Uchaguzi 2020 Ubunifu wa Godbless Lema na Halima Mdee utumike nchi nzima

Uchaguzi 2020 Ubunifu wa Godbless Lema na Halima Mdee utumike nchi nzima

Nunua flush toka china,jaza hotuba,gawa flush ziwe na audio visual
 
Tuna mbinu nyingi za kuwashinda hawa wezi kisiasa ikiwemo na hiyo uliyoshauri. So far tunatumia zingine kwanza
 
Alipoingia CHADEMA Magufuli alimwita fisadi na kuwa amemkimbia, lakini aliporudi CCM alikaribishwa live kwenye media, kuthibitisha mfumo ndio tatizo.

Uwanja mkubwa wa ndege kujengwa kijijini kwa Rais, na tenda kupewa mume mwenza ni dalili za ufisadi wa kitaasisi
Basi nchi hii hakuna fisadi
 
Make your point clear. Kama hauna cha kusema, ni busara kusoma na kupita kimya.
Kuna video clip pia ukitaka ya lema akimsema lowasa kabla hajasimama tena jukwaani 2015 na kumuombea kura za urais.
tapatalk_1564638877470.jpg
 
Kuna video clip pia ukitaka ya lema akimsema lowasa kabla hajasimama tena jukwaani 2015 na kumuombea kura za urais.View attachment 1590458
Mgombea wetu wa CCM akiwa Zanzibar anawaeleza Wazanzibar kuwa wasiondoke uwanjani hapo maana akimaliza hotuba bado Kuna show kabambe kutoka kwa wasanii na watamuona nae akicheza.... Wazenji nao viburi wakaondoka wakati anazungumza. Aisee!
 
Yawezekana unachoshauri kikawa na manufaa kwa upande mmoja kuaminisha wapiga kura kutokuaminika kwa mgombea husika. Kwa upande mwingine kufanya hivyo kunaweza kuathiri kuaminika kwa mgombea anayetumia njia hiyo kumdharilisha mgombea mwenzake pale asipoweza kuthibitisha uaminifu wake mwenyewe km fedha za mfuko wa jimbo zimetumikaje!

Wapiga kura si vijana wa vijiweni ambao hufurahia udaku. Wapiga kura watapenda kusikia mgombea atawatoaje kimaendeleo hapo walipofikishwa na Serikali ya ccm, ambayo ndiyo mtaji wao wa kura km afya, elimu, maji, miundo mbinu, na siyo siasa danganya za Uhuru, Haki na Maendeleo ya Watu.

Mpiga kura anaambiwa kuwa hayuko huru na hana haki wakati amekuja, kwa hiari yake, kumsikiliza huyo huyo anayemwambia hivyo. Ama mpiga kura anaambiwa, na mgombea jukwaani, kuwa wao watashughulikia maendeleo ya watu, lakini haelezwi yeye kama yeye, mpiga kura, ataendelezwaje?

Yawezekana mimi sijaelewa mada yako, nifafanulie. Mada za matukio hazisaidi wanaJF kuwa na maamuzi sahihi 28/10/2020
 
Kwa nini Lissu na wapinzani wengine wasitumie clip za Magufuli/Polepole nk pia kwenye majukwaa ya kampeni kuonyesha wasivyojali,
watu wanataka kusikia utaboresha vipi maisha yao
kuweka clips ni dalili ya kuishiwa sera
 
watu wanataka kusikia utaboresha vipi maisha yao
kuweka clips ni dalili ya kuishiwa sera
Sio dalili za kuishiwa sera Bali ni kuweka wazi tabia ya viongozi ambao ni waropokaji na wasio simamia kauli zao Kama Magu.
 
Lazima mabaya yenu yasemwe. Hamwezi kula rambirambi halafu mnategemea watu wasiseme. Sera zinasemwa na udikteta wa Magufuli pia. Watu wenywe ndio sisi. Ama wewe unafikiri watu ni wapi?
watu wanataka kusikia utaboresha vipi maisha yao
kuweka clips ni dalili ya kuishiwa sera
 
Wanatumia fact sana kuliko wale wa sanaa na maigizo
 
Lakini jamani kuna kitu cha ajabu sana hivi huyu nani sijui Magurudumu oooh sorry Makufuli pamoja na kupata fursa ya kutawala miaka mitano, ameshindwa kufanya vitu hata anaowatawala wamuamini? imefikia kuomba kura kwa kupiga magoti!!
 
Sawa kabisa. Wafanye hivyo nchi nzima. Hata mtumishi wa Mungu Askofu Mpemba amesema hivyo kuwa kiongozi anayevunja katiba, anayevunja sheria za nchi na ANAYEKANA/KUTOTIMIZA AHADI ZAKE hatufai kabisa. Hawa ni dhalimu. Wakitawala, nchi huugua.
 
Lazima mabaya yenu yasemwe. Hamwezi kula rambirambi halafu mnategemea watu wasiseme. Sera zinasemwa na udikteta wa Magufuli pia. Watu wenywe ndio sisi. Ama wewe unafikiri watu ni wapi?
ukishasema rambi rambi imeliwa halafu mwenzako anaonesha bonge la shule lipo kama university kwamba limekarabatiwa kwa michango ya rambi rambi,mpiga kura gani atakusikiliza?
acheni siasa nyepesi nyepesi chadema
 
Nani alikwambia kuwa rambirambi huwa inatumika kujenga shule za setikali? Mwaka huu mtatetea hata mavi. Nakwambia tena. Wapigakura ndio sisi.
ukishasema rambi rambi imeliwa halafu mwenzako anaonesha bonge la shule lipo kama university kwamba limekarabatiwa kwa michango ya rambi rambi,mpiga kura gani atakusikiliza?
acheni siasa nyepesi nyepesi chadema
 
CCM nao watakuja na clip za Lissu na wenzake wakimtukana Nyerere na Watanzania wengine..
 
Iko hivi 28 tunamuondoa meko na udhalimu wake yan🚮🚮🚮🚮
 
Mbona mnapenda sana kuabudu wanadamu? Katika akili yako unaona ni dhambi kumkosoa Nyerere? Nyerere mwenyewe alisema tujikosoe. Mwalimu alikuwa na akili kuliko ufuasi wako kipofu huo.
CCM nao watakuja na clip za Lissu na wenzake wakimtukana Nyerere na Watanzania wengine..
 
Back
Top Bottom