Ubungo waandamana ofisini kwa DC kudai Maji

Ubungo waandamana ofisini kwa DC kudai Maji

Safi sana....sehem zote tukionesha hali kama hii viongozi watashika adabu ....shubamitt
 
endeleeni kunuka vikwapa uko Dar , uku Mvuti maji tunaogeshea nguruwe
 
Sasa wameandamana wameyapata?

Tupunguze dharau. Yani watu wakae mwezi mzima bila maji, wakiandamana wewe waache hujui wamevumilia kiasi gani. Kama umeshiba usimcheke mwenye njaa.
 
It is about time.
dalecarnegiequote-___2970791867402183999___-.jpg
 
Kwani kuandamana ndio kunaleta maji?
Mkuu kuandama ni moja ya njia za kuwasilisha kero kwa mtu ambaye mnaona anawajibu wa kutatua kero zenu. Kwa suala maji wengi tunajua Serikali ndiyo inatuletea Maji kupitia taasisi zake kama dawaso kwa watu wa DSM. Ni ngumu sana kwa mtu wa DSM kujitafutia Maji aidha achimbe kisima kwa wenye Uwezo. Au aite gari za Maji nao pia kwa wenye Uwezo. Kwa mazingira ya DSM hizo ndiyo njia pekee za kupata Maji kama Dawasco hawajasupply Maji, vyanzo Vya Maji viko mbali hawawezi kwenda na ndoo mto ruvu. Nawaonea huruma.
 
Wakazi wa eneo la Luguruni Manispaa ya Ubungo jijini Dar es Salaam wameandamana hadi ofisi ya mkuu wa wilaya ya Ubungo (DC), Kheri James kudai huduma ya maji waliyoikosa kwa miezi mitatu sasa huku wakiletewa bili.

Wakazi hao wakiwa wamebeba ndoo zao zikiwa tupu walikuwa wakiimba nyimbo mbalimbali zilizokuwa zikiashiria kuwa wanahitaji maji huku wanawake wakiziweka kichwani na kumtaka mkuu wa wilaya hiyo kuwatua ndoo.

George Ngao ambaye ni mmoja wa wananchi katika eneo hilo amesema licha ya mgao wa maji uliopo lakini wao hawajapata maji kwa miezi mitatu sasa.

“Mbaya zaidi tunalipishwa bili za maji, pia maji haya tunayoyataka yanapita katika eneo letu, mitaa mingine yanakokwenda wanapata maji ila sisi hatuna.”

“Tumejitahidi kutafuta suluhisho bila mafanikio mwisho tumeamua kuja kwa mkuu wa wilaya atupe suluhu ya suala hili,” amesema

Kilio cha wakazi hawa kinakuja ikiwa ni baada ya kuwapo kwa mgao wa maji ndani ya jiji la Dar es Salaam uliotokana na kupungua kwa uzalishaji maji katika mto Ruvu ambao ndiyo chanzo kikuu cha maji kinachotegewa.

Scholastica Mwenda ambaye pia ni mkazi wa eneo hilo amesema kwa miezi hiyo mitatu walilazimika kununua dumu 1 kwa Sh1000 kwa maji ya bomba huku maji ya chumvi kwa Sh500.

“Kwa walioweza kutafuta kwa kichwa kwenye visima walifanya hivyo, ilifika hatua bajeti zetu za chakula zinachukuliwa maji, hata watoto kujisaidia unawapangia kwa sababu maji hakuna, vyoo vipo ndani nyumba itanuka,” amesema

Anasema athari yake ni magonjwa ya mlipuko kama kipindupindu huku akieleza hata maji ya kununua wanayotumia wakati mwingine hawajui vyanzo vyake na hata usalama wa vyombo vinavyotumika katika kubeba.

Hata hivyo, bado anasisitiza kuwa hakuna mwananchi wa kawaida anayeweza kununua maji ya Sh10,000 kwa siku kwa ajili ya matumizi ya nyumbani.

“Ukitaka kufua na kufanya usafi wa nyumba maji mengi yanatumika, kuoga mara moja kwa kutwa na makopo ya kuhesabu, sasa hili ni mimi ambaye nina familia ya watu watatu lakini jirani yangu ana familia ya watu 12 unaweza kuona wanaishije humo ndani.

Akizungumzia suala hilo mkuu wa wilaya ya Ubungo, Kheri James aliwahidi wananchi hao kuwa watapata huduma ya maji leo.

“Kuanzia 7:45 mchana kazi yangu itakuwa ni kupita na kuangalia maji yanatoka wapi na wapi hakuna maji, tuheshimu ratiba ya mgao wa maji tuliyoitoa, mnatekelezaje, Wananchi tumeshawaandaa kuwa tatizo lipo na hicho kidogo tutakigawana kwa mgao,” James.

Amesema inashangaza kukuta baadhi ya maeneo barabarani maji yanamwagika lakini Wananchi hawapati maji.

MWANANCHI
Siyo Mji Mzima sema Manispaa ya Kinondoni na Ubungo Ila kule Kigamboni,Temeke hata Ilala Maji yapo Watu walijitengenezea Mfumo binafsi usiokuwa unategemea serikali kwa maana Watu walichimba visima na Wakiobahatika kupata Maji yasiyo ya Chumvi walisambaza Kama wafanyavyo Dawasa .Hivyo huwezi sikia kero ya Maji Ilala Temeke Wala Kigamboni na Kama ikitokea ni Mara chache Sana . Ebu fikiri Watu wa Mbagala walivyo Wengi vile lakini Wapo kimya au kule Gezaulole au kule Gongo la mboto. Kwa ufupi Manispaa ya Kinondoni na Ubungo ndizo hasa waathirika zaidi hivyo Ondoa neno Mji Mzima..Halafu kumbukeni Ubungo siyo Jiji la Dar es Salaam
 
Wamekosa kazi, unaandamana kuenda kwa DC ambae hatokupa maji, huo Ni utoto ungetumia mda huo kutafuta maji kwingine.
Hapo Kwa DC hatua chache ndy hapo hapo ofisi za DAWASA LUGURUNI zilipo.

Wanainchi wameamua kwenda Kwa DC baada ya kuona hakuna mtetezi.


Walishakwenda DAWASA ofisini na kuonana na engineers,pamoja na viongozi kadhaa bila mafanikio.

Kinachofanyika ni Bomba la kibamba Kwa Mangi (DAWASA)
Linauza maji kwenye magari ambayo huuzia wanainchi Kwa sh 20000 Kwa 1000 litres.

Ili biashara Yao ya maji ifanyike vzr ni lazima wanainchi wafungiwe maji wasiyapate .
Na watu wa magari pamoja na DAWASA kupiga pesa,

Hili Bomba hata hayati MAGUFULI RIP alilipigia sana kelele,
Na lilikoma Kwa kipindi chote yupo madarakani.

Kabla ya kucomment jambo lolote kwanza uwe na ufahamu wa kinachoendelea.
 
Sasa hizo mita nani husoma?

Au hizo mita hupitisha nini hadi namba zibadilike?

Wakala wa Vipimo atueleze
Wanakadiria halafu wanakwambiya ni deni la zamani bill ilichelewa kusomwa.
 
Kwani kuandamana ndio kunaleta maji?
Kelele nyingi humfanya hata muhalifu kuogopa na kukimbia.

Bila maandamano tanzania nzima ingejuwa kama wakazi wa LUGURUNI KIBAMBA hawapewi maji Kwa miezi mitatu Sasa?

Hizi kelele nilishazipiga sana humu,
Lakini hazikupata ufumbuzi.

Go wanainchi go go go.
 
Ukitaka kujuwa DAWASA walikuwa wanafanya makusudi ,

Leo hii baada ya wanainchi kwenda Kwa mkuu wa wilaya,
Wameamua kuyafungulia maji usiku huu LUGURUNI KIBAMBA.,,

Kama maji walikuwa hawana haya waliyofungulia wametoa wapi?

Kweli kelele zinasidia sn.

RIP MAGUFULI.

Watanzania tumezoea kusukumwa ,,
 
Back
Top Bottom