📌Kwa kawaida mfumo wa interchange kama ule huwa unaondoa msongamano sehemu ulipojengwa na kuihamishia mahala pengine jirani...
Suluhisho la foleni za kudumu ni:
1.Kuwa na interchange/overpass/umderpass karibu kila junction iliyo busy.
2. Kuwa na flyovers zenye kutembea umbali mrefu "expressways", mathalini uwe na njia isiyoingiliwa toka Kibaha hadi Posta, yenyewe inakuwa na exits na entries sehemu kadhaa tu.
3. Dar isiwe Posta au Kariakoo tu.
4. City trains/BRTs za kutosha
Jioni kuna mabasi gani Morogoro road kuelekea Mbezi?
plans haziwekewi mikakati ya muda mrefu
Barbara kubwa kama ile vituo vya daladala hakuna wanashusha na kupakia abiria njiani,bajaji zinajipanga Baruti,Korogwe foleni itakosekana?
service road hakuna gari ikiharibika tunasota wote
Kwamba haujui kabisa kwamba toka daraja lianze kufanya kazi gari zinapita free zinakwenda kujaa njia ya Kimara na Mwenge?Unaongelea Ubungo Mbezi au unaongelea flyover? Ubungo Mbezi huwa sielewi foleni ni kwa sababu gani.
Kuwa na foleni upande ule sio sababu ya kusema flyover haijapunguza foleni
Kwamba haujui kabisa kwamba toka daraja lianze kufanya kazi gari zinapita free zinakwenda kujaa njia ya Kimara na Mwenge?
Kuna watu wanajiona wana akili ila watupu sana. Mtu anategemea interchange ya ubungo ikamalize foleni mlimani city ambako foleni yake inasababishwa na junction ya mwenge.Foleni zitakuwepo sana Dar, ipeni serikali kama miaka 10 ya ziada kukamilisha ujenzi wa 8 critical intersections
Flyover ile kazi yake ilikuwa kumaliza tatizo junction ubungo na imefanikiwa. Huko kimara au mwenge kunahitaji solution ingine.(mwenge iko kwenye plan)Kwamba haujui kabisa kwamba toka daraja lianze kufanya kazi gari zinapita free zinakwenda kujaa njia ya Kimara na Mwenge?
Mbaya zaidi hawajui flyover kwa kiswahili ni daraja la juu, wao wanahisi wakiita daraja badala ya flyover basi wanajiona wanakejeli wenyeweKuna watu wanajiona wana akili ila watupu sana. Mtu anategemea interchange ya ubungo ikamalize foleni mlimani city ambako foleni yake inasababishwa na junction ya mwenge.
Suluhisho ni hizo junctions kubwa zote ziwekwe flyovers kitu ambacho kinafanyika SASA hivi.
Ila pingapinga hawa hawa wanakataa na kubeza ujenzi wa miundombinu.
Mkuu sidhani kama hili ni suala linalohitaji mtaalamu au utaalamu, la hasha tunahitaji kuwa na mipango bora na endelevu tu...Sijui tunahitaji kupata wataalamu wafanye study na kisha kutupa ushauri wa kitaalamu wa kumaliza tatizo la foleni mikoani Dar-es-Salaam?
Yeah mkuu si pia lazima kunyanyua juu, zinaweza zikawepo hizo barabara hata chini ardhini lakini zinatambulika kama expressways...Nimekuelewa sana mzee mtu nane, Dar isiwe Posta na Kariakoo tu, Trams na BRT, namba mbili yaweza kuwa kubwa kuliko uchumi wetu though.
Lakini mbona kama barabara zetu bado tunazijenga kurudia makosa ya zamani, 8-lanes ya Dar-Kibaha, ina muingiliano sana na barabara za kando...Na huo ndio mpango mkakati wa serikali, tuwe wavumilivu
Dar Es Salaam ni kama nguo iliyochakaa unajaribu kuishona kila inapochanika badala ya kuitupa. Kuna haja ya kuhamisha juhudi maeneo mengine pembezoni mwa Dar.Hilo ndio swali langu kwani ninachokiona ni kupunguza kwa foleni katika eneo la mataa pale Ubungo ila mita chache kutoka hapo unakuta na foleni.
