla ya kuwepo ccm?

Jibu: Ubaguzi ulisababishwa na Serikali ya Usultani kabla ya 1964. lakini kwa kiasi kikubwa basi uliondolewa na ASP baada ya 1964. Mapinduzi ya ASP yaliondosha ubaguzi wa aina zote Zanzibar. CCM ndio inalea ubaguzi sasa.


4. Na unasemaji ubaguzi ambao nimetaja kua kuna kundi kubwa la wazanzibar limeathirika nao? Ikafika hatua ya kuwabagua hata wabara leo hii na kuwaita watwana?

Jibu: Tufuate misingi ya sheria na katiba. Yoyote mwenye kumbagua Mtanzania kwa aidha Rangi, Dini au kabila lake basi sheria ifuate mkondo full stop.

5.Je dawa ya ubaguzi wa kijamii utaisha tu pindi sefu akichukua nchi?

Jibu: Suali lako la 1 na la 5 linafanana. hata hivyo nitakujibu kwa faida yako tu. Seif anaweza kufanya pale ambapo CCM wameshindwa. Mbona magufuli kasaidia kuziba njia za kutokulipa kodi ambapo mkapa na kikwete walishindwa? Pengine Seif hatoweza kulimaliza hili tatizo kwa asilimia 100 lakini anaweza kulianza.
 
mwajua leo kuwa wazanzibara wanabaguana?mahala popote pakiwa hapana USAWA basi ubaguzi haukosekani? ikiwa upande mmoja unahisi kuwa hautendewi haki hasa katika kupiga hatua za kimaandeleo basi ubaguzi haukosekani.mifano ni Nigeria,sudan, na hata ZNZ hili liko wazi angalia hali ya pemba na unguja ilivyo!
nia yangu si kutia utambi dhana ya ubaguzi ila ni kutaka kuwaamsha na hatua stahiki wazichukue. lakini pia kwa Tanzania bara, ukiona nyumba ya jirani ugoma umeanza, tarajia kelele za vigoma nawe zukufikie na si ajabu hata usingizi utaukosa kwa kelele za vigoma. zanzibar wakibaguana na wakaachwa tu ujue na hata bara hali hautakuwa njema. kwa hiyo suala la zanzibar na bara linawahusu. ubaguzi usikemewe kwa matamko ya karatasi moja tu ya "taarifa kwa umma" , ubaguzi uondolewe kwa vitendo. wanasiasa wawahudumie wananchi bila ya kuwagawa na huduma pia zilingane si pemba si unguja!
mods pls msiifute hii comment.nia ni kujenga na si kubomoa
 
Duh,hii ni dhambi kubwa sana,dhambi ya ubaguzi. Hivi watu huwa wanajitoa fahamu kiasi hiki? Inasikitisha sana..
 
Back
Top Bottom