Uchaguzi 2020 Ubunifu wa Godbless Lema na Halima Mdee utumike nchi nzima

Uchaguzi 2020 Ubunifu wa Godbless Lema na Halima Mdee utumike nchi nzima

Omusolopogasi

JF-Expert Member
Joined
Aug 31, 2017
Posts
7,101
Reaction score
18,051
Waja JF,

Kwenye majukwaa ya kampeni za uchaguzi, Godless Lema na Halima Mdee wamekuwa wakitumia clips zenye maneno ya wapinzani wao kuonyesha jinsi walivyo vigeugeu katika maisha yao, wenye kutoa ahadi za uongo, nk. Leo wanasema hili na kesho wanasema lile na kwa hiyo wasiaminiwe na wananchi.

Kwa nini Lissu na wapinzani wengine wasitumie clip za Magufuli/Polepole nk pia kwenye majukwaa ya kampeni kuonyesha wasivyojali, wanavyobagua kwa kauli zao na matendo, wanavyodhalilisha wanawake, nk? Na pia zile ahadi uongo kama kompyuta kwa walimu wote, milioni 50 kila kijiji zinaweza kuonyeshwa kwenye majukwaa kuonyosha umma kuwa wanadili na mtu muongo. Kauli kama "Tume ikiwa huru CCM inaondoka Ikulu asubuhi na mapema" (Polepole), nk.

Kampeni za upinzani zina mambo mengi ya kuongelea na muda ni kidogo. Watumie mbinu za kisasa. Na zitumike nchi nzima. Clip za aina hii, zinaweza kutawanywa kwa wagombea ubunge na udiwani wote na kutumika katika majukwaa ya kampeni. Pia wakumbuke kuwa CHADEMA imekuwa ikisingiziwa kusema uongo katika mikutano yake. Kutumia clips za wasemaji wenyewe ni kama counterattack kwa upande wa CHADEMA. Ni vigumu mtu kukana kauli ambazo ziko kwenye clips.

Mahera na wenzie kwa hakika hawatotangaza mpinzani kushinda uchaguzi (regardless ya matokeo). Wameonyesha dalili zote za kutokufanya hivyo tangu mwanzo hado mwisho. Je, wapinzani wamejiandaeje kwa hili kama watashinda?

Nawatakia uchaguzi mwema.
 
Kwani hakieleweki ni nini hapo.

Nimemaanisha kila upande una vigeu geu. Si upinzani si chama tawala!
Mfano sisiemu walisema wasingetumia wasanii kwenye kampeni za mwaka huu, ila cha kushangaza ndio wamebeba karibia wasanii wote na wanatembea nao
Hebu leta mfano wa CHADEMA unasema wote wana vigeu geu!
 
Piga spana kwa Wasaliti wa Nchi Lissu atapigiwa kura na robert [emoji3][emoji3][emoji3]
Interesting....
FB_IMG_1601425432271.jpg
 
Ccm namba moja kwa ukigeugeu,maendeleo hayana vyama,Yana vyama.Mkichagua mwingine hampati maendeleo,utakuwa huru na haki,mbeleko zinatumika.na engine mengi.tusidanganyike ni muda wakuwaadhibu vikali,nafasi ndio hii.
Ni katika hali ya kibinadamu
 
Ubinadamu unathamini,utu,Uhuru na haki na sii vinginevyo.
Sijazungumzia utu hapa.

Ni kwamba binadamu anabadilika kati ya muda na muda.

Unaweza ukaamini hiki leo ila kesho ukabadili msimamo.
Hiko ndio nazungumzia. Sio utumbo wako huo.
 
Sijazungumzia utu hapa.

Ni kwamba binadamu anabadilika kati ya muda na muda.

Unaweza ukaamini hiki leo ila kesho ukabadili msimamo.
Hiko ndio nazungumzia. Sio utumbo wako huo.
Kama huzungumzii utu unazungumzia unyama au Nini.
 
Hakuna watu vigeu geu na wenye njaa kama CHADEMA..... Kura kwa JPM tu anatosha
 
Back
Top Bottom