Ubinafsishwaji Bandari tatizo la Watanzania ni lugha ya Kingereza, Mkataba upo sawa

2. Vyama vya serikali vinakubaliana kwamba utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya mradi na DPW unategemea kuhitimishwa kwa makubaliano thabiti ya mradi, haki za ardhi, na HGAs kwa kila mradi husika.
 
Mkuu kama unao huo mkataba naomba niusome tafadhali🙏🙏
 
Tuambie na unapovunjwa fidia yake inakuwaje?
 
Una utindio wa ubongo wewe.
Nani kakwambia watanzania hawajelewa mkataba.

Hebu tutafsirie wewe mwingireza tuone labda utakuja na uelewa tofauti na walivyoelewa watz wengine

Mbunge wako mdee aliushika mkataba ila matatizo akawa anayatoa kichwani.anaambiwa aonyeshe ye yuko na hisia tuh.
 
Wewe umetafsiri vip mkuu?
Alafu lugha na elimu wapi na wapi?
 
wewe unaejua kingereza ungetoka na kuuelimisha umma nadhani ungekuwa umefanya jambo la msingi sana

sasa umeishia kulalama hapa kwamba mamaako alitukanwa ungekuja kumtetea kwa hoja nadhani ungeeleweka sana

tofauti na hapo mtoa post hatukutofautishi na chawa wengine 😎
 
Mwenye tatizo kubwa kwenye hicho kiingereza, lazima.mojawapo ni wewe.

Mkataba unazungumzia kuwa termination ya mkataba inaweza kufanywa kwa makubaliano ya pande zote mbili. Umejiuliza, kama upande mmoja ukitaka kufanya termination, upande mwingine hautaki, kutatokea nini?

Na halafu unatakiwa kutofautisha kati ya contract termination na life of the contract. Watu hawaongelei termination, wanauliza life of the contract. Mkataba ni lazima uwe muda wake wa maisha, mambobyanayoweza kusababisha kukoma mkataba kabla ya muda wa mkataba kwisha.

Kwenye huo mkataba wamesema life ya the contract ni muda gani?
 
Usijiona unajua sana kumbe wewe ni kisoda kwenye pipa.

Mimi binafsi nimeshiriki kuandaa mikataba zaidi ya 30 ya multinational comapanies, ikihusisha makampuni na serijali, nje ya Tanzania. Mimi sikusomea sheria, lakini kwa namna nilivyofanya kazi kwenye haya masuala ya mikataba, mara nyingi nimekuwa na uelewa mkubwa maradufu ya wanasheria wengi nadharia. Na mara nyingi tulivyokuwa kwenye vikao vya mikataba, mara nyingi wengi walidhania nimesomea sheria, wengine hata nilipowaambia kuwa hiyo siyo fani yangu, hawakuamini. Ufahamu kuwa practice ndiyo iliyotengeneza theory ambayo wanaenda kufundishwa wale ambao hawajawahi ku-practice.

Hiyo unayosema ni framework, ukweli ndiyo mother contract. Mikataba mingine yote midogo midogo ni lazima iwe ndani ya mkataba mkuu.

Mkataba huu ndio unatoa mwongozo wa mikataba midogo itakayofuata. Hivyo mkataba mwongozo unatakiwa kuwa detailed and elaborative well eneough ili kuhakikisha hakutokei madudu kwenye mikataba midogo.

Yawezekana wewe ni mwanasheria nadharia. Watafute practical lawyers wakueleweshe.
 
Nakubaliana nawe kuwa wenye matatuzo ya uelewa mpo wengi sana.

Maana kama u ashindwa kuelewa umujimu wa mkataba mkuu, unasema eti hiyo ni framework tu! Kazi ya framework ni nini?

Kipi ni kikubwa kati ya hiyo unayoiita framework na mikataba midogo itakayosainiwa baadaye?
 
Huyu ni mwanasheria koko. Hajui kuwa kuna sheria inayozuia migogoro ya kiuwekezaji kuamliwa na mahakama za nje ya Tanzania. Halafu anajifanya eti ni mwanasheria.

Huenda ni hakimu wa mahakama ya mwanzo.
 
Upo sahihi kabisa. Kwa watu makini, mkataba ulistahili kuainisha ni mambo gani yatasababisha termination ya mkataba kabla ya muda wa uhai wa mkataba. Lakini mpaka sasa hakuna hata muda wa uhai wa mkataba.
 
Basi na mkataba kutohusisha bandari za Zanzibar ni tatizo letu la kielemu au kiingereza kama unavyotamani ionekane hivyo mtoa mada.
 
Unaamua kuandika chochote ulicho nacho kichwani!!

Tunataka useme kwenye mkataba na DP, uhai wa mkataba ni miaka mingapi? Mambo gani yatasababisha contract termination prior life of the contract.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…