Ubaguzi wa kisiasa, mikoa ya Kusini ni Soweto ya Tanzania

Ubaguzi wa kisiasa, mikoa ya Kusini ni Soweto ya Tanzania

Kusini msijione mko wenyewe, hata kaskazini kuko hivyo tena wao waliambiwa live 'wasubiri'! Hii awamu ni sheedah! kanda pendwa ndio wanaangaliwa zaidi kwa sasa.
Wapi ndugu yangu nenda mkoa wa Mara uone shida. Heri huko Lindi
 
Mambo ya vyuo sio jambo la msingi ,inawezekanaje Kila sehemu serikali ijenge chuo? Vyuo vinajengwa kimkakati.

Hoja ingekuwa kama mumenyimwa maendeleo mengine sawa lakini hiyo mikoa pamoja na mambo mengine ina uhakika wa mtandao wa barabara za lami kuunganisha mkoa na mkoa

Sasa nyie mkilalama watu wa Kigoma watasemaje maana hawana barabara hata moja ya lami ya kuunganisha mkoa huo na mikoa jirani yaani toka uhuru Hadi leo hii ukienda Kigoma lazima uchezee matope
Barabara ya Njombe Songea ilijengwa na malkia wa Uingereza miaka ya 1980, malkia alitoa zawadi kwa Mwalimu Nyerere.
Hii barabara haijafanyiwa marekebisho yoyote makubwa shukrani ziende kwa yule malkia na Mwalimu Nyerere bila hivyo hata hiyo barabara isingekuepo.
 
Pamoja na jamaa kuunga mkono juhudi lakini hakuna kilichofanyika? Hivi hii nchi swala la umeme usambazaji wa umeme tu bado tatizo?🙉🙉
Hakuna kitu cha maana yani ni ubabaishaji tu.
 
Mambo ya vyuo sio jambo la msingi ,inawezekanaje Kila sehemu serikali ijenge chuo? Vyuo vinajengwa kimkakati.

Hoja ingekuwa kama mumenyimwa maendeleo mengine sawa lakini hiyo mikoa pamoja na mambo mengine ina uhakika wa mtandao wa barabara za lami kuunganisha mkoa na mkoa

Sasa nyie mkilalama watu wa Kigoma watasemaje maana hawana barabara hata moja ya lami ya kuunganisha mkoa huo na mikoa jirani yaani toka uhuru Hadi leo hii ukienda Kigoma lazima uchezee matope
Wote hao ni wateja wazuri wa CCM
 
Wewe unaongelea Tanga kata Ruvuma, Huko ni maporini kama mapori mengine ya Tanzania

Je, Lizaboni, Majengo, Mahenge, Makambi hakuna umeme?

Kila nchi ina vijiji hata Marekani kuna vijiji havina umeme na lami wanatumia Solar power

Ruvuma hasa hapo Songea pameendelea sana huwezi linganisha na Singida, Dodoma au Manyara

Wewe hujatembea nchi hii, Songea kuna maji ya kutosha, Huduma za afya bora na umeme wa kutosha kwa sasa, kuna kila aina ya vyakula hapo ili uwe na afya bora

Nenda Dodoma ukaone maji ni shida hakuna mfano, Kila kitu kimepelekwa Dodoma lakini bado hapabebeki

Huko kata ya Tanga ni Songea vijijini taratibu Mtakuja kupata huduma


Hata Dar es Salaam kuna mitaa kama Buguruni, Mwananyamala, Sinza na mingine mingi ni hovyo huwezi kuishi mtu smart

Ni shida kila kona hapo Dsm maji ya shida kwenye madumu, uchafu kila kona mpaka mlangoni

Songea na Mtwara ni miji imepangwa

Mtwara mitaa kama Ligula, Raha Leo au Shangani pamepangwa kuliko mkoa wa mbeya

Mbeya mitaa kama kalobe, Iwambi, Nzovwe kufika gari nyumbani kwako tu ni shida

Hiyo ni mifano kidogo tu

mkoa wa Mbeya ni hovyo yaani slam huwezi linganisha na Mtwara au Ruvuma
Wewe umenena sababu mtoa maada nadhani haijui songea vzr.Namshauri awe anatembea mikoani ili ajiridhishe kabla ya kutoa uzi wake.songea mzunguko wa pesa ni mkubwa ni wazalishaji wakubwa wa mazao ya chakula na biashara,kuna machimbo mengi ya madini.sekta ya afya iko vzr,mbali na serikali wakatoliki wabenediktini wamewekeza Sana,peramiho,litembo,Lituhi mission nk.huduma za maji iko vzr.Mjini songea huhitaji kuchimba vyoo vya shimo.mifumo ya maji Safi na taka yameunganishwa.Mabwawa makubwa yamejengwa kiblang'oma na sijajua Kama hata tawi la St Augustine Kama lilifungwa ila St Joseph lkn bado kuna vyuo vingi vya Kati vingi vinavyotoa taaluma mbalimbali mikoani ruvuma,Lizaboni umeme ni muda wote.Sijajua mtoa maada Kama ana ufahamu mkubwa kutoka mikoa hiyo
 
Makosa makubwa ya Watu wa hiyo ( hii ) Mikoa tajwa ni....

1. Kuendekeza Majungu
2. Kupenda Ushirikina
3. Ngono kutawala sana Akili zao
4. Uvivu uliokomaa
5. Kupenda Lawama na Visasi

Na katika Kukuthibitishia hili hata Ndugu zao akina Hayati Mkapa na Premier Majaliwa wamefanya na wanafanya makubwa bado Wanawadharau.
Huo uliouandika Hapo ni ujinga mtupu na hiyo ni akili mgando.Kama wangeendekeza ngono basi karibu wote wangekuwa HIV positive.wangoni wako kila sekta nchi hii na wameshika nyazifa kubwa na Kama wangeendekeza ngono hata shule wangekuwa nyuma basi.Kwa nn ruvuma ni among the big five?
 
Barabara ya Njombe Songea ilijengwa na malkia wa Uingereza miaka ya 1980, malkia alitoa zawadi kwa Mwalimu Nyerere.
Hii barabara haijafanyiwa marekebisho yoyote makubwa shukrani ziende kwa yule malkia na Mwalimu Nyerere bila hivyo hata hiyo barabara isingekuepo.
Nimeshakwambia huko Kigoma hata hizo za msaada hakuna,Hadi leo hii tunaongea ukitaka kufika Kigoma na Katavi lazima ule tope
 
Wewe umenena sababu mtoa maada nadhani haijui songea vzr.Namshauri awe anatembea mikoani ili ajiridhishe kabla ya kutoa uzi wake.songea mzunguko wa pesa ni mkubwa ni wazalishaji wakubwa wa mazao ya chakula na biashara,kuna machimbo mengi ya madini.sekta ya afya iko vzr,mbali na serikali wakatoliki wabenediktini wamewekeza Sana,peramiho,litembo,Lituhi mission nk.huduma za maji iko vzr.Mjini songea huhitaji kuchimba vyoo vya shimo.mifumo ya maji Safi na taka yameunganishwa.Mabwawa makubwa yamejengwa kiblang'oma na sijajua Kama hata tawi la St Augustine Kama lilifungwa ila St Joseph lkn bado kuna vyuo vingi vya Kati vingi vinavyotoa taaluma mbalimbali mikoani ruvuma,Lizaboni umeme ni muda wote.Sijajua mtoa maada Kama ana ufahamu mkubwa kutoka mikoa hiyo
Hivyo vyuo vyote St. Joseph na St. Augustine vimefungwa, mzunguko wa pesa ni mdogo sana lakini vyuo hivyo vilikua vinasaidia kuchochea mzunguko wa pesa.

Wanategemea uzalishaji kwa kilimo lakini soko lisilo la uhakika ni tatizo kama tu ilivokua korosho ya Mtwara. Au matatizo ya wakulima katika taifa la Tanzania yanafahamika.

Mgodi wa makaa ya mawe ulikua unafanya kazi kule Liyombo Ntunduaro umefungwa.

Umeme umewekwa kata ya Tanga lakini mtaa wa Mitawa wameruka, kwanini?
 
Nimeshakwambia huko Kigoma hata hizo za msaada hakuna,Hadi leo hii tunaongea ukitaka kufika Kigoma na Katavi lazima ule tope
Hiyo hailalishi uduni wa maendeleo kwa mikoa ya kusini. Kwa sababu Kigoma au sehem nyingine yoyote Tanzania hakuna kitu fulani basi ni sawa kusini kupuuzwa na kubaguliwa.

Mikoa ya kusini hata mgombea wa chama tawala hakwenda huko kipindi cha kampeni unajua sababu ya kutokwenda huko?
 
Hata wanao ishi huko wametokea South Africa , so hakuna namna zaidi ya kuendelea kuwatenga wamekimbia Cape town , Wanaenda Songea , ujinga wa kiwango cha nzege

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huko hata hakwenda alimtuma waziri
Yah, jamaa hakwenda sasa watu wa kusini wanasema ni ubaguzi na dharau kubwa. Wanaona wametengwa na kupuuzwa hata kwenye maendeleo.

Hivi unaweza kuelewa ndani ya manispaa ya Songea umeme wameweka kata nzima ya Tanga lakini kwa mtaa uliokua umetoa diwani wa upinzani mwaka 2015 wameruka kueka umeme, hapo kata ya Tanga ni ndani ya manispaa na sasa iko stand kubwa/kuu ya mkoa mzima!
 
Yah, jamaa hakwenda sasa watu wa kusini wanasema ni ubaguzi na dharau kubwa. Wanaona wametengwa na kupuuzwa hata kwenye maendeleo.

Hivi unaweza kuelewa ndani ya manispaa ya Songea umeme wameweka kata nzima ya Tanga lakini kwa mtaa uliokua umetoa diwani wa upinzani mwaka 2015 wameruka kueka umeme, hapo kata ya Tanga ni ndani ya manispaa na sasa iko stand kubwa/kuu ya mkoa mzima!
Wananchi walisahau nguvu zao wamekubali kupokoywa mpini sasa ngoja wanyooshewe makali labda wataamka usingizini.
 
Wananchi walisahau nguvu zao wamekubali kupokoywa mpini sasa ngoja wanyooshewe makali labda wataamka usingizini.
Watanzania wengi hawajui hata elimu ya uraia, haki za msingi za raia etc. Unafikiri hawa watu lini watamka usingizini
 
Kuna mabadiliko makubwa -ve yametokea baada ya kuvifunga Vyuo vikuu 2 na matawi yake vilivyokuwepo (st. Joseph ICT na SAUTI& . Mji umepoa sana. Uchumi hauchangamki kama ilivyokuwa 2009-2015. Ongezeko la VIJANA barobaro na mademu wakali town kwishney. Nyumba za Kupanga bei imeporomoka HD 10,000 kutoka 25,000-50,000 those days! Simu,subwufer, sio Biashara tena. Ndio hivyo kwa uchache. Wakavizia uchaguzi waserikali za mitaa waonyeshe hasira zao wakapigwa asubuhi tu SAA 06.00am. Chama pendwa kikapita bila kupigwa Mkoa mzima. Uchaguzi mkuu sijui lkn ndio hivyo, hakuna namna. Maisha lazima yaendeleee hata kama una hasira. Ila kikubwa Serikali ifikirie kurejesha walau Chuo Kikuu kamoja. Hata kwa huruma tu. Mwenyeji Mungu wa Abrahamu na Yakobo atawabariki sana.
Mleta mada hebu tuambie:-
= Kutokuwepo kwa Chuo Kikuu kuna vijana wamekosa Elimu ya Chuo Kikuu? na iwapo hoja yako ni muhimu hebu tuambie mikoa ya magharibi (kigoma, tabora na katavi) kuna Chuo Kikuu?
 
Hapa tatizo sio kujenga. Vyuo vilikuwepo, wanafunzi wamegrsduate Mara kadhaaa na wanaitumikia Serikali hiihiii amvayo awamu ya tano 2016 wakaja na Sera ya Uhakiki wa vyuo na matokeo yake vyote vikafutwa. Sijui hawa wakubwa wzlioshiriki kufuta akiwemo Waziri wa Elimu wanajisiaje kwa kweli. Binafsi nimesikitishwa HD leo hii. Hayakuaa maamuzi sahihi hata kidogo. Juzi zimesoma tena mahali Walimu kutestiwa, tunarudi kulekuleeee vyeti feki.
Mambo ya vyuo sio jambo la msingi ,inawezekanaje Kila sehemu serikali ijenge chuo? Vyuo vinajengwa kimkakati.

Hoja ingekuwa kama mumenyimwa maendeleo mengine sawa lakini hiyo mikoa pamoja na mambo mengine ina uhakika wa mtandao wa barabara za lami kuunganisha mkoa na mkoa

Sasa nyie mkilalama watu wa Kigoma watasemaje maana hawana barabara hata moja ya lami ya kuunganisha mkoa huo na mikoa jirani yaani toka uhuru Hadi leo hii ukienda Kigoma lazima uchezee matope
 
Kigoma utafkri siyo sehemu ya Tanzania angalia mkoa ulivyo na aridhi nzuri mito mingi ya kutosha! Cheki barabara yakusafirishia mazao ya wakulima na pia umeme bado ni ndoto kwa wanakigoma
 
Siku hizi hata usipokuwa mteja, utakubalishwa tu. Yaani kupita bila kupingwa! Wengine wote hukosea kujaza lkn wale wa CCM ndio wasomi wenyewe with flaying colours! Yaani hakuna namna nyingine. Mi5 tena! Au sio ndugu Zangu! Hahahaaaaa
Wote hao ni wateja wazuri wa CCM
 
Back
Top Bottom