Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Ubunge Tarime: Wagombea, Kampeni na Uchaguzi

Status
Not open for further replies.
Mtikila inaonekana kama vile hajui anachokitaka, kwa kuwaambia kuwa viongozi wa chadema ndio wamemuuwa Wangwe hakuwasaidii chochote wananchi wa Tarime labda kama hii ishu inamsaidia yeye.
 
mtikila ni mchungaji lakini ameshindwa kusoma nyakati, sasa atajifunza kusoma nyakati kwa haya yaliyotokea kwake
 
Hapana mleta habari kutupasha kwa mbwembwe kuwa Mtikila yamemkuta hayo baada ya kuhutubia kuwa Mbowe na Chadema ndio waliomuua Wangwe. Hapo by implication hao watakuwa ni mashabiki wa Chadema,,,

wrong deduction; it just shows your bias. Kwanini hukufikiria possibilities nyingine. Ungependa nijaribu kukuorodheshea some?
 
MMh uyu baba nae anamambo mengi angeshika moja pengine ndio maana kapigwa nimungu kamlani huku uchungaji huku siasa wapi na wapi.
 
Pole sana mzee wetu Mtikila, mzee wa "kulipua mabomu". Hiyo ni ajali ya bomu kumlipukia mlipuaji. Uwe mwangalifu wakati mwingine! Lakini bado mshangao upo kuwa kwa nini polisi wanaona ni sawa Mtikila kulipua mabomu kama hayo wakati huu (sijui kama yana ukweli au la), lakini angesema ni CCM ingemuua Wangwe nadhani sasa hivi angekuwa na pingu hapo kitandani alipolazwa! Nguvu zinazotumika huko Tarime ziko largely imbalanced indeed.
 
Mwakaleli,

Inabidi Mtikila ajivue hata uchungaji awe full swing politician, yuko nusu nusu kama vile anaotea upepo hivi.
 
Mwakaleli,

Inabidi Mtikila ajivue hata uchungaji awe full swing politician, yuko nusu nusu kama vile anaotea upepo hivi.

Hivi huyu jamaa yuko relevant kweli? Kuna mtu anayemsikiliza siku hizi? Na chama chake vipi? Kipo au kipo jina tu? Halafu ni mchungaji wa kanisa gani huyu Mtikila?
 
"Kweli kiingiacho mdomoni Si haramu,bali kitokacho."
-ila jamani ushujaa mwingine unachekesha kweliX2!!
 
Yule mchungaji matata anayeitwa Mtikila, hivi pundwe amepelekwa hospitali kulazwa na kushonwa nyuzi baada ya kupigwa mawe na wananchi wenye hasira. Mtikila alipata dhahama hiyo baada ya kuhutubia kuwa Mbowe na CHADEMA yake ndio waliomuua Chacha Wangwe.

.......ndiyohiyo

Every Man Shall Reap What He Sowed!
 
teh teh teh
Na EPA nayo waachiwe akina wazee wa kuzuia rushwa,polisi na mahakam,ama unasema je?? kwi kwi kwi

Hapa nataka kusema hivi mtu yeyote anayeona kumechezwa ndivyo sivyo ana haki ya kusema lolote na yule anayeona hakutendewa haki anachukua mkondo wa sheria.

Sasa kama sheria yenyewe ndio ya mkononi si balaa hili.

Kumbe siku CHADEMA watakapo chukua nchi na MBOWE tukamwita majina mengi mfano FISADI,MHUNI,kumbe tutapigwa MAWE.kazi kweli kweli

NA yule kaka wa MAREHEMU kwenye ufunguzi wa kampeni mbona yeye hawajampa kipigo ama bado wanamuwinda??

Maoni ya kipuuzi.
 
mtikila ni mchungaji lakini ameshindwa kusoma nyakati, sasa atajifunza kusoma nyakati kwa haya yaliyotokea kwake

Hakuna kitu.
kupigwa mawe si sign ya kutenda maovu ama kutojua nyakati yawezekana ni matokeo ya ukweli.

Yesu alipigwa mawe si kwa sababu hakujua nyakati .Na wayahudi waliompiga mijeledi nao maneno yao yalikua yamelala kwenye falsafa hiyohiyo kwamba Yesu ni MCHOCHEZI.
 
Mtanzania mie si mwana CCM wala CHADEMA, lakini maneno aliyoongea Mtikila na kugawa yale makaratasi yamenistua sana. Nafkiri hata wanaCCM wengi yamewastua, au mwezetu? Yale yale ya Simba Vs Yanga?

IO, hata kama ungekuwa unayo haki ya kuchukizwa na uvunjaji wa sheria au kauli za kichochezi bila kujali zinatoka wapi na zinatolewa na nani. That is an obvious principle.
 
Mtikila inaonekana kama vile hajui anachokitaka, kwa kuwaambia kuwa viongozi wa chadema ndio wamemuuwa Wangwe hakuwasaidii chochote wananchi wa Tarime labda kama hii ishu inamsaidia yeye.

Mkuu Mtikila anafaidika kutokana na fedha aliyopewa na hao mabwana zake... Amepewa contract ya kuwachafua Mengi, Mbowe na Slaa.
 
Hivi hadi Mtikila anapigwa mawe na kujeruhiwa hivyo Kamanda Tossi na wenzake walikuwa wapi? au ndiyo yale ya kufumba macho ili Mtikila akomeshwe!? Sitoshangaa akipata nafasi atawalaumu Polisi kwa kumuacha abondwe. Au anajajibu kutafuta ushujaa wa kuwa mwanasiasa siyo tu aliyeswekwa lupango mara nyingi lakini pia alipigwa na wananchi?
 
We have polisi wa kutosha mpaka kutoka zanzibar...nyamongo na tarime sio safe place...better shut ur mouth when it comes politics...umemsikia msekwa kaomba nguvu ya dola zaidi?qoute"nimetumwa na amiri jeshi mkuu kuja kuangalia hali ya amani"Msekwa.

Guest zimejaa ma CID..wengi kama vile bush yuko hapa...na hili jimbo kama halitakwenda kwa CCM this time ntawaka point zangu watu wa tarime ni mashujaa...jamani polisi ni wengi mpaka unaona kweli ukipiga kula Chadema...hawata kuona na kukupoteza kabisa...
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom