Na serikali iwache haraka hii tabia yakusolve matatizo kwenye makaratasi huku site watu wakipigikaWabongo stop this culture of complaining ,si mliambiwa maji yapo 94% na mkashangilia?
Shenzi sana!View attachment 2416354
Kwani kuandamana ndio kunaleta maji?Wape ushauri waende wakamulalamikie nani kuhusu tatizo lao la Maji.
maji yapo wanafanya janja janja kupiga ela labda kama nawe mdau wao [emoji23]Wamekosa kazi, unaandamana kuenda kwa DC ambae hatokupa maji, huo Ni utoto ungetumia mda huo kutafuta maji kwingine.
Me nipo ngerengere chief cjarudi hukoDah nisaidie nimetume boda hapo aniletee dumu hata 6 mkuu. Yani Leo sijaoga kabisa hata kutoka nimeshidwa. Napigia wa magari siwaoni
Poa mwayaMe nipo ngerengere chief cjarudi huko
Kwani kuandamana ndio kunaleta maji?
Sasa wameandamana wameyapata?
Mkuu kuandama ni moja ya njia za kuwasilisha kero kwa mtu ambaye mnaona anawajibu wa kutatua kero zenu. Kwa suala maji wengi tunajua Serikali ndiyo inatuletea Maji kupitia taasisi zake kama dawaso kwa watu wa DSM. Ni ngumu sana kwa mtu wa DSM kujitafutia Maji aidha achimbe kisima kwa wenye Uwezo. Au aite gari za Maji nao pia kwa wenye Uwezo. Kwa mazingira ya DSM hizo ndiyo njia pekee za kupata Maji kama Dawasco hawajasupply Maji, vyanzo Vya Maji viko mbali hawawezi kwenda na ndoo mto ruvu. Nawaonea huruma.Kwani kuandamana ndio kunaleta maji?
Siyo Mji Mzima sema Manispaa ya Kinondoni na Ubungo Ila kule Kigamboni,Temeke hata Ilala Maji yapo Watu walijitengenezea Mfumo binafsi usiokuwa unategemea serikali kwa maana Watu walichimba visima na Wakiobahatika kupata Maji yasiyo ya Chumvi walisambaza Kama wafanyavyo Dawasa .Hivyo huwezi sikia kero ya Maji Ilala Temeke Wala Kigamboni na Kama ikitokea ni Mara chache Sana . Ebu fikiri Watu wa Mbagala walivyo Wengi vile lakini Wapo kimya au kule Gezaulole au kule Gongo la mboto. Kwa ufupi Manispaa ya Kinondoni na Ubungo ndizo hasa waathirika zaidi hivyo Ondoa neno Mji Mzima..Halafu kumbukeni Ubungo siyo Jiji la Dar es SalaamWakazi wa eneo la Luguruni Manispaa ya Ubungo jijini Dar es Salaam wameandamana hadi ofisi ya mkuu wa wilaya ya Ubungo (DC), Kheri James kudai huduma ya maji waliyoikosa kwa miezi mitatu sasa huku wakiletewa bili.
Wakazi hao wakiwa wamebeba ndoo zao zikiwa tupu walikuwa wakiimba nyimbo mbalimbali zilizokuwa zikiashiria kuwa wanahitaji maji huku wanawake wakiziweka kichwani na kumtaka mkuu wa wilaya hiyo kuwatua ndoo.
George Ngao ambaye ni mmoja wa wananchi katika eneo hilo amesema licha ya mgao wa maji uliopo lakini wao hawajapata maji kwa miezi mitatu sasa.
“Mbaya zaidi tunalipishwa bili za maji, pia maji haya tunayoyataka yanapita katika eneo letu, mitaa mingine yanakokwenda wanapata maji ila sisi hatuna.”
“Tumejitahidi kutafuta suluhisho bila mafanikio mwisho tumeamua kuja kwa mkuu wa wilaya atupe suluhu ya suala hili,” amesema
Kilio cha wakazi hawa kinakuja ikiwa ni baada ya kuwapo kwa mgao wa maji ndani ya jiji la Dar es Salaam uliotokana na kupungua kwa uzalishaji maji katika mto Ruvu ambao ndiyo chanzo kikuu cha maji kinachotegewa.
Scholastica Mwenda ambaye pia ni mkazi wa eneo hilo amesema kwa miezi hiyo mitatu walilazimika kununua dumu 1 kwa Sh1000 kwa maji ya bomba huku maji ya chumvi kwa Sh500.
“Kwa walioweza kutafuta kwa kichwa kwenye visima walifanya hivyo, ilifika hatua bajeti zetu za chakula zinachukuliwa maji, hata watoto kujisaidia unawapangia kwa sababu maji hakuna, vyoo vipo ndani nyumba itanuka,” amesema
Anasema athari yake ni magonjwa ya mlipuko kama kipindupindu huku akieleza hata maji ya kununua wanayotumia wakati mwingine hawajui vyanzo vyake na hata usalama wa vyombo vinavyotumika katika kubeba.
Hata hivyo, bado anasisitiza kuwa hakuna mwananchi wa kawaida anayeweza kununua maji ya Sh10,000 kwa siku kwa ajili ya matumizi ya nyumbani.
“Ukitaka kufua na kufanya usafi wa nyumba maji mengi yanatumika, kuoga mara moja kwa kutwa na makopo ya kuhesabu, sasa hili ni mimi ambaye nina familia ya watu watatu lakini jirani yangu ana familia ya watu 12 unaweza kuona wanaishije humo ndani.
Akizungumzia suala hilo mkuu wa wilaya ya Ubungo, Kheri James aliwahidi wananchi hao kuwa watapata huduma ya maji leo.
“Kuanzia 7:45 mchana kazi yangu itakuwa ni kupita na kuangalia maji yanatoka wapi na wapi hakuna maji, tuheshimu ratiba ya mgao wa maji tuliyoitoa, mnatekelezaje, Wananchi tumeshawaandaa kuwa tatizo lipo na hicho kidogo tutakigawana kwa mgao,” James.
Amesema inashangaza kukuta baadhi ya maeneo barabarani maji yanamwagika lakini Wananchi hawapati maji.
MWANANCHI
Hapo Kwa DC hatua chache ndy hapo hapo ofisi za DAWASA LUGURUNI zilipo.Wamekosa kazi, unaandamana kuenda kwa DC ambae hatokupa maji, huo Ni utoto ungetumia mda huo kutafuta maji kwingine.
Wanakadiria halafu wanakwambiya ni deni la zamani bill ilichelewa kusomwa.Sasa hizo mita nani husoma?
Au hizo mita hupitisha nini hadi namba zibadilike?
Wakala wa Vipimo atueleze
Kelele nyingi humfanya hata muhalifu kuogopa na kukimbia.Kwani kuandamana ndio kunaleta maji?
Nahangaika na maji kumbe nina ndugu yangu wa jf ana maji sio haki kabisa hiiMtume hapa kifuru-mwanzo huyo boda nimpe maji akuletee mkuu
Kwani wewe hutunzi risiti zao za nyuma?Wanakadiria halafu wanakwambiya ni deni la zamani bill ilichelewa kusomwa.