Kwa mfano, ukitoka Ubungo Interchange mida ya jioni hasa kuanzia saa moja kasoro usiku mpaka saa mbili, ukifika maeneo ya Mlimani City basi ni mwendo wa foleni mpaka Mwenge. Na hapo bado foleni ya kuelekea unakoenda kutoka Mwenge mfano kwenda Bunju.
Swali la msingi ni je, madaraja haya pekee ndio yataweza kumaliza hili tatizo?
Au tujiulize, kipi kinapaswa kuanza kati ya kujenga madaraja ya mabilioni na kupanua barabara zikiwemo highway na barabara zingine zinazounganisha maeneo mbalimbali ya Jiji?
Mfano, billion zaidi ya 200 zinazojenga daraja linalopita baharini zingetumika kuboresha/kujenga/ kupanua barabara zingine zinazounganisha maeneo mbalimbali ya jiji zisingekuwa na msaada zaidi katika kupunguza tatizo la foleni katika jiji hili?
Je, umefika wakati tuweke restrictions za magari binafsi kuingia katika ya Jiji kwa kuweka tozo maalumu za kuingia katikati ya Jiji?
Na bila kuboresha public transport, itakuwa sahihi kuweka restrictions kwa magari binafsi kuingia katika ya Jiji?
Kuna watu humu mna majibu ya kusomi sana. Big up.Kwa kawaida mfumo wa interchange kama ule huwa unaondoa msongamano sehemu ulipojengwa na kuihamishia mahala pengine jirani...
Suluhisho la foleni za kudumu ni:
1.Kuwa na interchange/overpass/underpass karibu kila junction iliyo busy.
2. Kuwa na flyovers zenye kutembea umbali mrefu "expressways", mathalini uwe na njia isiyoingiliwa toka Kibaha hadi Posta, yenyewe inakuwa na exits na entries sehemu kadhaa tu.
3. Dar isiwe Posta au Kariakoo tu.
4. City trains/BRTs za kutosha
Hivi hilo jengo la Tanesco, kila nikija Dar naliona bado tu lipo, waliahirisha kulivunja ama linasubiri subiri kwanza?Alafu ni la gharama kubwa mbali na hasara ya kuvunja jengo la TANESCO!!
Tumejaza mavyeti kwenye makabati lakini vichwani kweupe na haya ndio matokeo yake, na kibaya wanasiasa ndio wanaoamua karibu kila kitu!Mkuu sidhani kama hili ni suala linalohitaji mtaalamu au utaalamu, la hasha tunahitaji kuwa na mipango bora na endelevu tu...
Jambo la miaka 10, 20 au 30 ijayo linapaswa kupangwa leo, we need to be more proactive than reactive...
Mathalani, chukulia mfano namna muingiliano wa barabara kuu na barabara za pembeni ulivyojengwa Mbezi Mwisho...
Kwa nchi za wenzetu huwezi ukapata barabara iendayo mikoani/interstates zile zinakuwa na muingiliano na barabara za ndani ya mji...
Pale Mbezi Mwisho, sijui Temboni, Kwa Msuguri etc, kulipaswa kusiwe kabisa na ama T-junctions au Cross-junctions maana hizi ndio zilizozalisha foleni kila tunapojua sasa kuwa pana foleni...
Sasa sisi barabara ya mkoani kwenda Moro hata mbuzi, bata, ng'ombe wanaweza jikatizia tu
Ni kweli, wataboresha nadhani kwa siku zijazoLakini mbona kama barabara zetu bado tunazijenga kurudia makosa ya zamani, 8-lanes ya Dar-Kibaha, ina muingiliano sana na barabara za kando...
Tuchukulie tu mfano pale Kimara Stop Over, gari inayotoka upande wa kushoto kwenda kulia, ina umuhimu gani wa kukatiza 8-lanes?
Kwa nini kusingekuwa ama na over au under pass?