Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania watoa tahadhari ya uwepo wa tishio la shambulio la kigaidi

Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania watoa tahadhari ya uwepo wa tishio la shambulio la kigaidi

Sasa Chadema mkiambiwa msikusanye watu mpaka tishio liishe, mtasema mnaonewa, aliyesema ndio moja ya watu wenu. Na mtu wenu akiambiwa asifanye mkutano wa hadhara analia, akiachiwa akadhurika, anaililia serikaliView attachment 2495531
Mkuu umepangiwa wilaya gani katika mkeka wa mama wa leo? Au umebakishwa katika nafasi yako hii hii ya posho 7?
 
Ubalozi wa Marekani unasema tuwe makini na mashambulio ya kigaidi, hayo makundi ya kigaidi yanaweza kushambulia kwa kutoa onyo dogo au wasitoe kabisa, wanadai kuna dalili Dsm au maeneo mengine ya Tanzania yakashambuliwa na magaidi, maeneo hayo yanayoweza kushambuliwa ni kama hoteli, balozi, migahawa na masoko.
OK asante
 
Habari ya tahadhari juu ya panyaroad na wageni ndani ya nchi, Ila hofu kubwa ni wimbi la kampeni za kisiasa huenda wakaibuka wahalifu na kusistiza kuwa makini kwenye hayo maeneo...
 
Sasa Chadema mkiambiwa msikusanye watu mpaka tishio liishe, mtasema mnaonewa, aliyesema ndio moja ya watu wenu. Na mtu wenu akiambiwa asifanye mkutano wa hadhara analia, akiachiwa akadhurika, anaililia serikaliView attachment 2495531
Ndugu chinyeeembe,kwani uummoja ya wanufaika wa yale mazuri haramu,,🤔
 
Basi alert ni ya sehemu zinazopendwa kutembelewa na foreigners,mikutano ya chadema huwa na foreigners ?
Gaidi hachagui, ubalozi umefanya sampling ya maeneo machache
 
Hivi kama hawa jamaa huwa wanajua kuna dalili ya ugaidi, kwanini huwa hawatuambii hivyo vitisho vitatokea wapi ili vikamalizwe huko huko, kuliko wanavyofanya kutoa tahadhari pekee na kutuacha njia panda?
Baadhi ya info wanazopata hazipo directly kwamba ni sehemu gani,nadhani huwa wanafikia hivi kwa kusoma matendo ya watu wanaowafuatilia au informer wao walio huko kwa maadui huwapa hints na hao informer hawapewi info zote huko
 
Mungu atunusuru tu 🙏

Naimani vyombo vya ulinzi na usalama vitakuwa vimechukua taarifa hii kwa uzito wake
 
Hivi kama hawa jamaa huwa wanajua kuna dalili ya ugaidi, kwanini huwa hawatuambii hivyo vitisho vitatokea wapi ili vikamalizwe huko huko, kuliko wanavyofanya kutoa tahadhari pekee na kutuacha njia panda?
Mbona hiki unachokiuliza kimeelezwa hapo!
 
Ubalozi wa Marekani Nchini Tanzania umeonya juu ya kuwepo viashiria vya Shambulio la Kigaidi katika maeneo mbalimbali yanayotembelewa zaidi na Raia wa Nchi za Magharibi ikiwemo Marekani

Maeneo yaliyotajwa kuwa kwenye mipango ya kushambuliwa na Vikundi vya Ugaidi ni pamoja na Hoteli, Balozi mbalimbali, Maduka makubwa na Masoko, Vituo vya Polisi na Misikiti.

IMG_20230125_201956_259.jpg
 
Back
Top Bottom